Wizara ya Kazi ichunghuzeni kampuni ya mabasi ya Shabiby

Wizara ya Kazi ichunghuzeni kampuni ya mabasi ya Shabiby

sinafungu

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2010
Posts
1,527
Reaction score
865
NI Kampuni yenye jina kubwa na ni konge ktk huduma za usafirishaji hapa Nchini, mmiliki wake ni mbunge wa GAIRO na ni kiongozi anayeheshimika. Nasukumwa kuandika hili kwa matukio ya uonevu anayowafanyia WAFANYAKAZI WAKE.

Wako wengi wanafanya kazi katika kampuni hii miaka kadha lkn hawana ajira ya kudumu, wala ajira ya mikataba. Maana yake wanamfamyika kazi bila ya kuwa na mikataba ambayo kimsingi ni kwa mujibu wa sheria. Kwa maana hii kampuni hii inakwepa kodi sambamba na kuvunja sheria za nchi.

Kwa mfano ana kawaida inapotokea suala la short kwenye mahesabu ya hela, yeye huongea na mkuu wa kituo tu na wafanyakazi anaowakisia hata kama hawahusiki hukamatwa na kuwekwa ndani bila ya kufunguliwa mashitaka, na kulazimishwa kulipa hizo hela nje ya utaratibu. Wakilipa keshi inaishia hapohapo.

Juzi amekamata baadhi ya wafanyakazi wake kwa madai eti wameetengeneza hasara, walipelekwa kituo cha polisi pale Dododma Mjini, wamelala pale bila ya kufunguliwa mashitaka, huku wakilazimishwa walipe.

Hawapelekwi mahakamani kwani mwenyewe anajua akiwapeleka kule kesi itamuelemea, anawafanyisha kazi miaka kadha pasi na kuwatambua kisheria, wafanyakazi hao tangu mwezi Januar hawana mishahara.

Hivi huyu mkuu wa kampuni hii anajua kuwa kesho kuna hukumu toka kwa Mungu?
 
pole sana mkuu naamini wewe ni mfanyakazi wa shabiby hata muandiko wako unaonyesha hilo,mimi napenda tu kukutia moyo usichoke haki yako utaipata hata kama itachelewa lakini mwisho nakukumbusha "usishindane na mwenye pesa" ukiona hupati unachokitaka achana nae,nenda zako mungu atakulipia madeni yako.
 
Unajua sijui kwann madereva hawanaga mikataba katika kazi zao alafu ukizingitia tuna makampuni mengi ya isafirishaji aise.inakera mnoo alafu inafika hatua uonevu unafikia mpka mtu unapatwa na hasira ya kutaka kulia. Me mzee aliangusha lori za mzigo alikuwa anafanya kazi superstar lakn kilichotokea hawakujali nini wala nn wakampiga chini sababu ya kuangasha gari.mtu amefanya kaz kwa miaka 10 bila hta kuchubua gari popote.
 
Una ushahidi wa kutosha juu ya hayo yote uliyoyaandika na ambayo hujayaandika kiongozi?
 
Kama haya madai yana ukweli ndani yake basi mamlaka husika yachukue hatua stahiki.
 
Kampuni yake, kahassle kufika alipofika, umpangie aajiri namna gani?

Kama hutaki kazi unaacha unaenda pengine!!

Watanzania wengi ni wavivu na kupenda kulalamika tu kwa kila kitu!

Akiwa maskini atamlalamikia baba, mama, kaka, serikali, dini, kila aliyepo around.

Tujikomboe kifikra, na kupambania maisha yetu badala ya kusubiria kuajiriwa na kuteswa na waajiri.

Kuwa na vision ya kujipanga kujiajiri mwenyewe uweze kuwa huru. Ukishindwa usimlalamikie aliyekuajiri maana unaitumikia vision yake na ndivyo alivyoipanga.

Waajiri hawapangiwi💉💉😂😀
 
Kampuni yake, kahassle kufika alipofika, umpangie aajiri namna gani?

Kama hutaki kazi unaacha unaenda pengine!!

Watanzania wengi ni wavivu na kupenda kulalamika tu kwa kila kitu!

Akiwa maskini atamlalamikia baba, mama, kaka, serikali, dini, kila aliyepo around.

Tujikomboe kifikra, na kupambania maisha yetu badala ya kusubiria kuajiriwa na kuteswa na waajiri.

Kuwa na vision ya kujipanga kujiajiri mwenyewe uweze kuwa huru. Ukishindwa usimlalamikie aliyekuajiri maana unaitumikia vision yake na ndivyo alivyoipanga.

Waajiri hawapangiwi[emoji382][emoji382][emoji382][emoji23][emoji3]
Ukiwa mwajiri Kuna protocols inatakiwa ufate , just because kampuni ni ya shabbiby ndo anyanyase watu? Mamlaka husika zipo wapi?
 
