Mimi sikubaliani na wewe kabisa !
Hili jambo la kura ya siri au wazi halipo kisheria. Kura ya siri au wazi zote zinakubalika kidemokrasia, kinachobaki ni busara tu ya kutumia aina gani ya kura kulingana na mazingira na kitu kinachoamuliwa. Tunategemea wajumbe watatumia busara ambazo tunaamini wanazo kujadiliana na kutoa maamuzi sahihi. Whether watapiga kura ya siri ya wazi cha muhimu ni maamuzi sahihi !. Ukiambiwa uchague maamuzi sahihi au uwazi (in case huwezi kuvipata vyote kwa pamoja) nadhani kama una busara utachagua maamuzi sahihi. Na kama baadhi ya wajumbe wanasema hawataweza kufanya maamuzi sahihi kama kura itakuwa ya wazi inabidi ku-wa-accomodate kwani tusipofanya hivyo definetely maamuzi yao yatakuwa sio sahihi wakati hayo haswa ndio tunayoyahitaji.
Vile vile mimi siikubali hii dhana iliyoenea kwamba hawa wabunge wameongea na wananchi wao na hapo walipo wamebeba mawazo ya wananchi wao ! Huo ni uongo wa mchana kweupe kabisa ! Hebu mkuu naomba unieleze mbunge mmoja tu....si zaidi ya hapo...MMOJA TU, ambaye alikutana na wananchi wake akakusanya maoni yao !. Hata kama itakuwa ni wachache lakini lazima kuwe na process ya hao wananchi kushiriki kwenye mjadala, hata kama watatofautiana hapa na pale lakini mwishoni wakakubaliana kwa hoja ambazo wakasema, hizi mbunge wetu nenda katusemee....HAKUNA hata mmoja aliyefanya hivyo ! Sana sana itakuwa ni watu wawili walio karibu naye wakiwemo family members, au marafiki zake au watu wawili watatu anaoweza kukutana nao..basi !. Kivipi maoni ya aina hiyo yanakuwa maoni ya wananchi wa jimbo lake ?
Tusidanganyane, hakuna mtu anayeweza kusema wananchi wangu wanataka kitu fulani na akawa sahihi.....hawa watu wamechaguliwa watumie judgement yao na uzoefu wao wa kutoka katika maeneo wanayoishi wananchi, lakini kusema wanawakilisha mawazo ya wananchi (kwa maana hiyo literally) ni kuongea kitu ambacho ni theory tu lakini kisicho na uhalisia ! After all hawa wabunge hawakuchaguliwa ili waandike katiba, walichaguliwa watunge sheria kwenye Bunge, ila wakajiconvert wenyewe wakawa wajumbe wa bunge la katiba !