Wizara ya Fedha ifumuliwe upya, ufisadi wake ni msiba mkubwa

Wizara ya Fedha ifumuliwe upya, ufisadi wake ni msiba mkubwa

Criterion

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2008
Posts
11,797
Reaction score
11,891
Wakati watanzania wanalia kwa ajili ya tozo na wengine wakizozana kuhusu mikopo, na ugumu wa maisha, Wizara ya fedha inaufisadi wa kutisha. Waziri mkuu alitangazia taifa kugundua wizi wa mabilioni ndani ya miezi 3. Kuanzia March 2021, hadi Mei 2021. Miradi mingi imekwama, na mashirika mengine ya umma yana suffer, lakini fedha zinaibiwa wizara ya fedha kwa njia ya kalamu as if hakuna auditors, hakuna supervision wala regulations.

Tangu Waziri mkuu atoe agizo la uchunguzi, taarifa gani imetoka? Ni kweli mtindo huu umeanza mwezi March baada ya Rais Magufli kufariki au umekuwepo kabla? Ni wizara hii tu ama ni mtindo wa Serikai yote? Kama haya mambo yanaokana ni kawaida, maana yake uvunjaji wa kanuni na sheria ni donda ndugu katika Serikali. Kama sivyo, serikali inachukua hatua gani za kulinusuru taifa na Wizara inayohalalisha ubadhilifu wa namna hii, hasa ukizingatia ni Wizara inayotarajiwa kutunza raslimali za taifa?

Serikali inawezaje kuwa na imani na Wizara ya namna hii, hata kuendelea kuwaamini wafanye maamuzi kwa ajili ya maslahi ya taifa? Ushauri wangu kwa Serikali, ifumue hii wizara na kuweka watu wapya wanaojali maslahi ya taifa. La sivyo ninanusa harufu kali ya rushwa ili kupotosha maamuzi, ushauri mbaya kwa serikali na conspiracy kubwa ya wizi wa mali za Umma.

Hii wizara ni msiba mkubwa kwa Watanzania maskini.

 
Mama anamkubali sana mwiguru sahau hilo.
Sina hakika nimemtaja Mwigulu Nchemba. Naomb uwe makini kabla huja comment. Nimeongelea wizara ya fedha. Na isitoshe, ni jambo zuri rais akiwakubali wateule wake. Lakini kufumua Wizara zenye uharifu kama hii ni kumsaidia Waziri na Watanzania.

Au wewe huoni ufisadi hapo?
 
Sina hakika nimemtaja Mwigulu Nchemba. Naomb uwe makini kabla huja comment. Nimeongelea wizara ya fedha. Na isitoshe, ni jambo zuri rais akiwakubali wateule wake. Lakini kufumua Wizara zenye uharifu kama hii ni kumsaidia Waziri na Watanzania.

Au wewe huoni ufisadi hapo?
Kwani wizara inaongozwa na nani na kama kuna wizi nani anawajibika
 
Haya mambo yanatisha na kutia hasira sana. Alafu wahusika wapo.
 
Haya mambo yanatisha na kutia hasira sana. Alafu wahusika wapo.
Actually kusema nchi haina fedha, kiasi cha kukopa fedha eti mlipe madeni, wakati fedha za uma zinafanywa shamba la bibi huku mamlka zikiona, ni jambo la huzuni sana. Ni kuwatesa, kuwadharau na kuwafedhehesha Wananchi wasiokuwa na hatia kitu ambacho ni dhambi mbaya. Hali kama hizi zisiposhughulikiwa zinazidi kuondoa imani kwa wananchi juu ya serikali na kujiona watumwa katika nchi yao kiasi cha kusema "afadhali ukoloni".
 
Kwani wizara inaongozwa na nani na kama kuna wizi nani anawajibika
Mkuu, naona mengine si kiwango chako. Kuuliza swali bila kusoma ukaelewa na kusikiliza clip huelewi, unaonekan, siyo.

Huwezi kubeba vitu vipana. Naona sasa unamtuhum Rais kwamba hana uelewa, ame compromise standards ama anajali zaidi mahusiano yake na mtu kuliko ustawi wa taifa kitu ambacho si sahihi. Vinginevyo, unamwambia Waziri Mkuu mwongo.

Kwa heri aisee.
 
Wizi ila Kassimu fiksi sana huyo anachosema hakitimii.
Ndiyo sababu tunaomba Kiongozi Mkuu wa Serikali achukue hatua ya kulifumua li wizara lote. Kwa sabbau kinachoonekana ufisadi huu ni syndicate na bila hivyo Wananchi tutaendelea kuhenya kwa manufaa ya wafanya kazi wa wizara ya fedha wasiojali hata chembe mateso ya wananchi maskini.

