Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna aliyetumwa na Watu Kuwawakilisha!

Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna aliyetumwa na Watu Kuwawakilisha!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Kile kitendawili cha chaguo kati ya kura ya siri au kura ya wazi, kitapatiwa ufumbuzi wiki hii, ambapo waheshimiwa wabunge wetu, wa Bunge Maalum la Katiba, watapiga kura kuamua kama kura ziwe za wazi au za siri.

Kikawaida uchaguzi wowote unaoitwa huru na wa haki, kura hupigwa kwa siri "secret ballot" ili kulinda uhuru na haki ya mpiga kura!.

Hata hivyo kuna wenye hoja ya msingi kuhusu kura ya wazi kwa kisingizio eti kwa sababu wao ni wawakilishi wa wananchi, wanadai wanapaswa kupiga kura ya wazi, ili wale wananchi waliowatuma, wawaone na kuujua msimamo wao, wazi wazi na wengine hadi kudiriki kudai kuwa wanataka wananchi wawashuhudie wakifanya kile wananchi hao walichowatuma!.

Ukweli wa mambo ni kuwa, hoja hiyo ni uongo mtu, uongo mtakatifu! unaotumiwa ili kuhalisha ubabe na kuburutwa na CCM na vibaraka wake, wakiwemo makuwadi wa siasa za ukandamizaji!. Ukiondoa wale wawakilishi 201 ambao ni wateule wa Rais, hao angalau wametumwa/jituma kuziwakilisha taasisi zao, au vikundi vyao, na sina uhakika kama wanachama wote wa taasisi hizo, auvikundi hivyo, walikaa pamoja na kuwatuma mkifika huko mfanye hili au lile zaidi ya kuwatuma wakatetee maslahi yao!. Kwa vile hivi ni vikundi tuu vya watu, hawa ni wawakilishi wa vikundi na sio wawakilishi wa watu!, yaani wananchi kwa sababu hakuna mwananchi aliyewachagua wala kuwatuma!.

Tukija kwa waheshimiwa wabunge wetu wa bunge la JMT na BLW, hawa kweli ni wawakilishi halali wa wananchi na tumewachagua kwa kura zetu, waende kutuwakilisha ndani ya mabaraza ya kutunga sheria Bunge na BLW, tulichowatuma ni kwenda kutuwakilisha bungeni!, na sio kwenda kutuandikia katiba!.

Hivyo hakuna mbunge yoyote au mwakilishi yoyote aliyetumwana na mwananchi yoyote kwenda kule kwenye Bunge Maalum la Katiba kumwakilisha!, ila uwakilishi huo ni by proxy ya kwa kwa vile tulimtuma kihalali kwenda kutunga sheria, na miongoni mwa sheria halali waliotunga, ni ile sheria ya mabadiliko ya katiba, na kwa sheria hiyo, wakajipendekeza wao ndio wajigeuze wawakilishi wetu kwenye Bunge Maalum, then wao kuwa ni wawakilishi wa wananchi ni saawa kisheria, ila hakuna mwananchi yoyote aliyewatuma!, hivyo wapige kura za siri, na sio kusingizia eti wananchi wamewatuma!.

Wabunge hao, hawana kitu kinachoitwa "people mandate", kwa sababu hakuna mwananchi aliyepata fursa ya kumchangua mwakilishi wake hata mmoja ndani ya bunge maalum, zaidi ya huo uwakilishi by proxy, hivyo kura halali ni kura za siri!. Period!.

Kufuatia Mapendekezo ya Tume ya Warioba kupendekeza serikali 3, na Chama cha Mapinduzi, kuweka wazi msimamo wake ni wa serikali mbili, zikipigwa kura za wazi, hakuna mwana CCM yoyote atakayethubutu kupigia kura serikali tatu, hivyo kwa kuhofia kwenda kinyume cha matakwa ya chama chake, hivyo kutopiga kura kwa uhuru na haki. bali kufuata matakwa ya chama chake.

Mahakama zinapotoa uamuzi wa haki, pia huwa zinazingatia madhara yasiyorekebishika "irreparable damegge!", vivyo hivyo katika kupiga kura za wazi, yule mwana CCM mwenye kupenda serikali tatu, atapata "irrepable damegge" kama atakwenda kinyume cha msimamo wa chama chake!. Matokeo yatakuwa ni kushinda kwa hoja ya serikali mbili, hivyo kuendelea na sherikali mbili kwa ushindi wa kitisho, hivyo kukosa haki japo uhalali!.

Lakini kama CCM kimewapika vizuri makada wake kuunga mkono hoja ya serikali mbili na wote wakaikubali ndani ya mioyo yao, hata zikipigwa kura za siri, hao makada wake wote watapigia kura serikali mbili, hivyo hoja ya serikali mbili itakuwa imepita kwa kura ya huru na ya haki, hivyo kuendelea na serikali mbili kwa haki na kihalali.

Waheshimiwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Please, Don't let us down!.

Mungu Ibariki Tanzania.

Mungu wabariki Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Kuona Kweli, Kutenda Haki, na Kufanya Kweli!.

