Wimbi la Ujambazi: Waziri Mkuu asema ni jukumu la kila Mtanzania kushiriki kwenye ulinzi

Ngoja nikatafute manati yangu ya mzungu...nikikuhisi ni jambazi nakumaliza
 
Tunashiriki vipi kwenye ulinzi na mikono mitupu, nchi hii kumiliki silaha ndogo kama pistol ni kama kumiliki madawa ya kulevya, yaani mlolongo mrefu wa kutafuta vibali hadi kwa mwenyekiti wa kitongoji, mwisho wa siku mtaa mzima wanajua unamiliki silaha, tayari unakuwa kwenye hatari ya kuwindwa....kwa nini sehemu ya kusajili isiwe sehemu moja, mfano polisi wilaya.
 
Kipindi cha JPM mbona haya mambo ni kama yaliisha kabisa tatizo nini apa.................
 
Democrasia ina gharama zake

Marekani pamoja na kuwa wazuri kiusalama

Lakini ujambazi unawasumbua sana.
 
Mkuu wa wilaya za ilala , temeke na kinondoni WATEULIWE kutoka JWTZ. Na wakati huo huo, wilaya za kipolisi za ilala, temeke na kinondoni zifutwe.pia ufungaji wa CCTV camera jiji la Dsm uzingatiwe.
Nasikia dar wanaichek yote sasa sijui hzo cctv wanazitumia kuangalia wadada wanaova vimini na kutetemesha makalio?
 
Na pia ni jukumuu letu kugawana Mapato ya nchi katika mazingira ya haki , sio mwingine anapewa nafuu ya biashara mwingine hapewi
 
Nawaombeni MAJAMBAZI muache tabia hiyo. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kazi Inaendelea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…