Wizi wa wahudumu wa kwenye vituo vya kujaza mafuta

Wizi wa wahudumu wa kwenye vituo vya kujaza mafuta

... how possible is this? Kwa sababu, unless ulimkuta ile handle kaishikilia mkononi, ila ikisharudishwa mahali pake na kunyanyuliwa tena automatically ina-clear digits zote to zero. Yaani anawezaje kuanzia kiwango tofauti na zero? Naomba kuelimishwa.
Kuna namna wanaitegesha haifiki mwisho na kuruhusu kutoa risiti, wale binadamu wa mbinu sana, nami nilidhani nawasingizia ila nimekuja kugundua wameshagundua kuwa kuna namna ule mkonga ukiutegesha bila kuufikisha mwisho basi haita-clear zile digits pale kwenye meter reading na risiti haitoki.
 
Hivi ni Umeandika bila kujua unachoandika na sijui hujui kweli au unafanya makusudi kupotosha ili uchangamshe jukwaa..

Wizi unaosema haupo na hakuna namna yoyote uneweza ukaibiwa Kwa staili hiyo uliyoileta .mkono wa pampu ukirudishwa kwenye mashine wakati wa kutoa unaanza zero mpaka bei uliyoset au utakapoishia

Kuibiwa ni kama ataendelea kupima bila kurudishwa mkono kwenye mashine tena ikiwa mwanzoni hakuset bei wakati anampimia mteja wa kwanza
 
Elfu 5 tu unalialiaaaa. We tip huwa unaacha kweli
Kaka nitumie basi kwenye namba yangu 0621 111 123, nalia kwa sababu jasho nnalotoka kuipata linaniumiza sana, elfu 5 kwangu napata matunda ya kutosha sana kwenda kuwaongezea vitamin wanangu na kujenga heshima kwa mama yoyoooo. Mimi sitoi tip na wala huwa siendi hizo sehemu za kuacha acha tips, ninakula kwa mama ntilie, huko hakuna tip, tunadai hadi mia inayobaki baada ya kunywa kandoro!
 
Hivi ni Umeandika bila kujua unachoandika na sijui hujui kweli au unafanya makusudi kupotosha ili uchangamshe jukwaa..

Wizi unaosema haupo na hakuna namna yoyote uneweza ukaibiwa Kwa staili hiyo uliyoileta .mkono wa pampu ukirudishwa kwenye mashine wakati wa kutoa unaanza zero mpaka bei uliyoset au utakapoishia

Kuibiwa ni kama ataendelea kupima bila kurudishwa mkono kwenye mashine tena ikiwa mwanzoni hakuset bei wakati anampimia mteja wa kwanza
Kaka au dada, hata mimi nilidhani kuwa macho yangu yananidanganya kama unavyobisha wewe, nakuhakikishia kuwa makini, mpaka naamua kuandika nimefanya utafiti na kujiridhisha, mimi nina uhakika 100% ya nilichoandika, vinginevyo nawe ukitaka kunibishia vema fanya nawe utafiti mdogo kama wangu!
 
Kuna namna wanategesha ule mkonga wa kuwekea mafuta hausukumi ile lock na kwa hivyo risiti haitoki, na hii hutokea sana kwa watu wasiohitaji risiti.
Mkonga huwezi kukaa nafasi yake bila lock kuingia mkuu pia kama inawezekana ndani ya sekunde tano ukichomoa mkonga mafuta hayatatoka mpaka ustart tena

Wizi unaongela ni wa miaka ya zamani kabla pump hazijhamia kwenye digital pump Kwa sasa pump za namna hakuna mahali popote ndani ya Tanzania
 
Mkonga huwezi kukaa nafasi yake bila lock kuingia mkuu pia kama inawezekana ndani ya sekunde tano ukichomoa mkonga mafuta hayatatoka mpaka ustart tena

Wizi unaongela ni wa miaka ya zamani kabla pump hazijhamia kwenye digital pump Kwa sasa pump za namna hakuna mahali popote ndani ya Tanzania
Ndugu yangu, naomba tutafutane, twende pamoja pale na tukawahoji walioniibia kwa style hiyo watupe uzoefu, najua yaweza kuwa ngumu kupata ushirikiano, ila nakuhakikishia mimi ntawapa hata pesa ya kula waweze kutupitisha kwenye uzoefu huo.
 
Habari za majukumu wanajamii,

Habari hii ni kupata uzoefu zaidi, kutahadharishana na kuwekana sawa wakati huu mgumu wa uchumi wa kati.

Nimekutana na matukio mawili kwa nyakati tofauti ya kuibiwa na wahudumu wanaotoa huduma ya kuweka mafuta katika kituo kimoja cha mafuta cha TOTAL kilichopo Oysterbay (pale ambapo kuna vituo pacha katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi karibu na mataa ya kwenye makutano ya kuelekea St. Peter, kile kilichopo upande wa FAO, upande ambao kuna JANGID BUILDING).

