Yajue usiyoyafahamu kuhusu Vita ya Kagera

Yajue usiyoyafahamu kuhusu Vita ya Kagera

Nimesoma stori nying za Vita ya Kagera zingine zisizokuwa na mashiko zikisema tanzania ndio tulianza chokochoko, ila ukweli ulio wazi , Iddi Amin is a mastermind his own downfall,

Kwa mujibu wa wikipedia uwiano wa kivita tu ulionyesha Iddiamin alishapigwa kabla hata ya kipenda kupulizwa

1544537997257.png


by the way nilipopitia wikipedia ya hii vita nimependa kipande hiki cha chini, watu wengi wanasema vita hii ilichangia kututia umaskini had watu wakala maharage ya njano lakini, hapo chini imeelezwa jinsi gani vita ilitutia umaskini

Tanzania
Tanzania received no help from other countries in the Organization of African Unity, which had denounced what was seen as an aggression by Tanzania (and its role as a backer of the 1977 coup in the Seychelles which brought France-Albert René to power) as a breach of national sovereignty. As a result, the government in Dar es Salaam had to foot the bill for the invasion and subsequent peacekeeping role from its own funds, further driving the country into poverty; Tanzania would not fully recover from the cost of the war until Uganda paid its debt back to Tanzania in 2007.[19]
The Tanzanian Government struck and distributed a campaign medal, known as the Nishani ya Vita. The obverse bears the inscriptions Vita-1978-1979 (top) and Tanzania (bottom). The reverse is plain.[citation needed]
 
Nyerere naye alituzingua sana, Utampaje hifadhi mtu aliyepinduliwa huku ukipanga naye njama za kumrudisha madarakani kijeshi?, huyo ambaye anakalia kiti kwa muda huo atakubali kweli?.
Halafu pia utawapaje hifadhi waasi dhidi ya serikali ya Uganda ndani ya mipaka yako?, kama huo siyo uchokozi ni kitu gani?
Hii tunayoambiwa vita ilianza 1978 hadi 1979 kumbe ilishaanza toka mwaka 1971 tulipoanza njama za kumchokonoa nduli
 
Katika toleo lililopita tulisimulia namna majeshi ya Idi Amin yalivyoivamia Tanzania Jumatatu ya Oktoba 30, 1978 kupitia Kukunga, Masanya, Mutukula na Minziro na kuua raia na hatimaye kuteka eneo la kilomita za mraba 1,800 na kutangaza kuwa mpaka halali wa Tanzania ni Mto Kagera.

Habari za kutekwa kwa Kagera zilimfikia Rais wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere ambaye siku hiyo hiyo aliwaita makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) nyumbani kwake na kukubaliana kuwa kazi ya kumng’oa Idi Amin ianze mara moja.

Siku mbili baada ya kukutana na makamanda wa Jeshi la Wananchi Novemba mosi, 1978, Mwalimu Nyerere alilitangazia Taifa kuhusu “uvamizi wa Idi Amin na uamuzi wa Tanzania wa kumpiga”. Akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwenye ukumbi wa mikutano wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, Mwalimu Nyerere alieleza uvamizi huo na jinsi Tanzania ilivyoamua kupambana na majeshi ya Idd Amin.

“Nimewaombeni mkusanyike tena hapa niwaelezeni jambo ambalo kwa sasa wote mnalijua. Lakini naona si vibaya nikieleza. Nitajaribu kueleza kwa ufupi.

“Wakati nilipokuwa ziarani Songea kuanzia juma la pili la mwezi uliopita (Oktoba), zilitangazwa habari kutoka Uganda kwamba jeshi la Tanzania limeingia Uganda na limechukua sehemu kubwa na kuua watu ovyo.

“Siku zilipotangazwa habari hizo nilikuwa nimekaribishwa chakula cha jioni na vijana wetu wa jeshi pale Songea, na nikakanusha. Na kwa kweli nikachukua nafasi hiyo kuvishutumu vyombo vya habari vya nje ambavyo vinapenda kutangazatangaza uongo wa Amin,” alisema Nyerere.

“Kila anapotangaza uongo, wao huurukia na kutangaza kama kwamba ni kweli. Huo ndio uliokuwa uongo wake wa kwanza, na aliendelea endelea.

“Baadaye akabadili sura, akaongeza uongo wa pili katika shabaha hiyohiyo kuwa Watanzania wanaua watu ovyo na kwamba wanasaidiwa na majeshi kutoka Cuba. Uongo huo nao tukaukanusha.

“Kwa hivyo, alivyozidi kusema habari hizo za uongo tuliendelea kuzikanusha na kuzipuuza. Lakini Alhamisi akatuma ndege za kivita Bukoba. Vijana wetu walizitupia risasi zikakimbia. Siku hiyohiyo ikarudi tena moja, ikaangushwa.

“Ijumaa zikaja ndege eneo la Kyaka. Zikatupa mabomu. Vijana wetu walizitupia risasi, na mbili zikaangushwa.”

Nyerere pia alizungumzia ndege za Tanzania zilizopotea uwanjani wakati zikitoka Dar es Salaam kwenda Mwanza ambazo kutokana na kasi yake zilihisiwa kuwa ni za adui na kutunguliwa. Nyerere alisema Tanzania imechoshwa na uongo huo wa Idi Amin na hivyo wameamua zikionekana ndege za kivita, zitunguliwe.

“Kwa hiyo vijana wetu wamekwishaambiwa kuwa ndege za kivita zikionekana, zipigwe. Kama vile zile za Bukoba na Kyaka zilipigwa, basi na hizi zikapigwa zilipofika Musoma. Walidhani ni za adui. Tukapoteza ndege tatu,” alisema Nyerere.

“Lakini katika mambo ya vita ajali hutokea. Na vijana hawa walishaambiwa ndege zikionekana zipigwe. Wangeziacha? Wanajuaje ni za adui? Kwa hiyo ikatokea bahati hiyo mbaya.

“Matukio haya hatukuyatangaza. Hata kule kupigwa kwa ndege za Amin hatukutangaza. Hatukutangaza kwa sababu hatukutaka jambo lenyewe kulipa uzito mno. Tulisema akiendeleaendelea kuleta ndege zake, tutaendelea kuziangusha kila zinapokuja.

“Uwezo wa kuziangusha upo, na mwenyewe alijua uwezo upo. Ni vizuri akijua yeye. Tulijaribu. Tulikuwa tunaepuka kulipa uzito jambo lenyewe ambalo mwanzo wake ni uongo kabisa wa kuzua.”

Nyerere alisema jinsi Idd Amin alivyoendelea kuidanganya dunia na jinsi Tanzania ilivyomjibu hadi alipoamua kuvamia.

“Sasa Jumatatu ndiyo akaivamia nchi yetu. Akaingiza majeshi yake kwa nguvu, nguvu kubwa. Yakachukua sehemu kubwa. Yakaingia ndani mpaka Kyaka. Hii tukatangaza kwa sababu lilikuwa ni jambo la kweli na yeye kama kawaida yake akakana akasema haikutokea hivyo,” alisema Nyerere.

“Akaendelea kusema kwamba Watanzania ndio wako Uganda, ndio wamechukua sehemu ya Uganda. Akakana ukweli huo. Lakini tukawaeleza jamaa na mabalozi walioko Dar es Salaam kuwa huo ndio ukweli.

“Huyu mtu ameivamia nchi yetu. Sasa jana ametangaza mwenyewe kwamba ni kweli majeshi yake yameivamia nchi yetu na yamechukua sehemu hiyo ya Tanzania iliyoko kaskazini mwa Mto Kagera na kwamba tangu sasa, eti sehemu hiyo ni ya Uganda na itatawaliwa kijeshi kama Uganda inavyotawaliwa.”

Alisema kauli hiyo ya Idi Amin iliisaidia Tanzania kutangaza kutokea kwa uvamizi huo.

“Sasa hiyo ndiyo hali. Tufanye nini! Tunayo kazi moja tu. Watanzania sasa tunayo kazi moja tu—ni kumpiga,” alisema Mwalimu Nyerere.

“Uwezo wa kumpiga tunao. Sababu ya kumpiga tunayo, na nia ya kumpiga tunayo. Tunataka dunia ituelewe hivyo. Kwamba hatuna kazi nyingine.

“Na tunaomba marafiki zetu wanaotuomba maneno ya suluhu, waache maneno hayo. Kuchukua nchi ya watu wengine siyo kwamba majeshi yamekosea njia na kusema kuwa sasa sehemu hiyo umeichukua na kutangaza vita kwa nchi ile nyingine. Si sisi tuliofanya hivyo. Amefanya hivyo mwendawazimu.

