Wizara ya Afya, mnawaachiaje watu wenye dalili ya Corona waendelee na shughuli zao?

Wizara ya Afya, mnawaachiaje watu wenye dalili ya Corona waendelee na shughuli zao?

Tatizo linguine nchi nzima vipimo vinafnyikia national lab, hili ni tatizo, sababu mgonjwa yeyote mwenye. Ugonjwa wa mlipuko hutakiwi kurefer, so unakaa nae pale ukisubiri majibu toka national lab kulikojaa siasa unagegemea watakuletea positive result kweli,, CCM hivi ndio mmeamua kutumaliza

Sent using Jamii Forums mobile app
Wee tulia watu wafanye kazi zao , usiwafundishe kazi kama kufa utakufa tu kelele za nini.
Wewe huko kazini kwako nani anakuingiliaga maamuzi???
 
Tume survive Ebola, Nzige....nina imani hata hili litapita.
Mtanzania ukigundulika na huo ugonjwa walai madaktari wanakuzika ukiwa hai useendelee kuueneza
View attachment 1388084

Leo hii hata ukienda Uchina nchi ambayo mlipuko ulianzia, lazima wakuweke karantini siku kumi na nne haijalishi umepimwa umekutwa na virusi vya corona au hukukutwa navyo.

Kitu kingine wataalamu wanasema Mtu mwenye Corona anaweza kuonyesha dalili za Corona Corona lakini ukampima mara kadhaa usione kama ana kirusi lakini vipimo vya baadae ndo huonyesha ana kirusi.

Cha ajabu nimesoma taarifa za wizara ya afya juu ya washukiwa wa kuugua Corona kutoka nchi fulani za Ulaya, Wizara inasema eti pamoja na hao watu kuonyesha dalili za mafua huku mmoja na mwongine akionekana kulegea isivyokawaida wamewapima na kuwakuta negative KISHA WAKAWAACHIA WAENDELEE NA SHUGHULI ZAO.

Naishangaa sana wizara kuwaachia hao watu kipindi hiki badala ya Kuwashuku na kuwaweka kwenye Karantini huku wakiendelea kumonita maendeleo ya afya zao.

Hivi Waziri Ummy Mwalimu anavyoona mpaka Trump anafunga mipaka na kuzuia wazungu wenzie kutoka ulaya wasiingie marekani anaona hii ni hali ya mchezomchezo?

Wizara ya afya na serikali wanatuangusha sana jinsi wanavyochukulia hili jambo bila userious sana.

Iwapo hili janga litaibuka nchini, wananchi wakaanza kufa, hawa viongozi wa serikali wanaocheza na maisha yetu watawajibika kwa hakika, wananchi hatutokubali hata kidogo incompentency ya aina hii kuweka rehani maisha yetu, kwa hakika watawajibika.

Serikali haiko serious kabisa na hili janga!

Missile of the nation(Kombora hatari kabisa la ulinzi wa Taifa)
 

Attachments

  • Abstract.PNG
    Abstract.PNG
    35 KB · Views: 1
Missile of the Nation,
aliyekuambia jitihada za wizara ya afya ndio vinaifanya tanzania kuwa salama pasi na milipuko ya magonjwa kama ebola na corona ni nani vile! Mungu asipoulinda mji walinzi hukesha bure! Tz tupo salama kwa kuwa Mungu ndie atulindaye! Siyo huyu waziri Ummy na jamaa zake!
 
ilipaswa Ummy (wizara) ifanye juhudi za makusudi kudhibiti hao wageni (quarantine)


badala yake anafanya juhudi za makusudi kuwaruhusu na kuwaacha waende na wakazagae huko mtaani..


''...ee Mola tuokoe na hiki kiama" hard blasters

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ujue hii nchi inaendeshwa Kiswahili swahili sana! Nchi za wenzetu mwenye kuonyesha dalili anakuwa in isolation angalau kwa siku 14. Huku kwetu eti vipimo vimepelekwa Dar leo kesho mtu anaruhusiwa kwenda na mambo yake.

