Uchaguzi 2020 Wizara ya Mambo ya Ndani yawataka Viongozi wa Dini kutofanya kampeni

Uchaguzi 2020 Wizara ya Mambo ya Ndani yawataka Viongozi wa Dini kutofanya kampeni

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imewaasa viongozi wa kidini kutojihusisha na kampeni za kisiasa kwa kuwaambia waumini wao kuhusu viongozi wa kuwachagua bali wabaki kuhubiri amani, upendo na umoja

Wizara imesema jumuiya za kijamii na taasisi za dini husajiliwa na Wizara ya Mambo ya ndani kwa mujibu wa Sura ya 337 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Namba 3 ya mwaka 2019

Wizara imesema kiongozi wa dini kutoa maelekezo kwa waumini juu ya mgombea wa kumchagua ni kinyume na kifungu cha 17(c) cha Sheria ya Jumuiya

Wizara imewataka viongozi wa dini wazingatie sheria za Jumuiya ambayo inakataza viongozi wa kidini kujihusisha na vitendo hivyo, kwa kuwa vinaingilia uhuru wa kikatiba wa kila mtu kumchugua mgombea anayemtaka.

Huyu Simbachawene sijui amekula maharagwe ya wapi. Shehe wa Dar alimpigia kampeni Magufuli hadharani hakuona, viongozi wa dini wamekusanywa Dodoma na CCM kumuombea Magufuli hakuona, viongozi wamekuwa wakifanywa dua chini ya udhamini wa CCM na Majaliwa haoni!

Baada ya Shehe Ponda kuingia kazini Simbachawene anatoka mafichoni kama amevamiwa na nyuki!
 
Yule anayejiita Rashid kule Kawe mbona kaingia mzima mzima anagombea na ubunge, au yeye hafanyi kampeni ama siyo askofu siku hizi, kuweni serious..
 
Ila matatizo mengine serkali inayatengeneza,nikwanini wanawaita viongozi wa dini kwenye majukwaa ya kampeni?

Mbona bungeni kuna dua maalum kila siku kukiwa na vikao vya bunge lakini hakuna shehe wala padri anayeomba dua hizo kwenye chombo hicho nyeti.

Acheni kutengeneza matatizo halafu yakawasumbua kuyatatua
Simbachawene acha kutuhadaa. Watanzania wanajua sana. Suala la viongozi wa dini kupanda majukwaani na kuomba kura kwa mgomeba fulani si kosa kisheria. Suala hili liachwe kwa mamlaka ya dhehebu husika kuhusu viongozi wake kufanya au kutofanya kampeni.
 
Huu uonevu kuna kitu kinaitwa Arab Springs. Hawawez wakanielewa sababu lugha hawaijui nlotumia. Kuna kitu kingine kinaendelea Nigeria kwa sasa. Hii nayo hawawez jua sababu siasa za kimataifa hawazifatilii.

Ila haya mambo hua yana mwisho wake. Either mbaya au mzuri.

Ajuaye ni MUNGU
Naona hii hali inatengenezwa nchini. Wenye maamuzi ya watanzania wasifike huko ni Tume ya uchaguzi kutenda haki tu...
 
Tena naona yule shehe ambaye anahubiri mambo ya Muhamadi na Yesu kwa pamoja wamuite akajieleze.

Amechanganya hata baadhi ya waumini.
Yule ana hadhi moja na musiba,bashite heri James ktk nchi hii hata siro mahera hawezi wagusa Hawa watashinda njaa.
 