“Na amefanya hivyo kwa jambo ambalo aliwahi kutangaza zamani. Aliwahi kusema zamani kidogo kuwa mpaka wa haki wa Uganda na Tanzania ni Mto Kagera, na kuwa siku moja atachukua sehemu hiyo. Ametimiza hivyo.”

Nyerere aliwaomba marafiki wa Tanzania kuielewa hali hiyo na kuisaidia katika kuyaondoa majeshi ya Uganda na kwamba wale waliokuwa wakitaka suluhu haitawezekana.

“Hatukupenda kufanya hivyo. Maadui zetu ni mabeberu, na kwa hivi sasa wako Kusini. Serikali ya Afrika, hata kama hatupendi matendo ya viongozi wao, hatuwahesabu kama adui wetu,” alisema Nyerere.

“Na kama Amin angekuwa amesema tu kwamba Tanzania ni adui wetu, sisi tungeendelea kumpuuza kama ni maneno hayo. Lakini kafanya kitendo cha uadui, hatuwezi.

“Ameingia Tanzania mwenyewe. Na mtu huyu ni mshenzi. Ameua watu wengi sana. Kwa hiyo nasema tuna kazi moja tu. Tutampiga. Vijana wetu wako mpakani sasa hivi. Wako kule. Wako kule na mapambano yanaendelea.

“Sasa hayo si mapambano ya TPDF peke yake, ni yetu wote. Kwa hiyo ninachowaombeni wananchi, hiyo kazi iliyoko mbele yetu muielewe.

“Pili, tuwasaidie vijana wetu. Kila mtu kwa mahali alipo. Tutaendelea na kila mapambano yanavyoendelea kueleza nini la kufanya na nani afanye nini.

“Tutaelezana wakati wote huo mpaka tumemuondoa huyu nyoka katika nyumba yetu. Na tunawaomba mtulie. Katika mambo haya ya vita, na hasa kama watu mlikuwa mmezoea amani mnaweza kubabaika sana.

“Msibabaike, tulieni. Fanyeni kazi kama kawaida. Lakini mjue vitendo hivyo kazi yake ni hiyo moja; kumpiga mshenzi huyu aliyekuja katika nchi yetu.”

Itaendelea kesho

Source Gazeti la Mwananchi la leo.
 
Jana tuliona jinsi majeshi ya Idi Amin wa Uganda yalivyoshambulia ardhi ya Tanzania na jinsi kiongozi huyo wa Uganda alivyokuwa akiiambia dunia kuhusu mashambulizi hayo. Kitendo hicho kilimuudhi Rais wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere ambaye aliamua kuitisha mkutano wa viongozi mkoani Dar es Salaam na kutoa ile hotuba maarufu ya “sababu za kumpiga tunazo, nia ya kumpiga tunayo na uwezo wa kumpiga tunao”. Mwalimu Nyerere alielezea kwa kina jinsi Tanzania ilivyopuuzia madai ya Idi Amin hadi alipofanya uamuzi huo wa kujibu mashambulizi. Sasa endelea...

SEHEMU YA NNE (4)

Baada ya amri ya Rais Julius Nyerere aliyoitoa Jumatatu ya Oktoba 30, 1978 ya kutaka Jeshi la Wananchi (JWTZ) kuingia vitani, Brigedi ya Kusini ilipewa jukumu la kuanza kujibu mashambulizi.

Brigedi ya Kanda ya Kusini iliyokuwa na makao yake huko Songea, chini ya Brigedia James Luhanga, ilikuwa na wapiganaji kati ya 4,000 na 5,000. Kwa mujibu wa gazeti The Citizen la Oktoba 14, 2014, halikuwa jambo la bahati mbaya kwamba brigedi hiyo kuwa tayari kwa vita.

“Brigade hii ilikuwa imeandaliwa ili baadaye iweze kutumwa nchini Namibia kujiunga na askari wa msituni wa Swapo,” linaandika gazeti hilo.

Brigedi hiyo ilianza safari Alhamisi ya Novemba 2, 1978, siku ambayo Mwalimu Nyerere alikuwa akilitangazia taifa kuhusu “uvamizi wa Idi Amin na uamuzi wa Tanzania kumpiga”.

Askari wa brigedi hiyo walilazimika kusafiri na zana zao za kivita kwa umbali wa kilometa 1,600 kutoka Songea hadi uwanja wa vita.

Baada ya safari hiyo ya tabu kubwa kutokana na mvua iliyokuwa inanyesha na barabara kuharibika vibaya, wanajeshi waliwasili na mara moja kuanza kuchimba mahandaki kwa ajili ya kujihifadhi kwa shambulizi lolote la anga ambao halikutarajiwa.

Mjini Dar es Salaam, Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine alitoa maelekezo kwa wakuu wote wa mikoa 20 ya Tanzania kuhamasisha matumizi ya mali za serikali na za watu binafsi kutumika katika vita.

Mabasi na malori kutoka serikalini na kwa kampuni binafsi yalitumika kupeleka wapiganaji na vifaa kwenye viwanja vya vita. Kwa watu waliokuwa na magari mabovu waliiona fursa hiyo kwa sababu magari yao yalifanyiwa matengenezo.

Ingawa yaliteka eneo la Kagera kwa urahisi, majeshi ya Idi Amin yalihofia sana Jeshi la Tanzania kujibu mapigo. Waandishi wa kitabu cha Deadly Developments, Stephen na Downs Reyna wameandika katika ukurasa wa 117 kuwa kwa kuhofia hilo, wanajeshi wa Uganda waliamua kulipua daraja la Mto Kagera eneo la Kyaka.

Toleo la 348 la jarida New African liliandika kuwa “huu ulikuwa mwanzo wa mwisho wa utawala wake (Idi Amin)” nchini Uganda.

Luteni Kanali Marajani wa Uganda alitumia ndege za MiG kulipua daraja hilo. Kazi hiyo ilifanyika Novemba 1 na 2, lakini walishindwa kuliharibu daraja hilo la Kagera. Wanajeshi wa Tanzania walizirushia makombora na baadhi ya ndege hizo zilitunguliwa. Marubani waliobakia wakavunjika moyo wa kuendelea na kazi hiyo.

Baadaye Marajani akapata wazo la kutumia bomu la kutegwa. Akaenda machimbo ya shaba ya Kilembe, kiasi cha kilometa 225 kwenye milima ya Ruwenzori. Meneja wa machimbo hayo, ambaye alikuwa Mwingereza, alikubali na akatuma timu yake ya wataalamu kwenda kutega mabomu daraja la Mto Kagera.

Usiku wa Ijumaa ya Novemba 3, 1978, wategaji wa mabomu hayo walifika darajani na kufanya kazi hiyo bila kuonekana. Kabla ya kupambazuka daraja likawa limelipuliwa. Mmoja wa wanajeshi wa Uganda aliyekuwa na watega mabomu hayo ni Sajini Kifulugunyu.

Kifulugunyu aliliambia gazeti Daily Monitor la Uganda (Aprili 23, 2016) kwamba wataalamu hao wa mabomu walikuwa watatu, lakini utafiti wa gazeti hilo uligundua kuwa walikuwa wanne—Muitaliano mmoja na Waganda wanne.

Baada ya hapo, ilikuwa ni furaha tele.

“Tulifanya sherehe hapa hadi Kampala. Tuliridhika kuwa Jeshi la Tanzania halingeweza kutushambulia tena baada ya kuharibu daraja ambalo wangetumia kuvuka na kuingia Uganda,” Kifulugunyu aliliambia gazeti hilo.

Mmoja wa marubani waliotumika kujaribu kulilipua daraja hilo ni Meja John Amunga (maarufu kwa jina la Kassim Semugabi). Alikuwa mmoja wa marubani bora zaidi wa kijeshi wa Jeshi la Uganda, akiendesha ndege aina ya MiG-21. Wanajeshi wenzake walimbatiza jina la “Mharibifu wa Tanzania”.

Mwingine alikuwa ni John Carse kutoka Seychelles na ambaye alikuwa ni mtaalamu wa ubomoaji. Ndiye anayedaiwa kuwa alilipua daraja hilo.

Lakini, katika ukurasa wa 149-150 wa kitabu cha Guardian Angel: The Moshi Conspiracy kilichoandikwa na Arnold Spero Bisase, kuna maelezo tofauti.

