Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna aliyetumwa na Watu Kuwawakilisha!

Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna aliyetumwa na Watu Kuwawakilisha!

Mara nyingi nimesikia watu wakisema wabunge wa bunge hili ni watu wazima ,na rais kachagua wanasiasa wa zamani
na wasomi kwa misingi ya hekima zao na kama ni wabunge wa majimbo tayari waliishachaguliwa na wananchi wao
na wale wa makundi maalum wametumwa na makundi hayo kwa kuamini kwamba watawawakilisha vema
sasa huu woga wa kusema tunataka kura ya wazi ili tuone wanachokifanya unatoka wapi?
Hii inanipa maswali kama vile,wamewekwa kwa makusudi na hivyo aliyewaweka ana wasiwasi kwamba wanaweza mtosa endapo hawatafanya kwa wazi, hivyo anataka uwazi ili aweze kuwabana au hatuna uhakika na uwezo wao wa kimaamuzi maana wamezoeshwa kuendeshwa kama roboti.Vinginevyo tuamini kwamba watafanya maamuzi kama tulivyowaamini.
Kama hoja ni kuwaona wakituwakilisha,Kura ya wazi itawanufaisha waliomijini ni asilimia ndogo huku asilimia kubwa ya watanzania ipo vijijini ambako hakuna umeme na sehemu zenye umeme ni wachache wenye vingamzi kuona runinga
Hivyo dhana hii ya uwazi naona imewalenga wenye maslahi binafsi wanaoishi mijini ili kufanikisha malengo yao.
 
Nakubaliana na wewe kabisa kuwa huenda hakuna mjumbe aliyeuliza wapigakura ila ni lazima anajua watu wake wanataka nini na kama hajui basi atapiga kura kinyume na matakwa yao na kwa vile kura itakuwa wazi hapo ndio pa kumwajibisha,pia tofautisha kura ya kumchagua rais na na hii tunayoiongelea,kwani ile ya rais ni matakwa ya mpiga kura binafsi hii ya sasa ni matakwa ya waliokutuma hata kama wewe binafsi hukubaliani nao. Kuhusu wajumbe walioteuliwa na Rais hao ni wawakilishi wa makundi maalum na wanawakilisha misimamo ya makundi yao na sio wao binfsi.

Nataka kura ya siri ili Tanganyika irejee. Hakuna Tanzania bila Tanganyika na Zanzibar. Kura ya wazi ni kutaka kuzuia Tanganyika isiwepo ukizingatia wajumbe wa bunge la muungano hatukuwa tumewachagua ili kutuwakilisha katika bunge la katiba. Na hawakurudi kutuuliza badala yake wanaingia kwa msimamo wa vyama vyao. kwa maana vyama vyao vimewapa misimamo. Na sisi tusio na vyama au makundi nani anatusemea? Kwa hiyo msimamo ni KURA YA SIRI.
 
Labda hukunielewa nimesema wawakilishi rasmi wa vya walioteuliwa kuwakilisha vyama vya siasa,lazima wasimamie msimamo wa vyama vilivyowatuma hata kama wao binafsi hawataki, na wakikiuka sharti wawajibishwe bila huruma,maana kura sio zao binafsi ila ni za wale waliowatuma. Nikasema hata wabunge kura ni za wananchi wao si zao binfsi au vyama vyao.

hakuna chama kama chama kilichojisimamisha wenyewe msimamo lazima urudi kwa wananchi wanataka nini siyo kufuata chama., ww anzisha chama chako peke yako halafu utaenda kule bungeni utoe msimamo wa chama chako kilichokutuma
 
hakuna chama kama chama kilichojisimamisha wenyewe msimamo lazima urudi kwa wananchi wanataka nini siyo kufuata chama., ww anzisha chama chako peke yako halafu utaenda kule bungeni utoe msimamo wa chama chako kilichokutuma

Bado naona hunielewi,zipo nafasi rasmi za wawakilishi wa vyama vya siasa,hawa lazima wasimamie msimamo wa vyama vyao, na wabunge wasimamie hoja za wananchi wa majimbo yao kwa uwazi ili kila anayewakilishwa aone namna alivyowaskilishwa.
 
