Wizi wa wahudumu wa kwenye vituo vya kujaza mafuta

Wizi wa wahudumu wa kwenye vituo vya kujaza mafuta

Sio kweli kaka labda unaziamini kwa kuwa hazina wizi.ila kwa ubora wa mafuta na kuifanya engine yako idumu ni vituo viwili tu. Kwanza kabisa PUMA ukiikosa puma basi nenda TOTAL
Utakuja kunielewa siku za usoni, Puma sikanyagi! Nilishawatumiaga nikiwa mkoani gari inakuwa nzito na miss miss za ajabu. Tena kipindi cha mgomo wa bei ya mafuta ule. Huwa nawekaga Total tu nikibadili ni Lake Oil!
 
Mkuu sisi haya maswahibu hayatukuti, sisi wazee wa vidumu!! Yaani wese la buku kumi haibi hata mia...anaanzaje kwanza!!
Tatizo la kidumu kaka unakuwa unarisk maisha yako lakini pia huwezi kuwa na chombo cha moto halafu ukafika kituo cha mafuta ukashuka na kidumu wakati tank lipo na linafunguka! Hii mbinu ni nzuri sana kama upo kwenye dharula.
 
Kuna namna wanaitegesha haifiki mwisho na kuruhusu kutoa risiti, wale binadamu wa mbinu sana, nami nilidhani nawasingizia ila nimekuja kugundua wameshagundua kuwa kuna namna ule mkonga ukiutegesha bila kuufikisha mwisho basi haita-clear zile digits pale kwenye meter reading na risiti haitoki.

Sasa hapa anaibiwa tajiri mwenye sheli au tajiri mwenye gari au wote kwa pamoja?

Nijuavyo, EFD mashine isipotoa risiti maana yake hesabu haiingii yaani kwenye mfumo huwezi kuona kiasi Cha mafuta kilichotoka
 
Nilishawahi kupigwa Simba Oil ilioko kwenye junction ya kwenda kambini na njia ya kwenda maji chumvi! Wizi wa kipumbavu sana.

Alinipiga buku 6 na ilikuwa naweka mafuta nikalaze gari mi huwa silazi gari bila kuweka mafuta ya kulalia.[emoji16]! Gauge huwa inatick after 1.5-2 Km ukiona haijatick jua mafuta hayajaingia.
Hiko kituo si kipya na raia wanapenda sana jioni pale kujazia wese
 
Kaka mimi nakwambia wizi huu umenitokea TOTAL
TOTAL wizi upo na saingine ni pampu flani specific inakuwa inaiba nahisi wameiseti iibe!

Jaribu kujaza kwenye pampu tofauti tofauti kwenye sheli hio hio mafuta ya bei moja. Tafiti hili kimya kimya utaona kuna Pump flani ukijaza mafuta yanakaa sana ila ukijaza pampu flani yanawahi kuisha. Unakuta inakuibia mpaka litre unajaza litre 5 ila kumbe imekutilia litre 4. Nikichezaga na trip meter ya gari nagunduaga hilo mapema sana.

Hili mie hulifanyaga hili mara nyingi kwenye sheli nazojazaga na nimegundua kuna pump zimeminywa flani hivi so nakimbiliaga ile ambayo nikiweka mafuta yake yanakaa.
 
Tatizo la kidumu kaka unakuwa unarisk maisha yako lakini pia huwezi kuwa na chombo cha moto halafu ukafika kituo cha mafuta ukashuka na kidumu wakati tank lipo na linafunguka! Hii mbinu ni nzuri sana kama upo kwenye dharula.
Si kidumu physical kaka; yaani unaweka mafuta ya buku kumi kumi - akishaona una buku kumi hagusi....weee

Nyie mnaoweka full tank lazima aamzie na 20,000 - maisha magumu afanyaje sasa na yeye ana familia.
 
Sasa hapa anaibiwa tajiri mwenye sheli au tajiri mwenye gari au wote kwa pamoja?

