Wito: Watu Wenye Uwezo, Tujitokeze Tujitolee Kumsaidia TAL na Kuisaidia Chadema to Play Real Politics, No Reforms No Election ni Utopian Politics!.



Naona tuna zungushwa zunguswa tu Lissu hajapata jibu kutoka kwa yeyote
 
Naona tuna zungushwa zunguswa tu Lissu hajapata jibu kutoka kwa yeyote
Hakuna kitu kizuri kama ukweli, kuukubali ukweli jinsi ulivyo.

Ukiuliza swali, au ukitoa hoja, halafu hakuna anayekujibu, kuna mawili
1. Hoja yako ni ngumu na hawana majobu.
2. Hoja ni utopia, wana ku ignore!.
No reforms ni very valid hoja
No election, ni utopian politics.
3. Kama Chadema wangesema
No reforms, Chadema, no election, then this is valid, lakini no election it is as if Chadema ndio the determinant, kitu ambacho sio kweli ni utopia!.

P
 

P,
Imesha elezewa ni kwamba tu makada mnajitoa ufahamu makusudi. Hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi Lissu kashasema hakuna uchaguzi maana yake watatafuta kila njia kupinga chaguzi zifanyike ikiwa ni pamoja na migomo na kushinikiza. Je ni kitu gani kigumu kuelewa hapo. Kama Serikali ikilazimisha sawa lakini no election inaonyesha malengo yao kama seriakli wakilazimisha chaguzi sawa lakini ujumbe utakuwa clear. Raisi Samia kwa chaguzi ambazo hazitakuwa za haki na kuna migomo kama hiyo itaharibu historia yake hasa ukizingatia ndiyo uchaguzi wa kwanza wa yeye kupigiwa kura. Kama ameingia kwa njia hiyo hata sisi dispora wengi tutamtangaza kama Raisi ambaye ni mwizi wa kura sifa mbayo kwa sasa hana bado kwasababu aliingia kama makamu wa Raisi. Kwa hali ya sasa ni bora mara 100% hivyo kuliko kuingia chaguzi kwa sheria hizi na chaguzi za 2019,2020 na 2024. No reform no election
 
Wewe, TAL, Chadema na wote mnao amini no reform no election, endeleeni kuamini hivyo kwasababu hata utopian politics ni siasa, hoja ya bandiko hili ni TAL, Chadema na wapinzani wengine wote wanatakiwa kusaidiwa kuachana na siasa za kiharakati za utopia, na kufanya siasa za ukweli za pragmatic, pragmatisim, you fight for what is possible sio kuleta siasa hewa!.

TAL ni bwana mdogo wangu pale Ilboru, nitam reach out, nitamsaidia kwa kumshauri, uchaguzi wa 2025 TAL, ana fursa ya a Golden Chance, with the right people and the right strategies, TAL anakwenda kuwa Trump wetu, Kamala keshatangazwa!, haya makida makida ya nini?. Huu muda uliobakia kabla ya uchaguzi, sio muda wa kufanya political activisim, huu ni muda wa kufanya siasa za kimikakati, SMART politics zenye strategic objectives ambazo ni Smart, TAL anatusua kama nilivyosema hapa Japo Lowassa Alikuwa a Liability CCM, Akawa Asset Chadema. Lissu is a Very Bad Liability, but is The Only Asset Chadema Has Kuwangiza Ikulu!. Je... ? TAL asaidiwe kupunguza liabilities awe asset, hebu achaneni na hizi utopian zenu, be real

P
 
What????? Umerukwa na akili au? Mana Samia ni Kamala Harris?
Duh...!, inawezekana nikawa nimerukwa na akili mimi, ndio maana niliwahi kuandika humu, Kuwa kichaa sio mpaka kuokota makopo! Je, Tanzania tuna vichaa wengi kuliko tunavyojidhania? hivyo mimi nikawa ni kichaa, au inawezekana wewe ndio kichaa, umeparamia bandiko kubwa kuliko uwezo wako wa kufikiri, hivyo huujui mukhtadha wa ushabihiano wa uchaguzi wetu wa 2025 na ule ushindani wa Tirampu na Kamala, TAL ndio Tirampu wetu, Kamala wetu ameisha tangazwa!.

Kwa vile binadamu hatufanani, kwa faida yako na vichaa wengine kama wewe, pitia haya mabandiko yangu matatu, yakutoe hicho kichaa chako cha msimu!.
  1. Wengi wetu humu walifuatilia uchaguzi wa Marekani kupitia media, sisi wengine tulikwaa pipa tukaenda kuushuhudia na sio kuhadithiwa! Inawezekana Wamarekani ni wajinga ajabu? Wamemchagua mwanaume na kumtosa Mwanamke. 2025 Watanzania tuchague mwanamke kuonesha tuna akili zaidi yao?
  2. Je, Wajua? Wamarekani ni Wabaguzi wa Kichinichini. Wanaendekeza Mfumo Dume, Ubaguzi wa Jinsia, Racism na Kuwabagua Wahamiaji
  3. Kilichotokea Uchaguzi wa Marekani, kinaweza kutokea Uchaguzi 2025?. Tuyatumie matokeo yao kama shamba darasa la 2025 au wao ni wao, na sisi ni sisii?