Wengi wetu hata huku tulipo hakuna umeme wala luninga. Na hata luninga ikiwepo nasikia TBC ni noma sana! Mnadhani tutawaonaje? Wanaosema tumewatuma kwa msimamo wa kura ya wazi ni waongo wanaotaka kupitisha hoja zao kwa hila. Twajua kuwa kura ya kidemokrasia ni ile ya siri!
 
Nimefuatilia sana malumbano yanayoendelea kwenye bunge maalum la Katiba kuhusu mambo mbalimbali,kama akidi,jinsi ya upigaji kura na mengine. Kwa leo nijadili kidogo tu kuhusu kura ya WAZI na SIRI.

Kwa namna yoyote ile kura ya WAZi ndio sahihi kutumika kwa sababu wajumbe ni wawakilishi wa watu wengine kwa hiyo hawapigi kura kwa dhamira zao binafsi ila kwa mujibu wa wale wanaowawakilisha. Kama mjumbe ametokana na jimbo la uchaguzi lazima apige kura kulingana na wananchi wake wanavyotaka hata kama yeye binafsi hapendi na lazima watu wake wajue kama mwakilishi wao amewawakilisha vilivyo na akienda kinyume na matakwa ya wananchi wake inabidi wananchi wamwajibishe moja kwa moja na wala sio chama chake.

Kwa wale wanaowakilisha vyama vya siasa ambao ni kama 42 hivi kila mmoja anatakiwa kupiga kura ya wazi kulingana na msimamo wa chama chake na akienda tofauti anastahili kuwajibishwa bila huruma kwani kura si ya kwake binafsi bali ni ya wale waliomtuma,kwa hiyo anawajibika kupigia kura msimamao wa waliomtuma hata kama yeye binafsi hakubaliani nao. Vivyo hivyo wabunge wa viti maalum wanawajibika kwa wanawake waliowapeleka huko na si vyama vyao, utaratibu ni huo huo kwa wale wa makundi maalum wanawajibika kupiga kura kwa matakwa ya waliowawakilisha na si kwa matakwa yao binafsi.

Watu wengi kwa sasa wanaogopa kura ya wazi kwa hofu kwamba watabanwa na misimamo ya vyama vyao,huu ni "uhuni" chama kinatakiwa kuwabana wawakilishi wao rasmi tu, ambao ni kama wawili watatu kwa kila chama wengineo wanabanwa na wale wanaowawakilisha,na kama mwakilishi rasmi wa chama akienda tofauti na msimamo wa chama huyo lazima awajibishwe ila sio mwanachama wa chama fulani anawakilisha wananchi wake hata wasio na vyama alazimike kufuata matakwa au msimamo wa chama chake.

Kwa mawazo hayo kama itapigwa kura ya siri wanachi watajuaje kama matakwa yao na si matakwa binafsi ya mwakilishi wao yamezingatiwa? Hebu tutafakari pamoja kwa nguvu ya hoja...
Kura ya wazi imewatia hofu wajumbe wengi kutokana na msimamo wa CCM kutaka wawakilishi wote ambao wanatokana na Wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano pamoja na Wajumbe wanaotokana na Baraza la Wawakilishi Zanzibar kupitia chama hicho ccm wapige kura kwa matakwa ya chama chao wala sio utashi wa wananchi wanaowawakiliaha. Tayari habari zinasema Wabunge 90 wa CCM wamekuwa BLACK LISTED na chama chao na wanaitwa mmoja mmoja kuhojiwa kutokana na msimamo wao wa wazi unaokinzana na matakwa ya chama. hayo ni mabavu ya ccm kujaribu kuwalazimisha wawakilishi wa wananchi. Kwa mtazamo huu, KURA YA SIRI NI MUHIMU.
 