Sitaki kujua ulikubalije kutumikishwa bila hizo taratibu unazozitaja hapa (mikataba) kwasababu nina uhakika ni shida ndiyo ilikuingiza hapo

Ila ninachojua watu wengine wanajali sana dunia wengine wanajali akhera na wengine wanajali dunia na akhera kwahiyo mimi cha kukushauri ndugu yangu ni moja kati ya haya

A. Achana naye MwenyeziMungu atakusimamia (kwamaana lipa hicho anachotaka umlipe mambo mengine mwachie Mola ahukumu)

B. Kama umenuia kwelikweli kushindana naye na upo hamsini kwa hamsini, liwalo na liwe, huna cha kupoteza endelea kupaza sauti kila unapoweza kufikisha ujumbe fikisha ilimradi tu unaongelea haki

Tanbihi;
Hiyo herufi B kama ukiishika usiwe na moyo wa kurudi nyuma hapo mbeleni na ukubaliane na matokeo yoyote yale
 
Nawe ni mwanafunzi wa Yesu ? Mkipewa mikataba mtaanza kulia kodi inakatwa kwenye mishahala yenu inakuwa midogo.

Hakuna mfanyabiashara anae kubali hasara itokee kwake kwa hiyo pambaneni tu na hari pia isomeni number. Ila niliskia baba enu atatekeleza mpate mikataba na sheria itafanyiwa marekebisho za magari makubwa

Enzi za JK hizi kelele hazikuwepo sijui kwa nn
 
NI Kampuni yenye jina kubwa na ni konge ktk huduma za usafirishaji hapa Nchini, mmiliki wake ni mbunge wa GAIRO na ni kiongozi anayeheshimika. Nasukumwa kuandika hili kwa matukio ya uonevu anayowafanyia WAFANYAKAZI WAKE.

Wako wengi wanafanya kazi katika kampuni hii miaka kadha lkn hawana ajira ya kudumu, wala ajira ya mikataba. Maana yake wanamfamyika kazi bila ya kuwa na mikataba ambayo kimsingi ni kwa mujibu wa sheria. Kwa maana hii kampuni hii inakwepa kodi sambamba na kuvunja sheria za nchi.

Kwa mfano ana kawaida inapotokea suala la short kwenye mahesabu ya hela, yeye huongea na mkuu wa kituo tu na wafanyakazi anaowakisia hata kama hawahusiki hukamatwa na kuwekwa ndani bila ya kufunguliwa mashitaka, na kulazimishwa kulipa hizo hela nje ya utaratibu. Wakilipa keshi inaishia hapohapo.

Juzi amekamata baadhi ya wafanyakazi wake kwa madai eti wameetengeneza hasara, walipelekwa kituo cha polisi pale Dododma Mjini, wamelala pale bila ya kufunguliwa mashitaka, huku wakilazimishwa walipe.

Hawapelekwi mahakamani kwani mwenyewe anajua akiwapeleka kule kesi itamuelemea, anawafanyisha kazi miaka kadha pasi na kuwatambua kisheria, wafanyakazi hao tangu mwezi Januar hawana mishahara.

Hivi huyu mkuu wa kampuni hii anajua kuwa kesho kuna hukumu toka kwa Mungu?
CCM hao, waliipenda wenyewe, wapambane na hali zao.
 
Hakuna mtu anaependa kuwest money!


Ukishasema ipelekwe polis tyr ni hela.

Km makosa yamejitokeza na uhakika upo sema tu walitereza kuto kunukuu ushahidi polis uende kufanya nini?


Isitoshe kampuni ni yake sio ya serikali,, usimpangie cha kufanya au namna ya kuajiri.

Pia sijakuelewa ulipoweka swala la ubunge wake hapo, kwamba hiyo kampuni ni ya umma au!!!?


NB: Huwezi acha kazi.
 
Kampuni yake, kahassle kufika alipofika, umpangie aajiri namna gani?

Kama hutaki kazi unaacha unaenda pengine!!

Watanzania wengi ni wavivu na kupenda kulalamika tu kwa kila kitu!

Akiwa maskini atamlalamikia baba, mama, kaka, serikali, dini, kila aliyepo around.

Tujikomboe kifikra, na kupambania maisha yetu badala ya kusubiria kuajiriwa na kuteswa na waajiri.

Kuwa na vision ya kujipanga kujiajiri mwenyewe uweze kuwa huru. Ukishindwa usimlalamikie aliyekuajiri maana unaitumikia vision yake na ndivyo alivyoipanga.

Waajiri hawapangiwi[emoji382][emoji382][emoji23][emoji3]

Ndio watu wafanye kazi bila mikataba mkuu?
 
Back
Top Bottom