Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna aliyetumwa na Watu Kuwawakilisha!

Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna aliyetumwa na Watu Kuwawakilisha!

yangu macho ila naona hapa kuna kamchezo kachafu.:nono: akili inagoma kukubali eti kula za wazi
 
kama RASIMU YA KATIBA IMEANDIKWA KWA MISINGI YA SERIKALI TATU,

UKISOMA KUANZIA A IBARA YA KWANZA INAANDIKWA KWA MTIRRRIKO WA MUUNDO WA SERIKALI TATU,

ISIPOKUWA IBARA CHACHE ZENYE MAMBO YA KIJUMNLA JUMLA

HAKUNA UWEZEKANO WA KUIPINGA HII RASIMU HATA IWEJE NA BADO BUNGE LIENDELEE KUWAPO SAS LITAJADILI NINI,

KUIKATAA RASIMU YA SERIKARI TATU ITAPELEKEA KULIVUNJA BUNGE AUTOMATICALLY
SIJUI KAMA CCM WANALIJUA HILI

HAKUNA MAHALA AMBAPO RASIMU IMEPENEDEKEZA SERLIKALI MBILI,

WAJUMBE WANAO TAKA SERIKALI MBILI WATAPIGAKURA KUPITISHA SERIKALI MBILI KUTOKANA NA RASIMU IPI?

AMBAYO MTIRIRIKO WA IBARA ZAKE UKOJE NA AMBAYO IMETOKANA NA TUME IPI NA INAWAKILISHA MAONI YA WANANCHI WEPI NA WANGAPI??

NATABIRI TUTARUDI KULE AMBAKO TULIKUKIBIA MWANZO KUTAFUTA MUAFAKA WA KITAIFA KWANZA JUU YA MUUNDO WA MUUNGANO, THEN NDO TUANDAE RASIMUYA KATIBA
 
Pasco, umenena vema. kuna wahuni wanaojenga hoja kupitia ujinga. Ati wamewakilisha wananchi,hivyo hawanabudi kupiga kwa wazi waonekane na waliowatuma. Hii kitu ipeleke magazetini.
 
Last edited by a moderator:
Nani asiyejua kuwa ukienda kinyume na matakwa ya chama unang'olewa meno na kucha? Naunga mkono hoja, kura iwe ya siri.
 
Mmbunge maana yake ni representative of the people na anachaguliwa na watu, sasa sijui iweje tena mtu anaamua kubadili maana wakati the whole purpose of representing is to hear as many demands of society as possible through their rep. Hiyo ndio sababu kuu ya uchaguzi kwa maana hiyo haki kwa wapiga kura kujua umechagua nini. Hili haki itendeke kwa wapiga kura kama unalilia kura ya siri walau wapiga kura wafahamu msimamo wako vinginevyo inakuwa ni maslahi binafsi na ulaghai unaweza waongopea baadae kama ukiulizwa na kujibu kwa kupima upepo.

Kwa maana hiyo siku zote mmbunge huwa anasimama kwa niaba ya watu na chama chake kwakuwa hakuna mgombea binafsi ambae anaweza dai yeye kachaguliwa kwa misimamo binafsi, hivyo basi kwa misingi hiyo kura ya wazi ndio njia pekee yenye misingi ya demokrasia.

Vilevile vyama vya siasa vina misingi yake na katiba zao ambazo ndio nguzo za chama, ilikukipa chama long term stability na wanachama wake. CCM ni zao la TANU na ASP vikitokea bara na visiwani hivyo unaweza ona nini misingi ya chama hicho na muungano wa serikali mbili kwanini unapewa priority kwa sababu za stability ya chama na muungano wenyewe wa kitaifa, wajumbe wanaoenda nyume na hapo maana yake wwanaenda vunja stability na nguzo za chama.

