Wizara ya Afya, mnawaachiaje watu wenye dalili ya Corona waendelee na shughuli zao?

Wizara ya Afya, mnawaachiaje watu wenye dalili ya Corona waendelee na shughuli zao?

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
IMG-20200314-WA0040.jpg


Leo hii hata ukienda Uchina nchi ambayo mlipuko ulianzia, lazima wakuweke karantini siku kumi na nne haijalishi umepimwa umekutwa na virusi vya corona au hukukutwa navyo.

Kitu kingine wataalamu wanasema Mtu mwenye Corona anaweza kuonyesha dalili za Corona Corona lakini ukampima mara kadhaa usione kama ana kirusi lakini vipimo vya baadae ndo huonyesha ana kirusi.

Cha ajabu nimesoma taarifa za wizara ya afya juu ya washukiwa wa kuugua Corona kutoka nchi fulani za Ulaya, Wizara inasema eti pamoja na hao watu kuonyesha dalili za mafua huku mmoja na mwongine akionekana kulegea isivyokawaida wamewapima na kuwakuta negative KISHA WAKAWAACHIA WAENDELEE NA SHUGHULI ZAO.

Naishangaa sana wizara kuwaachia hao watu kipindi hiki badala ya Kuwashuku na kuwaweka kwenye Karantini huku wakiendelea kumonita maendeleo ya afya zao.

Hivi Waziri Ummy Mwalimu anavyoona mpaka Trump anafunga mipaka na kuzuia wazungu wenzie kutoka ulaya wasiingie marekani anaona hii ni hali ya mchezomchezo?

Wizara ya afya na serikali wanatuangusha sana jinsi wanavyochukulia hili jambo bila userious sana.

Iwapo hili janga litaibuka nchini, wananchi wakaanza kufa, hawa viongozi wa serikali wanaocheza na maisha yetu watawajibika kwa hakika, wananchi hatutokubali hata kidogo incompentency ya aina hii kuweka rehani maisha yetu, kwa hakika watawajibika.

Serikali haiko serious kabisa na hili janga!

Missile of the nation(Kombora hatari kabisa la ulinzi wa Taifa)
 
Jmn si wamewafanyia uchunguzi wakagundulika hawana. Tatizo liko wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app

Corona unaweza kumpima mtu usiione kwenye vipimo mpaka umpime tena wakati mwingine.

Hao hawakupaswa waachwe wandelee na shughuli zao, hao walipaswa wawe monitored closely huku wakiwa wamewekwa kwenye karantini maalum.

Kitendo cha kuwaachia waingie mtaani wanaweza kusambaza virusi kama wanavyo
 
Ujue hii nchi inaendeshwa Kiswahili swahili sana! Nchi za wenzetu mwenye kuonyesha dalili anakuwa in isolation angalau kwa siku 14. Huku kwetu eti vipimo vimepelekwa Dar leo kesho mtu anaruhusiwa kwenda na mambo yake.

Hivi huyu waziri wa afya taaluma yake ni mambo ya afya au? Maana unaweza kukuta ni fundi mchundo alafu anapewa wizara nyeti namna hiyo.
 
Ujue hii nchi inaendeshwa Kiswahili swahili sana! Nchi za wenzetu mwenye kuonyesha dalili anakuwa in isolation angalau kwa siku 14. Huku kwetu eti vipimo vimepelekwa Dar leo kesho mtu anaruhusiwa kwenda na mambo yake.

Hivi huyu waziri wa afya taaluma yake ni mambo ya afya au? Maana unaweza kukuta ni fundi mchundo alafu anapewa wizara nyeti namna hiyo.

Hawa viongozi wa wizara ya Afya ambao ni madaktari, elimu yao ichunguzwe, hivi kweli walipitia medical school au?
 
Ni ajabu sana.

Kiufupi kila mgeni kutoka China, Ulaya, Iran na nchi zote zilizopigwa sana walitakiwa wawekwe karantini siku 14 bila kujali umempima umemkuta nao au la.
 
Back
Top Bottom