Wizara ya Afya chukueni ushauri huu kuhusu madakatari wenye maslahi binafsi

Wizara ya Afya chukueni ushauri huu kuhusu madakatari wenye maslahi binafsi

Ngarob

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
661
Reaction score
2,204
Wizara ya Afya / Waziri wa Afya tunawapa pongezi kwa jitihada mbalimbali mnazofanya lengo likiwa ni kuimarisha afya ya mtanzania.

Kuna changamoto kadhaa hasa kwa baadhi ya madaktari katika kutibu wagonjwa mbalimbali kutanguliza maslai binafsi katika hospitali za u make badala ya tiba sahihi kwa mgonjwa. Naomba niorodheshe baadhi.

I) Madaktari wengi hawakai kwa muda sahihi katika kuhudumia wagonjwa, wengi wao huondoka mapema kazini wakikimbilia hospitali binafsi kwa ajili ya manufaa yao

II) Baadhi ya madaktari wa Serikali wasio waaminifu huwaelekeza wagonjwa kwenda katika hospitali binafsi (private clinic) kwa ajili ya maslai binafsi, na baadhi yao huweka appointment huko katika hospitali binafsi.

III) Baadhi ya Madaktari wa Serikali wasio waaminifu huwaelekeza wagonjwa kwenda nje ya kituo kwa ajili ya vipimo (hata vidogo kama ultra sound) kwa ajili ya kujipatia fedha za ziada / Manufaa binafsi.

IV) Baadhi ya madaktari wa Serikali hujihakikishia wakitoka mapema kazini au baadhi yao hukwepa kabisa kwenda kazini kwa ajili ya private clinic.. Hujipatia kipato kikubwa 50,000 kwa siku au zaidi na baadhi yao huwa wanalipwa kwa mwezi 1,000,000 na fedha hizi hazina makato (TRA Hawajui).

V) Baadhi ya Madaktari wa Serikali wasio waaminifu hujaribu kuzuia ajira za madaktari wachanga waliotoka vyuoni wasiajiriwe katika hospitali binafsi kwakuwa wao hutoka mapema mno kazini (Serikalini) ili waje wafanye kazi private hospital.

Waziri / Wizara ya Afya natumaini baadhi ya malalamiko haya yatafanyiwa kazi. Baadhi ya Madaktari hawaridhiki na ajira zao, wanataka kuwa sehemu mbili mpaka tatu kwa wakati mmoja hali ambayo itapunguza ufanisi wa matibabu.
 
Aysee, mwisho wa siku tutakufa tutaacha kila kitu hapa
 
Chief ,huduma katika hospital za serikali bado ni Duni sana hakuna madawa hakuna vipimo na machine zilizopo either reagents hakuna au Mbovu.

Gharama za Matibabu serkalini ni Rahisi Kama huduma zitaboreshwa kwa kuwepo nguvu kazi ya kutosha, madawa ya kutosha, vipimo vya kutosha na wataalamu wa kutosha Hakuna mgonjwa ataacha huduma Bora aende huko private kwenye gharama kubwa.
 
Yaani daktari akilipwa 50,000 kwa Siku au milion 1 kwa mwezi inaonekana ni pesa nyingi, daah tubafilikeni jamani.

Kuna taasisi za kimataifa daktari analipwa milion 108 kwa mwaka, part time ni 98 milion.... na hapo wanamwomba.

Embu tuheshimu tasnia za watu jamani
 
Yaani daktari akilipwa 50,000 kwa Siku au milion 1 kwa mwezi inaonekana ni pesa nyingi, daah tubafilikeni jamani...
Kuna taasisi za kimataifa daktari analipwa milion 108 kwa mwaka, part time ni 98 milion.... na hapo wanamwomba.
Embu tuheshimu tasnia za watu jamani

Sent from my SM-J415F using JamiiForums mobile app
Jaribu kuelewa kiini cha ujumbe..

Ufanisi wa kazi unakuwa mdogo kutokana na kutokukukaa sehemu moja.. na hii inaathiri matibabu kwa wagonjwa, na kuzuia ajira za madaktari wapya.. we mtu unafanya kazi hospitali tatu.. ufanisi lazima upungue tu, na unazuia wengine kuajiriwa
 
Nia ya serikali, ni watu wake wote wawe na afya njema na si kuongeza kipato kupitia magonjwa. Kuna tatizo gani mgonjwa akitibiwa popote na akawa na afya?
 
