Wizara ya Afya yapiga marufuku watu kuzikwa usiku, yaagiza ndugu washirikishwe

Wizara ya Afya yapiga marufuku watu kuzikwa usiku, yaagiza ndugu washirikishwe

Tumechelewa
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Awafute Kazi Hao
Walikuwa Wapi
 
Kufuatia hotuba ya Mh Rais John Pombe Magufuli, aliyoitoa wakati wa kumuapisha Waziri wa Sheria Mh Mwigulu Nchemba (Mb) kuwa haina haja ya Marehemu kuzikwa usiku kwani inaleta taharuki.

Tunakuomba Mh Rais Magufuli tolea tamko na hili, "Wale Marehemu waliozikwa usiku katika kipindi hiki bila makubaliano na ndugu wa Marehemu, waruhusiwe kuhamisha Maiti kabla hazijaharibika."
 
Nilipomsikia leo , alipokuwa analaumu jinsi alivyozikwa yule aliyekuwa mkuu wa Wilaya Mtwara, nilitegemea kitu kama hiki .

Hapa kuna mambo kadhaaa ya kuangalia:

1) Huenda watendaji(wasaidizi) wa Rais wanafanya mambo kwa kujiamulia tu bila kufuata sheria, wakiona hawakemewi wanajua Rais ameafiki , hivyo wanaendelea.

2) Au ni maagizo na amri toka kwa Rais na vyombo vingine vya juu vya Utawala.

3) Watendaji wanafanya mambo bila weledi,hekima na busara.

Pamoja na kufanya majukumu yao ya kazi na sheria za kazi ,vilevile waangalie kuna sheria nyingine za kimabavu siyo kila mahali zitumike.
NB: Ni maoni tu, si sheria.
 
Ila hali sio ya kwaida na kwa nini watu wazikwe usiku halafu na kama sugu asingeongea bado wasingetoa tamko
 
Sasa maziko yoote kufanyika mchana na ndugu kushirikishwa na
IMG_20200503_132932.jpg


=========

Wizara ya Afya na Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeelekeza maafisa Afya na waganga wakuu wa wilaya na mikopa kuhakikisha familia za wafiwa zinashirikishwa kikamilifu na bila hofu na haraka katika kuandaa mazishi ya wapendwa wao

Pia Wizara imewataka raia kutotumia dawa zinazoshauriwa na watu wasio na utaalamu katika masuala ya tba, badala yake wasubiri muongozo kutoka Wizarani. Kwa sababu hakuna dawa ya kutibu au kuzuia #CoronaVirus hadi sasa
-
Dawa zinazotumika na wengi zinatumika kutibu maradhi mengine na sio #CoronaVirus. Hivyo wizara imewataka Baraza la Famasia kusimamia uuzwaji holela wa dawa hizo ambazo zinashauriwa a watu mitandaoni

Wizara imesema haya baada ya kuzuka uvumi mtandaoni kuwa kuna dawa zinatibu #CoronaVirus hali iliyopelekea baadhi ya wananchi kutumia dawa kiholela hasa dawa za Azithromycin, Aspirin, Prednsolone, Zinc, Ascorbic Acid (Vitamini C) na ARV. Wizara imekanusha, dawa hiz haziwezi kutibu #CoronaVirus

Kuhusu tiba asili/mbadala za mitishamba, wizara imesema itatoa maelezo baada ya kupata ushahidi kamili kutokana na Tafiti zinazoendelea


1588505824179.png

1588505843612.png
 
Back
Top Bottom