Wizara ya Afya na TAMISEMI mbona mko kimya sana?

Wizara ya Afya na TAMISEMI mbona mko kimya sana?

Redpanther

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2019
Posts
2,823
Reaction score
3,816
Habari gani ndugu wanajamvi la Habari mchanganyiko.

Ngoja niende moja kwa moja kwenye Maada. Mnamo aprili 16 2022 kulitangazwa nafasi za Kazi upande wa Afya na Elimu/Ualimu.

Ni miezi sasa imepita toka dirisha la kutuma maombi lifungwe. Huenda mimi ni mgeni au sina uzoefu sana kwenye haya mambo. Naona kama wamechelewa sana kutoa hayo majina ya waliopata hizo ajira.

Leo tarehe 14/9/22 Bajeti ya Wizara ya Fedha imesomwa kama ilikuwa kusubiri kuanza kwa mwaka wa Fedha mwingine tayari bajeti imeshatoka toeni hayo majina. Majina kutoka itasaidia kuweza kujua watu kama anaendelea kupambana na Kodi ya Kichwa pendekezwa au Atakatwa PAYE.

NB: Mimi pia niliomba nataka niione maisha ya Kuajiriwa maana hii Battle na TRA kwenye Biashara daah 😅. Btw, Mimi ni Mtanzania sio ubaya kuchangia maendeleo ya Nchi yangu.

14565969-E659-40E3-B0B6-42B9469D866A.jpeg

Nawasilisha 🙏🏾🙏🏾
 
Back
Top Bottom