Wizara ya Habari: Bidhaa za kigeni ziandikwe kwa Kiswahili

Wizara ya Habari: Bidhaa za kigeni ziandikwe kwa Kiswahili

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Naibu Waziri Wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Abdallah Ulega amesema bidhaa zote za kigeni zinazoingia nchini zitafutiwe utaratibu wa kutafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili.

Na bidhaa ambazo zinazalishwa nchini ziwekewe utaratibu wa kuwa na maelezo ya Kiswahili ili kumrahisishia mtumiaji wa bidhaa ambaye anafahamu Kiswahili.

Ametoa mfano wa Dawa ambazo mtumiaji anapaswa ajue tahadhari za kutumia dawa hiyo na sio kuishia kujua idadi ya vidonge vya kutumia kwa siku. Malezo hayo yakiwa kwa Kiswahili itasaidia hili.

Amesema hayo ni kwa mujibu wa Kanuni zilizopo hivyo Wizara ya Habari itakaa na Mamlaka ili kuhakikisha utekelezaji wa Kanuni inayotaka bidhaa ziwe na maelezo ya Lugha ya Kiswahili.

 
Safi sana mkuu, kabisa zibadirishwe ziandikwe kwa lugha ya kiswahili. Kwasababu dawa zote huwa zinaandikwa maelezo yote ambayo mtu anaweza kuyaelewa bila hata kumsubiri daktari ampe maelezo.
 
Itakuwaje kwa dawa za hospitali?? Watatoa agizo huko india na ulaya kwamba dawa za kuja Tz ziandikwe kiswahili?


Unajua International Protocol!??? It means kama hawana Waswahili, basi watalazimika kuwaajiri maproxy Tanzania wa kuwafanyia ^ubalidishaji lugha^ -- AJIRA HIYOO!!!
 
Naibu Waziri Wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Abdallah Ulega amesema bidhaa zote za kigeni zinazoingia nchini zitafutiwe utaratibu wa kutafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili.

Na bidhaa ambazo zinazalishwa nchini ziwekewe utaratibu wa kuwa na maelezo ya Kiswahili ili kumrahisishia mtumiaji wa bidhaa ambaye anafahamu Kiswahili.

Ametoa mfano wa Dawa ambazo mtumiaji anapaswa ajue tahadhari za kutumia dawa hiyo na sio kuishia kujua idadi ya vidonge vya kutumia kwa siku. Malezo hayo yakiwa kwa Kiswahili itasaidia hili.

Amesema hayo ni kwa mujibu wa Kanuni zilizopo hivyo Wizara ya Habari itakaa na Mamlaka ili kuhakikisha utekelezaji wa Kanuni inayotaka bidhaa ziwe na maelezo ya Lugha ya Kiswahili.


Kwa sababu jiwe kiingereza kimeshamshinda na kiswahil kwa sasa anakimudu kiasi Ndio anataka kila kitu kiwe kiswahili
 

Attachments

  • twitter_20210206_211558.mp4
    846.2 KB
  • English please .mp4
    3.6 MB
Unajua International Protocol!??? It means kama hawana Waswahili, basi watalazimika kuwaajiri maproxy Tanzania wa kuwafanyia ^ubalidishaji lugha^ -- AJIRA HIYOO!!!
Hapa sasa ni fursa maana napata hisia kuwa huko viwandani ulaya na Asia wakenya wameshaanza kupiga jaramba la ukalimani.
 
Smartphone kwa kiswahili inaitwa rununu,
Tv inaitwa luninga,
Paracetmol sijui inaitwaje
 
Sasa hivi ni kwenda na beat ya mzee, kahamishia CD kwenye kiswahili kwa hiyo kila waziri atatoka na mpango mkakati wa kutaka kuonyesha yeye ni mzalendo sana wa lugha🤣
 
Inasikitisha sana kuona kwamba hata bidhaa zinazozalishwa hapahapa nchini zina maelekezo muhimu na ya utumiaji katika lugha za kigeni, mathalani Kifaransa na Kiingereza, hakuna Kiswahili. Neno pekee la Kiswahili kwenye kifungashio kizima ni ^Tanzania^ kwenye ^Made in Tanzania!^ Hii ni hatari na nusu. Tusipokuwa makini, muda si mrefu tutakuwa taifa ajinabi linalozungumza Kiswahili, badala ya kuwa taifa janibu linalozungumza lugha za kigeni. Tuokoe bidhaa hii adimu, adhimu, adhihi, adinati na azizi ya lugha ya Kiswahili.
 
Kwanini tunafikiria bidhaa kutumika Tanzania tu? Kwa hatutaki masoko ya kimataifa!? Kwa tabia hii ndio maana mapato ya kigeni kwetu yanaendelea kupungua. Hakuna bidhaa zinatengenezwa na global manufacturers kwa ajili ya Tanzania tu!!

Kuna jambo tulishachelewa. Tulishachelewa kuifanya lugha ya Kiswahili kuwa ya kibiashara na kitaaluma. Dunia inazidi kuwa moja kiteknolojia, sijui huko tutaingiaje na kiswahili!

Ni rahisi kubadilisha mambo kuwa katika Kiingereza kuliko Kiswahili! Cancel culture imeanza kutuingia - tunaelekea kuwaita waTanzania wanaosoma nje sio wazalendo!!
 
Naibu Waziri Wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Abdallah Ulega amesema bidhaa zote za kigeni zinazoingia nchini zitafutiwe utaratibu wa kutafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili.

Na bidhaa ambazo zinazalishwa nchini ziwekewe utaratibu wa kuwa na maelezo ya Kiswahili ili kumrahisishia mtumiaji wa bidhaa ambaye anafahamu Kiswahili.

Ametoa mfano wa Dawa ambazo mtumiaji anapaswa ajue tahadhari za kutumia dawa hiyo na sio kuishia kujua idadi ya vidonge vya kutumia kwa siku. Malezo hayo yakiwa kwa Kiswahili itasaidia hili.

Amesema hayo ni kwa mujibu wa Kanuni zilizopo hivyo Wizara ya Habari itakaa na Mamlaka ili kuhakikisha utekelezaji wa Kanuni inayotaka bidhaa ziwe na maelezo ya Lugha ya Kiswahili.

Nasubiri toyota itakavyoandikwa kwa kiswahili
 
Back
Top Bottom