Aliyekuwa mfungwa wa Tanzania ambaye hakutaka jina lake litajwe, na ambaye wakati kitabu hicho kinaandikwa mwaka 2012 alikuwa anaishi nchi za Scandinavia, alimwambia mwandishi wa kitabu hicho kuwa aliwahi kuwa katika gereza moja na John Carse mkoani Dodoma ambako aligundua kuwa raia huyo wa Seychelles hakuhusika kulipua daraja hilo.

Siku daraja hilo lilipolipuliwa, JWTZ ilikumbana na kikwazo kingine. Ndege zake tatu zilikuwa zikitoka uwanja wa ndege wa Ngerengere mkoani Morogoro kuelekea Mwanza, zikapita juu ya Ziwa Victoria ambako askari wa JWTZ walishaambiwa wakae chonjo.

Kitengo cha Musoma hakikuwa na taarifa ya kuwasili kwa ndege hizo. Ndege zote tatu zililipuliwa kwa makombora na kuua marubani wake.

Akilitangazia Taifa tukio hilo, kwa masikitiko Mwalimu Julius Nyerere alisema: “Katika mambo ya vita ajali hutokea, na vijana hawa walikwishaambiwa ndege zikionekana zipigwe. Wangeziacha? Wanajuaje ni za adui? Kwa hiyo ikatokea bahati mbaya hiyo.

“Matukio haya hatukuyatangaza. Hata kule kupigwa kwa ndege za Amin hatukutangaza. Hatukutangaza kwa sababu hatukutaka jambo lenyewe kulipa uzito mno. Tulisema akiendeleaendelea kuleta ndege zake, tutaendelea kuziangusha kila zinapokuja.”

Mara baada ya maneno hayo, alipanda ndege kwenda Beira, Msumbiji kukutana na Rais Samora Machel na kushauriana juu ya uvamizi wa Idi Amin. Nyerere alimwambia Machel kuwa kikosi cha Jeshi la Tanzania kilichokuwa kwenye mpaka wa Msumbiji na Rhodesia (Zimbabwe) kilirudi Tanzania kwa ajili ya Vita ya Kagera.

Itaendelea kesho

Source Gazeti la Mwananchi la leo.
IMG_20181213_105041.jpeg
 
Jana tuliona jinsi majeshi ya Idi Amin wa Uganda yalivyoshambulia ardhi ya Tanzania na jinsi kiongozi huyo wa Uganda alivyokuwa akiiambia dunia kuhusu mashambulizi hayo. Kitendo hicho kilimuudhi Rais wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere ambaye aliamua kuitisha mkutano wa viongozi mkoani Dar es Salaam na kutoa ile hotuba maarufu ya “sababu za kumpiga tunazo, nia ya kumpiga tunayo na uwezo wa kumpiga tunao”. Mwalimu Nyerere alielezea kwa kina jinsi Tanzania ilivyopuuzia madai ya Idi Amin hadi alipofanya uamuzi huo wa kujibu mashambulizi. Sasa endelea...

SEHEMU YA NNE (4)

Baada ya amri ya Rais Julius Nyerere aliyoitoa Jumatatu ya Oktoba 30, 1978 ya kutaka Jeshi la Wananchi (JWTZ) kuingia vitani, Brigedi ya Kusini ilipewa jukumu la kuanza kujibu mashambulizi.

Brigedi ya Kanda ya Kusini iliyokuwa na makao yake huko Songea, chini ya Brigedia James Luhanga, ilikuwa na wapiganaji kati ya 4,000 na 5,000. Kwa mujibu wa gazeti The Citizen la Oktoba 14, 2014, halikuwa jambo la bahati mbaya kwamba brigedi hiyo kuwa tayari kwa vita.

“Brigade hii ilikuwa imeandaliwa ili baadaye iweze kutumwa nchini Namibia kujiunga na askari wa msituni wa Swapo,” linaandika gazeti hilo.

Brigedi hiyo ilianza safari Alhamisi ya Novemba 2, 1978, siku ambayo Mwalimu Nyerere alikuwa akilitangazia taifa kuhusu “uvamizi wa Idi Amin na uamuzi wa Tanzania kumpiga”.

Askari wa brigedi hiyo walilazimika kusafiri na zana zao za kivita kwa umbali wa kilometa 1,600 kutoka Songea hadi uwanja wa vita.

Baada ya safari hiyo ya tabu kubwa kutokana na mvua iliyokuwa inanyesha na barabara kuharibika vibaya, wanajeshi waliwasili na mara moja kuanza kuchimba mahandaki kwa ajili ya kujihifadhi kwa shambulizi lolote la anga ambao halikutarajiwa.

Mjini Dar es Salaam, Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine alitoa maelekezo kwa wakuu wote wa mikoa 20 ya Tanzania kuhamasisha matumizi ya mali za serikali na za watu binafsi kutumika katika vita.

Mabasi na malori kutoka serikalini na kwa kampuni binafsi yalitumika kupeleka wapiganaji na vifaa kwenye viwanja vya vita. Kwa watu waliokuwa na magari mabovu waliiona fursa hiyo kwa sababu magari yao yalifanyiwa matengenezo.

Ingawa yaliteka eneo la Kagera kwa urahisi, majeshi ya Idi Amin yalihofia sana Jeshi la Tanzania kujibu mapigo. Waandishi wa kitabu cha Deadly Developments, Stephen na Downs Reyna wameandika katika ukurasa wa 117 kuwa kwa kuhofia hilo, wanajeshi wa Uganda waliamua kulipua daraja la Mto Kagera eneo la Kyaka.

Toleo la 348 la jarida New African liliandika kuwa “huu ulikuwa mwanzo wa mwisho wa utawala wake (Idi Amin)” nchini Uganda.

Luteni Kanali Marajani wa Uganda alitumia ndege za MiG kulipua daraja hilo. Kazi hiyo ilifanyika Novemba 1 na 2, lakini walishindwa kuliharibu daraja hilo la Kagera. Wanajeshi wa Tanzania walizirushia makombora na baadhi ya ndege hizo zilitunguliwa. Marubani waliobakia wakavunjika moyo wa kuendelea na kazi hiyo.

Baadaye Marajani akapata wazo la kutumia bomu la kutegwa. Akaenda machimbo ya shaba ya Kilembe, kiasi cha kilometa 225 kwenye milima ya Ruwenzori. Meneja wa machimbo hayo, ambaye alikuwa Mwingereza, alikubali na akatuma timu yake ya wataalamu kwenda kutega mabomu daraja la Mto Kagera.

Usiku wa Ijumaa ya Novemba 3, 1978, wategaji wa mabomu hayo walifika darajani na kufanya kazi hiyo bila kuonekana. Kabla ya kupambazuka daraja likawa limelipuliwa. Mmoja wa wanajeshi wa Uganda aliyekuwa na watega mabomu hayo ni Sajini Kifulugunyu.

Kifulugunyu aliliambia gazeti Daily Monitor la Uganda (Aprili 23, 2016) kwamba wataalamu hao wa mabomu walikuwa watatu, lakini utafiti wa gazeti hilo uligundua kuwa walikuwa wanne—Muitaliano mmoja na Waganda wanne.

Baada ya hapo, ilikuwa ni furaha tele.

“Tulifanya sherehe hapa hadi Kampala. Tuliridhika kuwa Jeshi la Tanzania halingeweza kutushambulia tena baada ya kuharibu daraja ambalo wangetumia kuvuka na kuingia Uganda,” Kifulugunyu aliliambia gazeti hilo.

Mmoja wa marubani waliotumika kujaribu kulilipua daraja hilo ni Meja John Amunga (maarufu kwa jina la Kassim Semugabi). Alikuwa mmoja wa marubani bora zaidi wa kijeshi wa Jeshi la Uganda, akiendesha ndege aina ya MiG-21. Wanajeshi wenzake walimbatiza jina la “Mharibifu wa Tanzania”.

Mwingine alikuwa ni John Carse kutoka Seychelles na ambaye alikuwa ni mtaalamu wa ubomoaji. Ndiye anayedaiwa kuwa alilipua daraja hilo.

Lakini, katika ukurasa wa 149-150 wa kitabu cha Guardian Angel: The Moshi Conspiracy kilichoandikwa na Arnold Spero Bisase, kuna maelezo tofauti.

Aliyekuwa mfungwa wa Tanzania ambaye hakutaka jina lake litajwe, na ambaye wakati kitabu hicho kinaandikwa mwaka 2012 alikuwa anaishi nchi za Scandinavia, alimwambia mwandishi wa kitabu hicho kuwa aliwahi kuwa katika gereza moja na John Carse mkoani Dodoma ambako aligundua kuwa raia huyo wa Seychelles hakuhusika kulipua daraja hilo.

