Wizi wa wahudumu wa kwenye vituo vya kujaza mafuta

Wizi wa wahudumu wa kwenye vituo vya kujaza mafuta

Hakikisha huwi na haraka wala madoido ufikapo kituo cha kujaza gari mafuta.

Usizubaishwe na uzuri wala story za kuzuga za mhudumu.

Epuka kukodolea macho msambwanda wa mhudumu Miele yako.

Macho yako yote kwenye pump reader hakikisha kabla hujawekewa mafuta isome 0000
NZALA HIYO
 
Habari za majukumu wanajamii,

Habari hii ni kupata uzoefu zaidi, kutahadharishana na kuwekana sawa wakati huu mgumu wa uchumi wa kati.

Nimekutana na matukio mawili kwa nyakati tofauti ya kuibiwa na wahudumu wanaotoa huduma ya kuweka mafuta katika kituo kimoja cha mafuta cha TOTAL kilichopo Oysterbay (pale ambapo kuna vituo pacha katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi karibu na mataa ya kwenye makutano ya kuelekea St. Peter, kile kilichopo upande wa FAO, upande ambao kuna JANGID BUILDING).

Mara ya kwanza nilimgundua muhudumu kuwa ameanza kunijazia mafuta hali ya kuwa kwenye pampu kulikuwa kunasomeka Tshs 5,000 ambayo inaonekana alimuwekea mteja aliepita na hakutoa risiti, nikamueleza alichofanya na akakiri kosa lake na kuniwekea mafuta yangu ya Tshs. 5,000 nikaridhika na kimoyomoyo nikasema kuwa haya ni matokeo ya malipo duni kutoka kwa waajiri na ugumu wa maisha, mara ya pili leo (ambayo imenilazimu kuandika uzi huu mrefu), muhudumu kama kawaida kanifanyia ujanja wa kuniita pampu ya mbele halafu baadae akabadili mawazo na kuniambia nisogee nyuma ili aniwekee kutokea pampu ya nyuma (kumbe hii ilikuwa janja yake ya kunifanya nisiweze kusoma vema pale kwenye pampu).

Nami kwa haraka haraka nikakumbuka nilichofanywa mara ya kwanza, nikashuka kwenye gari na kuwahi kusoma kwenye pampu, nikakuta keshaanza kuweka mafuta na kwa sekunde kama 5 tayari pampu imeshafika Tshs 12,000, nikamwambia dada najua umeanzia kwenye elfu 10, akataka kubisha na kuwa mkali, nikamwambia ntakuharibia kazi yako kwa sababu ya Tshs. 10,000 naomba uniwekee mafuta yangu kama pesa niliyokupa. Akataharuki na kuniwekea mafuta yangu yote kulingana na pesa niliyompatia, kwahiyo kwenye pampu ikasoma Tshs 10,000 zaidi ya ile pesa niliyompa aweke mafuta na risiti nikapata ikiwa na Tshs. 10,000 zaidi.

SOMO KWA WAMILIKI WA KITUO
Tafadhali sana wamiliki wa vituo hivi, siwaingilii kwenye biashara yenu ila ni vema kuwashauri kwa ustawi wa biashara yenu: Wale wahudumu sio waaminifu, fanyeni uchunguzi wenu na mkibaini hilo chukueni hatua stahiki, kwa sababu haya wanayoyafanya yatawaharibia biashara zenu na kuleta mdororo. Walipeni vizuri, wapeni mazingira mazuri ya kazi, hakikisheni mnaweka mashine nzuri zinazosomeka kwa ufasaha bila shida.

USHAURI KWA WATUMIAJI WA HUDUMA HII
Tuwe makini wakati wa kuwekewa mafuta, tuhakiki kuwa namba zote kwenye display ya pampu zinaanzia sifuri (zero) kwenye Lita na Kiasi cha pesa. Ikiwezekana tusikubali kuwekewa mafuta mpaka tushuke na kuhakiki kuwa pampu inasomeka vema na inaonesha inaanzia sifuri. Tusiwaamini wahudumu, nao ni binadamu, wanaingiwa na majaribu na vishawishi. Kuna mbinu nyingi za udanganyi kwenye hizi pampu tushirikishane ili tupambane na kuumizana huku ambako hakuna sababu. Tumuogope Mungu na kusema ukweli wakati wote, ikiwezekana unapokutana na uovu kama huu ukomeshe kwa njia yoyote inayowezekana ili kuwaokoa wengine na udhalimu huo.