Pasco.
 
Kweli,Makonda na Kingunge wametumwa na wananchi gani.halafu ktk bunge ambapo hupiga kura za siri,huwa hawajatumwa na wananchi wa majimboni kwao?
 
kama wanataka wananchi wawaone si kuna kipindi cha michango ya kuongea na maandishi ambayo itawekwa kwny hansard.tatizo nini?CCM wanatafuta sababu
 
Kura ya wazi ni kulinda masrahi ya wale walio watuma.
 
Kura iwe ya siri, kama kweli wanataka kila jambo wafanye kwa uwazi basi tuanze na ukaguzi wa matumizi ya posho walipwazo huko
 
Kura za wazi ni kutafutana ubaya tu...naona watu hawaaminiani. Isije ngoma ikatoka kinyume na yale waliyokubaliana
 
Mkuu, Watanzania wengi ni wanafiki sana. Jana wabunge wetu wamekataa kiapo cha pamoja na badala yake wanataka kiapo cha mmoja mmoja ili waonekane. Ila kwenye kura, wale wale wanaotaka uwazi wanaanza kuingiza usiri. Maajab haya yapo Tanzania tu
 
Kura za wazi ni kutafutana ubaya tu...naona watu hawaaminiani. Isije ngoma ikatoka kinyume na yale waliyokubaliana
Ubaya wa nini mkuu? Kama wewe msimamo wako upo sahihi, iweje uhangaike na aina ya kura?
 
Ubaya wa nini mkuu? Kama wewe msimamo wako upo sahihi, iweje uhangaike na aina ya kura?

Kura iwe ya siri maana watu wanaogopa kuja kukamatana mashati baadae. Kura za wazi utata mtupu kwa mtazamo wangu. However, hata ya open ikibidi sio mbaya.
 
Mmbunge maana yake ni representative of the people na anachaguliwa na watu, sasa sijui iweje tena mtu anaamua kubadili maana wakati the whole purpose of representing is to hear as many demands of society as possible through their rep. Hiyo ndio sababu kuu ya uchaguzi kwa maana hiyo haki kwa wapiga kura kujua umechagua nini. Hili haki itendeke kwa wapiga kura kama unalilia kura ya siri walau wapiga kura wafahamu msimamo wako vinginevyo inakuwa ni maslahi binafsi na ulaghai unaweza waongopea baadae kama ukiulizwa na kujibu kwa kupima upepo.

Kwa maana hiyo siku zote mmbunge huwa anasimama kwa niaba ya watu na chama chake kwakuwa hakuna mgombea binafsi ambae anaweza dai yeye kachaguliwa kwa misimamo binafsi, hivyo basi kwa misingi hiyo kura ya wazi ndio njia pekee yenye misingi ya demokrasia.

Vilevile vyama vya siasa vina misingi yake na katiba zao ambazo ndio nguzo za chama, ilikukipa chama long term stability na wanachama wake. CCM ni zao la TANU na ASP vikitokea bara na visiwani hivyo unaweza ona nini misingi ya chama hicho na muungano wa serikali mbili kwanini unapewa priority kwa sababu za stability ya chama na muungano wenyewe wa kitaifa, wajumbe wanaoenda nyume na hapo maana yake wwanaenda vunja stability na nguzo za chama.

Ndio maana wanachama wapya kwenye vyama vya siasa huwa wana apishwa kwa maneno ya watatii na kufuata taratibu za chama na hivyo wanakuwa binded na taratibu za chama. Sasa kama mtu anafahamu nguzo za chama na misimamo yake alifuata nini huko kama azikubali, na kama alijua kwanini leo akatae kusimama na wenzake ndio maana kwa wazungu upuuzi huu hawataki. Well hata CDM sio ndio maana kuna watu walifukuzwa na wengine kutokea mahakamani kwa madai ya kukiuka kanuni za chama, leo taratibu hizi kwa wengine zionekane tofauti.

CCM ZnZ bado hipo imara kwa maoni yangu maana hawaoni aibu kuwataja wasaliti CCM bara ndio legelege angekuwa Nyerere angeshatoa adhabu wengi leo wenye kelele za kuuvunja muungano wamerudi baada ya viongozi waliofuata na kifo cha JKN vinginevyo tungekuwa tumeshawasahau na wabishi leo consquences would have been felt.

Kwa maana hao ndio watu watakao kuwa siku zote wanayumbisha chama cha magamba ndio maana kuna ulazima wa wajumbe kupiga kura za kichama kama wanaelewa nguzo za chama chao, uingereza swala kama hilo sio ombi ni amri kwa mwanachama mmbunge vinginevyo unafukuzwa chama live.
 
Mmbunge maana yake ni representative of the people na anachaguliwa na watu, sasa sijui iweje tena mtu anaamua kubadili maana wakati the whole purpose of representing is to hear as many demands of society as possible through their rep. Hiyo ndio sababu kuu ya uchaguzi kwa maana hiyo haki kwa wapiga kura kujua umechagua nini. Hili haki itendeke kwa wapiga kura kama unalilia kura ya siri walau wapiga kura wafahamu msimamo wako vinginevyo inakuwa ni maslahi binafsi na ulaghai unaweza waongopea baadae kama ukiulizwa na kujibu kwa kupima upepo.

