Agenda gani hizo?
Mmbunge maana yake ni representative of the people na anachaguliwa na watu, sasa sijui iweje tena mtu anaamua kubadili maana wakati the whole purpose of representing is to hear as many demands of society as possible through their rep. Hiyo ndio sababu kuu ya uchaguzi kwa maana hiyo haki kwa wapiga kura kujua umechagua nini. Hili haki itendeke kwa wapiga kura kama unalilia kura ya siri walau wapiga kura wafahamu msimamo wako vinginevyo inakuwa ni maslahi binafsi na ulaghai unaweza waongopea baadae kama ukiulizwa na kujibu kwa kupima upepo.
Kwa maana hiyo siku zote mmbunge huwa anasimama kwa niaba ya watu na chama chake kwakuwa hakuna mgombea binafsi ambae anaweza dai yeye kachaguliwa kwa misimamo binafsi, hivyo basi kwa misingi hiyo kura ya wazi ndio njia pekee yenye misingi ya demokrasia.
Vilevile vyama vya siasa vina misingi yake na katiba zao ambazo ndio nguzo za chama, ilikukipa chama long term stability na wanachama wake. CCM ni zao la TANU na ASP vikitokea bara na visiwani hivyo unaweza ona nini misingi ya chama hicho na muungano wa serikali mbili kwanini unapewa priority kwa sababu za stability ya chama na muungano wenyewe wa kitaifa, wajumbe wanaoenda nyume na hapo maana yake wwanaenda vunja stability na nguzo za chama.
Ndio maana wanachama wapya kwenye vyama vya siasa huwa wana apishwa kwa maneno ya watatii na kufuata taratibu za chama na hivyo wanakuwa binded na taratibu za chama. Sasa kama mtu anafahamu nguzo za chama na misimamo yake alifuata nini huko kama azikubali, na kama alijua kwanini leo akatae kusimama na wenzake ndio maana kwa wazungu upuuzi huu hawataki. Well hata CDM sio ndio maana kuna watu walifukuzwa na wengine kutokea mahakamani kwa madai ya kukiuka kanuni za chama, leo taratibu hizi kwa wengine zionekane tofauti.
CCM ZnZ bado hipo imara kwa maoni yangu maana hawaoni aibu kuwataja wasaliti CCM bara ndio legelege angekuwa Nyerere angeshatoa adhabu wengi leo wenye kelele za kuuvunja muungano wamerudi baada ya viongozi waliofuata na kifo cha JKN vinginevyo tungekuwa tumeshawasahau na wabishi leo consquences would have been felt.
Kwa maana hao ndio watu watakao kuwa siku zote wanayumbisha chama cha magamba ndio maana kuna ulazima wa wajumbe kupiga kura za kichama kama wanaelewa nguzo za chama chao, uingereza swala kama hilo sio ombi ni amri kwa mwanachama mmbunge vinginevyo unafukuzwa chama live.
Wanabodi,
Kile kitendawili cha chaguo kati ya kura ya siri au kura ya wazi, kitapatiwa ufumbuzi wiki hii, ambapo waheshimiwa wabunge wetu, wa Bunge Maalum la Katiba, watapiga kura kuamua kama kura ziwe za wazi au za siri.
Kikawaida uchaguzi wowote unaoitwa huru na wa haki, kura hupigwa kwa siri "secret ballot" ili kulinda uhuru na haki ya mpiga kura!.
Hata hivyo kuna wenye hoja ya msingi kuhusu kura ya wazi kwa kisingizio eti kwa sababu wao ni wawakilishi wa wananchi, wanadai wanapaswa kupiga kura ya wazi, ili wale wananchi waliowatuma, wawaone na kuujua msimamo wao, wazi wazi na wengine hadi kudiriki kudai kuwa wanataka wananchi wawashuhudie wakifanya kile wananchi hao walichowatuma!.
Ukweli wa mambo ni kuwa, hoja hiyo ni uongo mtu, uongo mtakatifu! unaotumiwa ili kuhalisha ubabe na kuburutwa na CCM na vibaraka wake, wakiwemo makuwadi wa siasa za ukandamizaji!. Ukiondoa wale wawakilishi 201 ambao ni wateule wa Rais, hao angalau wametumwa/jituma kuziwakilisha taasisi zao, au vikundi vyao, na sina uhakika kama wanachama wote wa taasisi hizo, auvikundi hivyo, walikaa pamoja na kuwatuma mkifika huko mfanye hili au lile zaidi ya kuwatuma wakatetee maslahi yao!. Kwa vile hivi ni vikundi tuu vya watu, hawa ni wawakilishi wa vikundi na sio wawakilishi wa watu!, yaani wananchi kwa sababu hakuna mwananchi aliyewachagua wala kuwatuma!.