Ahsanteni sana
Nyingine ni kuchomeka mkonga wa pamp kwenye dumu la lita tano kwanza ndipo anakuwekea kwenye gari ukiwa na upungufu wa lita kadhaa! Ukiwa makini ww unapitia na kigaloni chake unasepa nacho! Hawa wahudumu wengine ni wa hovyo sana! Hii ipo sana Soweto Mbeya 'infinity'! Kuna mabinti pale makauzu kweli!
Mie niliona mchezo huo nikapotezea, nikalipa yote tu na kusepa!
Nyingine nilishuhudia ni pale wanamuwekea wa bodaboda kisha bila kuanzisha upya wanakuwekea na ww! Kimsingi ni umakini tu!
 
Daah! Asante kwa somo nikienda kununua mafuta ya taa nitakuwa makini na mita. Maana huwa nakuwaga bize na msambwanda pamoja na kile kifungo cha kwanza kilichoachwa wazi makusudi!
Jaman si tumekubaliana mafuta ya gari
 
Mimi iliwahi kunitokea,ameweka mafuta gauge yangu haikuamka ikawa inasoma zero,nikamshukia nikawasha moto vibaya kuwa hakuingiza mafuta,yule dada akasema ngoja aingize tena labda pump ina shida,wakati naondoka ilikuwa imenyanyuka kidogo sana,nikawa naondokoa huku maneno yananitoka kuwa ni wezi sana wale wahudumu,ilipofika kama km 1 hivi gauge ikapanda mara mbili ya kipimo cha kwanza,nikabakia naona aibu mimi...
Kuona aibu tu haitoshi,ulichukua hatua gani kulipia hayo mafuta uliyozidishiwa?
 
Nami kwa haraka haraka nikakumbuka nilichofanywa mara ya kwanza, nikashuka kwenye gari na kuwahi kusoma kwenye pampu, nikakuta keshaanza kuweka mafuta na kwa sekunde kama 5 tayari pampu imeshafika Tshs 12,000, nikamwambia dada najua umeanzia kwenye elfu 10, akataka kubisha na kuwa mkali, nikamwambia ntakuharibia kazi yako kwa sababu ya Tshs. 10,000 naomba uniwekee mafuta yangu kama pesa niliyokupa. Akataharuki na kuniwekea mafuta yangu yote kulingana na pesa niliyompatia, kwahiyo kwenye pampu ikasoma Tshs 10,000 zaidi ya ile pesa niliyompa aweke mafuta na risiti nikapata ikiwa na Tshs. 10,000 zaidi.
Nilimwona mmoja amelipa 65.000 akawekewa mafuta ya 55K
 
Ndo maana kweny kapikipiki kangu nikiweka ta 15k inajaa karibia full tank lakn juz kat ikawa yapo chin kiaina
 
Mimi nina kakangu watu wanasema ni bahiri sana akienda sheli anaenda na madumu yake ya lita 60 anawekewa wese anaenda kujiwekea mwenyewe kwenye gari lake,ukimuuliza anasema ni mjanja baada ya kuibiwa kwa mda mrefu na wauza mafuta sheli
 
... madereva wanaotoka nje sometimes wanapoteza sana muda especially rush hours. Hivi huwezi kukaa kwenye gari na bado ukasoma vizuri pump? Unless ni semi-trailer na tank liko kule nyuma kabisa ila kwa IST au Vitz, why should you get out of the car to be able to read the pump?

Kibajaji eti dereva "anatoka nje" kuhakiki mafuta; wanakera sana hawa ukiwa na haraka zako.

[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mimi iliwahi kunitokea,ameweka mafuta gauge yangu haikuamka ikawa inasoma zero,nikamshukia nikawasha moto vibaya kuwa hakuingiza mafuta,yule dada akasema ngoja aingize tena labda pump ina shida,wakati naondoka ilikuwa imenyanyuka kidogo sana,nikawa naondokoa huku maneno yananitoka kuwa ni wezi sana wale wahudumu,ilipofika kama km 1 hivi gauge ikapanda mara mbili ya kipimo cha kwanza,nikabakia naona aibu mimi...
Kwa umri huo mkuu hukujua kwamba gauge haipandi ghafla?
 
Hizo Petrol Station za ajabu ajabu huwa sijazagi mafuta labda itokee gari imenizimikia karibu na hizo sheli. Kwa sasa sheli za uhakika ni Oryx na Total zimekaa ki proffessional zaidi ila kwengine ambako napaamini ni Lake Oil!
Unaachaje kuitaja Puma baba lao?
 
Habari za majukumu wanajamii,

Habari hii ni kupata uzoefu zaidi, kutahadharishana na kuwekana sawa wakati huu mgumu wa uchumi wa kati.

