Wito: Waliomrekodi na kusambaza video ya Mbunge mstaafu Prof Jay akiwa ICU wachukuliwe hatua

Prof Jay in mgonjwa wa umma

Bado walipa kodi tunalipia matibabu yake

Anaigharimu serikali, a public charge

Tuna haki ya kujua anaendeleje kwa kumwona
 
Prof Jay in mgonjwa wa umma

Bado walipa kodi tunalipia matibabu yake

Anaigharimu serikali, a public charge

Tuna haki ya kujua anaendeleje kwa kumwona
Wewe binafsi umelipia kiasi gani?

Haya, kama unaona unanyanyaswa kwa kufichwa habari za ugonjwa wake, nenda kashtaki. Maana umeandika kwa uchungu sana.

Rais wenu aliepita mpaka alikata roho mkiwa mnafichwa, sembuse Prof Jize? Kua public figure, haimaanishi kila kitu chake kiwekwe wazi. Hata public figures pia wako na personal life which is non of your business!
 
Hii video ilinipita sema watu wanyama sanaa
 
Wewe binafsi umelipia kiasi gani?

Milioni 10

Niliagiza gari likachajiwa ushuru milioni 10, zimeenda kumtibia Prof Jay

Prof Jay is a public charge, anaigharimu nchi!

Baada ya kuwa ashalipwa kiinua mgongo milioni 400 na mshahara wa mil 10 kila mwezi miaka mitano…

Tuna haki ya kujua details za hali yake
 
Kwanini useme "tuna haki"? kwani wewe ni taasisi?

By the way, mimi pia ni mlipa kodi ila sioni kama kulipa kodi kunanipa haki ya kujua personal life ya watu wengine. Professor J sio mnufaika pekee wa kodi zetu, kila mtanzania ananufaika na kodi kwa namna moja au nyingine.

Hongera kwa kununua gari mkuu!
 
Serikali haipaswi kuwa na upendeleo kwa raia.

Prof Jay hana shida kuzidi mamilioni ya Watanzania wanaokufa kwa kukosa laki tatu za kutibiwa.

Vi nchi vichanga vyenye viongozi type za Waziri wa Afya Ummy Mwalimu wasio na exposure, weledi wala upeo ndio yanatolea mambo kama haya.
 
Nakubaliana na wewe kwamba tunayo mifumo mibovu ya afya, haki na usawa. Kuna upendeleo, na pia sioni mantiki ya serikali kumlipia gharama za hospitali mbunge mstaafu ambae kwa mshahara aliokua anapata pamoja na pensheni, naamini anazimudu.

Lakini sikubaliani na wewe kuhusu kuvujisha mitandaoni video yake akiwa ICU anapigania maisha. Huko ni kuingilia privacy yake. By the way, yeye hakuiomba serikali imlipie, lawama ziende kwa wanasiasa walioona anafaa kulipiwa kati ya mamilioni ya watanzania wasiojiweza!
 
Na ndio maana situpendi hutu tumbau mbau hata kidogo.
 
Unaandika habari bila video, jamii forum hatupendag hyo mambo
 
Hakuna aliye salama mbele ya huyo Mangi.

Mkumbusheni na Mama.
 
Hakuna aliye salama mbele ya huyo Mangi.

Mkumbusheni na Mama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…