Nijuavyo, EFD mashine isipotoa risiti maana yake hesabu haiingii yaani kwenye mfumo huwezi kuona kiasi Cha mafuta kilichotoka
Kwa hesabu za haraka haraka ni kwamba: anaibiwa mwenye kituo cha mafuta kwa sbb yale mafuta yameuzwa bila mashine ya risiti kurekodi, pia anaibiwa mwenye chombo anaewekewa mafuta maana analipia mafuta ambayo hakuwekewa! Hii kwa kifupi inaitwa DOUBLE IMPACT!
 
Hivi ni Umeandika bila kujua unachoandika na sijui hujui kweli au unafanya makusudi kupotosha ili uchangamshe jukwaa..

Wizi unaosema haupo na hakuna namna yoyote uneweza ukaibiwa Kwa staili hiyo uliyoileta .mkono wa pampu ukirudishwa kwenye mashine wakati wa kutoa unaanza zero mpaka bei uliyoset au utakapoishia

Kuibiwa ni kama ataendelea kupima bila kurudishwa mkono kwenye mashine tena ikiwa mwanzoni hakuset bei wakati anampimia mteja wa kwanza

Akili zinanituma kuwa wewe ni pump attendant/dispenser wa sheli.

Na sasa dona linaingia mchanga
 
Si kidumu physical kaka; yaani unaweka mafuta ya buku kumi kumi - akishaona una buku kumi hagusi....weee

Nyie mnaoweka full tank lazima aamzie na 20,000 - maisha magumu afanyaje sasa na yeye ana familia.
Tatizo ni kucheza na budget, mimi TVS yangu huwa najua nikiweka mafuta ya elfu 30 natumia wiki 2, sasa nikisema niweke nusu nusu nakuwa najitega mwenyewe, halafu nina imani kuwa tank ukilijaza mafuta ya kutosha unatunza pump, unalitunza tank lenyewe, unaboresha matumizi ya mafuta na performance ya chombo pia.
 
Kwa hesabu za haraka haraka ni kwamba: anaibiwa mwenye kituo cha mafuta kwa sbb yale mafuta yameuzwa bila mashine ya risiti kurekodi, pia anaibiwa mwenye chombo anaewekewa mafuta maana analipia mafuta ambayo hakuwekewa! Hii kwa kifupi inaitwa DOUBLE IMPACT!

Shukrani umenifumbua macho sana. Kweli mbongo hajui kuanzisha bali anajua kuharibu.

Ela inasakwa aisee 😀
 
Nilishawahi kupigwa Simba Oil ilioko kwenye junction ya kwenda kambini na njia ya kwenda maji chumvi! Wizi wa kipumbavu sana.

Alinipiga buku 6 na ilikuwa naweka mafuta nikalaze gari mi huwa silazi gari bila kuweka mafuta ya kulalia.😁! Gauge huwa inatick after 1.5-2 Km ukiona haijatick jua mafuta hayajaingia.
Pole sana mkuu. Si unaongelea kituo hiki ambacho kipo hapa kwenye kona kushoto kama unakuja mabibo jeshini?
 
Shukrani umenifumbua macho sana. Kweli mbongo hajui kuanzisha bali anajua kuharibu.

Ela inasakwa aisee 😀
Mimi huwa naumia sana roho nikigundua haya ya uharibifu.