Tukija kwa waheshimiwa wabunge wetu wa bunge la JMT na BLW, hawa kweli ni wawakilishi halali wa wananchi na tumewachagua kwa kura zetu, waende kutuwakilisha ndani ya mabaraza ya kutunga sheria Bunge na BLW, tulichowatuma ni kwenda kutuwakilisha bungeni!, na sio kwenda kutuandikia katiba!.
Hivyo hakuna mbunge yoyote au mwakilishi yoyote aliyetumwana na mwananchi yoyote kwenda kule kwenye Bunge Maalum la Katiba kumwakilisha!, ila uwakilishi huo ni by proxy ya kwa kwa vile tulimtuma kihalali kwenda kutunga sheria, na miongoni mwa sheria halali waliotunga, ni ile sheria ya mabadiliko ya katiba, na kwa sheria hiyo, wakajipendekeza wao ndio wajigeuze wawakilishi wetu kwenye Bunge Maalum, then wao kuwa ni wawakilishi wa wananchi ni saawa kisheria, ila hakuna mwananchi yoyote aliyewatuma!, hivyo wapige kura za siri, na sio kusingizia eti wananchi wamewatuma!.
Wabunge hao, hawana kitu kinachoitwa "people mandate", kwa sababu hakuna mwananchi aliyepata fursa ya kumchangua mwakilishi wake hata mmoja ndani ya bunge maalum, zaidi ya huo uwakilishi by proxy, hivyo kura halali ni kura za siri!. Period!.
Kufuatia Mapendekezo ya Tume ya Warioba kupendekeza serikali 3, na Chama cha Mapinduzi, kuweka wazi msimamo wake ni wa serikali mbili, zikipigwa kura za wazi, hakuna mwana CCM yoyote atakayethubutu kupigia kura serikali tatu, hivyo kwa kuhofia kwenda kinyume cha matakwa ya chama chake, hivyo kutopiga kura kwa uhuru na haki. bali kufuata matakwa ya chama chake.
Mahakama zinapotoa uamuzi wa haki, pia huwa zinazingatia madhara yasiyorekebishika "irreparable damegge!", vivyo hivyo katika kupiga kura za wazi, yule mwana CCM mwenye kupenda serikali tatu, atapata "irrepable damegge" kama atakwenda kinyume cha msimamo wa chama chake!. Matokeo yatakuwa ni kushinda kwa hoja ya serikali mbili, hivyo kuendelea na sherikali mbili kwa ushindi wa kitisho, hivyo kukosa haki japo uhalali!.
Lakini kama CCM kimewapika vizuri makada wake kuunga mkono hoja ya serikali mbili na wote wakaikubali ndani ya mioyo yao, hata zikipigwa kura za siri, hao makada wake wote watapigia kura serikali mbili, hivyo hoja ya serikali mbili itakuwa imepita kwa kura ya huru na ya haki, hivyo kuendelea na serikali mbili kwa haki na kihalali.
Waheshimiwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Please, Don't let us down!.
Mungu Ibariki Tanzania.
Mungu wabariki Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Kuona Kweli, Kutenda Haki, na Kufanya Kweli!.
Pasco.
kama RASIMU YA KATIBA IMEANDIKWA KWA MISINGI YA SERIKALI TATU,
UKISOMA KUANZIA A IBARA YA KWANZA INAANDIKWA KWA MTIRRRIKO WA MUUNDO WA SERIKALI TATU,
ISIPOKUWA IBARA CHACHE ZENYE MAMBO YA KIJUMNLA JUMLA
HAKUNA UWEZEKANO WA KUIPINGA HII RASIMU HATA IWEJE NA BADO BUNGE LIENDELEE KUWAPO SAS LITAJADILI NINI,
KUIKATAA RASIMU YA SERIKARI TATU ITAPELEKEA KULIVUNJA BUNGE AUTOMATICALLY
SIJUI KAMA CCM WANALIJUA HILI
HAKUNA MAHALA AMBAPO RASIMU IMEPENEDEKEZA SERLIKALI MBILI,
WAJUMBE WANAO TAKA SERIKALI MBILI WATAPIGAKURA KUPITISHA SERIKALI MBILI KUTOKANA NA RASIMU IPI?
AMBAYO MTIRIRIKO WA IBARA ZAKE UKOJE NA AMBAYO IMETOKANA NA TUME IPI NA INAWAKILISHA MAONI YA WANANCHI WEPI NA WANGAPI??
