Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna aliyetumwa na Watu Kuwawakilisha!

Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna aliyetumwa na Watu Kuwawakilisha!

Ninachojiuliza na sipati jibu wabunge wanaposema wanataka wananchi wawaone wanavyopiga kura wanamaanisha wananchi wote au wa mijini? Watafanya mbinu gani wananchi wa vijijini waweze kuwaona live wakipiga kura?
 
Kuwashinda CCM ni jambo ngumu si jambo rahisi, hata ikipigwa kura ya siri wanaweza kuweka mkakati wa mjumbe wa CCM ahakikishe anamuonyesha jirani yake kura yake hiyo ya siri kabla ya kuikusanya,hivyo wao kwa wao wakawa walinzi wa watakaonekana kwenda kinyume na kuweka mechanism ya kuhakisha hilo la KUONYESHANA linawezekana!bado hao jamaa kwa idadi yao nadhani wakidhamiria kwa namna km hii watapunguza uhuru wa mawazo ya mtu.

Ikumbukwe kwamba mjumbe wa bunge hili la katiba pamoja na kuwa anatoka katika kikundi au chama fulani lakini bado anao wajibu kwa taifa lake(maslahi mapana ya taifa) ana wajibu pia hata kwa kikundi chake anachokiwakilisha na zaidi anawajibu wa kufuata dhamira yake bila kushurutishwa kwa namna yeyote katika kufanya maamuzi.

Ili wajibu wa mjumbe utimie bila shuruti ni vyema kukawa na kura ya siri!Kimsingi bado hatuna demokrasi au utamaduni wa kuwavumilia wale ambao wapo kinyume na msimamo wa kikundi au chama huu ndio ukweli na tusidanganyane kwamba tuna uwazi wa kiasi hicho cha kura ya wazi!
 
Mungu wetu Baba wa Mbinguni nakuomba uliepushe Taifa letu ulilotuumbia sote dhidi ya Genge la walaji wa Taifa letu na makuwadi wao waliojificha chini ya mwamvuli wa chama chenye mlengo wa Ki Ibilisi kinachojiita ccm.
Mkuu Nyamigota, kukiita CCM ni chama chenye malengo ya kiibilisi, sio kuitendea haki CCM kama chama!, ibilisi ni baadhi tuu ya wana CCM, ila pia malaika wapo, na "masiya" wa ukombozi Tanzania pia yupo CCM!.

Siungi mkono kukiita CCM ni ibilisi!, CCM ni zimwi tuu, tena likujualo!. CCM is a devil, safari ya 2015, is a choice between a devil and a deep blue sea!, we are forced to choose between the devils!, a devil we know, and a devil, we don't know!, in between the two devils, choose the lesser!.
NB. kutumia majina ya Kiingereza, yana less impact, mfano a devil, na sio ibilisi au shetani!
Pasco
 
Tutakuja kutukanwa na wajukuu zetu.. Happy Feet usifananishe Misimamo ya Uingereza na Tanzania ..Hatufanani kwa Chochote kile...

Hatuwezi kufanana na watu walioanza mchakato wa kujenga taifa miaka 500 iliyopita huo ni ukweli, lakini tunaweza kujifunza kama tutajiuliza inakuaje wale viongozi wa chama kimoja hawatofautiani hadharani na misimamo ya chama ni mmoja, inakuaje wenzetu waishi bila ya kupigana kwa sababu za siasa wakati hakuna watu millioni 45 wanaweza kubaliana kwenye kila kitu (hata wazungu), ndio maana kila siku maandamano na wao.

Wenzetu walichojifunza kikubwa kwenye interest ni kwa faida ya kundi na hivyo misimamo lazima iheshimika kushinda mawazo ya mwanachama, pili ni interest za taifa lazima ziheshimike zaidi ya mawazo ya vyama.

Ina maana interest za taifa ndio kila kitu, na kikubwa hapo ni kuwa na mbinu za watu kuweza kushirikiana, kuishi pamoja na kueshimiana (watu ambao otherwise have differing perspectives). Na kwa sasa wanalenga umoja wa kimataifa wa watu wao kupitia Europe. If you ask me knowing mzungu does not take chances after he done his risk assessment, naweza sema wameshaona in the long run marekani na china inabidi wazibitiwe or else watakuwa vulnerable kwenye influence na interest za watu wao duniani (inahitaji thread yake).

Sasa nyie ndio kwanza mwenzenu kafa majuzi na kazi hajaimaliza leo tayari hamtaki kushirikiana maana hata bara kwenyewe bado mara sijui MoU zinapendelewa , mara sijui BAKWATA wanataka hivi, hiyo ni misingi mibovu na isiyokuwa na national interest na isiyolenga kujenga ushirikiano unaohitajika kwa ustawi wa jamii. Ndio maana akija mzungu sijui mwarabu dakika moja mpo vipande vipande (naanza kuona labda kweli sisi waafrika tuna laana ya mungu maana aiwezekani watu kutokuona the obvious outcome of their actions).
 