Nimekutana na matukio mawili kwa nyakati tofauti ya kuibiwa na wahudumu wanaotoa huduma ya kuweka mafuta katika kituo kimoja cha mafuta cha TOTAL kilichopo Oysterbay (pale ambapo kuna vituo pacha katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi karibu na mataa ya kwenye makutano ya kuelekea St. Peter, kile kilichopo upande wa FAO, upande ambao kuna JANGID BUILDING).

Mara ya kwanza nilimgundua muhudumu kuwa ameanza kunijazia mafuta hali ya kuwa kwenye pampu kulikuwa kunasomeka Tshs 5,000 ambayo inaonekana alimuwekea mteja aliepita na hakutoa risiti, nikamueleza alichofanya na akakiri kosa lake na kuniwekea mafuta yangu ya Tshs. 5,000 nikaridhika na kimoyomoyo nikasema kuwa haya ni matokeo ya malipo duni kutoka kwa waajiri na ugumu wa maisha, mara ya pili leo (ambayo imenilazimu kuandika uzi huu mrefu), muhudumu kama kawaida kanifanyia ujanja wa kuniita pampu ya mbele halafu baadae akabadili mawazo na kuniambia nisogee nyuma ili aniwekee kutokea pampu ya nyuma (kumbe hii ilikuwa janja yake ya kunifanya nisiweze kusoma vema pale kwenye pampu).

Nami kwa haraka haraka nikakumbuka nilichofanywa mara ya kwanza, nikashuka kwenye gari na kuwahi kusoma kwenye pampu, nikakuta keshaanza kuweka mafuta na kwa sekunde kama 5 tayari pampu imeshafika Tshs 12,000, nikamwambia dada najua umeanzia kwenye elfu 10, akataka kubisha na kuwa mkali, nikamwambia ntakuharibia kazi yako kwa sababu ya Tshs. 10,000 naomba uniwekee mafuta yangu kama pesa niliyokupa. Akataharuki na kuniwekea mafuta yangu yote kulingana na pesa niliyompatia, kwahiyo kwenye pampu ikasoma Tshs 10,000 zaidi ya ile pesa niliyompa aweke mafuta na risiti nikapata ikiwa na Tshs. 10,000 zaidi.

SOMO KWA WAMILIKI WA KITUO
Tafadhali sana wamiliki wa vituo hivi, siwaingilii kwenye biashara yenu ila ni vema kuwashauri kwa ustawi wa biashara yenu: Wale wahudumu sio waaminifu, fanyeni uchunguzi wenu na mkibaini hilo chukueni hatua stahiki, kwa sababu haya wanayoyafanya yatawaharibia biashara zenu na kuleta mdororo. Walipeni vizuri, wapeni mazingira mazuri ya kazi, hakikisheni mnaweka mashine nzuri zinazosomeka kwa ufasaha bila shida.

USHAURI KWA WATUMIAJI WA HUDUMA HII
Tuwe makini wakati wa kuwekewa mafuta, tuhakiki kuwa namba zote kwenye display ya pampu zinaanzia sifuri (zero) kwenye Lita na Kiasi cha pesa. Ikiwezekana tusikubali kuwekewa mafuta mpaka tushuke na kuhakiki kuwa pampu inasomeka vema na inaonesha inaanzia sifuri. Tusiwaamini wahudumu, nao ni binadamu, wanaingiwa na majaribu na vishawishi. Kuna mbinu nyingi za udanganyi kwenye hizi pampu tushirikishane ili tupambane na kuumizana huku ambako hakuna sababu. Tumuogope Mungu na kusema ukweli wakati wote, ikiwezekana unapokutana na uovu kama huu ukomeshe kwa njia yoyote inayowezekana ili kuwaokoa wengine na udhalimu huo.

Ahsanteni sana
Asante sana kwa thread iliyoshiba na yenye maelezo mazuri
 
Hivi ni Umeandika bila kujua unachoandika na sijui hujui kweli au unafanya makusudi kupotosha ili uchangamshe jukwaa..

Wizi unaosema haupo na hakuna namna yoyote uneweza ukaibiwa Kwa staili hiyo uliyoileta .mkono wa pampu ukirudishwa kwenye mashine wakati wa kutoa unaanza zero mpaka bei uliyoset au utakapoishia

Kuibiwa ni kama ataendelea kupima bila kurudishwa mkono kwenye mashine tena ikiwa mwanzoni hakuset bei wakati anampimia mteja wa kwanza
Wewe nawe unakurupuka. Hili la kweli na kuna namna wanaweka ule mkono. Unabisha nini sasa?
 
Back
Top Bottom