Ndio maana wanachama wapya kwenye vyama vya siasa huwa wana apishwa kwa maneno ya watatii na kufuata taratibu za chama na hivyo wanakuwa binded na taratibu za chama. Sasa kama mtu anafahamu nguzo za chama na misimamo yake alifuata nini huko kama azikubali, na kama alijua kwanini leo akatae kusimama na wenzake ndio maana kwa wazungu upuuzi huu hawataki. Well hata CDM sio ndio maana kuna watu walifukuzwa na wengine kutokea mahakamani kwa madai ya kukiuka kanuni za chama, leo taratibu hizi kwa wengine zionekane tofauti.

CCM ZnZ bado hipo imara kwa maoni yangu maana hawaoni aibu kuwataja wasaliti CCM bara ndio legelege angekuwa Nyerere angeshatoa adhabu wengi leo wenye kelele za kuuvunja muungano wamerudi baada ya viongozi waliofuata na kifo cha JKN vinginevyo tungekuwa tumeshawasahau na wabishi leo consquences would have been felt.

Kwa maana hao ndio watu watakao kuwa siku zote wanayumbisha chama cha magamba ndio maana kuna ulazima wa wajumbe kupiga kura za kichama kama wanaelewa nguzo za chama chao, uingereza swala kama hilo sio ombi ni amri kwa mwanachama mmbunge vinginevyo unafukuzwa chama live.

Huna uelewa.
 
Wanabodi,

Kile kitendawili cha chaguo kati ya kura ya siri au kura ya wazi, kitapatiwa ufumbuzi wiki hii, ambapo waheshimiwa wabunge wetu, wa Bunge Maalum la Katiba, watapiga kura kuamua kama kura ziwe za wazi au za siri.

Kikawaida uchaguzi wowote unaoitwa huru na wa haki, kura hupigwa kwa siri "secret ballot" ili kulinda uhuru na haki ya mpiga kura!.

Hata hivyo kuna wenye hoja ya msingi kuhusu kura ya wazi kwa kisingizio eti kwa sababu wao ni wawakilishi wa wananchi, wanadai wanapaswa kupiga kura ya wazi, ili wale wananchi waliowatuma, wawaone na kuujua msimamo wao, wazi wazi na wengine hadi kudiriki kudai kuwa wanataka wananchi wawashuhudie wakifanya kile wananchi hao walichowatuma!.

Ukweli wa mambo ni kuwa, hoja hiyo ni uongo mtu, uongo mtakatifu! unaotumiwa ili kuhalisha ubabe na kuburutwa na CCM na vibaraka wake, wakiwemo makuwadi wa siasa za ukandamizaji!. Ukiondoa wale wawakilishi 201 ambao ni wateule wa Rais, hao angalau wametumwa/jituma kuziwakilisha taasisi zao, au vikundi vyao, na sina uhakika kama wanachama wote wa taasisi hizo, auvikundi hivyo, walikaa pamoja na kuwatuma mkifika huko mfanye hili au lile zaidi ya kuwatuma wakatetee maslahi yao!. Kwa vile hivi ni vikundi tuu vya watu, hawa ni wawakilishi wa vikundi na sio wawakilishi wa watu!, yaani wananchi kwa sababu hakuna mwananchi aliyewachagua wala kuwatuma!.

Tukija kwa waheshimiwa wabunge wetu wa bunge la JMT na BLW, hawa kweli ni wawakilishi halali wa wananchi na tumewachagua kwa kura zetu, waende kutuwakilisha ndani ya mabaraza ya kutunga sheria Bunge na BLW, tulichowatuma ni kwenda kutuwakilisha bungeni!, na sio kwenda kutuandikia katiba!.

Hivyo hakuna mbunge yoyote au mwakilishi yoyote aliyetumwana na mwananchi yoyote kwenda kule kwenye Bunge Maalum la Katiba kumwakilisha!, ila uwakilishi huo ni by proxy ya kwa kwa vile tulimtuma kihalali kwenda kutunga sheria, na miongoni mwa sheria halali waliotunga, ni ile sheria ya mabadiliko ya katiba, na kwa sheria hiyo, wakajipendekeza wao ndio wajigeuze wawakilishi wetu kwenye Bunge Maalum, then wao kuwa ni wawakilishi wa wananchi ni saawa kisheria, ila hakuna mwananchi yoyote aliyewatuma!, hivyo wapige kura za siri, na sio kusingizia eti wananchi wamewatuma!.

Wabunge hao, hawana kitu kinachoitwa "people mandate", kwa sababu hakuna mwananchi aliyepata fursa ya kumchangua mwakilishi wake hata mmoja ndani ya bunge maalum, zaidi ya huo uwakilishi by proxy, hivyo kura halali ni kura za siri!. Period!.

Kufuatia Mapendekezo ya Tume ya Warioba kupendekeza serikali 3, na Chama cha Mapinduzi, kuweka wazi msimamo wake ni wa serikali mbili, zikipigwa kura za wazi, hakuna mwana CCM yoyote atakayethubutu kupigia kura serikali tatu, hivyo kwa kuhofia kwenda kinyume cha matakwa ya chama chake, hivyo kutopiga kura kwa uhuru na haki. bali kufuata matakwa ya chama chake.

Mahakama zinapotoa uamuzi wa haki, pia huwa zinazingatia madhara yasiyorekebishika "irreparable damegge!", vivyo hivyo katika kupiga kura za wazi, yule mwana CCM mwenye kupenda serikali tatu, atapata "irrepable damegge" kama atakwenda kinyume cha msimamo wa chama chake!. Matokeo yatakuwa ni kushinda kwa hoja ya serikali mbili, hivyo kuendelea na sherikali mbili kwa ushindi wa kitisho, hivyo kukosa haki japo uhalali!.

Lakini kama CCM kimewapika vizuri makada wake kuunga mkono hoja ya serikali mbili na wote wakaikubali ndani ya mioyo yao, hata zikipigwa kura za siri, hao makada wake wote watapigia kura serikali mbili, hivyo hoja ya serikali mbili itakuwa imepita kwa kura ya huru na ya haki, hivyo kuendelea na serikali mbili kwa haki na kihalali.

Waheshimiwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Please, Don't let us down!.

Mungu Ibariki Tanzania.

Mungu wabariki Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Kuona Kweli, Kutenda Haki, na Kufanya Kweli!.

Pasco.

Kura ya siri itatupatia katiba ya siri k
 
kama RASIMU YA KATIBA IMEANDIKWA KWA MISINGI YA SERIKALI TATU,

UKISOMA KUANZIA A IBARA YA KWANZA INAANDIKWA KWA MTIRRRIKO WA MUUNDO WA SERIKALI TATU,

ISIPOKUWA IBARA CHACHE ZENYE MAMBO YA KIJUMNLA JUMLA

HAKUNA UWEZEKANO WA KUIPINGA HII RASIMU HATA IWEJE NA BADO BUNGE LIENDELEE KUWAPO SAS LITAJADILI NINI,

KUIKATAA RASIMU YA SERIKARI TATU ITAPELEKEA KULIVUNJA BUNGE AUTOMATICALLY
SIJUI KAMA CCM WANALIJUA HILI

HAKUNA MAHALA AMBAPO RASIMU IMEPENEDEKEZA SERLIKALI MBILI,

WAJUMBE WANAO TAKA SERIKALI MBILI WATAPIGAKURA KUPITISHA SERIKALI MBILI KUTOKANA NA RASIMU IPI?

AMBAYO MTIRIRIKO WA IBARA ZAKE UKOJE NA AMBAYO IMETOKANA NA TUME IPI NA INAWAKILISHA MAONI YA WANANCHI WEPI NA WANGAPI??

NATABIRI TUTARUDI KULE AMBAKO TULIKUKIBIA MWANZO KUTAFUTA MUAFAKA WA KITAIFA KWANZA JUU YA MUUNDO WA MUUNGANO, THEN NDO TUANDAE RASIMUYA KATIBA


Mkuu,

Hili suala ni la muhimu sana sioni wadau wakiligusia...rasimu inatamka Serikali Tatu yaani Tanganyika imetakwa karibu kile ibara ya Rasimu...sasa wakianza na kukataa Serikali Tatu...bora kila mtu arudi makwao na huu mchakato wa Katibu ndio utakuwa umekufia hapo.
 
