Wosia wa Hayati Magufuli ”Mtanikumbuka” Unatimia

We amka toka ndotoni usije ukakojoa kitandani.
Kwa taarifa yako wenye nchi washagundua kosa walilofanya, hawarudii tena kumwachia nchi mshamba kama Jiwe
 
Kibaya chajitembeza kizuri kinajiuza uyo dikteta wenu mnamtembeza sana ila bado atabaki kua dikteta,killer, mzurumu haki na Mwizi wa uchaguzi wa 2020
Wewe hujitambui,mnaotembeza na kumuenzi ni nyinyi wajaa sumu dhidi yake.

Kila anayefeli leo,miaka 2 tangu Ameondoka bado atamtaja Magufuli tu.

Kila anayetaka Political Mileage....utamsikia Akilitumia jina la Magufuli.

Nyinyi mnampaisha kila uchao.
 
Yaani hakuna kiumbe ambae huwa namdharau kama anayeongea hiki kiroja! Hiki ni kiroja kinachotumiwa sana na watu wenye uwezo dhaifu wa kujenga hoja!

Na kwavile uwezo wao wa kujenga hoja ni dhaifu sana, labda kutokana na kukosa maarifa, mara zote wanaishia kutumia cheap argument "vyeti fake", mara "wapiga deal"

What a pity!

Pamoja na udanganyifu WOTE ambao ulifanyika kwenye Uchaguzi wa 2020 lakini bado Tundu Lissu alipata karibu kura 2 MILLION.... meaning, hao wote walikuwa hawataki JPM arudi madarakani?

Sasa hao wote ni Vyeti Fake?!

Lowassa alichaguliwa na zaidi ya watu 6 MILLIONI ambao kimsingi HAWAKUTAKA JPM aingie Ikulu... wote hao ni vyeti fake na wapiga deal?!

Hakika Mtaji Mkubwa Alioacha JPM Duniani ni Jeshi Kubwa la Wajinga Aliloliacha Nyuma Yake!
 
katika ishu za demokrasia na uhai wa watu siwezi kukukumbuka chuma(uliharibu sana mzee baba)ila kwa haya yanayoendelea kuhusu mgao wa umeme, mgao wa maji,vitu kupanda bei,upigaji serikalini etc!NAKUKUKUMBUKA SANA CHUMA!ulitutendea haki sana kwenye hizi ishu!!!
 
Duh!!
 
Haijalishi watu watamponda namna gani JPM, lakini ukweli utabaki pale pale kwamba, JPM alikuwa ni Kiongozi imara mwenye UZALENDO wa kweli na Nchi yetu.

Ni Kiongozi aliyedhamiria kwa dhati kabisa kupunguza au kuondoa kabisa adha mbalimbali walizokuwa wakizipata Watanzania na hasa Watanzania wanyonge/maskini.

Ni Kiongozi pekee aliyejitahidi sana kuziba mirija ya Wapigaji hata kama alijua kufanya hivyo ni sawa kabisa na kuvaa KITANZI shingoni.

Alijua kabisa nini kitatokea lakini hakurudi nyuma. Kwa hiyo, JPM aliwapigania Watanzania mpaka TONE lake la mwisho.
Mwenyezi Mungu ailaze pema peponi roho ya JPM. Amina.
 
Sasa Mabwawa ya hydroelectric yanafunguliwa kwa kuhujumiwa kama zamani,
Ili tu walioko kwenye mfumo waendelee kuleta utitiri wa miradi ya umeme kwa 10%.
Ila kwa sasa kweli hii awamu imekuwa kama ni 'fungulia mbwa' majizi, ma-mbwa mwitu yote yameinuka!
 
Hakuna mahali utakwenda akazungumziwa mabaya.

Kila ukipita mahali wanazungumzia mazuri yake kwa usimamizi wake wa miradi ya maendeleo. Wanazungumzia uwajibikaji wake kwa wananchi. Hali ya kiuchumi , usalama wa raia na mali zao. Raia wengi wanampenda na kumkumbuka sana na wanaomba kila siku apatikane mwingine kama yeye.

Wanaomchukia na kumsema kwa mabaya ni hao wanaotumia madaraka kujinufaisha.
 
Ukweli huu ndio hawaki kabisa kuusikia walina Asali wa Msoga team!

Wao wameshindwa kazi na badala yake wanaunda makundi kumchafua JPM ili wasionekane maovu na Ufisadi wao unaoendelea kwa kasi hivi sasa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…