#COVID19 Wizara ya Afya: Hadi Agosti 7, 2021, watu 105,745 walikuwa wamepatiwa chanjo ya UVIKO-19

#COVID19 Wizara ya Afya: Hadi Agosti 7, 2021, watu 105,745 walikuwa wamepatiwa chanjo ya UVIKO-19

Unawaza nini mzee? Mbona vitu ni rahisi pia.

Ni factors zipi unatumia?

Changamoto kubwa ni utayari wa watu kuchanjwa na uwepo wa chanjo.

Miundombinu haina shida. Hata wiki tu tunaweza chanja 30m+.
You can't be serious aisee.

Miundombinu gani uliyonayo ya kuchanja 30m kwa wiki moja hata kama wote watakua tayari hapa Tanzania?

Nimekupa mfano wa nchi kama South Afrika ambayo zaidi ya 80% wananchi wake wako tayari kwa chanjo lakini kwa miezi 7 wamechanja 3.5% ya population.

South kwenyewe ambapo kuna miundombinu bora zaidi ya Tanzania haiwezi kuchanja 30m kwa wiki moja sembuse Tanzania?

Naona labda huelewi, ngoja nikusaudie zaidi. Marekani aliacha chanjo mwezi December 2020, watu zaidi ya 200m walikua tayari na radhi kuchanjwa lakini ametumia miezi 8 kuchanja 150m, kwa wastani wa 18m people per month.

Tanzania hiyo miundombinu ya kuchanja watu 30m kwa wiki hata kama wako tayari kiasi gani inapatikana wapi?
 
Nasikia wengine tayari washaanza na Booster....

Muhimu ni let us all respect individual decisions - kuchanja au kutochanja. Maana mwisho wa siku bado kuvaa barakoa, kunawa mikono na tahadhari nyingine lazima ziendelee.
 
Wizara ya afya pia iweke wazi expiry date ya consignment ya chanjo.... ni maoni tu.

IMG-20210820-WA0000.jpg
 
Uandishi gani huu umejaa bold nyingi hivyo?

Siku 11, wamechanja watu 105,000, maana yake kwa siku wanachanja watu 9,535. Kwa mikoa 26 maana yake kila mkoa kwa siku unachanja watu 367. Hilo la kwanza.

La pili, kama kwa siku wanachanja wastani wa watu 9,535, iwao watanzania 50% watatakiwa kuchanjwa, yaani watu milioni 30 itahitajika siku 3,146 ama miaka 9 kuwachanja wote. Hilo halitoshi bado birth rate ni kubwa sana Tanzania maana yake hii chanjo haitaisha, itakua ni kuchanja for life.

Tukumbuke kabla ya kumaliza hata 1% ya watanzania, yaani 600,000 imeanza chanjo nyingine inaitwa booster shot ya kuipa nguvu hii chanjo iliyopo. Kwa maana kwamba kamaumechanjwa, utahitaji kuchanjwa tena hiyo booster vaccine.

Kwaa hiyo iwapo tutahitai kumaliza hizi zilizopo halafu tuanze booster ama tunaenda nazo concurrently itakua shughuli pevu.

Mimi nitakua wa mwisho kuchanja.
Chuo kikuu nilifundishwa kitu kinaitwa MATHEMATICAL REASONING.
 
Back
Top Bottom