Mara ya kwanza nilimgundua muhudumu kuwa ameanza kunijazia mafuta hali ya kuwa kwenye pampu kulikuwa kunasomeka Tshs 5,000 ambayo inaonekana alimuwekea mteja aliepita na hakutoa risiti, nikamueleza alichofanya na akakiri kosa lake na kuniwekea mafuta yangu ya Tshs. 5,000 nikaridhika na kimoyomoyo nikasema kuwa haya ni matokeo ya malipo duni kutoka kwa waajiri na ugumu wa maisha, mara ya pili leo (ambayo imenilazimu kuandika uzi huu mrefu), muhudumu kama kawaida kanifanyia ujanja wa kuniita pampu ya mbele halafu baadae akabadili mawazo na kuniambia nisogee nyuma ili aniwekee kutokea pampu ya nyuma (kumbe hii ilikuwa janja yake ya kunifanya nisiweze kusoma vema pale kwenye pampu).

Nami kwa haraka haraka nikakumbuka nilichofanywa mara ya kwanza, nikashuka kwenye gari na kuwahi kusoma kwenye pampu, nikakuta keshaanza kuweka mafuta na kwa sekunde kama 5 tayari pampu imeshafika Tshs 12,000, nikamwambia dada najua umeanzia kwenye elfu 10, akataka kubisha na kuwa mkali, nikamwambia ntakuharibia kazi yako kwa sababu ya Tshs. 10,000 naomba uniwekee mafuta yangu kama pesa niliyokupa. Akataharuki na kuniwekea mafuta yangu yote kulingana na pesa niliyompatia, kwahiyo kwenye pampu ikasoma Tshs 10,000 zaidi ya ile pesa niliyompa aweke mafuta na risiti nikapata ikiwa na Tshs. 10,000 zaidi.

SOMO KWA WAMILIKI WA KITUO
Tafadhali sana wamiliki wa vituo hivi, siwaingilii kwenye biashara yenu ila ni vema kuwashauri kwa ustawi wa biashara yenu: Wale wahudumu sio waaminifu, fanyeni uchunguzi wenu na mkibaini hilo chukueni hatua stahiki, kwa sababu haya wanayoyafanya yatawaharibia biashara zenu na kuleta mdororo. Walipeni vizuri, wapeni mazingira mazuri ya kazi, hakikisheni mnaweka mashine nzuri zinazosomeka kwa ufasaha bila shida.

USHAURI KWA WATUMIAJI WA HUDUMA HII
Tuwe makini wakati wa kuwekewa mafuta, tuhakiki kuwa namba zote kwenye display ya pampu zinaanzia sifuri (zero) kwenye Lita na Kiasi cha pesa. Ikiwezekana tusikubali kuwekewa mafuta mpaka tushuke na kuhakiki kuwa pampu inasomeka vema na inaonesha inaanzia sifuri. Tusiwaamini wahudumu, nao ni binadamu, wanaingiwa na majaribu na vishawishi. Kuna mbinu nyingi za udanganyi kwenye hizi pampu tushirikishane ili tupambane na kuumizana huku ambako hakuna sababu. Tumuogope Mungu na kusema ukweli wakati wote, ikiwezekana unapokutana na uovu kama huu ukomeshe kwa njia yoyote inayowezekana ili kuwaokoa wengine na udhalimu huo.

Ahsanteni sana
Ngoja Kiduku lilo aje atufokee
 
Wizi hutokea hasa kama umetangulizana na bodaboda. Bodaboda huwa wanajaza mafuta yasiyozidi 5000, kwa hio ukienda ww anaanzia pale alipoishia wa bodaboda. Kwa kuwa mara nyingi mafuta yanaweka ya 2000 ama 3000 basi ww kama hujaangalia pampu huwezi kushituka mapema kwamba kuna elfu 2 imeibwa. Ukiona unaitiwa kwenye pampu ilipotoka pikipiki basi uwe makini sana.
Hii style nimepigwa juzi aysee kile kituo cha Temboni! Ntamrudia yule dogo nimpe makavu live
 
Kuna namna wanaitegesha haifiki mwisho na kuruhusu kutoa risiti, wale binadamu wa mbinu sana, nami nilidhani nawasingizia ila nimekuja kugundua wameshagundua kuwa kuna namna ule mkonga ukiutegesha bila kuufikisha mwisho basi haita-clear zile digits pale kwenye meter reading na risiti haitoki.
... this makes sense! Hii tafsiri yake kuna mtu hatimizi jukumu lake ipasavyo - Weights and Measures Agency (WMA) wazee wa "flow-meters". Na wamiliki wa vituo wanatakiwa pia kuhakikisha pump zao haziwezi kuchezewa na wahudumu maana michezo hiyo haina faida yoyote kwao (wenye vituo) zaidi ya kuharibu reputation ya biashara zao.
 
Back
Top Bottom