Wizara ya Afya yapiga marufuku watu kuzikwa usiku, yaagiza ndugu washirikishwe

Nitoke nje ya mada.

Hatuwezi kuongozwa na wanasiasa kwenye hiki kipindi kigumu kisha tutarajie kuushinda huu ugonjwa.

Ingekuwepo kamati ya wataalamu wa afya na majanga ingekuwa heri mihemko na hisia zingepungua.

Ni kosa mawaziri, wabunge na Rais wawe ndiyo wasemaje wakuu. Hawa kazi yao ilikuwa kupokea ripoti kutoka kwa kamati ya wataalamu.

Wao wanajua walau kila kitu kuhusu magonjwa...hawana mihemko...hawana chuki...wala hawana mirengo ya kisiasa wanasimamia miiko ya kazi.
 
Kwan nisisi wananchi ndo tunaozika usiku?

Ni wenyewe hao ndo wametuanzishia kautaratibu ka kuwazika ndugu zetu usiku tena bila uwepo wa ndugu.

Uyu ameongea ili mradi kufifisha kile kinacholalamikiwa na watanzania.

Ukweli nikwamba ,Wanao kufa na Corona, ndio mnaowazika nyinyi usiku usiku.

Wanao kufa kwa magonjwa yao mengine, mnawapa ndugu wakazike.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijui hawa majamaa wanatuona sisi mazuzu,wanataka kusema kuwa hawakufahamu kinachoendelea??....si mlikuwa mnaficha idadi ya watu waliokufa kwa Corona ili tusijue idadi yao.

Wameona malalamiko yamekuwa mengi mitandaoni juu yaliyofiwa na ndugu,marafiki pamoja na wazaz wao ndo nameamua kuja na matamko uchwara...pumbavu sanaaa.

Sisi ngozi aisee!leo nimeamini baadhi ya watu fulani valivyokuwa wanasema kuwa sisi watu wenye ngozi nyeusi ni toleo la mwisho kwenye kuumbwa kwetu......

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanacheza mziki wa Rais taratibu..naomba kesho Rais aseme tena kua utaratibu wa kuzika usiku ni mzuri nisikie tena.
Kesho jtatu tunasubiri wanenguaji kutoka NIMR kuhusu matokea ya fenesi na papai kua na Corona kwasasa wanatengeneza mdandiko na kurudiarudia wimbo ili wasisahau ubeti.
 
Kumbe bhana walikuwa wanazika usiku daaah!!utu ni muhimu sana hakuna kitu kinauma kumzika ndugu yako kama ngombe au mbwa!!kwanza kuna plastic bags unaweza kumfunga mtu vizuri tu!

Kingine kuzika mtu bila kuzingati misingi ya dini yake siyo sawa!!hakuna shee wala mchungaji mbona wakubwa getruda,ndasa,Dc yule walipata heshima za ibada kwa dini zao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…