Siku daraja hilo lilipolipuliwa, JWTZ ilikumbana na kikwazo kingine. Ndege zake tatu zilikuwa zikitoka uwanja wa ndege wa Ngerengere mkoani Morogoro kuelekea Mwanza, zikapita juu ya Ziwa Victoria ambako askari wa JWTZ walishaambiwa wakae chonjo.

Kitengo cha Musoma hakikuwa na taarifa ya kuwasili kwa ndege hizo. Ndege zote tatu zililipuliwa kwa makombora na kuua marubani wake.

Akilitangazia Taifa tukio hilo, kwa masikitiko Mwalimu Julius Nyerere alisema: “Katika mambo ya vita ajali hutokea, na vijana hawa walikwishaambiwa ndege zikionekana zipigwe. Wangeziacha? Wanajuaje ni za adui? Kwa hiyo ikatokea bahati mbaya hiyo.

“Matukio haya hatukuyatangaza. Hata kule kupigwa kwa ndege za Amin hatukutangaza. Hatukutangaza kwa sababu hatukutaka jambo lenyewe kulipa uzito mno. Tulisema akiendeleaendelea kuleta ndege zake, tutaendelea kuziangusha kila zinapokuja.”

Mara baada ya maneno hayo, alipanda ndege kwenda Beira, Msumbiji kukutana na Rais Samora Machel na kushauriana juu ya uvamizi wa Idi Amin. Nyerere alimwambia Machel kuwa kikosi cha Jeshi la Tanzania kilichokuwa kwenye mpaka wa Msumbiji na Rhodesia (Zimbabwe) kilirudi Tanzania kwa ajili ya Vita ya Kagera.

Itaendelea kesho

Source Gazeti la Mwananchi la leo.View attachment 966708
Dah mkuu kwanini waileta vipande vipande?
 
Duuuhh kumbe mapenzi ndiyo yamesababisha hasara yote hii, binti huyu Mtanzania aliitwa nani na bado mzima? Na huyo askari wa Uganda je bado yupo? Hakika hawa sio watu wa kawaida. Wametengeneza historia.
 
Sorry wakuu nilipata shida kidogo kupata sehem ya 5. Endeleeni na hii sehem ya sita wakati nafanya mchakato.

SEHEM YA 6

Usiku wa Jumanne ya kuamkia Novemba 15, 1978, kikosi cha kwanza cha askari wa Tanzania, kikiwa chini ya Luteni Kanali Benjamin Noah Msuya, kilivuka Mto Kagera kwa mashua ndogo na kuingia ng’ambo ya pili.

Hadi kufikia wakati huo (wa kuvuka mto), zaidi ya Watanzania 1,000 walikuwa wameuawa, alisema Msuya katika mahojiano na gazeti The Monitor la Uganda la Jumamosi ya Mei 3, 2014 nyumbani kwake Kunduchi, Dar es Salaam.

Msuya aliongoza batalioni ya 19 ya JWTZ iliyokuwa chini ya Brigedi ya 208 iliyoongozwa na Brigedia Jenerali Mwita Marwa. Kazi yake ilikuwa ni kuivamia na kuitwaa Kampala, lengo ambalo hatimaye lilifikiwa Jumanne ya Aprili 10, 1979.

Baada ya kufanikiwa, Luteni Kanali Msuya akaitawala Kampala kama meya wake na pia kama rais wa Uganda kwa siku tatu hadi nchi hiyo ilipompata Yusuf Kironde Lule kuwa rais.

Alfajiri ya Jumapili ya Novemba 19, Luteni Kanali Msuya alituma kikosi kingine cha askari kwenda ng’ambo ya Mto Kagera, kikitumia mashua nyingine ndogo. Huko walishangazwa sana kuona uporaji na mauaji yaliyofanywa na askari wa Idi Amin.

Miili ya Watanzania waliouawa na majeshi ya uvamizi ilikuwa imeshaanza kuoza. Kikosi hicho kiligundua kuwa miili mingine ilikuwa imekatwa viungo, ishara kwamba wengi wao waliteswa kabla ya kuuawa.

Serikali ya Tanzania ilisema kiasi cha wakazi 40,000 walivuka Mto Kagera kukimbia majeshi ya Uganda, wakiacha kiasi cha raia kati ya 5,000 na 10,000 wakihofiwa kuuawa.

Miongoni mwao, kwa mujibu wa gazeti la Serikali la Daily News, walikuwako Watanzania 485 waliopelekwa gereza la Mutukula upande wa Uganda, ambako waliuawa kwa kulipuliwa kwa baruti.

Habari iliyoandikwa na John Darntonnov kwenye gazeti The New York Times la Alhamisi ya Novemba 23, 1978 inasema katika maeneo yaliyovamiwa na majeshi ya Idi Amin, hasa ya biashara, “kitu pekee chenye uhai kilichoonekana (baada ya uvamizi) ni mbwa mweusi aliyekonda” baada ya raia Watanzania wengi kuyakimbia majeshi ya Idi Amin.

Maduka yote, kwa mujibu wa The New York Times, yaliporwa.

“Katika duka moja lililoporwa, kilichokuwa kimesalia dukani hapo ni picha ya harusi ya mmiliki wa duka, Zaharan Salum na bibi harusi wake, ambayo ilikuwa inaning’inia ukutani,” liliandika gazeti hilo.

Kati ya ng’ombe 12,000 waliokuwa ranchi ya Narco, ni ng’ombe 100 tu walisalia baada ya wengine kuporwa. Wamiliki wa ranchi hiyo, ambao ni raia wa Australia, hawakuonekana baada ya uporaji huo na ilihofiwa kuwa nao waliuawa. Kiwanda ha sukari cha Kagera na shamba la miwa, viliteketezwa.

Doria ya Luteni Kanali Msuya ilifika hadi mpakani mwa Uganda Jumatano ya Novemba 22. Kwa wakati wote huo askari wa Amin hawakuonekana. Lakini doria hiyo ilipofika eneo la Minziro, iliona kiasi cha askari 30 wa Amin na vifaru viwili vikiwa eneo la kanisa. Askari hao wa doria hawakufanya shambulio lolote bali walirudi hadi Kyaka.

Ijumaa ya Novemba 24, vikosi kadhaa vya JWTZ, vikiongozwa na mabrigedia watatu; James Luhanga, Mwita Chacha Marwa na Silas Mayunga vikawa vimetanda kuzingira maeneo yaliyotekwa.

Siku hiyo hiyo daraja la dharura la Mto Kagera likaanza kujengwa kwa ajili ya kuvusha vifaru na zana nyingine za kivita. Kazi hiyo ilikamilika na siku iliyofuata na zana za kivita zikaanza kuvushwa.

Wakati daraja la dharura likijengwa, Rais Nyerere alizuru eneo hilo. Ingawa awali makamanda wa JWTZ walitaka kumzuia. Akiwa uwanja wa vita, alitumia darubini kutazama wapiganaji wa Amin wakiwa vilimani, umbali wa kilometa kumi kutoka mpakani, tayari kuishambulia Tanzania.

Ziara hiyo ya Nyerere ilimshawishi kukubaliana na makamanda wa JWTZ kuwa eneo la Kagera haliko salama na kwamba ili usalama uwepo, ilikuwa ni lazima jeshi la Tanzania livuke mpaka.

Usiku wa Jumapili ya Novemba 21, 1971 askari wa Tanzania walivuka mpaka na kuingia Uganda. Kikosi cha kwanza kilisaidiwa na vifaru na kiliongozwa na Luteni Kanali Salim Hassan Boma.

Vikosi kadhaa vilijizatiti maeneo ya misitu kuzunguka mji wa Mutukula. Kabla ya kupambazuka, kikosi kimojawapo kilichoongozwa na Luteni Kanali Salim Hassan Boma, kikisaidiwa na vifaru, kilitembea katika barabara kuu ya kuelekea Mutukula. Hii ilikuwa ni mbinu ya kuwavuta adui na ilifanikiwa.

Wakati majeshi ya Idi Amin yakifuatilia nyendo za kikosi cha Luteni Kanali Boma kilichokuwa mbele yao, yalishtukiwa yakishambuliwa na kikosi kingine cha JWTZ kutoka nyuma yao. Kwa jinsi askari wa Idi Amin walivyopagawa, walilazimika kukimbia na kutelekeza silaha zao.