NATABIRI TUTARUDI KULE AMBAKO TULIKUKIBIA MWANZO KUTAFUTA MUAFAKA WA KITAIFA KWANZA JUU YA MUUNDO WA MUUNGANO, THEN NDO TUANDAE RASIMUYA KATIBA
kwa hiyo kama hawajatumwa wamekwenda dodoma kutafuna tu hela ya umma? na kwanini unataka kura ya siri kama hujawatuma. kwa taarifa yako, tumewatuma kwenda kujadili rasimu ya katiba. na ndio maana watanzania wamerizika kuwalipa lakitatu kwa siku. kama ingekuwa hakuna ulazima wa kuijadilii rasimu, wasingeenda dodoma kukaa siku 70.ingetosha tu rasimu ile ikawa katiba bila hata watu kwenda dodoma. tatizo tukipenda chama, tunapenda na kauli za viongozi wa vyama hata kama ni za kijinga. unapopiga kura ya siri kumchagua mbunge, ni kwa sababu unachagua mmoja kati ya wagombea wengi. kwa raisi hivyohivyo. kwenye katiba humchagui mtu. unapigia vifungv vya rasimu ya katiba. vifungu hivi vikipita ndio sheria mama ya nchi. ni lini, na ni wapi sheria za nchi zikapitishwa kwa siri? labda ziwe sheria za kikandamizaji. kilichopo hapo, ni woga tu wa wajumbe kufukuzwa kwenye vyama. na kiongozi anayeogopa kufukuzwa kwenye chama hana sifa ya kuwa kiongozi. kwa sababu analinda maslahi yake ktk chama, sio maslahi ya wananchi. kura ziwe ya uso kwa uso.Wanabodi,
Kile kitendawili cha chaguo kati ya kura ya siri au kura ya wazi, kitapatiwa ufumbuzi wiki hii, ambapo waheshimiwa wabunge wetu, wa Bunge Maalum la Katiba, watapiga kura kuamua kama kura ziwe za wazi au za siri.
Kikawaida uchaguzi wowote unaoitwa huru na wa haki, kura hupigwa kwa siri "secret ballot" ili kulinda uhuru na haki ya mpiga kura!.
Hata hivyo kuna wenye hoja ya msingi kuhusu kura ya wazi kwa kisingizio eti kwa sababu wao ni wawakilishi wa wananchi, wanadai wanapaswa kupiga kura ya wazi, ili wale wananchi waliowatuma, wawaone na kuujua msimamo wao, wazi wazi na wengine hadi kudiriki kudai kuwa wanataka wananchi wawashuhudie wakifanya kile wananchi hao walichowatuma!.
Ukweli wa mambo ni kuwa, hoja hiyo ni uongo mtu, uongo mtakatifu! unaotumiwa ili kuhalisha ubabe na kuburutwa na CCM na vibaraka wake, wakiwemo makuwadi wa siasa za ukandamizaji!. Ukiondoa wale wawakilishi 201 ambao ni wateule wa Rais, hao angalau wametumwa/jituma kuziwakilisha taasisi zao, au vikundi vyao, na sina uhakika kama wanachama wote wa taasisi hizo, auvikundi hivyo, walikaa pamoja na kuwatuma mkifika huko mfanye hili au lile zaidi ya kuwatuma wakatetee maslahi yao!. Kwa vile hivi ni vikundi tuu vya watu, hawa ni wawakilishi wa vikundi na sio wawakilishi wa watu!, yaani wananchi kwa sababu hakuna mwananchi aliyewachagua wala kuwatuma!.
Tukija kwa waheshimiwa wabunge wetu wa bunge la JMT na BLW, hawa kweli ni wawakilishi halali wa wananchi na tumewachagua kwa kura zetu, waende kutuwakilisha ndani ya mabaraza ya kutunga sheria Bunge na BLW, tulichowatuma ni kwenda kutuwakilisha bungeni!, na sio kwenda kutuandikia katiba!.
Hivyo hakuna mbunge yoyote au mwakilishi yoyote aliyetumwana na mwananchi yoyote kwenda kule kwenye Bunge Maalum la Katiba kumwakilisha!, ila uwakilishi huo ni by proxy ya kwa kwa vile tulimtuma kihalali kwenda kutunga sheria, na miongoni mwa sheria halali waliotunga, ni ile sheria ya mabadiliko ya katiba, na kwa sheria hiyo, wakajipendekeza wao ndio wajigeuze wawakilishi wetu kwenye Bunge Maalum, then wao kuwa ni wawakilishi wa wananchi ni saawa kisheria, ila hakuna mwananchi yoyote aliyewatuma!, hivyo wapige kura za siri, na sio kusingizia eti wananchi wamewatuma!.
