Nilipoandika huu Uzi nilijua tu kuwa kuna Majuha na Wapuuzi watakurupuka na Kutonielewa na ningeshangaa kama wasingejitokeza.
Jamani GENTAMYCINE sijawa Mshindi wa Jukwaa hili la Michezo ( Sports ) kwa Mwaka jana ( 2022 ) kwa Kubahatisha bali ni kwa Uwezo wangu wa Kitaarifa, Uchambuzi na Uibuaji wa Hoja Tunduizi zenye Mvuto na Ushawishi kwa Wasomaji.
Na leo narudia tena ( na hii itakuwa ni mara ya mwisho ) kuwaambieni kuwa GENTAMYCINE najuana na nipo karibu kwa 95% na Wachezaji wa Simba na Yanga na pia kwa 75% na Viongozi na Watendaji wa hivi Vilabu Vikubwa hivyo nikija na Taarifa hapa jueni kuwa nimepenyezewa na hao hao na bahati nzuri niliyonayo ni kwamba Wote nipo nao ila hawajui na hawatokuja kujua kuwa Mimi ndiyo GENTAMYCINE wa JamiiForums.
Kingine nikisema kuwa katika Soka la Tanzania ( Bongo ) kuna Michezo michafu mingi ( hasa utoaji wa Rushwa kwa Waamuzi, Wachezaji na Timu ) muwe mnanielewa kwani hata Mimi GENTAMYCINE mwaka 2012 Yanga SC ilipofungwa Goli / Bao zile 5 kwa 0 nilishiriki kwa 100% katika Umafia kwa Kushirikiana na Wachezaji Waandamizi wa Yanga SC na Kufanikiwa.
Na hapa isionekane labda GENTAMYCINE naisema tu Simba SC ( ambayo naishabikia ) ila ukweli ni kwamba hata Yanga SC nao kwa 100% wanafanya hivyo hivyo isipokuwa kwa sasa Maovu ya Yanga SC yanafichwa na Kikosi chake Imara, Mahiri na Bora tofauti na chetu Simba SC ambacho ni cha Kujitafuta ( Kibovu ) na hakitoi Matumaini yoyote yale kwa hii Misimu / Miaka miwili mfululizo.
Kilichofanyika leo ni Wachezaji wa Mtibwa Sugar FC Kupoozwa ( Kulainishwa ) na Mafia wa Simba SC ili Wasikaze na Simba SC icheze Mpira mwingi na ishinde Bao / Goli nyingi ili Kurejesha matumaini kwa Mashabiki wa Simba SC ambao 97% wameshakata Tamaa na Kuchukizwa na Soka Bovu na Ushindi wa Mungu Nisaidie ( wa Kubahatisha ) na wajitokeze kwa wingi tarehe 18 Machi, 2023 Uwanja wa Mkapa Simba SC ikicheza Mechi muhimu ( ya Kimaamuzi ) kwa CAFCL na Watu wapige Pesa kwa Nyomi litakalokuwepo.
GENTAMYCINE nawajua hadi Wachezaji waliopewa Mzigo mpaka Waratibu wa Zoezi hilo ( ambao Watatu walishawahi kuwa Wachezaji wakubwa hadi Manahodha ) na Viongozi Wawili wa Klabu hiyo ambao wamefanikisha Kimafia Simba SC kushinda leo.
Namalizia kwa kusema kuwa sikulazimishi na sijakulazimisha Uamini nilichokisema hapa ila Siku zote Silaha Kuu ya GENTAMYCINE ni Kujiamini kwa Mambo yangu na Taarifa na huwa sibahatishi / sizibahatishi kwani huwa ni za uhakika na zinatoka Jikoni kwenyewe na siyo Sebuleni au Kibarazani.
Na ukiona Umekwazika / Umechukizwa nami GENTAMYCINE kwa nilichokiandika au basi tu hunipendi kutokana na Umaarufu wangu mkubwa hapa JamiiForums au kwa Uwasilishaji wangu wa Kipekee wa Masuala Mtambuka nakurahisishia Kazi tafuta popote pale Sumu ya Panya changanya na Dawa ya Mbu katika Kikombe cha Maji kisha ukinywe ili Ufe na ukatuandalie Makazi mema Ahera.
Imeisha hiyo...........................Kudadadeki
Mimi ndiyo GENTAMYCINE The King!!!!
Cc:
KANYIMBI,
Tui,
Cashman,
Kalpana,
mganda og,
Vontec