Kwa njia hiyo JWTZ ikajipatia silaha mbalimbali kuanzia vifaru hadi bunduki za kawaida. Katika mapambano hayo, kikosi cha Luteni Kanali Boma kilipoteza wanajeshi watatu na wengine kadhaa kujeruhiwa. Hata hivyo, bila ujasiri huo ilikuwa ni vigumu kuvunja ngome ya jeshi la Uganda katika vilima vya eneo hilo.

Kwenye mapigano ya Mutukula, idadi kubwa ya raia waliuawa.

“Kila kitu kiliharibiwa na kila kilichokuwa na uhai kiliuawa,” imeandikwa katika kitabu cha War in Uganda.

“Mabuldoza yalifukia nyumba zote za udongo. Vikongwe ambao hawakuweza kukimbia waliuawa kwa kupigwa risasi. Kufikia mchana (Jumatano ya Novemba 22, 1978) Mutukula haikuwapo tena isipokuwa kwenye ramani.”

Jeshi la Tanzania “lilianza kulipiza kisasi kwa namna isiyotofautiana na ile ya Idi Amin” wakati akiteka eneo la Kagera.

Habari za ushindi wa kuitwaa Kagera zilimfariji Mwalimu Nyerere, lakini inasemekana, hakufurahishwa na habari za mauaji yaliyofanywa na jeshi lake.

Baadaye Nyerere alitoa amri ya maandishi kwa jeshi lake litofautishe jeshi na raia na mali zao. Vyovyote iwavyo, ushindi wa kwanza ukawa umepatikana kwa kuikomboa Mutukula.

Soma zaidi: VITA VYA KAGERA: Nyerere, Samora wakubaliana kumpiga Idi Amin-5

Siku JWTZ ilipovuka mpaka, Serikali ya Uganda ilitangaza kuwa wanajeshi zaidi ya 1,000 wa Tanzania wameingia maili 100 ndani ya Uganda na kuteka miji mitatu ya Kyotera, Kakuto na Kalisizo.

Itaendelea kesho
 
Jana tuliona habari za ushindi wa kuitwaa Kagera zilivyomfariji Mwalimu Nyerere, lakini inasemekana, hakufurahishwa na habari za mauaji yaliyofanywa na jeshi lake. Baadaye Nyerere alitoa amri ya maandishi kwa jeshi lake litofautishe jeshi na raia na mali zao. Vyovyote iwavyo, ushindi wa kwanza ukawa umepatikana kwa kuikomboa Mutukula. Siku JWTZ ilipovuka mpaka, Serikali ya Uganda ilitangaza kuwa wanajeshi zaidi ya 1,000 wa Tanzania wameingia maili 100 ndani ya Uganda na kuteka miji mitatu ya Kyotera, Kakuto na Kalisizo.

SEHEMU YA 7

Miezi miwili ya mwanzo wa vita ilikuwa ni ya kuongeza idadi ya wanajeshi jeshini. Katika lile juma la kwanza vikundi vya wanamgambo vilianza kufanya mazoezi baada ya saa za kazi.

Miongoni mwa wanamgambo hawa walikuwamo wakulima wadogo na wale ambao hawakuwa na ajira. Jeshi la Polisi lilichangia askari wake kiasi cha 2,000.

Juma moja baada ya uvamizi wa Uganda wakuu wa mikoa yote 20 ya Tanzania walikutana mjini Dodoma kujadiliana kuhusu uandikishaji wa wapiganaji. Kila mkoa ulipewa idadi ya kikomo cha wapiganaji 2,000 na wakuu hao walipewa maelekezo ya kuwapokea wale tu ambao walikuwa wamehitimu mafunzo ya mgambo.

Pamoja na hayo, mkuu wa Mkoa wa Mara alipotangaza mkoani mwake kuwa yeyote ambaye anataka kujiunga na jeshi ajitokeze, wananchi wengi walimiminika kwenye vituo vya kuandikishwa. Vituo vya kijeshi mkoani Mara vilielemewa na idadi kubwa ya waombaji, mwishowe Rais Nyerere alikwenda mwenyewe mkoani humo kulikabili tatizo hilo.

Hatimaye mkoa huo ulikubaliwa kuandikisha wapiganaji 4,000 badala ya 2,000 wa kikomo waliokubaliwa awali, ilimradi tu hawakuwa na tatizo la akili, wana elimu ya angalau darasa la saba na ni wanachama wa CCM.

Kwa kutumia utaratibu huo wanamgambo 40,000 waliingizwa jeshini na kufanya idadi ya wapiganaji kufikia 75,000—au zaidi. Hatimaye wapiganaji 45,000 wa Tanzania wakaingia Uganda.

Ingawa wanamgambo wanawake nao walipata mafunzo ya kijeshi sawasawa na wale wa wanaume, hakuna mgambo mwanamke aliyeingia jeshini kupigana vita isipokuwa tu wale waliotumika kama wauguzi.

Mara baada ya uvamizi wa Kagera, Tanzania ilianza kuwahamasisha Waganda waliompinga Idi Amin kupigana dhidi ya Idi Amin. Kufikia hatua hii, mkataba wa Mogadishu— ambao ulilitaka jeshi letu kukaa umbali wa kilomita 16 au zaidi kutoka kwenye mpaka wa Uganda—ukawa umekufa rasmi.

Mkataba huo ulioitwa ‘Mazungumzo ya Mogadishu’ uliafikiwa nchini Somalia Alhamisi ya Oktoba 5, 1972. Ulikuwa ni sehemu ya usuluhishi wa mgogoro kati ya Tanzania na Uganda. Somalia iliepusha vita kati ya Tanzania na Uganda kwa miaka sita tangu 1972 hadi ilipokuja kuzuka baadaye mwaka 1978 na sasa, wakati vita inaendelea, ukawa hauna kazi tena.

Walioshiriki katika mazungumzo hayo ni mawaziri wa mambo ya nje ambao ni John Samuel Malecela (Tanzania), Joshua Wanume Kibedi (Uganda) na Umar Arteh Ghalib au Omer Carte Qalib (Somalia). Mwingine aliyeshiriki ni Katibu Mkuu wa OAU, Nzo Ekangaki.

Kufikia hatua hii Rais Nyerere alisema waziwazi kuwa anaunga mkono wanaompinga Idi Amin na kwamba angetoa mafunzo, silaha na fedha kwa Waganda wowote ambao wangekuwa tayari kwenda Uganda kumpiga.

Wito huo uliitikwa na makundi mbalimbali. Wengine walikuwa wanaishi nchini Tanzania, Kenya, Zambia, nchi za Ulaya na Amerika pamoja na Waganda waliokuwa ndani ya Uganda kwenyewe.

Baadhi ya hawa hawakuwa wapiganaji. Wengine walikuwa wafanyabiashara, walimu au waandishi wa habari. Kwa hiyo hawakuwahi kubeba silaha wakati wowote.

Sehemu kubwa ya hawa ilitokea Tanzania, hususan kwenye kambi ya wakimbizi ya Tabora.

Wengi wao walikuwa katika jeshi la Obote, lakini tangu waliposhindwa katika jaribio lao la mwaka 1972 la kumwangusha Idi Amin hawakuendelea tena kupata mafunzo ya kijeshi.

Baadhi ya wengine hawangeweza tena kuingia kwenye mapambano ya kivita kwa sababu ya uzee.

Hata hivyo, siku chache baada ya uvamizi wa Idi Amin, Obote ambaye alikuwa amekwenda Zambia, alirejea Tanzania haraka na kuanza kuwakusanya makomandoo wa kijeshi kutoka Dar es Salaam na kwingineko.

Wanajeshi wote wa zamani wa Uganda walitakiwa kukutana Tabora kwa mkakati maalumu dhidi ya Idi Amin. Ndani ya wiki moja tu ya wito huo wakakutana 800 chini ya Kanali Tito Okello, ambaye ndiye alikuwa kamanda wa lile jaribio la mapinduzi la mwaka 1972.

Kufikia katikati ya Novemba 1978 kiasi cha wapiganaji 300 miongoni mwao wakawa wamepewa sare za kijeshi na kupelekwa Mwanza ambako walikutana na wenzao wengine ili wapelekwe vitani Uganda.

Mwalimu Nyerere alitaka kikosi cha Waganda hao kiende vitani haraka iwezekanavyo, lakini Obote akapinga akidai kikosi chake cha Tabora kimeganyika na kilihitaji muda kuwekwa sawa. Lakini wengine walisema Obote alihisi kikosi hicho kinamtii zaidi Kanali Okello kuliko yeye.