Hivi BAKWATA ni chama cha siasa sio??
Bakwata iliasisiwa na ccm lengo kuu ni kuwanyamazisha waislamu wasidai haki zao.
Thus haijawahi shutumu juu ya manyanyaso ya waislamu zikiwemo teuzi, kukamatwa kwa waislamu
 
Yani cha ajabu matamko hutolewa pale tu wapinzani wakifanya jambo. BAKWATA usiku na mchana inahamasisha watu wachague CCM hilo halikuwa kosa na maisha yaliendelea kama kawaida. Kwa vile Ponda kapanda jukwaa la upinzani basi ghafla sheria imechukuwa mkondo wake.
Siku wakiondolewa madarakani, watafute pa kujificha
 
Mzee Ponda na Bagonza Keisha habari yao! Viongozi wasimamie viapo au kama vipi wavue kora wavae magandwa, sio kujificha nyuma ya migongo ya madhabahu!
Hawa je
 

Attachments

  • Screenshot_20201021_133440.jpg
    Screenshot_20201021_133440.jpg
    91.1 KB · Views: 2
Chadema mtajuta kusimamisha msaliti wa Nchi Lissu atapigiwa kura na robert tu
Nakushauri kwa faida yako ya siku za mbeleni kuwa tafuta chuo kinachofundisha propaganda hata kwa njia ya mtandao ukasome upate ujuzi wa kufanya propaganda!
Hili unachokifanya sio propaganda Bali ni person attack kwa uliyemlenga na siku akikupatia nafasi ya kukushughulikia utaiona siasa chungu! Kama anakukera mtafute umwambie ana kwa ana! Mr.polepole propaganda ulisomea chuo kipi? Unafeli Sana ndugu!
 
Rashid Gwajima alijiuzulu nafasi Yake like kwenye kabisa lake? Kila jumapili anaongoza ibada siyo? Wizara inaweza kutuhakikishia kuwa katika mahubiri take hapigi kampeni? Na hili siyo kosa kwa mujibu wa Sheria hiyo?
 
Usaliti ni laana ? Huko Chadema huwa mnashughulikiana?
Nakushauri kwa faida yako ya siku za mbeleni kuwa tafuta chuo kinachofundisha propaganda hata kwa njia ya mtandao ukasome upate ujuzi wa kufanya propaganda!
Hili unachokifanya sio propaganda Bali ni person attack kwa uliyemlenga na siku akikupatia nafasi ya kukushughulikia utaiona siasa chungu! Kama anakukera mtafute umwambie ana kwa ana! Mr.polepole propaganda ulisomea chuo kipi? Unafeli Sana ndugu!
 
Huu uonevu kuna kitu kinaitwa Arab Springs. Hawawez wakanielewa sababu lugha hawaijui nlotumia.
Kuna kitu kingine kinaendelea Nigeria kwa sasa. Hii nayo hawawez jua sababu siasa za kimataifa hawazifatilii
Ila haya mambo hua yana mwisho wake. Either mbaya au mzuri. Ajuaye ni MUNGU
waswahili daima husema mdharau mwiba humchoma. Daima kila alalae huamka. Tuombe uhai tu tuje kuwa mashahidi watu wakiamka.
 
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imewaasa viongozi wa kidini kutojihusisha na kampeni za kisiasa kwa kuwaambia waumini wao kuhusu viongozi wa kuwachagua bali wabaki kuhubiri amani, upendo na umoja

Wizara imesema jumuiya za kijamii na taasisi za dini husajiliwa na Wizara ya Mambo ya ndani kwa mujibu wa Sura ya 337 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Namba 3 ya mwaka 2019

Wizara imesema kiongozi wa dini kutoa maelekezo kwa waumini juu ya mgombea wa kumchagua ni kinyume na kifungu cha 17(c) cha Sheria ya Jumuiya

Wizara imewataka viongozi wa dini wazingatie sheria za Jumuiya ambayo inakataza viongozi wa kidini kujihusisha na vitendo hivyo, kwa kuwa vinaingilia uhuru wa kikatiba wa kila mtu kumchugua mgombea anayemtaka.

Hii barua haina tofauti na toilet paper! Mmeshachelewa Sheikh Ponda keshatoa maelekezo kilichobaki tarehe 28/10/2020 natekeleza maelekezo yake. Kula yangu na familia yangu ni kwa lissu
 
..Simbachawene ni mgombea ktk uchaguzi huu.

..angekuwa na busara angemuachia Katibu Mkuu wa Wizara atoe taarifa hiyo.
 
Back
Top Bottom