Wimbi la walimu kuhama CWT Tanzania limeshika kasi

Wimbi la walimu kuhama CWT Tanzania limeshika kasi

Hakuna mkataba wa kisheria kati ya cwt na walimu. Kinachotokea mwalimu akiajiriwa cwt inamkata pesa kwenye mshahara wake bila ya ridhaa yake. Yaani wanatumia mabavu kuwaibia walimu fedha zao. Walimu hawapewi fomu ya kujiunga na chama hiko kwa ridhaa yao wenyewe
Kuna haja ya kuwachunguza maafisa utumishi wote walioshiriki kuwaingizia walimu wetu makato ya Cwt pasipo hao walimu kujaza fomu Tuf 15 ambayo ndio hutoa authority kwa mwajiri kuingiza makato ya trade union yeyote wakiwemo hao misiwitii . Kwa wale ambao bado wako maofisini wafikishwe mahakamani haraka na kwa wale waliotangulia mbele za haki makaburi yao yapigwe pingu.
 
Kauli ya Majaliwa isije kuwa green light ya michango isiyoelewaka na wapigaji kutumia mwanya huo kujinemeesha
.
 
Ukisikia fursa jua wewe ndio fursa.
Wafanyakazi wengine pia wana matatizo, Ila walimu ndio wamepata mkombozi. MULIKA MWIZI MEEN!
Na huko wakijaa waliokosa fursa CWT katiba inabadilishwa, makato yanaongezeka
 
Ukisikia fursa jua wewe ndio fursa.
Wafanyakazi wengine pia wana matatizo, Ila walimu ndio wamepata mkombozi. MULIKA MWIZI MEEN!
Na huko wakijaa waliokosa fursa CWT katiba inabadilishwa, makato yanaongezeka
Ukisikia kutapatapa kwa viongozi wa CWT, ndiyo huka sasa. Haki ya nani hilo tawi lenu la ccm litawafia tu mikononi mwenu! Maana hakuna namna nyingine.

Mtajuta ni kwa nini hamkuwasikiliza walimu wakati wanalalamika kuhusu makato yenu kandamizi ya ada ya uanachama kwa mfumo wa 2% kwenye mishahara yao, badala ya kuwakata kwa kiwango sawa (flat rate) kila mwezi.

Kwa kweli ikiwapendeza, wahame wote! Halafu tuone mtaishi vipi mjini. Na ikumbukwe anguko lenu, pia ni mwanzo wa anguko tarajiwa la ccm.
 
JPM alikuwa nabii
View attachment 2619915
Katika moja ya hotuba zake, Rais Magufuli alizungumzia michango ya 2% ambayo walimu hukatwa kwenye mishahara yao ili kuchangia Chama Cha Waalimu (CWT). Magufuli alisema michango hiyo hukipa CWT zaidi ya bilioni 3 kila mwezi, na walimu wamekuwa hawajiulizi ni kwa namna gani fedha hizo zimekuwa zikitumika.

Katika hotuba hiyo Magufuli alitoa wito kwa waalimu kulalamikia kuhusu matumizi ya michango yao kama ambavyo wamekuwa wakifanya katika kuidai serikali. Pia amezungumzia benki ya walimu ambayo amesema kwa sasa haifanyi vizuri na pia imekuwa ikinufaisha wafanya biashara badala ya walimu
Kwani Lengo ya hivi vyama ni nini..??
 
Back
Top Bottom