Mchakato huu ni wa kitaifa, kwa maana unawagusa watanzania. Rasimu inayojadiliwa kinadharia inatokana na wao.

Wajumbe waliochaguliwa kuwawakilisha wanatokana na wao. Wangependa maoni na mawazo ya wajumbe wa bunge yatokane na wao.

Katika muktadha huo wangependa kuwa na democratic faith dhidi ya wajumbe wao. Democratic faith haijengwi kizani. Democratic faith haijengwi mafichoni bali hujengwa hadharani na mbele ya macho ya wengi. Kura iwe wazi. Hili ni moja.

Pili wanafalsafa wanasema binaadamu kwa asili yake ni mbinafsi. Ili kuepuka ubinafsi wa mwanadamu katika muktadha unaogusa maslahi ya wengi unatafutwa mfumo ambao uta neutralize matakwa binafsi ya mwanadamu na hatimaye tunamvisha kilemba cha matakwa ya wengi. Kura ya wazi ni kilemba sahihi.

Tatu, hoja inayotumika kuhalalisha kura ya wazi ni hoja nyepesi. Vitisho na hofu katika historia ya demokrasia duniani havijawahi kutumika kuwa nyenzo za kuhalalisha maamuzi yanayogusa maslahi ya Taifa. Hoja zinazotumika ni uwezo wa methodolojia katika kukidhi matakwa ya wengi lakini siyo hatari ya methodolojia kutoa mwanya kwa wawakilishi kutishwa na vyama vyao.

Kwa maana hiyo wanaohalalisha kura ya siri wamekosa msingi wa hoja yao.
Watu wanajaribu kuhalarisha mambo yao ya Siri kwa kutumia hoja nyepesi kwamba kura zote hupigwankwa siri. Wanashindwa kutofautisha kati ya kura ya kumchagua kiongozi na kura ya kupitisha hoja bungeni. Katika mifumo yote ya kibunge duniani utaratibu wa kupitisha hoja hufanywa kwa uwazi kwani unaenda sambamba na mjadala wa wabunge kuhusu hoja inayopitishwa.

Hata hivyo kiwango cha uwazi kiwe hivi.

Katika kupitisha kifungu kwa kifungu cha rasimu itumike kura ya wazi kwa sababu inagusa maeneo mahsusi ambayo kwa kiasi kikubwa kilemba cha matakwa ya wengi kinahitajika zaidi na wanye mchakato (watanzania) wangependa kuona ni jinsi gani matakwa yao yanawasilishwa.

Baada ya mchakato huo, katika kupitisha rasimu ya mwisho basi kura ya siri itumike kwani itakua tayari kila kipengele kimepitishwa katika mfumo wa wazi ambapo ubinafsi ulizikwa. Hivyo kama watavyofanya watanzania katika kura ya maoni basi ifanyike hivyo kuanzia bungeni kwa uwingi wa kura kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba.
 
Mchakato huu ni wa kitaifa, kwa maana unawagusa watanzania. Rasimu inayojadiliwa kinadharia inatokana na wao.

Wajumbe waliochaguliwa kuwawakilisha wanatokana na wao. Wangependa maoni na mawazo ya wajumbe wa bunge yatokane na wao.

Katika muktadha huo wangependa kuwa na democratic faith dhidi ya wajumbe wao. Democratic faith haijengwi kizani. Democratic faith haijengwi mafichoni bali hujengwa hadharani na mbele ya macho ya wengi. Kura iwe wazi. Hili ni moja.

Pili wanafalsafa wanasema binaadamu kwa asili yake ni mbinafsi. Ili kuepuka ubinafsi wa mwanadamu katika muktadha unaogusa maslahi ya wengi unatafutwa mfumo ambao uta neutralize matakwa binafsi ya mwanadamu na hatimaye tunamvisha kilemba cha matakwa ya wengi. Kura ya wazi ni kilemba sahihi.

Tatu, hoja inayotumika kuhalalisha kura ya wazi ni hoja nyepesi. Vitisho na hofu katika historia ya demokrasia duniani havijawahi kutumika kuwa nyenzo za kuhalalisha maamuzi yanayogusa maslahi ya Taifa. Hoja zinazotumika ni uwezo wa methodolojia katika kukidhi matakwa ya wengi lakini siyo hatari ya methodolojia kutoa mwanya kwa wawakilishi kutishwa na vyama vyao.