Kwa maana hiyo siku zote mmbunge huwa anasimama kwa niaba ya watu na chama chake kwakuwa hakuna mgombea binafsi ambae anaweza dai yeye kachaguliwa kwa misimamo binafsi, hivyo basi kwa misingi hiyo kura ya wazi ndio njia pekee yenye misingi ya demokrasia.

Vilevile vyama vya siasa vina misingi yake na katiba zao ambazo ndio nguzo za chama, ilikukipa chama long term stability na wanachama wake. CCM ni zao la TANU na ASP vikitokea bara na visiwani hivyo unaweza ona nini misingi ya chama hicho na muungano wa serikali mbili kwanini unapewa priority kwa sababu za stability ya chama na muungano wenyewe wa kitaifa, wajumbe wanaoenda nyume na hapo maana yake wwanaenda vunja stability na nguzo za chama.

Ndio maana wanachama wapya kwenye vyama vya siasa huwa wana apishwa kwa maneno ya watatii na kufuata taratibu za chama na hivyo wanakuwa binded na taratibu za chama. Sasa kama mtu anafahamu nguzo za chama na misimamo yake alifuata nini huko kama azikubali, na kama alijua kwanini leo akatae kusimama na wenzake ndio maana kwa wazungu upuuzi huu hawataki. Well hata CDM sio ndio maana kuna watu walifukuzwa na wengine kutokea mahakamani kwa madai ya kukiuka kanuni za chama, leo tarati
bu hizi kwa wengine zionekane tofauti.

CCM ZnZ bado hipo imara kwa maoni yangu maana hawaoni aibu kuwataja wasaliti CCM bara ndio legelege angekuwa Nyerere angeshatoa adhabu wengi leo wenye kelele za kuuvunja muungano wamerudi baada ya viongozi waliofuata na kifo cha JKN vinginevyo tungekuwa tumeshawasahau na wabishi leo consquences would have been felt.

Kwa maana hao ndio watu watakao kuwa siku zote wanayumbisha chama cha magamba ndio maana kuna ulazima wa wajumbe kupiga kura za kichama kama wanaelewa nguzo za chama chao, uingereza swala kama hilo sio ombi ni amri kwa mwanachama mmbunge vinginevyo unafukuzwa chama live.

Huna akili unadhani tunatunga katiba ya chama
 
Huna akili unadhani tunatunga katiba ya chama
Unapoenda sehemu kupitia njia kama mwakilishi wa kundi fulani na umefikia hapo kupitia hilo kundi unabanwa na misimamo ya kikundi kwa maslahi ya kundi kumbuka ukulazimishwa kujiunga, ulijiunga kwa sababu unakiamini kikundi na umechaguliwa na wapiga kura kwa sababu za kulikubali hilo kundi.

Siasa umejifunza wapi we mbona kitu basic hicho politically. Ndio maana waelevu kama kina Shivji waliwaonya kukwepa haya mntakiwa kudai bunge la wananchi sio hili la sasa lenye makundi ya siasa, hapo party interest hazikwepeki na ni democratically right.
 
kama wanataka wananchi wawaone si kuna kipindi cha michango ya kuongea na maandishi ambayo itawekwa kwny hansard.tatizo nini?CCM wanatafuta sababu

Katiba ni sheria Mama na Baba ya Tanzania .cha kujiuliza Baba na Mama saa wanatunga kupata watoto .wanatungaga kwa uwazi au kwa siri ???? Na haswa pale kwenye kitendo cha kutia kura kwenye kiboksi kitakacho amua mtoto ata zaliwa ama laa .
 
Wanabodi,

Kile kitendawili cha chaguo kati ya kura ya siri au kura ya wazi, kitapatiwa ufumbuzi wiki hii, ambapo waheshimiwa wabunge wetu, wa Bunge Maalum la Katiba, watapiga kura kuamua kama kura ziwe za wazi au za siri.
Pasco.

Mwenye majibu wa haya maswali,hapo penye red pananichanganya! je watapiga kura za wazi au za siri katika kuamua kura ziwe za siri au za wazi? makubaliano ya kupiga kura za wazi au za siri katika kuamua kura ziwe za wazi au za siri yatapatikana namna gani?
 
Mwenye majibu wa haya maswali,hapo penye red pananichanganya! je watapiga kura za wazi au za siri katika kuamua kura ziwe za siri au za wazi? makubaliano ya kupiga kura za wazi au za siri katika kuamua kura ziwe za wazi au za siri yatapatikana namna gani?
Watapiga kura ya siri!.
Pasco
 
Mkuu Pasco uko sahihi 100% ..

Haswa kwa Nchi inayoendelea Kama Tz..Hatuwezi kutengeneza katiba kwa maslahi ya kikundi..

Tutakuja kutukanwa na wajukuu zetu.. Happy Feet usifananishe Misimamo ya Uingereza na Tanzania ..Hatufanani kwa Chochote kile...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom