Wito kwa Malinzi ajiuzulu

Viol

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2009
Posts
25,420
Reaction score
18,298
Hatuwezi kufungwa kila siku, mpaka timu za ajabu ajabu zinatufunga hata droo tunashindwa?

Malinzi ndo aliyemleta huyu kocha na kumtimua Kim kisa tu alikuwa ameletwa na Tenga, Uongozi wa Malinzi ndo wa hovyo kabisa.

Real Madrid walimfukuza kocha wao kwa kukosa ubingwa mwaka huu na wakati alishawahi kuchukua kombe. Mnaua soka la bongo heri ujiuzulu maana umeshindwa!
 
Mkuu toka lini ukaona mkuu wa shirikisho la mpira akajiuzuru kisa timu imefungwa?
Hapa wakulalamikiwa ni wachezaji , hata angekuwa Morinho hii timu kufungwa ingefungwa tu.
Wapeleke maombi FIFA wasipangiwe mechi yoyote ndani ya miaka miwili ili wajitazame kwanza
 
Nadhani issue si kujiuzuru anatakiwa aoneshe kuchukizwa na matokeo haya na achukue hatua Amfukuze huyu Kocha mara moja amrudishe Kim Poulsen haraka sana aichukue timu kujiandaa na mechi ya Nigeria na kwa Kim itakuwa kazi rahisi maana sehemu kubwa ya wachezaji wenye viwango vya kuchezea Taifa Stars kipindi hiki kawatengeneza yeye.
 
Malinzi amelala.. hyu kocha ni wa kutimua.
 
hakuna cha ajabu hapo, Tanzania ni mbumbumbu wa mambo yote kuanzia elimu, siasa, uchumi na michezo
 
ajiuzuru ili afe njaa
 
nyie si ndio mlimsifia sana wakati anachaguliwa, endeleeni kuugulia maumivu ya vipigo kila siku.

siku hizi sitaki hata kujua stars kacheza na nani sembuse matokeo yake.
 
Ule moto aliongia nao wa kumtimua Kim Poulsen kwa nini asiutumie kumtimua Nooij?
 
Kuna ulazima wa kuwa na timu ya taifa?
Ingefutwa kuliko aibu hizi
 
Hivi nani yuko na historia ya huyu kocha toka ameanza career yake nahisi itareflect kinachotokea sahv
 
Mi nimefurahi sana tulivyo pigwa na Mimi nasema tuendelee kupigwa tu!
 
mfumo wote wa soka ufumuliwe, tutabadilisha makocha hadi mourinho atakuja lakini tutafeli. Mfano kama jana tungeshinda au droo wote tungesahau kuwa mpira wetu ni mbovu kupita kiasi.

Malinzi apewe assignment ya kukaa na watu wake atuletee Roadmap ya soka tanzania. Hatutaki matokeo ya kimsisimko tunataka mfumo imara wa kisoka na endelevu.
 

Aonyeshe basi msimamo wake,yule kocha wa hovyo sana,na wachezaji pia wapo hovyo
 

Huu mfumo wa soka wa sasa haufai kabisa,wanapeleka siasa kwenye soka
 
Hawa wachezaji na kocha wao pamoja na malinzi hawana strategies za ushindi wapo pale kama kutega hela washindwe wasishindwe wanapata yao
 
soka la bongo kama siasa za chama chetu cha mishe mishe
 
Hivi nani yuko na historia ya huyu kocha toka ameanza career yake nahisi itareflect kinachotokea sahv

Huyu kocha sijui hata historia yake,nadhani itakuwa mbovu tu kufungwa kote kule na timu za ajabu unadhani ana historia kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…