Hiyo kura ya kuamua iwe siri au wa.. itapigwa kwa njia gani,
 
CCM sasa ktk hoja wamezidiwa hasa ktk swala la kura ya wazi kufikia hatua baadhi ya makada wake kuanza kutoa vilio vya samaki ambavyo huenda havina machozi wanapoambiwa ukweli juu ya hoja na kura ya siri. Wamekosa hoja wametunga vioja lakini hoja za wanaharakati ambazo zinakwenda sambamba na matamko au makubaliano ya taifa letu dhidi ya makumbaliano mbalimbali ya umoja wa mataifa na jumuiya tofauti tofauti yakiwemo ya haki za binadam na yale yenye dhamira za haki za binadamu ya kupiga kura kwa njia ya siri. Ni utamaduni wa kawaida ambao hata wabunge raisi madiwani hata uchaguzi wa serikali wa mtaa ambapo huwa tunachagua kwa njia ya siri. Sasa mpira uko fainali jr kanali JK ametinga dodoma ambapo wataalam wanaona kama udhaifu wa kutoenda kwa kasi kwa mabadiliko haya yanatokana na udhaifu ya rais dhidi ya chama chake kwa hofu ambayo haitakiwi kuwepo kama dhamira yake ni kupata katiba mpya. Sasa tusubirie keshi kuona itakuwaje. CCM kukubali kipigo mapema au bado watalazimisha hadi bunge lifanyike wakati hawana hoja? Misingi yote ya demokraisa ipo wapi mwisho wa siku anayetoa maamuzi hatakiwi kujengewa hofu kidemkrasia sio SA wala USA wala Kenya wala Roma ktk mchakato wa kumtafuta papa na kwingineko ikiwepo china marafiki wakubwa wa ccm ambapo kura huwa siri wala kwingineko ambapo kura huwa ni za siri ili hata baada ya kura maisha yaendele kwa amani. Ambacho sijawahi kuona ni lini taifa kama tanzania likapita ktk mchakato huu mhim na majaribu mengine bila kumwaga damu. Historia haisemi hivyo lakini inawezekana maana ktk hili historia inaweza kuundwa tanzania ikawa huru zaidi ikiwa na katiba ya maendeleo bila kumwaga damu tatizo jtk hili ni rais JK hajui anachokitaka au anajua ila hajui afikieje malengo hayo. Kama tulijitawala bila kumwaga damu kwa nini tupate katiba mpya baada ya kumwaga damu? Jk hataki kumfuata JK mwenzie ktk hili la kura ya siri na kitu ambacho ndio pekee kinaweza kumpa sifa hata akiwa msoga walau tuweze kumfikiria ktk MO Ibrahim prizes ambayo amezuiliwa so far na vitu vingi ikiwemo uuzaji wa meno ya tembo na madawa ya kulevya kushamiripia matendo ovu ya mapolisi hasa dhidi ya wapinzani je hataki kujiosha? Kilichobaki ni rais kujaribu kukubali maoni ya warioba na awaeleze ni jinsi gani hayana madhara kwao na familia zai zaidi kuna manufaa mapana zaidi ya kitaifa yaani Tanzania. Nyerere amewahi kuwashauri mambo magumu zaid dhidi ya haya na yeye alikuwa muumini wa wachache waheshimiwe zaidi ktk mchakato wowote angalia ushauri alioutoa dhidi ya SA kwa Nelson mwenyewe pia kwa ccm dhidi ya mchakato wa vyama vya siasa mwaka 1992. Madiba foundations tunaungana na wapigania haki za raia nchini kuungana na wengineo nchini ili tanzania ipate katiba bila kumwaga damu kama ilivyotokea zanzibar na kenya
 
JK naye anaendeshwa hakuna kitu ndugu., si umeona waziri mkuu Pinda amepewa maneno na mtu kama Ole Sendeka kashindwa ata kufurukuta, CCM wote wanaishi kwa wogawoga tu, wanaogopana
 
Jitahidi kuweka paragraph mkuu,kuhusu machozi ya samaki au dhaifu subiri kesho!!!Rais ameenda kufungua bunge la katiba,hizo kanuni namna 37 na 38 zitasomwa tu.
 
Wanabodi,

Kile kitendawili cha chaguo kati ya kura ya siri au kura ya wazi, kitapatiwa ufumbuzi wiki hii, ambapo waheshimiwa wabunge wetu, wa Bunge Maalum la Katiba, watapiga kura kuamua kama kura ziwe za wazi au za siri.

Kikawaida uchaguzi wowote unaoitwa huru na wa haki, kura hupigwa kwa siri "secret ballot" ili kulinda uhuru na haki ya mpiga kura!.

Hata hivyo kuna wenye hoja ya msingi kuhusu kura ya wazi kwa kisingizio eti kwa sababu wao ni wawakilishi wa wananchi, wanadai wanapaswa kupiga kura ya wazi, ili wale wananchi waliowatuma, wawaone na kuujua msimamo wao, wazi wazi na wengine hadi kudiriki kudai kuwa wanataka wananchi wawashuhudie wakifanya kile wananchi hao walichowatuma!.

Ukweli wa mambo ni kuwa, hoja hiyo ni uongo mtu, uongo mtakatifu! unaotumiwa ili kuhalisha ubabe na kuburutwa na CCM na vibaraka wake, wakiwemo makuwadi wa siasa za ukandamizaji!. Ukiondoa wale wawakilishi 201 ambao ni wateule wa Rais, hao angalau wametumwa/jituma kuziwakilisha taasisi zao, au vikundi vyao, na sina uhakika kama wanachama wote wa taasisi hizo, auvikundi hivyo, walikaa pamoja na kuwatuma mkifika huko mfanye hili au lile zaidi ya kuwatuma wakatetee maslahi yao!. Kwa vile hivi ni vikundi tuu vya watu, hawa ni wawakilishi wa vikundi na sio wawakilishi wa watu!, yaani wananchi kwa sababu hakuna mwananchi aliyewachagua wala kuwatuma!.

Tukija kwa waheshimiwa wabunge wetu wa bunge la JMT na BLW, hawa kweli ni wawakilishi halali wa wananchi na tumewachagua kwa kura zetu, waende kutuwakilisha ndani ya mabaraza ya kutunga sheria Bunge na BLW, tulichowatuma ni kwenda kutuwakilisha bungeni!, na sio kwenda kutuandikia katiba!.

Hivyo hakuna mbunge yoyote au mwakilishi yoyote aliyetumwana na mwananchi yoyote kwenda kule kwenye Bunge Maalum la Katiba kumwakilisha!, ila uwakilishi huo ni by proxy ya kwa kwa vile tulimtuma kihalali kwenda kutunga sheria, na miongoni mwa sheria halali waliotunga, ni ile sheria ya mabadiliko ya katiba, na kwa sheria hiyo, wakajipendekeza wao ndio wajigeuze wawakilishi wetu kwenye Bunge Maalum, then wao kuwa ni wawakilishi wa wananchi ni saawa kisheria, ila hakuna mwananchi yoyote aliyewatuma!, hivyo wapige kura za siri, na sio kusingizia eti wananchi wamewatuma!.

Wabunge hao, hawana kitu kinachoitwa "people mandate", kwa sababu hakuna mwananchi aliyepata fursa ya kumchangua mwakilishi wake hata mmoja ndani ya bunge maalum, zaidi ya huo uwakilishi by proxy, hivyo kura halali ni kura za siri!. Period!.

Kufuatia Mapendekezo ya Tume ya Warioba kupendekeza serikali 3, na Chama cha Mapinduzi, kuweka wazi msimamo wake ni wa serikali mbili, zikipigwa kura za wazi, hakuna mwana CCM yoyote atakayethubutu kupigia kura serikali tatu, hivyo kwa kuhofia kwenda kinyume cha matakwa ya chama chake, hivyo kutopiga kura kwa uhuru na haki. bali kufuata matakwa ya chama chake.

