Wizi mkubwa unafanywa hivi manunuzi ya magari ya Serikali, pikipiki, ambulance nk, vifaa vya kielectronic vya umma, na manunuzi yote ya Serikali

Wizi mkubwa unafanywa hivi manunuzi ya magari ya Serikali, pikipiki, ambulance nk, vifaa vya kielectronic vya umma, na manunuzi yote ya Serikali

polokwane

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2018
Posts
3,361
Reaction score
5,842
Sijui ni kwanini Serikali kwenye suala la manunuzi ya mali zake huwa haipo makini kila manunuzi ya Serikali yanapofanyika kuna pesa ya wizi inapita huko na kuna njia mbalimbali zinazotumika hapa ili kuiibia Serikali

1. Kuagiza vitu kwa idadi kubwa tofauti na mahitaji halisi ya Serikali sasa hapa kuna mambo, kwanza vinaagizwa vitu vingi na ndani yake inaingizwa order yao binafsi (Mafisadi) kwa hiyo mfano mahitaji ni 200,000 basi vitaombwa 250,000, hivyo elfu hamsini watajua wao watakavyoupeleka mchakato kati ya wanunuzi na watu wa store na record za ledger book ila Serikali itatoa hela ya 250,000 maana yake hapo kuna vitakavyoingizwa kwenye ledger na kuonekana vimetoka au visiingizwe kabisa kwenye ledger book.

2. Kuongeza gharama za manunuzi mara mbili au zaid ya bei halisi kama kitu kinauzwa Tsh.200,000/ basi serikali itauziwa kati ya Tsh.300,000 hadi Tsh. 350,000/- au zaid

3. Kununua vitu ambavyo ni low quality wakati vinavyohitajika na pesa iliyotoka serikalini ni ya vifaa vyenye high quality ( hili lilijitokeza kwenye vishkwambi, mashine za kusajili wapiga kura, mifumo ya kimtandao ya serikali , servers nk ndio maana mifumo mingi ya Derikali haiishi kusumbua kila mara)

4. Kuchanganya bidhaa original na feki zake, hasa zile zinazohitajika kwa wingi mf. Vifaa vya afya , vifaa vya kielectronic ,vifaa vya miradi ,vifaa vya kazi maalumu nk.

Yaani hapa iko hivi mfano vinahitajika vifaa 200,000 ambavyo bei yake ni Tsh.600,000/- kila kimoja ambacho ni original na high quality, kitakachofanyika ni kununua vifaa 100,000 original kabisa ambavyo navyo unaweza kukuta bei iliongezwa , halafu hivyo 100,000 vilivyo baki vinatafutwa feki yake vifananavyo na vinavyoweza kufanya kazi ile ile ila sio kwa ubora lakini kwa bei ya chini labda Tsh 250,000/- na hapa huwa order inatolewa China maana ndio kuna local industries zenye ubingwa wa kutoa copy za vitu kwa bei ndogo ili pesa ya juu watu waibe

5. Kuleta vitu vilivyoagizwa kwa mafungu mafungu yani kama vilihitajika vifaa labda 200,000 vinaletwa kwanza 130,000 halafu wanasikilizia kwanza kama kutakuwa na kelele wakiona kimya ndio imetoka hiyo vilivyobaki haviji tena pamoja na kwamba Serikali inakuwa ilishatoa hela ya vyote 200,000 na baada ya hapo wanacheza na watu wa record kwenye ledger book idadi inajazwa lakini vitu havipo.

Zipo njia nyingi zaidi na sitaki kuamini kwamba serikali haijui
 
Mathematitian wa ccm
JamiiForums2129585548.jpg
JamiiForums1950632822.jpg
JamiiForums-1848343657.jpg
 
kuna njia mbali mbali zinazo tumika hapa ili kuiibia serikali

Sio kuibia Serikali bali kuibia nchi, ni lini serikali ilikuwa na pesa zake??!

Zipo njia nyingi zaidi na sitaki kuamini kwamba serikali haijui

Watendaji wa serikali ndio wezi sasa wewe unataka mwizi ajue/ajitambue yeye mwenyewe kwa wizi wake??!


Ila tunashukuru kwa kutufumbua macho.

Halafu wewe umejuaje kwamba kuna wizi wa aina hizo huko serikalini??!, wewe umesomea upelelelezi??!😀
 
Bila sheria ya kumalizana kiuchumi hadi kizazi cha 3 wizi na ufisadi hautaisha serikalini. Hela nyingi inapotea mikononi mwa watu badala ilete maendeleo.
Ni tqtizo kubwa sana, Imagine watu wanagundua kwamba mtu fulani kafanya hili na fanywi lolote.
 