Kwa maana hiyo wanaohalalisha kura ya siri wamekosa msingi wa hoja yao.
Watu wanajaribu kuhalarisha mambo yao ya Siri kwa kutumia hoja nyepesi kwamba kura zote hupigwankwa siri. Wanashindwa kutofautisha kati ya kura ya kumchagua kiongozi na kura ya kupitisha hoja bungeni. Katika mifumo yote ya kibunge duniani utaratibu wa kupitisha hoja hufanywa kwa uwazi kwani unaenda sambamba na mjadala wa wabunge kuhusu hoja inayopitishwa.

Hata hivyo kiwango cha uwazi kiwe hivi.

Katika kupitisha kifungu kwa kifungu cha rasimu itumike kura ya wazi kwa sababu inagusa maeneo mahsusi ambayo kwa kiasi kikubwa kilemba cha matakwa ya wengi kinahitajika zaidi na wanye mchakato (watanzania) wangependa kuona ni jinsi gani matakwa yao yanawasilishwa.

Baada ya mchakato huo, katika kupitisha rasimu ya mwisho basi kura ya siri itumike kwani itakua tayari kila kipengele kimepitishwa katika mfumo wa wazi ambapo ubinafsi ulizikwa. Hivyo kama watavyofanya watanzania katika kura ya maoni basi ifanyike hivyo kuanzia bungeni kwa uwingi wa kura kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba.

Hayo unayoyaasema ni kwenye highly democratic countries ndiko mtu anaweza kuonyesha matakwa yake bila woga. Sio TZ kwa CCM ambao mtu kuonnyesha nia ya kugombea urais anaitwa kukanywa! Acha habari hiyo ya western world ambako democracy ni kupindukia!
 
Kwa hali ya Bunge letu la Katiba lilivyo, mawazo nje ya box yanahitajika kuliko kung'ang'ania na nadharia ya Democratic faith!
 
Kwa mawazo yako mfu ya maccm basi tuanze kura ya wazi kule kalenga kila mtu asimame nyuma ya mgombea kwani demokrasia imekua.
 
Mchakato huu ni wa kitaifa, kwa maana unawagusa watanzania. Rasimu inayojadiliwa kinadharia inatokana na wao.

Wajumbe waliochaguliwa kuwawakilisha wanatokana na wao. Wangependa maoni na mawazo ya wajumbe wa bunge yatokane na wao.

Katika muktadha huo wangependa kuwa na democratic faith dhidi ya wajumbe wao. Democratic faith haijengwi kizani. Democratic faith haijengwi mafichoni bali hujengwa hadharani na mbele ya macho ya wengi. Kura iwe wazi. Hili ni moja.

Pili wanafalsafa wanasema binaadamu kwa asili yake ni mbinafsi. Ili kuepuka ubinafsi wa mwanadamu katika muktadha unaogusa maslahi ya wengi unatafutwa mfumo ambao uta neutralize matakwa binafsi ya mwanadamu na hatimaye tunamvisha kilemba cha matakwa ya wengi. Kura ya wazi ni kilemba sahihi.

Tatu, hoja inayotumika kuhalalisha kura ya wazi ni hoja nyepesi. Vitisho na hofu katika historia ya demokrasia duniani havijawahi kutumika kuwa nyenzo za kuhalalisha maamuzi yanayogusa maslahi ya Taifa. Hoja zinazotumika ni uwezo wa methodolojia katika kukidhi matakwa ya wengi lakini siyo hatari ya methodolojia kutoa mwanya kwa wawakilishi kutishwa na vyama vyao.

Kwa maana hiyo wanaohalalisha kura ya siri wamekosa msingi wa hoja yao.
Watu wanajaribu kuhalarisha mambo yao ya Siri kwa kutumia hoja nyepesi kwamba kura zote hupigwankwa siri. Wanashindwa kutofautisha kati ya kura ya kumchagua kiongozi na kura ya kupitisha hoja bungeni. Katika mifumo yote ya kibunge duniani utaratibu wa kupitisha hoja hufanywa kwa uwazi kwani unaenda sambamba na mjadala wa wabunge kuhusu hoja inayopitishwa.

Hata hivyo kiwango cha uwazi kiwe hivi.

Katika kupitisha kifungu kwa kifungu cha rasimu itumike kura ya wazi kwa sababu inagusa maeneo mahsusi ambayo kwa kiasi kikubwa kilemba cha matakwa ya wengi kinahitajika zaidi na wanye mchakato (watanzania) wangependa kuona ni jinsi gani matakwa yao yanawasilishwa.

Baada ya mchakato huo, katika kupitisha rasimu ya mwisho basi kura ya siri itumike kwani itakua tayari kila kipengele kimepitishwa katika mfumo wa wazi ambapo ubinafsi ulizikwa. Hivyo kama watavyofanya watanzania katika kura ya maoni basi ifanyike hivyo kuanzia bungeni kwa uwingi wa kura kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba.



user-offline.png
Jabirimakame Join Date : 15th January 2014

“No one can make you feel inferior without your consent.”
 