P
 
Ni lini uliona hayo maridhiano yakitumika, wakati mzuri kuyaona ilikuwa ni kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, lakini tulishuhudia CCM wakiugeuza kuwa mtihani wa kusoma na kuandika wa darasa la nne! Tulishuhudia makundi ya wanafunzi yakiandikishwa kuwa wapiga kura! Pia tulishuhudia vijana wa Chadema wakikamatwa barabarani eti kwanini wanakwenda Mbeya! Hata hivyo waliachiwa bila kesi japo baadhi walipoteza mali zao.
Maridhiano aliyasema mwenyekiti wa CCM huku CCM na polisi wakiwa hawajaelimishwa maana yake! Hapo ndipo upuuzi ulipokuwa. TAL na Chadema hawajawahi kuwa sahihi kwako, hii ni kejeli dhidi ya TAL hasa unapotoa wito eti watu wenye uwezo toka CCM wamsaidie TAL! CCM hii iliyojaa magarasa na manyangarakasha! Acha hizo.
 
TAL na Chadema hawajawahi kuwa sahihi kwako, hii ni kejeli dhidi ya TAL hasa unapotoa wito eti watu wenye uwezo toka CCM wamsaidie TAL! CCM hii iliyojaa magarasa na manyangarakasha! Acha hizo.
Ukinisoma with pre coiceived bias kuwa mimi ni kada wa CCM, hutaiona the rationale kwenye ushauri wangu, ili ukijaaliwa uwezo wa kumsoma mtu in between the lines, nawasaidia sana Chadema kuliko hata chama changu!.
P
 
P,
Sijui kama utaelewa lakini hakuna siasa zozote zitasaida kama usalama wa taifa na Polisi wataendelea kuingilia uchaguzi. Kama wagombea wataendelea kutenguliwa bila sababu za msingi na kama wagombea watatangazwa hata kama hawajashinda. Unaweza kufanya siasa Tanzania lakini huwezi kufanya chaguzi kwa mazingira haya. Huwezi kwenda kwenye uchaguzi kwa mazingira haya ya chaguzi za 2019,2020, na 2024. Hivyo wote tunataka chaguzi huru basi Tume na taratibu za chaguzi huru zirekebishwe kwanza. Kama Watanzania hawatakuwa na imani na kura zao hapo ni tatizo. Kwenda kwenye chaguzi kwa mazingira haya ndiyo utopian wa kweli
 
Hakuna haja ta uchaguzi wowote Tanzania kwa sasa. Wale watakaoteuliwa kuwakilisha CCM, watangazwe rasmi kuwa ni washindi kuokoa kupotezeana muda, pesa na kufanya maigizo yasiyo na tija.

Lissu yupo sahihi, campaign yake inahitaji kuwafikia wengi na kujumuisha Watanzania wote ili iwe hata na nafasi ya kufanikiwa. Kusiwe na makundi ndani na nje ya chama.
 
Ukinisoma with pre coiceived bias kuwa mimi ni kada wa CCM, hutaiona the rationale kwenye ushauri wangu, ili ukijaaliwa uwezo wa kumsoma mtu in between the lines, nawasaidia sana Chadema kuliko hata chama changu!.
P
Naona umechukua sehemu ndogo isiyomuhimu umeacha la maridhiano na uharakati wa TAL, nimesema mwenyekiti wa CCM alileta maridhiano ambayo chama chake na polisi hawayaelewi, na hicho ndicho TAL alisema ni upuuzi na ndivyo ulivyokuwa na yameshindwa kutekelezwa si kwa Chadema tu bali kwa vyama vyote.
 
Vikao vya maridhiano vilikuwa vinakwenda vizuri, wakafikia makubaliano ya kugawana nusu mkate, kabla makubaliano kusainiwa, TAL akatua nchini kutoka Ubelgiji, akajoin the talk. Kwenye vikao vya ndani, hasemi resevations zake, bali anaitisha mikutano yake binafsi not coordinated na chama, na kuongea vitu kama hivi
View: https://youtu.be/Qa59DIQs2yINikawauliza Chadema
Msikie Tundu Lissu Hapa, Anauliza Kama Wenzake Wana Akili Kweli! Maridhiano Ayaita Ujinga. Je, Lissu Bado ni Asset or Sasa ni A Liability?

In such situation, mazungumzo yangeweza kuendelea?. Hivi ndivyo mazungumzo yalivyokufa, TAL bila kusaidiwa hawezi kubadilika!, Chadema will lose big time!.

Huu ni muda wa siasa za mikakati sio muda wa utopia!,
Naendelea kusisitiza wapinzani nchi hii, wasaidiwe, tujenge serious and credible opposition.
P
 
Hakuna haja ta uchaguzi wowote Tanzania kwa sasa. Wale watakaoteuliwa kuwakilisha CCM, watangazwe rasmi kuwa ni washindi kuokoa kupotezeana muda, pesa na kufanya maigizo yasiyo na tija.
Ushauri kama huu na mimi niliwahi kuutoa ile 2015 Kwa kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?, ila kwa uchaguzi wa mwaka huu nimewashauri Pre GE2025 - Kama Upinzani unataka mafaniko ya kweli 2025, Iachane na Urais, Ujikite Serikali za Mitaa, Ubunge na Udiwani, Urais labda 2030!
Lissu yupo sahihi, campaign yake inahitaji kuwafikia wengi na kujumuisha Watanzania wote ili iwe hata na nafasi ya kufanikiwa. Kusiwe na makundi ndani na nje ya chama.
Naheshimu mawazo yako.
P
 
Ili upate maridhiano kamili inabidi yasiwe ya watu wawili tu, ni lazima yahusishe vyama vyote na vyombo vya usalama.
Tunawezaje kufanya uchaguzi chini ya tume iliyosilimu! Tulienda kulala ikiwa NEC na tulipoamka tukakuta imebadili dini, eti INEC! Tanzania ni nchi ya viwango vya chini kwa kila kitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…