Wizara ya Afya: Hakuna tishio la UVIKO-19, likiwepo tutatoa taarifa

Naunga mkono Tamko LA Serikali Kuwa Hakuna tishio la Corona.

Walitoa waraka wakati mwingine wanapokea maagizo kutoka nje
 
Sasa kama hatuna maambukizi ya COVID-19, mbona tahadhari iliyopo kwa sasa ni ndogo sana?

Ni kama vile tunalala milango wazi, tukiamini hakuna wezi wala wadudu pori wataovamia ndani ya nyumba yetu...
 
Kanimaliza kusema tuache wanasayansi wafanye kazi yao. Sijui ana maanisha wana sayansi hawa wa kwetu au wale original? Nchi hii kazi tunayo ngoja niandike kwa herufu kubwa. HATUTAKI LOCKDOWN TUNATAKA KUAMBIWA UKWELI ILI TAHADHARI ZIWE KWA WATU WOTE BILA KUCHAGUWA WEWE UNAAMINI NINI, TO DEAL NA FACTS SIO MAONO YA MTU KAMA TUNABISHANA SIMBA NA YANGA.
 
Hizo taarifa rasmi za serikali azisubiri yeye sisi tunachukua tahadhari zote za kujikinga na korona.
Hivi anafikiri hawa maaskofu hawasimamii mahospitali tena za maana kuliko hizo za serikali na kwamba wanajua in and out ya kile kinachoendelea huko mahospitalini kwa sasa?
 

Magufuli kajubali korona ipo basi na ccm watakubali kweli corona ipo , ivi kweli mtu mmoja anasemea anawaendesha hivi ???
 
Msameheni molleli wa watu bure, asingeweza kusema zaidi ya hicho alichosema kwani uwezo wake wa kusema ulikua unaishia hapo, mlitaka aende zaidi ya hapo afanyiwe ya ndugu yake ndugulile? Raisi Magufuli aliwahi kusema "Watanzania sio wajinga" nafikiri hata sasa kauli hii inatufaa sana mintarafu uviko-19 toleo jipya.
 
Ukiingia kwenye siasa unajifunza kuwa laghai hata kama wewe ni mwanasayansi inaikataa sayansi! Mbaya unawafanya watu wote ni wajinga na kwamba wewe tu ndiyo mwerevu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…