Hivi kuna watu wenye matatizo ya akili humu JF?

Maana naona kuna watu wamekuwa wabobezi wa kuandika pumba tu.

Sasa mtu kama huyu mleta mada si anatia huruma tu?

Hemu tazameni jinsi alivyo andika kwanza, huko kwenye hoja ndio upuuzi mtupu.

Hivi ni nani kasema kura ya wazi itazuia chochote?
 
naunga mkono hoja. kura ya siri ndo mpango mzima. wasituletee za kuleta, ujanja ujanja kwenye mambo ya msingi haufai mbona kura zingine zote huwa ni za siri kwanini hizi za kupitisha ibara za rasimu ndo ziwe za wazi?. nyambafu.
 
Mchakoto huu toka mwanzo ni batili,sina sababu yeyote ya kukubali huu uchafu
 
Wanaoshikilia msimamo kura iwe ya wazi ni wabaya wa Taifa hili La Tanzania na hao wanafaa kupigwa vita ,popote pale penye hofu penye mavutano basi kura ya siri ndio suluhisho.

Kura ya siri huwezi kuonekana mbaya wala mzuri ,baada ya kutoka matokeo utakuwa uwamuzi ulio na busara kubwa wala hakutokuwa na kunyoosheana vidole wala kulipiza kisasi au kufukuzana ,na hata wale waliokuwa au pale panapoashiria watu kutishana ikiwa utapigia huku au kule ,kutakuwa hakupo ,hataweza mtu kumshuku au kumtuhumu mwengine zaidi ya kila mmoja kumtolea mijicho mwenziwe ,lakini hawezi kumwambia kitu kwani hapo ndio pale umdhania ndie kumbe sie.
 
Bado naona hunielewi,zipo nafasi rasmi za wawakilishi wa vyama vya siasa,hawa lazima wasimamie msimamo wa vyama vyao, na wabunge wasimamie hoja za wananchi wa majimbo yao kwa uwazi ili kila anayewakilishwa aone namna alivyowaskilishwa.

hakuna ulazima labda iwe msimamo wa chama ndio msimamo wa wananchi.,
 
Hivi kuna watu wenye matatizo ya akili humu JF?

Maana naona kuna watu wamekuwa wabobezi wa kuandika pumba tu.

Sasa mtu kama huyu mleta mada si anatia huruma tu?

Hemu tazameni jinsi alivyo andika kwanza, huko kwenye hoja ndio upuuzi mtupu.

Hivi ni nani kasema kura ya wazi itazuia chochote?

naona sindano inakuingia taribuuu
 
Semea nafsi yako sio wananchi wote wanataka kura ya siri mimi binafsi kura ya siri sioni kama ina mantik yoyote ktk kupitisha katiba hao wajumbe walioko bungeni kila mtu ana interest zake sio ccm tu hata cdm hao mnaowasikiliza hakuna anaetafuta katiba ya wananchi pale wote wanafiki tu! lakini kiuhalisia tukiacha na ushabiki wa kisiasa kura ya dhahiri ndio inayofaa kutoa maamuzi kuhusu katiba kwa sababu hii ni serious inshu kwa ajili ya wananchi wote na si kwa ajili ya watu fulani
 
kuna watu vichwa ngumu sana hivi nani hajui kama ccm wana wasi wasi kupiga kura ya siri kwa sababu kuna wana ccm wengi tu ambao hawakubaliani na msimamo wa chama chao? kura ya wazi ni kulazimisha maamzi.
 
Nani amewaroga ccm?ukiwaona kwa macho utazania ni watu.kumbe mioyo yao inakutu ya kutaka kuchonganisha.kama ccm mnatetea kura ya wazi,basi pendekezeni katiba mpya itamke tuwe tunapiga kura ya wazi kwenye uchaguzi mkuu.acheni ulimbukeni.tumewachoka.
 
Back
Top Bottom