Ya Gekul hayajaisha, Wakili Madeleka kukata rufaa

Ya Gekul hayajaisha, Wakili Madeleka kukata rufaa

Wewe brother acha kuendelea kujishushia heshima eti na wewe ni mwanasheria .
Pumbavu sana wewe brother ni mwanasheria bwege.
Hivi hujui kuna "The African Court on Human and Peoples’ Rights".
Ndio utaratibu unafanyika kesi hii itafikishwa huko mfumo wa ndani wa kisheria usipotoa haki

The African court on Human and Peoples Rights nakumbuka Tanzania tulijitoa,kama status bado inasoma tumejitoa je communication itaenda vipi kwenye hiyo mahakama mana haina jurisdiction kwa Tanzania.
 
Acha kuwa narrow minded eti shahidi ni yule dogo tu haujui kama kuna ripoti za madaktari hata video clips za kina gekuli na pia tambua mashauri ya kisheria yanaweza kiutaratibu kupelekwa Kwenye mahakama nyingine za kimataifa mfano suala hili mahakama za ndani zikilipiga danadana linaweza kupelekwa The African Court on Human and Peoples’ Rights ambao wanaweza kulitolea maamuzi ambayo yanaweza kuiaibisha serikali
we ni mpumbavu sana. Mahakama ya Africa inaweza kumtia mtu hatiani? au ni mahakama ya rufaa? na je? maamuzi yake ni binding kwetu au persuasive? acheni kuingilia fani msizozijua.
 
Kabla hata sherehe za kufurahia Gekul kufutiwa kesi iliyomkabili , ile ya kumtumbukiza Chupa makalioni kijana mmoja huko Manyara haijaanza , Tayari Mawakili wa Mlalamikaji huyo wametangaza kukata rufaa kupinga Uamuzi wa DPP wa kuifuta kesi hiyo.

Tayari nyaraka zimeanza kukusanywa ili kulianzisha upya jambo hilo.
---
Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini imeondoa Kesi ya namba 179 ya mwaka 2023 ya shumbulio la mwili iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria ambaye ni Mbunge wa Babati Mjini Pauline Gekul ambapo upande wa Mbunge huyo ilikuwa ikiwakilishwa na wakili Ephraim Kisanga huku upande wa mlalamikaji Hashimu Ally ikiwakilishwa na mawakili watatu ambao ni Thadei Lista,Peter Madeleka na Joseph Masanja.

Kesi hii kwa mara ya kwanza imesikilizwa hii Leo katika mahakama ya wilaya ya Babati Mkoani Manyara na Hakimu wa mahakama hiyo Victor Kimario ambapo amesema kesi hiyo imeondolewa kwa mujibu wa sheria namba 91 kifungu kidogo cha( 1) cha sheria ya mwenendo wa mashauri ya jinai sura namba 20 Kama ilivyorekebishwa mwaka 2022, ambayo inampa mkurugenzi wa mashitka mamlaka ya kuondoa kesi yeyote ya jinai mahakamani kabla haijafikia hukumu.

Kwa upande wa Mawakili wa mlalamikaji wameelezwa kutokuridhishwa na kitendo kilicho endelea mahakamani hususani kufutwa kwa kesi hiyo na wameeleza kukata rufaa.
Si jambo lingine limepelekea kufutwa kwa kesi hiyo isipokua rushwa. Dpp hiyo sheria inayompa madaraka kufuta kesi bila kutoa sababu inampa fursa kua duka la kuuza haki. Hapo kuna nguvu kubwa ya vigogo imemshukia hata kama sio mapenzi yake kesi ifutwe.
Ngoja tuone nini kinaendelea ila la wazi wananchi watapata fursa tena kuona tuna utawala wa aina gani tanzania.
 
we ni mpumbavu sana. Mahakama ya Africa inaweza kumtia mtu hatiani? au ni mahakama ya rufaa? na je? maamuzi yake ni binding kwetu au persuasive? acheni kuingilia fani msizozijua.
Wewe ndiye mpumbavu kwani huko anakwenda kushtakiwa mtu.
Huko inakwenda kushtakiwa serikali iliyoamua kutokutenda haki
 
Back
Top Bottom