Nia ya serikali, ni watu wake wote wawe na afya njema na si kuongeza kipato kupitia magonjwa. Kuna tatizo gani mgonjwa akitibiwa popote na akawana afya?
Popote sawa... Mgonjwa aende mwenyewe...... Sio kupelekwa na daktari kisa anayo percent huko
 
Huyu atakua mfamasia, nimecheka sana.

Haya DOCTORS njooni mjibu tuhuma KWa kupangua hoja sio matusi, MFAMASIA KACHEFUKWA HUKU
 
Nyie si ndo mnasema kuajiriwa ni kazi bure,, hata akiajiriwa basi haina maana kwao[emoji1787][emoji1787]
wanafunzi hawapo competent kwenye field zao, wanafanya kazi kwa personal gain hawana altruism kabisaaa yani ni zero.

As long serikali inawalipa basi hawana time na kuwa best in what they do, hata kwa hicho basic wanachokijua wako shallow kinyama[emoji23][emoji23] vuteni popcorn tucheki hii movie,, mambo mazuri yanakuja.

Mika 30 ijayo kupata the best in any profession kutakuwa ni kutafuta kwa tochi
 
Acha ushamba, elfu 50, nayo inakutoa roho
KWa fani zao zilivyo iyo anaweza kuwa anaipata just for consultation kwenye sim hata akiwa katika kituo chake Cha kazi, Kuna wengine ndio wakazin na wanatimiza majukum yao ila ni family doctors KWa familia 5 n.k na KILA family inamlipa, sio shida maana wanapatiwa matibabu katika utaratibu unaolinda afya zao,
Nimecheka sana leo na uzi huu
 
Nyie si ndo mnasema kuajiriwa ni kazi bure,, hata akiajiriwa basi haina maana kwao[emoji1787][emoji1787]
wanafunzi hawapo competent kwenye field zao, wanafanya kazi kwa personal gain hawana altruism kabisaaa yani ni zero,
As long serikali inawalipa basi hawana time na kuwa best in what they do, hata kwa hicho basic wanachokijua wako shallow kinyama[emoji23][emoji23] vuteni popcorn tucheki hii movie,, mambo mazuri yanakuja

Mika 30 ijayo kupata the best in any profession kutakuwa ni kutafuta kwa tochi
Hii nayo naikataa , sio kweli wapo wazuri Sana , wazuri na kiasi, maana hata hivyo binadam wote ni sawa ila sio sawasawa
 
Sawa Sawa
Sasa Namuita Waziri Wa Afya Kwa Hatua Baada Ya Kupitia Michango Yote


CC: Ummy Waziri Wa Afya
 
Popote sawa... Mgonjwa aende mwenyewe...... Sio kupelekwa na daktari kisa anayo percent huko
Siri yangu Mie ya ungonjwa ,analijua doctor anaenitibu, Sasa akinielekeza ambapo nitapata huduma tokana na tatizo langu nitakataa vipi, yani niambiwe nenda Mloganzila Mimi niende sijui wapi ninapopataka !!?
 
Walipeni sitting allowances, millage na mishaha ra mapurupu kama ya Waheshimiwa Wabunge muone kama watajitaabisha na kuitesa hiyo miili na akili zao kwenda kwenye hizo part time jobs.
 
Sasa hapa unataka Madaktari wakujibu nini ndugu yangu maana unalalamika tuu, unashindwa kuelewa kua daktari hasa wale mabingwa kuna Intetnal Standards ambazo haziwabani kukaa kwenye vituo vyao ya kazi muda wote na ndio maana kuna calls.

Daktari siyo nesi anayetakiwa kukaa na mgonjwa kutwa nzima. Akishawaona wagonjwa wake anaweza kwenda kuwaona wengine.

Kwakua ninyi huenda ni watoto sana hamjui mambo, serikali ilishawahi kusema huko nyuma kupitia kupitia kwa waziri wa Afya wa wakati huo Hussein Mwinyi na Mwaka 1995 enzi za mzee Mkapa kua haiwabani madaktari kutofanya kazi kwenye hospitali binafsi.

Sasa kama wewe ni Mfamasia cheti chako kinaa duka la Famasi unataka usikae humo na sheria inakutana hivyo hiyo ni juu yako wewe usijifananishe na daktari 😃😊.

Kumbuka wewe unasoma miaka 4 mwenzako miaka 5, kuna tofauti hapo.
 
Back
Top Bottom