''..Baada ya mchakato huo, katika kupitisha rasimu ya mwisho basi kura ya siri itumike kwani itakua tayari kila kipengele kimepitishwa katika mfumo wa wazi ambapo ubinafsi ulizikwa. Hivyo kama watavyofanya watanzania katika kura ya maoni basi ifanyike hivyo kuanzia bungeni kwa uwingi wa kura kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba..''

Kama kila kifungu kitakuwa kimepita unapiga kura ya siri mwishoni ili iweje?!

Kisheria hiyo haipo sawa.kwa mfano una mambo kumi ambayo yote yamekubalika ama kupitishwa kwa kura za wazi kwa namna ya kupitia jambo moja moja sasa unapiga kura ya jumla mwishoni iwe ya wazi ama siri ili iweje kama yote yameshapita?!
 
Mchakato huu ni wa kitaifa, kwa maana unawagusa watanzania. Rasimu inayojadiliwa kinadharia inatokana na wao.

Wajumbe waliochaguliwa kuwawakilisha wanatokana na wao. Wangependa maoni na mawazo ya wajumbe wa bunge yatokane na wao.

Katika muktadha huo wangependa kuwa na democratic faith dhidi ya wajumbe wao. Democratic faith haijengwi kizani. Democratic faith haijengwi mafichoni bali hujengwa hadharani na mbele ya macho ya wengi. Kura iwe wazi. Hili ni moja.

Pili wanafalsafa wanasema binaadamu kwa asili yake ni mbinafsi. Ili kuepuka ubinafsi wa mwanadamu katika muktadha unaogusa maslahi ya wengi unatafutwa mfumo ambao uta neutralize matakwa binafsi ya mwanadamu na hatimaye tunamvisha kilemba cha matakwa ya wengi. Kura ya wazi ni kilemba sahihi.

Tatu, hoja inayotumika kuhalalisha kura ya wazi ni hoja nyepesi. Vitisho na hofu katika historia ya demokrasia duniani havijawahi kutumika kuwa nyenzo za kuhalalisha maamuzi yanayogusa maslahi ya Taifa. Hoja zinazotumika ni uwezo wa methodolojia katika kukidhi matakwa ya wengi lakini siyo hatari ya methodolojia kutoa mwanya kwa wawakilishi kutishwa na vyama vyao.

Kwa maana hiyo wanaohalalisha kura ya siri wamekosa msingi wa hoja yao.
Watu wanajaribu kuhalarisha mambo yao ya Siri kwa kutumia hoja nyepesi kwamba kura zote hupigwankwa siri. Wanashindwa kutofautisha kati ya kura ya kumchagua kiongozi na kura ya kupitisha hoja bungeni. Katika mifumo yote ya kibunge duniani utaratibu wa kupitisha hoja hufanywa kwa uwazi kwani unaenda sambamba na mjadala wa wabunge kuhusu hoja inayopitishwa.

Hata hivyo kiwango cha uwazi kiwe hivi.

Katika kupitisha kifungu kwa kifungu cha rasimu itumike kura ya wazi kwa sababu inagusa maeneo mahsusi ambayo kwa kiasi kikubwa kilemba cha matakwa ya wengi kinahitajika zaidi na wanye mchakato (watanzania) wangependa kuona ni jinsi gani matakwa yao yanawasilishwa.

Baada ya mchakato huo, katika kupitisha rasimu ya mwisho basi kura ya siri itumike kwani itakua tayari kila kipengele kimepitishwa katika mfumo wa wazi ambapo ubinafsi ulizikwa. Hivyo kama watavyofanya watanzania katika kura ya maoni basi ifanyike hivyo kuanzia bungeni kwa uwingi wa kura kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba.

Hivi wewe elimu yako ni ya darasa la ngapi?, hivi unashindwa kujua kwamba hakuna hata mjumbe mmoja ambaye anawakilisha wananchi?, ni lini umemchagua mtu na kumtuma dodoma kukuandikia katiba?, eti wawakilishi wao', wote walivyo ni yupi anayewajibika kwako au atakayewajibika kwako kwa michango atakayoitoa?, kumbuka vizuri kama uliwahi kumtuma mbunge wako aende kuandika katiba. Kama wewe ni kijana nina wasiwasi na taifa la kesho utakalolijenga.
 
Imepita kuwa upigaji kura ni wasiri ,kuna mtu kanibeep sasa hivi.
 
yaani hii ni kumaanisha sera za susuemu ni potofu?
cc L Mutuz na binamu zake le Professor Anna binti kajumulo wa Tibaijuka
 
Itakuwa vizuri sana kama Itakuwa imepita Kuwa Kura iwe Siri
 
Back
Top Bottom