mwanyaluke
JF-Expert Member
- Jan 22, 2015
- 704
- 2,435
Halmashauri ni mali ya wananchi na wanamiliki Halmashauri kupitia Baraza la Madiwani.
Halmshauri inasimamiwa moja kwa moja na Madiwani, inasikitisha sana Halmashauri ndipo pesa zinapigwa sana, huku wasimamizi wapo kila siku na wanaendelea kula posho za vikao.
Tatizo la kuibiwa ni matokeo ya kuwa na madiwani wa ovyo ambao wamechaguliwa na sisi wananchi, msimu wa uchaguzi wananchi huwa tunajadili sana nafasi ya Ubunge na Urais huku tukiacha eneo sensitive sana ambalo ni madiwani. Tumejikuta tuna madiwani wa ovyo kiasi kwamba hawawezi kutambua upuuzi unaofanywa na wafanyakazi wa Halmshauri.
Nadhani uchaguzi wa madiwani ungetenganishwa na uchaguzi wa Wabunge na Urais ili tu kutengeneza umakini na wananchi kufikiria ni aina gani ya diwani wanamtaka na anastahili kuwa Diwani wao, otherwise tutabaki kulalamika miaka na miaka na hakuna kitakachobadilika.
How come mimi mtumishi kwetu Tandahimba niwe na uchungu na wananchi wa Njombe? Diwani ndiye mwenye uchungu na ndiye yupo na wananchi kila siku ,lakini kwa bahati mbaya madiwani wengi vilaza hasa hawa wa CCM matokeo yake ni haya pesa zinapigwa, maendeleo yanasua sua.
Mwizi ni mtu anayetumia akili so unahitaji mlinzi wa mali awe na akili zaidi ya mwizi, sasa sisi Tanzania ni kinyume madiwani wengi uwezo wao upo chini.
Halmshauri inasimamiwa moja kwa moja na Madiwani, inasikitisha sana Halmashauri ndipo pesa zinapigwa sana, huku wasimamizi wapo kila siku na wanaendelea kula posho za vikao.
Tatizo la kuibiwa ni matokeo ya kuwa na madiwani wa ovyo ambao wamechaguliwa na sisi wananchi, msimu wa uchaguzi wananchi huwa tunajadili sana nafasi ya Ubunge na Urais huku tukiacha eneo sensitive sana ambalo ni madiwani. Tumejikuta tuna madiwani wa ovyo kiasi kwamba hawawezi kutambua upuuzi unaofanywa na wafanyakazi wa Halmshauri.
Nadhani uchaguzi wa madiwani ungetenganishwa na uchaguzi wa Wabunge na Urais ili tu kutengeneza umakini na wananchi kufikiria ni aina gani ya diwani wanamtaka na anastahili kuwa Diwani wao, otherwise tutabaki kulalamika miaka na miaka na hakuna kitakachobadilika.
How come mimi mtumishi kwetu Tandahimba niwe na uchungu na wananchi wa Njombe? Diwani ndiye mwenye uchungu na ndiye yupo na wananchi kila siku ,lakini kwa bahati mbaya madiwani wengi vilaza hasa hawa wa CCM matokeo yake ni haya pesa zinapigwa, maendeleo yanasua sua.
Mwizi ni mtu anayetumia akili so unahitaji mlinzi wa mali awe na akili zaidi ya mwizi, sasa sisi Tanzania ni kinyume madiwani wengi uwezo wao upo chini.