World Cup 2014, Brazil: June 12 - July 13

Robben anastahili uchezaji bora wa mashindano ingawa FIFA wanaweza kumpa Messi(atakuwa kapendelewa) kama Argentina wakichukua.

Sio kama anachukua bali atachukua!!Messi kesho napiga bao na kutangazwa mchezaji bora hata ww huwezi lalamika
 
Wadau niwatakie usiku mwema,mlale unono wote,kwa wakristo msisahau kwenda kanisani asubuhi,kwa waislam muendelee na ibada njema ya funga.
Nawe pia,tukutane kesho,ili tuimbe we are the champions,ingawa sita timu,hiyo hiyo itakayoshinda nitafurahi nayo
 
Reactions: BAK

Belo yupo Sahihi,ukiondoa kuyt,RVp,Robben,Sneidner waliobaki wengi ni kama chipukizi . wasingeweza kupata wala kufikiriwa kwa Holland ya 1996-2002.In fact hata hao niliowata labda wasingeweka mguu katika Holland ya miaka hiyo.


Nyie Manure hamtupi shida hata hamfahamu maana ya chipukizi. Mbwa ukimjua jina wala hakusumbui hata mlipompa timu MoNo mlisema hivyo hivyo chacha nyege yenu ipo kwa van Gaffe khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Hii timu bora apewe Maximo sasa huyu Scholari kaishiwa mbinu, chuki zake za kukwepa wachezaji wanaomzidi umaarufu zimeighalimu timu. Alibahatika mwaka 2002 kumuacha Romario kibabe na bado akabeba kombe mwaka huu imekula kwake, natamani rais wa Brazil angekuwa Keneth Kaunda lazima angelala Segerea huyu mpuuzi.
 
Nyie Manure hamtupi shida hata hamfahamu maana ya chipukizi. Mbwa ukimjua jina wala hakusumbui hata mlipompa timu MoNo mlisema hivyo hivyo chacha nyege yenu ipo kwa van Gaffe khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Mkuu unatudharirisha Arsenal fans wengine, I feel so ashamed to have you as Arsenal fan-mate. Maybe umeanza kufuatilia soka juzi juzi ndo maana huna knowledge kubwa na umeshindwa kuelewa alichoongea Belo regardless ya tofauti ya ushabiki facts ni facts Holland imejengwa na chipukizi unless chipukizi ina maana tofauti kwako. I suggest kazania kupost picha tu.
 
Hilo nalikataa kata kata. Tuna matatizo ndiyo lakini kamwe hilo la kuwa kama wanyama mwitu siliafiki kabisa. Kwanini unapenda kujidhalilisha Mkuu?

Kwa hiyo mkuu unakataa kuwa sisi Africans kwenye soka sio kama tu wanyama mwitu?
 
Thanks wish the same to you too everlenk

Wadau niwatakie usiku mwema,mlale unono wote,kwa wakristo msisahau kwenda kanisani asubuhi,kwa waislam muendelee na ibada njema ya funga.
 
Last edited by a moderator:
Hilo nalikataa kata kata. Tuna matatizo ndiyo lakini kamwe hilo la kuwa kama wanyama mwitu siliafiki kabisa. Kwanini unapenda kujidhalilisha Mkuu?

Unakumbuka nafasi aliyo ipoteza Jordan Ayew na Germany?Angetoa ile pasi Ghana angeongoza 3-1 na mchezo ungeishia hapo na Ghana angeingia round ya pili!!
Unakumbuka vioja vya akina Yaya walipocheza na Greece?Na kikubwa zaidi unakumbuka Cameroon walipo chapana wao kwa wao siku wamecheza na Croatia?

Sasa kama wanapigana hadi ngumi wao kwa wao kwa nn wasichukue sifa ya kuitwa WANYAMA MWITU?Je huamini sample ndogo inaweza beba taswira ya bara zima?
 
Mashabiki wa bongo mnatia huruma...wapo waliotangaza toka awali kabisa kuwa bingwa wa kombe la Dunia 2014 anayesubiri tu kukabidhiwa kombe rasmi ni Brazil ; sisi wengine tunaofuatilia kandanda linavyotandazwa uwanjani tukaguna nnh! Mashabiki hao hao sasa wamegeuka wanapowaponda wachezaji wale wale wa Brazil eti kwa kuonesha viwango duni! Mimi najikuta naguna tena nnh! Najiuliza, hivi ingekuwaje kama Brazil ndio ingeifunga Ujerumani, hao akina Luiz, Marcelo, Dante, Alves, Victor na mlinda mlango Ceaser mngewaponda kweli? Kwa nini hamko tayari kukubali kirahisi kuwa timu ya Ujerumani ni timu bora kuliko ya Brazil?

Badala ya kuwakashifu hao wachezaji mnaowapenda, kwa nini msielekeze sifa pale kunakostahili kwa wachezaji wa Ujerumani? Haya, imetokea tena leo; pamoja na Silva kuwa ndani Brazil imezidi kuvuna ilichopanda, kwa nini Mholanzi asipewe sifa? Kwa nini Roben, Ron, Paul, Joel na kipa wao Michael hamuwapi haki yao? Okay kesho kuna kinyang'anyiro kingine kati ya Argentina na Ujerumani na mpaka sasa ni Ujerumani ndiyo imeonesha kiwango cha juu katika haya mashindano...nawaomba muwe tayari kupokea matokeo bila kinyongo; msiruhusu ushabiki uwafunike macho hadi mshindwe kuenjoy gozi linavyosakatwa hadi mshindi apatikane na kupongezwa. Usiku mwema!
 
Holland safi wengine tulijua tu kuwa Brazil bila mbereko mambo hayaendi na yaliyowakuta watakwenda andika kitabu kama Historia vile !
 
Ndio maana nikasema tuna matatizo lakini si ya kujifananisha na wanyama. Wanyama hawawezi kuwasumbua Wajerumani kwa 120 minutes. Waingereza pia hawakwenda popote lakini huwezi kusikia wanajifananisha na wanyama.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…