Okello na wapiganaji wengi walikuwa wa kabila la Acholi na ingawa wakati mmoja Obote alidai kuwa watu hao wa Tabora walikuwa watiifu kwake, wakimbizi wengi wa kabila la Acholi waliona kuwa Obote aliwapuuza wakati wa utawala wake kabla ya kupinduliwa na Idi Amin mwaka 1971.

Wengi wao walikuwa wakidai kuwa wakati Obote akiwa madarakani aliwapendelea watu wa kabila lake la Langi kwa kuwapa ajira na fursa nyingine ambazo wao walinyimwa.

Hata hivyo Nyerere alimsikiliza sana Obote na hivyo aliamuru wapiganaji 300 waliokuwa wameshawasili Mwanza warudi Tabora ambako Obote na Okello wangekubaliana kuwa hao wawe kwenye batalioni moja. Kwa mujibu wa kitabu cha War in Uganda, Tanzania iliwapatia silaha na makamanda wa Uganda wakaanza kutoa mafunzo mara moja.

Wakati huohuo, Nyerere alianzisha kambi ya mafunzo ya Uganda huko Tarime karibu na Musoma. Ilikuwa na uwezo wa kutoa mafunzo kwa wapiganaji 1,200. Nyerere aliwataka Waganda wengine, akiwamo Robert Serumaga na Roger Makasa.

Wengine ni Andrew Adimola wa chama cha Ugandan Redemption and Reconciliation Union. Robert Bellarmino Serumaga ambaye alikuwa mwandishi, aliukimbia utawala wa Idi Amin mwaka 1977. Adimola alikuwa waziri kabla hajakimbia. Mwingine ni Aleker Ejalu. Nyerere aliwasihi wote hawa wahamasishe wapiganaji.

Itaendelea kesho
 
SEHEMU YA 8

Hadi ilipofika Krismasi mwaka 1978, zaidi ya wafuasi 50 wa watu hawa wakawa wamewasili. Wiki chache baadaye wakawasili wengine zaidi ya 100 tayari kwa mafunzo.

Januari 1979 Serumaga na Ejalu walimwambia Nyerere kuwa katika miji ya Kampala na Jinja kuna maelfu ya wanajeshi wanaompinga Idi Amin na kwamba wakipata msaada kidogo tu wataasi.

Nyerere alikubaliana nao, akaruhusu Waganda 200 wapelekwe Uganda kwa kazi hiyo, 50 kwa ajili ya Serumaga na Ejalu na 150 kwa ajili ya Tito Okello. Lakini walipokaribia ufukwe wa Ziwa Victoria upande wa Uganda baadhi ya mashua zao zilizama, baadhi walifanikiwa kurejea Mwanza.

Muda mfupi baadaye Ejalu na Serumaga wakatuma mashua za doria ziwani, lakini walipowasili karibu na mji wa Jinja wote walikamatwa na kuuawa. Baada ya matukio haya, kambi ya mafunzo ya Tarime ikafungwa rasmi.

Kwa upande wa uchumi wa nchi, bidhaa zilianza kupaa bei. Hii ilitokana na kuongezeka kwa kodi ili kulipia mahitaji ya vita. Novemba 15, 1978, jarida la Africa Contemporary Record 1978-1979 lilimnukuu Waziri wa Fedha wa Tanzania, Edwin Mtei akitangaza kuwa vita vimeifanya Serikali kuongeza kodi kwa bidhaa za walaji.

Vita ilipoanza kupamba moto, Tanzania ilianza kuwatafuta marafiki na washirika wake, lakini ikaonekana kusingekuwa na msaada mkubwa kutoka kwao. Rafiki wa kwanza ambaye Tanzania ilimwona alikuwa ni Jamhuri ya Watu wa China (RPC).

Kwa mujibu wa kitabu cha Routledge Handbook of Chinese Security kilichohaririwa na Lowell Dittmer na Maochun Yu, mwaka 1963 kiongozi wa China, Mao Zedong alianzisha falsafa mpya ya kimkakati aliyoiita “mapinduzi ya dunia”.

Nadharia yake akaiita “Two Middle Areas” (liangge zhongjian didai) ambayo aliamini kuwa katikati ya mataifa mawili makubwa Marekani na Urusi kulikuwa na maeneo mawili makubwa katikati yake. Eneo la kwanza lilikuwa ni baadhi ya nchi za bara la Asia, Afrika na Amerika ya Kilatini ambazo ama zilikuwa tayari zimejipatia uhuru au zilikuwa katika harakati ya kujipatia uhuru.

Kwa kufuata falsafa hiyo, mwaka 1964 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China, Zhou Enlai aliitembelea Tanzania. China ilitoa misaada na mafunzo ya kijeshi. Hadi mwishoni mwa 1978, wakati Vita vya Kagera ilipoanza na kupamba moto, Tanzania ilikuwa imeshapokea misaada na zana mbalimbali za kivita kutoka China.

Katika ukurasa wa 42 wa kitabu hicho, waandishi Dittmer na Maochun Yu wanaandika kuwa katika bara la Afrika, nchi ambayo Mao aliipa ‘kipaumbele cha juu’ ni Tanzania. Kuanzia mwaka 1964 Tanzania ilipewa msaada wa silaha mbalimbali vikiwamo vifaru, ndege vita na mfumo kamili wa usalama.

Kitabu cha China into Africa: Trade, Aid, and Influence kilichohaririwa na Robert I. Rotberg (chapa ya mwaka 2008) katika ukurasa wake wa 159 kinasema “...Zana za kivita kutoka China kwenda Afrika tangu 1966 hadi 1977 ilikuwa ni pamoja na boti za doria, vifaru na ndege za kivita aina ya MiG-17, MiG-19 na MiG-21 kwa ajili ya Tanzania.

Katika ukurasa wa 110 wa kitabu chake, Arms for Africa: Military Assistance and Foreign Policy in the Developing World, mwandishi Bruce Arlinghaus ameandika “China ilitoa (kwa Tanzania) asilimia 60 ya mahitaji yote ya kijeshi...”

Pamoja na historia yote hiyo ya urafiki kati ya Tanzania na China tangu 1964 hadi 1978, Tanzania ilipoiendea kwa ajili ya msaada wa zana za kivita za kupambana na Idi Amin, Jamhuri ya Watu wa China iliiambia Tanzania kuwa haitajihusisha kwa namna yoyote na mgogoro kati ya Tanzania na Uganda. Zaidi ya hilo, China iliishauri Tanzania ikae mezani na Uganda kumaliza mgogoro huo.

Kilichofanywa na Serikali ya China ni kuwasilisha tu zana za vita zilizokuwa zimenunuliwa kabla vita haijazuka lakini hakuna silaha za ziada ambazo China ilitoa hata vipuri. Jeshi la Wananchi wa Tanzania likaanza kutegemea vipuri kama betri za vifaru kutokana na silaha walizoteka kwa majeshi ya Idi Amin.

Kwa upande wa Uganda, zana za kijeshi ambazo ilikuwa ikizipata kutoka Urusi hazikuendelea tena kutolewa. Kufikia katikati ya mwaka 1978 Serikali ya Idi Amin ilikuwa inazidi kutengwa.

“Kati ya 1975 na 1978 Uganda ilipata zana za kivita kutoka Urusi, Libya, Iraq, Uswisi na Libya,” kinasema kitabu cha Arms and Warfare: Escalation, De- escalation and Negotiation (chapa ya 1994) cha Michael Brzoska na Frederic Pearson.

Jumatatu ya Novemba 10, 1975 Idi Amin alitishia kuvunja uhusiano na Urusi ndani ya saa 48 ikiwa hangepata alichokitaka kutoka kwao. Alitishia pia kuwa angemfukuza nchini mwake balozi wa Urusi, Andrei Zakharov.

Aliilaumu Urusi kwa kuingilia mambo yake ya ndani. Pia aliilaumu kwa kumnyima vipuri kwa ajili ya ndege zake za kijeshi aina ya MiG-17 na MiG-21.

“Novemba 11, 1975 Idi Amin akatangaza kuwa Urusi imlete balozi wake mwingine ambaye ‘hana ubeberu’ kama aliyekuwapo,” kinaandika kitabu cha Who Influenced Whom: Lessons from the Cold War cha Dale Tatum.

Katika matangazo ya Redio Uganda, Idi Amin alisikika akifoka, “Mimi si kibaraka na sishurutishwi na yeyote.”

Mara baada ya hapo, kinaandika kitabu hicho, “Urusi waliamua kuvunja uhusiano na Uganda, lakini cha kushangaza Urusi iliurejesha uhusiano huo siku nne baadaye Novemba 15, 1978.”