Mahakama zinapotoa uamuzi wa haki, pia huwa zinazingatia madhara yasiyorekebishika "irreparable damegge!", vivyo hivyo katika kupiga kura za wazi, yule mwana CCM mwenye kupenda serikali tatu, atapata "irrepable damegge" kama atakwenda kinyume cha msimamo wa chama chake!. Matokeo yatakuwa ni kushinda kwa hoja ya serikali mbili, hivyo kuendelea na sherikali mbili kwa ushindi wa kitisho, hivyo kukosa haki japo uhalali!.

Lakini kama CCM kimewapika vizuri makada wake kuunga mkono hoja ya serikali mbili na wote wakaikubali ndani ya mioyo yao, hata zikipigwa kura za siri, hao makada wake wote watapigia kura serikali mbili, hivyo hoja ya serikali mbili itakuwa imepita kwa kura ya huru na ya haki, hivyo kuendelea na serikali mbili kwa haki na kihalali.

Waheshimiwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Please, Don't let us down!.

Mungu Ibariki Tanzania.

Mungu wabariki Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Kuona Kweli, Kutenda Haki, na Kufanya Kweli!.

Pasco.
kwa hiyo kama hawajatumwa wamekwenda dodoma kutafuna tu hela ya umma? na kwanini unataka kura ya siri kama hujawatuma. kwa taarifa yako, tumewatuma kwenda kujadili rasimu ya katiba. na ndio maana watanzania wamerizika kuwalipa lakitatu kwa siku. kama ingekuwa hakuna ulazima wa kuijadilii rasimu, wasingeenda dodoma kukaa siku 70.ingetosha tu rasimu ile ikawa katiba bila hata watu kwenda dodoma. tatizo tukipenda chama, tunapenda na kauli za viongozi wa vyama hata kama ni za kijinga. unapopiga kura ya siri kumchagua mbunge, ni kwa sababu unachagua mmoja kati ya wagombea wengi. kwa raisi hivyohivyo. kwenye katiba humchagui mtu. unapigia vifungv vya rasimu ya katiba. vifungu hivi vikipita ndio sheria mama ya nchi. ni lini, na ni wapi sheria za nchi zikapitishwa kwa siri? labda ziwe sheria za kikandamizaji. kilichopo hapo, ni woga tu wa wajumbe kufukuzwa kwenye vyama. na kiongozi anayeogopa kufukuzwa kwenye chama hana sifa ya kuwa kiongozi. kwa sababu analinda maslahi yake ktk chama, sio maslahi ya wananchi. kura ziwe ya uso kwa uso.
 
wananchi walio wengi walipendekeza serekali tatu. lakini haingii kabisa akilini kwamba waliopendekeza serekali tatu, ndio waliopendekeza muundo wa muungano. muundo wa muungano kwa namna nilivyouona kwenye rasimu ni muundo uliopendekewa na watu wa ndani ya serekari. na nilivyouona, ni dhahiri kabisa kwamba utakapoanza kufanyakazi ni sawasawa na kuwa na sesekali moja.
 
Nakumbuka hata primary tulichagua viongozi wetu kwa Kura za Siri
 
kwa hiyo kama hawajatumwa wamekwenda dodoma kutafuna tu hela ya umma? na kwanini unataka kura ya siri kama hujawatuma. kwa taarifa yako, tumewatuma kwenda kujadili rasimu ya katiba. na ndio maana watanzania wamerizika kuwalipa lakitatu kwa siku. kama ingekuwa hakuna ulazima wa kuijadilii rasimu, wasingeenda dodoma kukaa siku 70.ingetosha tu rasimu ile ikawa katiba bila hata watu kwenda dodoma. tatizo tukipenda chama, tunapenda na kauli za viongozi wa vyama hata kama ni za kijinga. unapopiga kura ya siri kumchagua mbunge, ni kwa sababu unachagua mmoja kati ya wagombea wengi. kwa raisi hivyohivyo. kwenye katiba humchagui mtu. unapigia vifungv vya rasimu ya katiba. vifungu hivi vikipita ndio sheria mama ya nchi. ni lini, na ni wapi sheria za nchi zikapitishwa kwa siri? labda ziwe sheria za kikandamizaji. kilichopo hapo, ni woga tu wa wajumbe kufukuzwa kwenye vyama. na kiongozi anayeogopa kufukuzwa kwenye chama hana sifa ya kuwa kiongozi. kwa sababu analinda maslahi yake ktk chama, sio maslahi ya wananchi. kura ziwe ya uso kwa uso.