Bila sheria ya kumalizana kiuchumi hadi kizazi cha 3 wizi na ufisadi hautaisha serikalini. Hela nyingi inapotea mikononi mwa watu badala ilete maendeleo.
Ndio maana akija mtu kuwabana watatoa mapovu balaa.
 
Bila sheria ya kumalizana kiuchumi hadi kizazi cha 3 wizi na ufisadi hautaisha serikalini. Hela nyingi inapotea mikononi mwa watu badala ilete maendeleo.


Ni lazima ifike hatua tukubali kuwa hii nchi na nyingi za Africa bado hazijawa tayari kutawaliwa kidemokrasia, hii nchi inataka sheria kandamizi kusha wawepo watu wa kuzisimamia haswa, ndani ya miaka 3 tu hela ya umma itaogopeka vibaya.

Katiba irekebishwe ili kusiwepo na kiongozi yoyote aliye na kinga, mihimili ipewe nguvu halisi ya kujitegemea.

Akigundulika yoyote kufanya ufisadi, kwanza anyang'angwe mali zake ZOTE, kisha kesi za ufisadi zisiwe na dhamana, ziendeshwe harakaharaka na kifungo kiwe miaka 30 au kunyongwa bila huruma.

Ukionyesha mfano kwa chambo kama watatu hivi, hakuna raia watakaokuwa wanakimbilia teuzi tena.

Bila kudhibiti rushwa tusitarajie maendeleo yoyote yale, hela zinapotea nyingi sana huko.
 
Sijui ni kwanini Serikali kwenye suala la manunuzi ya mali zake huwa haipo makini kila manunuzi ya Serikali yanapofanyika kuna pesa ya wizi inapita huko na kuna njia mbalimbali zinazotumika hapa ili kuiibia Serikali

1. Kuagiza vitu kwa idadi kubwa tofauti na mahitaji halisi ya Serikali sasa hapa kuna mambo, kwanza vinaagizwa vitu vingi na ndani yake inaingizwa order yao binafsi (Mafisadi) kwa hiyo mfano mahitaji ni 200,000 basi vitaombwa 250,000, hivyo elfu hamsini watajua wao watakavyoupeleka mchakato kati ya wanunuzi na watu wa store na record za ledger book ila Serikali itatoa hela ya 250,000 maana yake hapo kuna vitakavyoingizwa kwenye ledger na kuonekana vimetoka au visiingizwe kabisa kwenye ledger book.

2. Kuongeza gharama za manunuzi mara mbili au zaid ya bei halisi kama kitu kinauzwa Tsh.200,000/ basi serikali itauziwa kati ya Tsh.300,000 hadi Tsh. 350,000/- au zaid

3. Kununua vitu ambavyo ni low quality wakati vinavyohitajika na pesa iliyotoka serikalini ni ya vifaa vyenye high quality ( hili lilijitokeza kwenye vishkwambi, mashine za kusajili wapiga kura, mifumo ya kimtandao ya serikali , servers nk ndio maana mifumo mingi ya Derikali haiishi kusumbua kila mara)

4. Kuchanganya bidhaa original na feki zake, hasa zile zinazohitajika kwa wingi mf. Vifaa vya afya , vifaa vya kielectronic ,vifaa vya miradi ,vifaa vya kazi maalumu nk.

Yaani hapa iko hivi mfano vinahitajika vifaa 200,000 ambavyo bei yake ni Tsh.600,000/- kila kimoja ambacho ni original na high quality, kitakachofanyika ni kununua vifaa 100,000 original kabisa ambavyo navyo unaweza kukuta bei iliongezwa , halafu hivyo 100,000 vilivyo baki vinatafutwa feki yake vifananavyo na vinavyoweza kufanya kazi ile ile ila sio kwa ubora lakini kwa bei ya chini labda Tsh 250,000/- na hapa huwa order inatolewa China maana ndio kuna local industries zenye ubingwa wa kutoa copy za vitu kwa bei ndogo ili pesa ya juu watu waibe

5. Kuleta vitu vilivyoagizwa kwa mafungu mafungu yani kama vilihitajika vifaa labda 200,000 vinaletwa kwanza 130,000 halafu wanasikilizia kwanza kama kutakuwa na kelele wakiona kimya ndio imetoka hiyo vilivyobaki haviji tena pamoja na kwamba Serikali inakuwa ilishatoa hela ya vyote 200,000 na baada ya hapo wanacheza na watu wa record kwenye ledger book idadi inajazwa lakini vitu havipo.

Zipo njia nyingi zaidi na sitaki kuamini kwamba serikali haijui
umezungumza ukweli sana, ingawa kumsaidia Mh. rais tungeainisha njia za ku mitigate hizi challenge, ingawa kwa sasa upo mfumo wa Nest ambao nadhani utatatua baadhi ya changamoto ulizozianisha.
 
Back
Top Bottom