Huu ni ule wakati ambao Idi Amin alikuwa mwenyekiti wa Nchi Huru za Afrika (OAU).

Uganda ilipovamiwa na makomandoo wa Israel katika kile killichoitwa ‘Operation Entebbe’ au kama ilivyojulikana kwa wengine, ‘Operation Thunderbolt’, Jumapili ya Julai 4, 1976 na ndege zake za kijeshi kuharibiwa vibaya, Urusi iliahidi kuimarisha kikosi cha anga cha Jeshi la Uganda na kuwapa ndege nyingine za kivita.

Kwa ahadi hiyo uhusiano kati ya Uganda na Urusi ukaanza kuimarika tena. Marubani wa ndege za jeshi za Uganda walipelekwa mafunzoni Urusi.

Itaendelea kesho
 
Okay well, itaendelea kesho, lakini itakapoendelea kesho ulete narative sahihi kuhusu muamuzi wa Uganda aliyewaleta vitani.

Kusema Kanali Juma wa kikosi cha Malire ndio aliamua Uganda ije vitani Tanzania bila kupata sahihi, dokezo, baraka wala hata kujulishwa dikteta Iddi Amini Dada is simply ridiculous.

Nduli Amini hawezi kusafishwa kwa kumlaumu Kanali Juma wa Uganda kwamba ndie aliyeamua vita kwa sababu Amini alikuwa ameshaeleza mapema sana kwamba anakwenda kuishambulia Tanzania siku za usoni.

Kwanza Iddi Amini mwenyewe alionyesha mwili wa kamanda wa polisi wa Tanzania, RPC Pope wa Ziwa Magharibi, aliyeuawa na Waganda kabla ya mwaka 1978. Vita iliamuliwa na Amini.
kweli aisee............
 
Naweza sema urafiki wa Mwl na Obote nao ulichangia mbona dictotor Amin haku kwaruzana na Kenya ? Hili kwetu liwe funzo tusiwaingilie wengine kwa personal interests !
 
Mkuu wa Jeshi la Nigeria, Luteni Jenerali Theophilus Yakubu Danjuma, akitokea Uganda alikokutana na Idi Amin Dada aliwasili Dar es Salaam Jumanne ya Novemba 14, 1978 na kukaa hadi Alhamisi ya Novemba 16.

Luteni Jenerali Danjuma alitua Uganda kwanza kabla ya kufika Tanzania. Katika mazungumzo ya mjini Kampala, kwa mujibu wa jarida Africa Research Bulletin, Idi Amin alimwambia Danjuma kuwa yuko tayari kuyaondoa majeshi yake mpakani iwapo tu OAU itamhakikishia kuwa Tanzania itasimamisha mapigano na “kuichokoza Uganda”.

Baada ya kuondoka Uganda ndipo akaja Tanzania kumletea Rais Nyerere ujumbe kutoka kwa Rais wa Nigeria, Jenerali Olusegun Obasanjo, ukimtaka kukubali mazungumzo na kusitisha mapigano mara moja.

Nyerere alimkabili Danjuma. Alimwambia, “(Idi) Amin amefanya kitendo cha uvamizi dhidi ya Tanzania. Hebu fikiria ikiwa atayaondoa majeshi yake au kuyarudisha nyuma. Sisi tuseme ‘imetosha’ halafu tumwache tu ajiendee zake? Si rahisi hivyo kumwachia mchokozi aende zake.”

Simon Chesterman katika kitabu cha Just War Or Just Peace: Humanitarian Intervention and International Law (uk. 77) ameandika, “Amin alidai kuwa uvamizi wake kwa Tanzania ulikuwa ni kitendo cha kujilinda dhidi ya matendo ya Tanzania kuunga mkono na kusaidia waasi wa Uganda ... Novemba 8 (1978) aliahidi kuondoa majeshi yake iwapo tu OAU itamhakikishia kuwa Tanzania haitaivamia Uganda wala kuwasaidia wakimbizi wa Uganda waliopo Tanzania. Nyerere alilikataa sharti hilo na Novemba 12 (Nyerere) akatangaza kuwa Tanzania imeanza kushambulia (Uganda).”

Kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi naye akaingia vitani upande wa Idi Amin. Alipomtaka Nyerere aache kuipiga Uganda, Nyerere alimjibu: “...Tumepigana kwa ajili ya usalama wa nchi yetu. Hatupigani kwa sababu ya kumng’oa (Idi Amin) … Sisi tunapigania usalama wa nchi yetu.”

Baadaye Kanali Gaddafi alimtuma mjumbe wake kumpelekea Nyerere risala iliyodai kuwa tangu mgogoro ulipoanza yeye (Gaddafi) alijitahidi sana kusuluhisha, lakini sasa baada ya uchunguzi wa muda mrefu, aliamini Watanzania ndio wachokozi.

Mwalimu Nyerere hakuchelewesha majibu. Aliwaita wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam na kuwapasha habari hizo. Aliwaambia: “...Vita tunavyopigana sisi ni vita vya usalama wa nchi yetu. Hatukusudii kumtoa Amin … Tumeishi naye miaka minane. Tunataka kuwa na hakika kuwa anajua kuwa vita si lelemama. Vita si mchezo. Akishajua hilo, madhali tuliishi naye miaka minane, tuko tayari kuishi naye miaka mingine minane.”

Katika mkutano wa wakuu wa nchi za OAU mjini Monrovia, Rais Nyerere na Rais Gaafar Muhammad an-Nimeiry wa Sudan walirushiana maneno makali, Nimeiry akimtuhumu Nyerere kwa kuivamia Uganda. Ajenda kuu ya mkutano ilikuwa ‘kitendo cha Tanzania kumpindua Idi Amin’.

Baada ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) kushindwa kutimiza sharti la Tanzania la kumlaani Idi Amin kwa kuitaka na kuiteka ardhi ya Tanzania, uliamua kuteua kamati ya mataifa tisa ya kujaribu kuleta suluhisho.

Ikiongozwa na Meja Jenerali Henry Edmund Olufemi Adefope wa Jeshi la Nigeria, kamati hiyo ilikutana mjini Nairobi, lakini katika kila kikao walichofanya kilikaribia kuvunjika kwa sababu ya kurushiana maneno makali.

Katibu Mkuu wa OAU, Edouard Kodjovi Kodjo (alijulikana zaidi kama Edem Kodjo) ndiye aliyetoa hadidu za rejea.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Benjamin Mkapa alikataa hoja iliyosema ‘Majeshi ya Uganda yameondoka kwa hiari katika ardhi ya Tanzania.’ Kisha akahoji, “Kusema kwamba majeshi ya Uganda yameondoka kwa hiari ni tusi kubwa kwa vijana wetu waliouawa wakipigana.”

Mkapa akaiambia kamati hiyo kuwa OAU ilishindwa kumlaani Idi Amin alipoteka sehemu ya ardhi ya Tanzania na pia ikashindwa kutofautisha kati ya mchokozi na aliyechokozwa.

Akijibu hoja za Mkapa, mwakilishi wa Uganda ambaye alikuwa ni Waziri wa Nchi katika Wizara ya Mambo ya Nje, Matias Lubega alipinga lakini Mkapa akasimamia msimamo wake.

Baada ya mjadala wa Nairobi kuwaka moto kamati hiyo iliamua kusafiri kwenda Kampala na Dar es Salaam kuonana na Idi Amin na Nyerere.

Walipofika Uganda, Idi Amin aliiambia kamati hiyo kuwa Uganda ilivamiwa na Watanzania, Wamarekani, Waisraeli na Wacuba. Baada ya kumsikiliza kamati iliondoka Kampala kuelekea Dar es Salaam.

Nyerere alikuwa kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri wakati kamati ikiwasili. Mkapa aliwahakikishia wajumbe hao kuwa Nyerere alikuwa na shauku kubwa ya kukutana nao na kwamba angekutana nao jioni. Kamati ilisubiri katika Hoteli ya Kilimanjaro, lakini Nyerere hakutokea. Hatimaye wakaamua kuondoka kurejea Nairobi. Walipoondoka tu hotelini hapo ndipo Nyerere akatuma neno akisema sasa alikuwa tayari kukutana nao saa 11:30 jioni.

Mkapa alilazimika kuwakimbilia wajumbe hao hadi Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam kuwapasha habari hizo. Lakini walisema wameshachelewa na kwamba kama watafanya mkutano huo watachelewa ndege ya kuwarejesha Nairobi.