Wabunge hao, hawana kitu kinachoitwa "people mandate", kwa sababu hakuna mwananchi aliyepata fursa ya kumchangua mwakilishi wake hata mmoja ndani ya bunge maalum, zaidi ya huo uwakilishi by proxy, hivyo kura halali ni kura za siri!. Period!.
Kufuatia Mapendekezo ya Tume ya Warioba kupendekeza serikali 3, na Chama cha Mapinduzi, kuweka wazi msimamo wake ni wa serikali mbili, zikipigwa kura za wazi, hakuna mwana CCM yoyote atakayethubutu kupigia kura serikali tatu, hivyo kwa kuhofia kwenda kinyume cha matakwa ya chama chake, hivyo kutopiga kura kwa uhuru na haki. bali kufuata matakwa ya chama chake.
Mahakama zinapotoa uamuzi wa haki, pia huwa zinazingatia madhara yasiyorekebishika "irreparable damegge!", vivyo hivyo katika kupiga kura za wazi, yule mwana CCM mwenye kupenda serikali tatu, atapata "irrepable damegge" kama atakwenda kinyume cha msimamo wa chama chake!. Matokeo yatakuwa ni kushinda kwa hoja ya serikali mbili, hivyo kuendelea na sherikali mbili kwa ushindi wa kitisho, hivyo kukosa haki japo uhalali!.
Lakini kama CCM kimewapika vizuri makada wake kuunga mkono hoja ya serikali mbili na wote wakaikubali ndani ya mioyo yao, hata zikipigwa kura za siri, hao makada wake wote watapigia kura serikali mbili, hivyo hoja ya serikali mbili itakuwa imepita kwa kura ya huru na ya haki, hivyo kuendelea na serikali mbili kwa haki na kihalali.
Waheshimiwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Please, Don't let us down!.
Mungu Ibariki Tanzania.
Mungu wabariki Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Kuona Kweli, Kutenda Haki, na Kufanya Kweli!.
Pasco.
kwa hiyo kama hawajatumwa wamekwenda dodoma kutafuna tu hela ya umma? na kwanini unataka kura ya siri kama hujawatuma. kwa taarifa yako, tumewatuma kwenda kujadili rasimu ya katiba. na ndio maana watanzania wamerizika kuwalipa lakitatu kwa siku. kama ingekuwa hakuna ulazima wa kuijadilii rasimu, wasingeenda dodoma kukaa siku 70.ingetosha tu rasimu ile ikawa katiba bila hata watu kwenda dodoma. tatizo tukipenda chama, tunapenda na kauli za viongozi wa vyama hata kama ni za kijinga. unapopiga kura ya siri kumchagua mbunge, ni kwa sababu unachagua mmoja kati ya wagombea wengi. kwa raisi hivyohivyo. kwenye katiba humchagui mtu. unapigia vifungv vya rasimu ya katiba. vifungu hivi vikipita ndio sheria mama ya nchi. ni lini, na ni wapi sheria za nchi zikapitishwa kwa siri? labda ziwe sheria za kikandamizaji. kilichopo hapo, ni woga tu wa wajumbe kufukuzwa kwenye vyama. na kiongozi anayeogopa kufukuzwa kwenye chama hana sifa ya kuwa kiongozi. kwa sababu analinda maslahi yake ktk chama, sio maslahi ya wananchi. kura ziwe ya uso kwa uso.
Huu mdau ni uongo tena mchana kweupe! Mijadala ni ya wazi, upigaji kura za SIRI uwe wa WAZI kwa maana wakati anatumbukiza kikaratasi tumwone akiweka kwenye Kisanduku. Kura zihesabiwe kwa uwazi, na matokeo yatangazwe wote tukishuhudia, nani kapigia No au Yes jambo gani iwe SIRI yake ili kumlinda, huo Uwazi unaotajwa hapa leo una NIA OVU! Una lengo la kunyoosheana vidole baadae. Na kipengele ambacho kitawafanya watu wanyoosheane vidole ni Muundo wa Muungano. Leo katika Medani za Siasa Star Tv, nilimsikiliza mwalim Olouch akisema CCM wanataka serikali 2, ila akasema wakipita kwenye corridor, Wabunge wengi tena wengine akasema ni viongozi waandamizi wanataka serikali3, lakini wanadai kuwa hawana jinsi ikiwa wazi, basi wataunga mkono serikali2 kwa kulinda Maslahi yao! Akasema CUF,CHADEMA wao wanataka serikali3 lakini kuna wabunge wao pia wanapenda serikali2, lakini ikiwa wazi hawatathubutu kuunga mkono hoja ya serikali2. Akasema njia iliyobora na ni ya Kidemokrasia ni kura ya wazi