World Cup 2014, Brazil: June 12 - July 13

World Cup 2014, Brazil: June 12 - July 13

Leo mbuyu mwingine unaangushwa, utasikia ooh mwisho wa dunia wee subiri tu!. England wanafunga virago usiku huu kama wenzao Spain, wabakie wacheza mpira na sio maneno mengi.
 
kipindi kile 1990 cameroon ilikuwa ngangali, Roger Miller, Kunde, Yekeke, Mfede, Omam Biyik, Andre Biyik, Makanaki, Nkono, Ebwele
England ilibidi wapewe penati ili wasonge mbele Gary Lineker alijiangusha.

https://www.youtube.com/watch?v=xVnIzAOraiA
Ahsante sana mkuu. Hii mechi niliwahi hadithiwa tu lakini leo nimeiona mwenyewe. Kwanza nimejifunza vitu vingi, lakini kimojawapo na chenye umuhumu zaidi ni "KUJITUMA" sio siri wachezaji wazamani walikua wakijituma sana tofauti na hawa wasasa. Naimani wao waliamini ktk kuitetea heshima ya nchi yao, tofauti na wasasa wanatetea maslah yao, kwanza matumbo yao araf kisha ndio heshima ya taifa lao.
 
Lol tumemtolea nje Cesc ndo tutamchukuwa Song? nilisikia mnamtaka kumreplace Fletcher. Dah kumbe hawa wala nyani na ngedere walifungwa 4 bila. Bora nililala mapema baada ya kufungwa goli la pili.

Afadhali ulivyokwenda kulala ila ulikosa kitu kimoja tuu wabeba vyuma wa Yaounde walitaka kupigana wenyewe kwa wenyewe uwanjani wakati game inaendelea
 
Leo mbuyu mwingine unaangushwa, utasikia ooh mwisho wa dunia wee subiri tu!. England wanafunga virago usiku huu kama wenzao Spain, wabakie wacheza mpira na sio maneno mengi.

Dah tujumuike hapa pamoja wakati wa mechi hiyo ili tuuone huo "mbuyu"
 
Lol tumemtolea nje Cesc ndo tutamchukuwa Song? nilisikia mnamtaka kumreplace Fletcher. Dah kumbe hawa wala nyani na ngedere walifungwa 4 bila. Bora nililala mapema baada ya kufungwa goli la pili.
Me, nilivyoona SONG kapewa kadi ya nyekundu tu, nikazima na luninga yenyewe.
 
Africa ni kichwa cha mwendawazimu...yaani timu zote shiriki inayoleta matumaini ni ivory costs tuu..

huu ni ushenzi sanaa...ndoo mana mechi ya cameroon jana saikutaka hata kupoteza usingizi wangu...nyambafu zao...

Hivi taifa stars ndo tulikuwa tunang'ang'ania kushiriki si ingekuwa historia ya magoli kuwahi kutokea
Taifa stars hatuta shiriki michuano hii, naikitokea tukashiriki, basi mwaka huo huo tunabebe kombe
 
Kupenda kubaya eeh. Pole sana kwa kipigo cha leo!

Mkuu katafute Live statistics za mechi, nakwambia Chile iliizidi spain kwa kucheza rafu tu..otherwise Spain walikuwa juu sana isipokuwa Hawakuwa na bahati ya kufunga.

Pili hali ya hewa ya Brazil himewaathiri sana Sain kuliko Chile.

Mwisho naomba matokea ya mechi ya Cameroon
 
Leo mbuyu mwingine unaangushwa, utasikia ooh mwisho wa dunia wee subiri tu!. England wanafunga virago usiku huu kama wenzao Spain, wabakie wacheza mpira na sio maneno mengi.
Harafu hii gem itakua yakukata na mundu, kwani yeyote atakae poteza ndio mwisho wa safari yake. Binafs naimani Uruguay lazima ashinde hii gem. Sisemei ushabiki (sababu mm sizipendi tim za wazungu) lakini England hawako kitim tofauti na Uruguay. Leo Suarez anaanza huku Forlan akisubili.
 
Mkuu katafute Live statistics za mechi, nakwambia Chile iliizidi spain kwa kucheza rafu tu..otherwise Spain walikuwa juu sana isipokuwa Hawakuwa na bahati ya kufunga.

Pili hali ya hewa ya Brazil himewaathiri sana Sain kuliko Chile.

Mwisho naomba matokea ya mechi ya Cameroon
Kwenye mpira hakuna bahati, bali kuna kujua. Ukizidiwa tu basi ujue ushakalia pala. Hispania jana kacheza mpira wake uleule wa kilasiku (wakibrza meni) hajui kua watu washaistukia staili ile. Wao nakaa na mpira weeh! Wenzao wakiukamata tu wanaenda kumuona Khadija kopa.
 
Mechi ya England & Uruguay, hata nikipewa ela ya msiba, napandia Uruguay anashinda. Tena hata sare hawapati England.
 
Maumivu leo Africans yanatuanza mapema kabisa!Ivory Coast HAWEZI mfunga Colombia!
 
Mechi ya England & Uruguay, hata nikipewa ela ya msiba, napandia Uruguay anashinda. Tena hata sare hawapati England.

Coach wa Uruguay muda si mrefu kasema Suarez HAYUPO fit kucheza!Kama Suarez hachezi England anampiga au anapata sare kwa Uruguay!!
 
Ivory Coast HAIWEZI mfunga Colombia kesho maana beki yao manguvu sana lkn wana nafasi ya kusonga mbele wakimchapa Turkey mechi ya mwisho

Turkey hawapo kaka kwenye 2014 WC hii. Nadhani ulikuwa una maana ya Greece.
 
Mkuu katafute Live statistics za mechi, nakwambia Chile iliizidi spain kwa kucheza rafu tu..otherwise Spain walikuwa juu sana isipokuwa Hawakuwa na bahati ya kufunga.

Pili hali ya hewa ya Brazil himewaathiri sana Sain kuliko Chile.

Mwisho naomba matokea ya mechi ya Cameroon

What is this?
2-0 bado unaniambia aliyepigwa ndiye kacheza?Spain na mpira wao wa kuremba hauna nafasi tena ktk soka la leo!Siku hizi tunataka mido kama Pirlo inapiga pasi ndefu inakimbia inahama kutoka A kwenda B then C kwenda D!Siyo kama Xavi au Iniesta wanapiga vipasi wapo hapo hapo wanazunguka!

Best team won,hatuhesabu chenga
 
Back
Top Bottom