Katika mazingira kama haya, hata akibakiza watu wengine, akasema alete kuwachanganya, hao waliozoea ufisadi watakuwa mwiba kwa watendaji wapya na ama watawakwamisha au kuwahujumu kwa namna yoyote, ili mfumo fisadi uendelee. NI wakati muafaka wa kuchukua maamuzi magumu na kureform Wizara nzima.
 
Actually kusema nchi haina fedha, kiasi cha kukopa fedha eti mlipe madeni, wakati fedha za uma zinafanywa shamba la bibi huku mamlka zikiona, ni jambo la huzuni sana.

Niufisadi wakutisha.
Kwa kiwango walicho piga hao jamaa kwa muda na mazingira kama hayo,nadhani ilitakiwa isikike pia kauli ya mkuu wa nchi kukazia uchunguzi ilikuwaaminisha wanachi kwamba hakuna mchezo katika kusimamia matumizi bora ya kodi zetu.
 
serikali yote ni msiba
watu wanahama kutoka sector binafsi kwenda serikali kusaka fursa
Hahahah

Huo ndiyo ukweli!

Zaidi ya hapo tuendelee kupigwa sindano

Maana hakuna namnaa,zaidi ya kuishiaa kulalama tu huku tunapunguza idadi ya miaka kuishi

Ova
 
Niufisadi wakutisha.
Kwa kiwango walicho piga hao jamaa kwa muda na mazingira kama hayo,nadhani ilitakiwa isikike pia kauli ya mkuu wa nchi kukazia uchunguzi ilikuwaaminisha wanachi kwamba hakuna mchezo katika kusimamia matumizi bora ya kodi zetu.
Ukitaka kuona kwamba hana watu sahihi sehemu sehemu na anahitaji support ktka azma ya kujenga nchi, angalia majuzi hadi kawaambia TAKUKURU Wachukue hatua dhidi ya watu waliotajwa kwenye report ya CAG.
Hivi kweli ulitegemea idara kama hiyo kusubiri amuri ya mkuu wa nchi kuchukua hatua ambazo tayari ziko mezani kwao?

Kama wakichukua hatua kwa agizo la mkuu, atakuwa na uhakka gani wataifanya ipasavyo na si kuwalinda watuhumiwa ambao wanaonewa kigugumizi kuchukuliwa hatua?

Kama hali iko hivyo, ni mashauri mangapi ya walala hoi yanaozea kwenye makasiki ya TAKUKURU? Walala hoi wangapi wanatendewa haki?

Unakumbuka mamia ya watu waliofutiwa kesi ya kubambikizwa na idara hii?
Mkuu wa nchi anatakiwa achukue hatua ngumu sana dhidi ya baadhi ya wizara kwenye serikali. Ninatamani angeajiri task force kutoka nchi moja makini itusaidie kwenye reformation ya hizi habari kwa sababu waliopo wame compromise na wamelewa na wameshakuwa mumiani.
 
Halafu wakati huohuo imagine anaejiita kuwa ni Rais wa Tanzania baada ya kutumia vyombo vya dola kupora chaguzi,
anapenda urais kuliko kawaida🤣🤣🤣
 
serikali yote ni msiba
watu wanahama kutoka sector binafsi kwenda serikali kusaka fursa
Na milango ya fursa haram iko wazi. Kama mtu anaona serikali inaruhusu upigaji, maadamu uwe mwenzao, wakati sekta binafsi inawekwa katika mazingira ya kuponda kokoto, akiwa na moyo mwepesi, anakwenda kupiga.,
 
Halafu wakati huohuo imagine anaejiita kuwa ni Rais wa Tanzania baada ya kutumia vyombo vya dola kupora chaguzi,View attachment 2069708View attachment 2069710View attachment 2069714anapenda urais kuliko kawaida🤣🤣🤣
Halafu unamskia Waziri wa fedha akisema Wtanzania hawatalipa madeni bali serikali italilpa. Anaendeleza kuwafanya Watz kuwa mapumbavu na majuha wasiojua fedha za Serikali zinatoka kwao.
La ajabu mkuu anasema hukaa n ahuyu huyu waziri, katibu mkuu kiongozi kujadili masuala ya mikopo wakitegemea huyu ndiye awape ushaur wa kitaalam!.
Ina maana Makamu wa Rais kazi yake ni nini? Na kama Wizara ya fedha ndio washauri wa rais katika masuala ya uchumi, tumekwisha Wtz.
 
Back
Top Bottom