Ingawa Mkapa aliwaambia yuko tayari kuwapatia malazi na kila walichohitaji ili tu mkutano huo ufanyike, baadhi walimwambia hawakuja na miswaki na wengine wakasema hawakuja na nguo za ndani za kubadilisha. Kisha wakapanda ndege wakaondoka zao. Usuluhishi mwingine wa OAU ukawa umeshindwa.

Wakati Nyerere akikabiliana na kile alichodhani ni kuingiliwa matakwa yake na Nigeria, Sudan, Libya na OAU, zipo nchi ambazo hazikuishutumu Tanzania lakini ujumbe haukuwa tofauti na zile zilizoishutumu.

Waandishi Richard Bissell na Michael Radu katika kitabu chao, cha Africa in the Post-Decolonization Era (uk. 172) wameandika kuwa, “...baada ya OAU kushindwa kukemea na kuilaani Uganda kwa kitendo chake cha kuivamia na kuikalia sehemu ya ardhi ya Tanzania, Nyerere aliliamrisha jeshi lake kuingia Uganda.”

Awamu ya pili ya Vita ya Kagera ikaanza.

Itaendelea kesho.
 
Kuingia ndani ya Uganda ilikuwa ni awamu ya pili ya Vita vya Kagera. Kabla awamu hiyo haijaanza, kulifanyika mabadiliko ya uongozi kwenye uwanja wa vita. Baada ya kufanya kazi kwa muda wa miezi mitatu akiwapanga wapiganaji wa JWTZ na kuirejesha ardhi ya Tanzania iliyotekwa na Idi Amin, Brigedia Jenerali Tumainieli Kiwelu alirejeshwa Dar es Salaam. Kazi ya kuingia Uganda ikaenda mikononi mwa kamanda mwingine, Meja Jenerali David Msuguri.

Ilipangwa miji ambayo ingeanza kutekwa ambayo ni Masaka na Mbarara. Hii ikabatizwa jina la Mapigano ya Masaka ambayo ilidumu kwa siku mbili tu; Ijumaa na Jumamosi ya Februari 23 na 24, 1979 na ikamalizika.

Lakini kabla Masaka haijafikiwa kulikuwa na miji midogo midogo ya kutekwa. Mmojawapo ni Lukoma ambako kuna uwanja mdogo wa ndege uliojengwa mahsusi kwa shughuli za kivita na ni umbali wa kilomita 20 kutoka mpaka wa Tanzania.

Ndege za kijeshi zilizoishambulia Tanzania zilipaa kutoka katika uwanja huo uliozungukwa na vilima vya Nsambya, Kikandwa na Simba. Vilima vyote hivi askari wa Idi Amin walikuwa wametanda wakiwa na silaha kali za kivita vikiwamo vifaru na mizinga mikubwa.

Brigedi tatu zilizokamilika 201, 207 na 208 zilitumwa kuingia Masaka. Mpango wa awali ulikuwa ni kuzitumia brigedi za 201 na 208 kushambilia vilima vya Simba kutokea Kusini-Magharibi na Brigedi ya 207 ishambulie kutokea Mashariki.

Lakini baadaye taarifa za kiintelijensia zilisema kulikuwa na zaidi ya askari 500 wa Idi Amin wakiwa na vifaru na mizinga mikubwa eneo la Katera kwenye rasi ya Sango Bay, eneo la Kakuuto upande wa pili wa Ziwa Victoria. Kuwaacha hawa ingefanya eneo la upande huo wa Tanzania kuwa hatarini zaidi kushambuliwa.

Kwa hiyo iliamuliwa Brigedi ya 207 ianze kushambulia Katera. Kulikuwa na njia mbili za kufika Katera kutokea Minziro. Njia ya kwanza na rahisi zaidi ilikuwa ni barabara kuu, lakini kwa kutumia njia hiyo jeshi la Tanzania lingekutana na mashambulizi ya uso kwa uso kutoka jeshi la Idi Amin.

Njia ya pili na ngumu zaidi ni kupita kwenye uchochoro wenye mabwawa yaliyojaa maji kutokana na mvua iliyokuwa ikinyesha. Huu ni upande wa pili wa Ziwa Victoria.

Askari wachache waliozaliwa katika vijiji vilivyozunguka ziwa karibu na Bukoba na ambao walijua lugha na tamaduni za eneo hilo walichaguliwa wasonge mbele, wakivalia nguo za kiraia na kubeba matairi ya baiskeli na bidhaa nyingine kama vile wanakwenda sokoni. Askari waliobaki nyuma wakawafuatilia kwa kufuata nyayo zao.

Siku iliyofuata walirudi wakiwa wamechoka kupita kiasi na wengine wakiwa wagonjwa. Waliripoti kuwa mvua kubwa iliyonyesha iliharibu sana barabara kiasi cha kutopitika.

Pamoja na ripoti ya wanajeshi hao, Kamanda wa brigedi hiyo, Brigedia John Butler Walden, aliamua ni lazima wasonge mbele hata kama hali ya hewa ni mbaya kiasi gani. Huyu ni brigedia aliyeitwa ‘Black Mamba’.

Kwa kuwa alijua wanajeshi wake wasingepata moyo wa kusonga mbele bila yeye kwenda nao bega kwa bega, aliamua kutembea nao kwa mwendo wa zaidi ya kilomita nane za kwanza kutoka Minziro hadi kilima cha Bulembe.

Brigedia Walden alidhani mwendo kwa hizo kilomita nane ungewachukua saa chache kupita kwenye msitu mnene, lakini iliwachukua karibu saa 11 wakipambana na matope, madimbwi makubwa ya maji, mbu na mbung’o na maeneo mengine walilazimika kutembea kwenye madimbwi ya maji yaliyowafika mabegani karibu kabisa na kuzama.

Hatimaye walipofika eneo ambalo lilikuwa kavu kwa kiasi fulani, Brigedi ya 207 ilipumzika kidogo kisha ikaanza tena matembezi marefu kuelekea Kaskazini umbali wa kilomita 28 kuingia ndani ya Uganda katika mji wa Katera.

Walipodhani masaibu yamekwisha, ndipo yalipoongezeka. Wadudu kama mbu na mbung’o wakaongezeka. Brigedi ya 207 ikajikuta katika vita ya aina mbili kupambana na jeshi la Idi Amin na wadudu wanaokera katika msitu mnene, huku mvua ikinyesha na barabara yenye madimbwi kujaa maji.

Silaha walizokuwa nazo zikalowa maji. Kutokana na barabara kutopitika kwa gari hata zile gari za jeshi askari wa brigedi hii walilazimika kubeba vichwani mwao silaha zao na zana zingine za kivita.

Hatari kubwa zaidi kuliko mbu na mbung’o ilikuwa ni wanyama kama mamba na viboko waliokuwa maeneo hayo, hususan kuelekea Sango Bay. Kwa hiyo kulikuwa na hofu nyingine ya wanajeshi hao kushambuliwa na hata kuliwa na wanyama hao wakali.

Kwa umbali wa kilomita 28, na kutokana na ubovu mkubwa wa njia waliyopita ikiwa na madimbwi makubwa yaliyojaa maji, ikijumlishwa na mashambulizi ya wadudu, brigedi hiyo ilitumia muda wa saa zaidi ya 50 bila kupumzika wala kula.

Redio za mawasiliano walizokuwa nazo zililowa maji hata zikashindwa kufanya kazi. Kwa hiyo walipoteza mawasiliano kabisa na makao makuu ya kikosi chao.

JWTZ ilianza kuwatafuta wanajeshi hao bila mafanikio. Kukawa na hofu kubwa kuwa Brigedi ya 207 imeshambuliwa na kufyekwa yote. Hakukuwapo na namna yoyote ambayo yeyote katika brigedi hiyo angeweza kufikiwa.

Hatimaye ilipofika saa 11 jioni ya siku ya tatu, brigedi hiyo ikaibuka kutoka kwenye mabwawa ya maji na matope. Angalau sasa redio zikaanza kufanya kazi na wakaweza kuwasiliana na kituo chao cha kazi.

Ingawa hakuna mwanajeshi hata mmoja aliyepoteza maisha, zaidi ya 200 miongoni mwao walikuwa wagonjwa na wachovu mno kiasi kwamba walishindwa kusonga mbele. Wengine walifikia hatua ya kushindwa hata kutembea kiasi kwamba ilitumwa helikopta ya jeshi kuwabeba.

Kwa kuwa wanajeshi wa JWTZ walikuwa wamechoka sana, iliamuliwa kuwa wasubiri hadi kupambazuke ndipo mashambulizi yaanze. Je, walianza kushambulia? Na walishambuliaje?

Itaendelea kesho
 
Back
Top Bottom