Huu mdau ni uongo tena mchana kweupe! Mijadala ni ya wazi, upigaji kura za SIRI uwe wa WAZI kwa maana wakati anatumbukiza kikaratasi tumwone akiweka kwenye Kisanduku. Kura zihesabiwe kwa uwazi, na matokeo yatangazwe wote tukishuhudia, nani kapigia No au Yes jambo gani iwe SIRI yake ili kumlinda, huo Uwazi unaotajwa hapa leo una NIA OVU! Una lengo la kunyoosheana vidole baadae. Na kipengele ambacho kitawafanya watu wanyoosheane vidole ni Muundo wa Muungano. Leo katika Medani za Siasa Star Tv, nilimsikiliza mwalim Olouch akisema CCM wanataka serikali 2, ila akasema wakipita kwenye corridor, Wabunge wengi tena wengine akasema ni viongozi waandamizi wanataka serikali3, lakini wanadai kuwa hawana jinsi ikiwa wazi, basi wataunga mkono serikali2 kwa kulinda Maslahi yao! Akasema CUF,CHADEMA wao wanataka serikali3 lakini kuna wabunge wao pia wanapenda serikali2, lakini ikiwa wazi hawatathubutu kuunga mkono hoja ya serikali2. Akasema njia iliyobora na ni ya Kidemokrasia ni kura ya wazi
 
Huu mdau ni uongo tena mchana kweupe! Mijadala ni ya wazi, upigaji kura za SIRI uwe wa WAZI kwa maana wakati anatumbukiza kikaratasi tumwone akiweka kwenye Kisanduku. Kura zihesabiwe kwa uwazi, na matokeo yatangazwe wote tukishuhudia, nani kapigia No au Yes jambo gani iwe SIRI yake ili kumlinda, huo Uwazi unaotajwa hapa leo una NIA OVU! Una lengo la kunyoosheana vidole baadae. Na kipengele ambacho kitawafanya watu wanyoosheane vidole ni Muundo wa Muungano. Leo katika Medani za Siasa Star Tv, nilimsikiliza mwalim Olouch akisema CCM wanataka serikali 2, ila akasema wakipita kwenye corridor, Wabunge wengi tena wengine akasema ni viongozi waandamizi wanataka serikali3, lakini wanadai kuwa hawana jinsi ikiwa wazi, basi wataunga mkono serikali2 kwa kulinda Maslahi yao! Akasema CUF,CHADEMA wao wanataka serikali3 lakini kuna wabunge wao pia wanapenda serikali2, lakini ikiwa wazi hawatathubutu kuunga mkono hoja ya serikali2. Akasema njia iliyobora na ni ya Kidemokrasia ni kura ya wazi

Sorry, kasema ni kura ya SIR TU!
 
ccm hawana jinsi kura ya siri kura ya wazi ni dilly dalling tu.

ngoma bado mbichi, ngomanzito iliyoko mbele ni kwamba ccm wakikataa serikali tatu na rasimu yote itaondolewa maanake bunge litavunjwa,

nawaonea huruma ambao walishapigia hesabu posho ya siku 90 kwani watazikosa,

vile vile matatizo mengine makubwa yataanza baada ya kurudi kwenye katiba ya zamani,

hakika nchi inaweza kutikisika salama yetu ni ccm kukuballi na kuipitisha rasimu kama ilivyo
 
CCM-Samaki.jpg
 
Salama yetu ni kupaza sauti kuwaambia ccm waelewe hatupo kulinda matumbo ya wachache tunaangalia taifa kwa mapana marefu. JK inaonekana hana control hata na kisection cha ccm hili tatizo dogo maana amepata all briefing za warioba ana info zaidi lakini muoga sana yeye mwenyewe
 
Back
Top Bottom