Najiuliza sana maswali yasiyo na majibu: Hivi akili hizo wanazotumia hawa vibaka kuturudisha nyuma kwanini wasizitumie katika ubunifu wa mambo yenye kunufaisha jamii?!
 
jana mbichii... nimeenda petro station. nikamwambia weka elfu 30, basi akaclear number akaandika 3,000... nikamwangalia tu akachomeka mpira wake mafuta yakaanza kutoka akajifanya bize akazunguka upande wa pili... mashine imeshakata yeye anajifanya bize.... akaenda funga kifunik akatoa risiti akaniletea, nikampa 30,000 akapokea na kuniambia karibu tena... akashangaa siondoki nikamwambia bado mafuta yangu hayajakamilika umeweka ya elf tatu.... bila hata kuangalia akajifanya kujichangamsha eti samahani daaa kumbe nimeandika elfu tatu.... dah... nina mawazo.... akakuta nimekunja uso namwangalia tu.... nikafungua tank akaandika 27,000 akajaza yaliyobaki..... nikaondoka bado anajichekesha mie simjibu kitu. Huu ni wizi kuweni waangalifu.
 
jana mbichii... nimeenda petro station. nikamwambia weka elfu 30, basi akaclear number akaandika 3,000... nikamwangalia tu akachomeka mpira wake mafuta yakaanza kutoka akajifanya bize akazunguka upande wa pili... mashine imeshakata yeye anajifanya bize.... akaenda funga kifunik akatoa risiti akaniletea, nikampa 30,000 akapokea na kuniambia karibu tena... akashangaa siondoki nikamwambia bado mafuta yangu hayajakamilika umeweka ya elf tatu.... bila hata kuangalia akajifanya kujichangamsha eti samahani daaa kumbe nimeandika elfu tatu.... dah... nina mawazo.... akakuta nimekunja uso namwangalia tu.... nikafungua tank akaandika 27,000 akajaza yaliyobaki..... nikaondoka bado anajichekesha mie simjibu kitu. Huu ni wizi kuweni waangalifu.
Yaani ndio hivyo hivyo, na sijui ni nani aliebuni mbinu ya kuweka hawa wahudumu wa jinsi ya kike, maana akijichekesha tu unamsamehe, mimi nimeshikwa sana na hasira asubuhi, nikatamani kumpa walau kelbu mbili aamke, nikawaza jela, nikakumbuka familia yangu nikajikuta narudisha moyo nyuma!
 
Pole sana mkuu. Si unaongelea kituo hiki ambacho kipo hapa kwenye kona kushoto kama unakuja mabibo jeshini?
Sijui kama ndio hapo ila ni kituo kipya kipya. Huku njia inayotoka External kuelekea maji Chumvi
 
Mimi huwa naumia sana roho nikigundua haya ya uharibifu.

Najiuliza sana maswali yasiyo na majibu: Hivi akili hizo wanazotumia hawa vibaka kuturudisha nyuma kwanini wasizitumie katika ubunifu wa mambo yenye kunufaisha jamii?!

Hela za kutafuta kihalali hazitoshi. Ukisikia kujiongeza ndiyo huko.

Tatizo ni pale mtu unagundua kwamba pale fulani kanipiga. Wapo wanaojenga kwa pesa za sheli.

Maisha ni kupigana na kupiga ndiyo huko uonavyo
 
jana mbichii... nimeenda petro station. nikamwambia weka elfu 30, basi akaclear number akaandika 3,000... nikamwangalia tu akachomeka mpira wake mafuta yakaanza kutoka akajifanya bize akazunguka upande wa pili... mashine imeshakata yeye anajifanya bize.... akaenda funga kifunik akatoa risiti akaniletea, nikampa 30,000 akapokea na kuniambia karibu tena... akashangaa siondoki nikamwambia bado mafuta yangu hayajakamilika umeweka ya elf tatu.... bila hata kuangalia akajifanya kujichangamsha eti samahani daaa kumbe nimeandika elfu tatu.... dah... nina mawazo.... akakuta nimekunja uso namwangalia tu.... nikafungua tank akaandika 27,000 akajaza yaliyobaki..... nikaondoka bado anajichekesha mie simjibu kitu. Huu ni wizi kuweni waangalifu.
Hii kipigo chake ni cha Mbwa koko 😂😂😂 usingeona yangekukuta ya Vocha za Voda 😝😝😝
 
Back
Top Bottom