Hivi huyu waziri wa afya taaluma yake ni mambo ya afya au? Maana unaweza kukuta ni fundi mchundo alafu anapewa wizara nyeti namna hiyo.
Ummy Mwalimu amepiga sheria pale UDSM akafanya masters ya sheria kule Pretoria South Africa.Naibu waziri Dr.Faustine Ndungulie yeye ndio Medical Doctor(MD) na MPH,waziri hatoi maamuzi peke yake anajadiliana na makamu wake.

Kuwa waziri hakuitaji huwe mtaaram wa sekta uliyopewa,japo sijawahi kuwa waziri ila natamani sana hicho cheo .
 
Ni heri ithibitike kuwa ipo ili watu waanze kutumia akili. Rais mzima anasema hata usiku msipigane mabusu na patakuwa na raha tu halafu anasema eti tunapambana na corona? Naona sasa wana show zao za kusalimiana kwa miguu!
kama hukumuelewa rais usikurupuke kumbeza!
 
Ummy Mwalimu amepiga sheria pale UDSM akafanya masters ya sheria kule Pretoria South Africa.Naibu waziri Dr.Faustine Ndungulie yeye ndio Medical Doctor(MD) na MPH,waziri hatoi maamuzi peke yake anajadiliana na makamu wake.

Kuwa waziri hakuitaji huwe mtaaram wa sekta uliyopewa,japo sijawahi kuwa waziri ila natamani sana hicho cheo .
Basi washauri wa huyo waziri hawako makini. Au na yeye hashauriki kama mzee baba?
 
Missile of the Nation, Serikali yetu ni dhaifu sana katika mambo mengi. Yawezekana hawana weledi, lakini kinashangaza ni kuwa wanakosa hata ile intelligent reasoning.

Wanakosa ubunifu lakini wanashindwa hata kutazamia na kucopy. Inashangaza sana!!
 
Basi washauri wa huyo waziri hawako makini. Au na yeye hashauriki kama mzee baba?
Makamu ndio anamshauri waziri na ndiye mtaaramu kwenye hiyo sekta,yeye ndio kasomea udktari wa binadamu na afya ya jamii sasa unasemaje kwamba hamshauri vizuri au unakitaka cheo cha unaibu huwe mshauri wa waziri???
 
huyu bi dada wanam-0713!
Ila uzuri mmoja huu ugonjwa hauchagui, uwe tajiri;/masikini, msafi/mchafu, waziri/layman etc!

So waendelee kufanya mzaha na afya za watanzania, na kama hayo ndo maelekezo alopewa ayaropoke.
Uingie tu nchini, pengine utatusaidia kupunguza wafuasi wa mbogamboga za kijani maana wamezidi kumsifu "MASIHA",

Pengine pia unaweza ukapenya pale nyumba kubwa na masiha akaupata angalau turelax, tushachoka
 
Makamu ndio anamshauri waziri na ndiye mtaaramu kwenye hiyo sekta,yeye ndio kasomea udktari wa binadamu na afya ya jamii sasa unasemaje kwamba hamshauri vizuri au unakitaka cheo cha unaibu huwe mshauri wa waziri???
Soma mada ya mleta uzi kisha soma comment yangu.
 
Jmn si wamewafanyia uchunguzi wakagundulika hawana. Tatizo liko wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Fuatilia uelewe huo ugonjwa.

Vipimo pekee havitoshi kuthibitisha kuwa mtu hana corona. Vipimo, dalili, historia yake - vyote kwa pamoja vinasaidia kumwelewa aliyeambukizwa.

Huko ulikoanzia, wanasema kuwa kuna wagonjwa wa corona ambao vipimo vinaonesha negative, lakini wanao. Taarifa za karibuni kabisa zinasema kuwa wamegundua hata wagonjwa waliotibiwa, ikaaminika wamepona, wakaruhusiwa, lakini baadhi bado wameinekana wana uwezo wa kuambukiza.

Mengi hayajafamika kuhusu huu ugonjwa. Mapya yanazidi kugundulika.
 
Back
Top Bottom