Yajuwe yaliyodhaniwa hayawezekani kabla ya Oct 7 Gaza

Mambo hayo yanaenda pamoja na uchumi. Nchi yako tanzania ikiingia vitani na waisraeli unadhani hii kauli yako itadumu hapa kwa masaa mangapi? Ile iron dome kuiendesha tu unahitaji bajeti nzito sana. Hatuzungumzii mavifaru mandege vita nk.

Mkuu si uchumi wa nchi husika tu:



Usiwasahau na wajomba zetu pia.

Kumbuka huyu ana support overt na covert toka kwa wajomba zake wa kumwaga.
 

1. Huku ni kushabikia vita ndugu?



2. Ingekuwa ni kushabikia vita watanzania wasingekuwa Congo, Darfur, Mozambique, Zimbabwe, Namibia, Uganda, nk.

3. Zaidi sana ujumbe huu unaweza kuwa unahusu wabinafsi waliopitiliza kama wewe:



4. Disgrace!
 
Waliambiwa kuwa hakuna vita inayoisha bila makubaliano
Hata mmarekani alizikimbia silaha zake Afghanistan na kuomba maridhiano
Hapo Vijana wa Hamas
Lebanon nako Hezbollah na watoto wa baba wako Yemen pia
Yaani wameshikwa pabaya Suez natamani wasomali nao warudi wale pirates
Hao ni dollars tu wanakamua kotekote

🇺🇸 atajigawa sehemu ngapi? Hata Zele kashtukiwa na mirija inakatwa
 
Sisi tunawaogopaga hata Panyarodi tu Ndugu !! Sembuse magari ya washawasha ??!!😂😂😂🙏

Katiba ni ndoto labda wapende wenyewe !!🙏🙏

Kwa hakika CCM wakomae hapo hapo. Hakuna kuachia katiba mpya wala nini. LATRA nao nauli endelea kupandisha juu. CCM endelea kuiba kura. Ewura pandisha bei mafuta. Umeme, maji endeleza mgao. Ajira funga, kodi na tozo pandisha! Nk, Nk:



Hadi mazezeta yapate akili kutoka chini ya meza!

Bila kusahau:

Kushindwa uchaguzi ni pamoja na kuibiwa kura, kulikoni kulia lia

Cc: denoo JG
 
Hatar sana !!
Kizazi cha kudai Katiba bora mpya bado hakijazaliwa !!
Muda ule ukifika hutowaona watu wakibishania imani zao za dini !!
Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu !
Huo muda bado haujafika !! 🙏🙏
 
Kwa miaka 70 hamas amekuwa akipambana na israel na washirika wake ni mungu amekuwa akiwapigania ukiangalia uwezo wa israel na uwezo wa hamas utagundua mungu yupo
 
Exactly kabla ya oct 7 mtu angeyasema haya angeonekana kichaa ila leo wote tumeshuhudia hadi meli zikigoma kwenda israel
 
Simply raia wanaodai Katiba Mpya hawana vifaru, sijui kwanini umelinganisha vita ya Israel na Hamas sawa mapambano ya kuidai Katiba Mpya mpaka useme tayari tumeshashindwa!

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

1. Mkuu hakuna popote raia wana vifaru.

2. Hata HAMAS hana wala haitakaa popote awe navyo raia.

3. Vita vya HAMAS ni vita vya ukombozi:



4. Kuvitenganisha vita vya HAMAS na ukombozi ni kukubali kushindwa mapema asubuhi.

5. Hapa ndipo tunapofeli:

Your browser is not able to display this video.


6. Hapo ndipo Nyerere alipofanikiwa.

7. Hatuwachukii CCM, Israel, Makaburu au madhwalimu wowote kwa sababu ya sura zao.

8. Tunawachukia wote sawa sawa kwa sababu ya ubaguzi wao, chuki zao, udhwalimu wao, manyanyaso yao nk.

9. Itachukua miaka mingi sana kulirejesha taifa lilillkokuwa na Nyerere.

10. Vyama na hata nchi Leo haijulikani tunasimamia nini; hatujui kwanini yule ni adui au rafiki na kwa nini:

Mbowe, Lissu wafundeni wafuasi Falsafa ya Chama

11. Hatuna principle tumekuwa kama mazuzu au mazombi tu.

12. Kama ndivyo yote heri wacha tuwasubiri CCM wakisha shiba watatuletea ushindi mezani.

Cc: mzeewaSHY
 
Hatar sana !!
Kizazi cha kudai Katiba bora mpya bado hakijazaliwa !!
Muda ule ukifika hutowaona watu wakibishania imani zao za dini !!
Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu !
Huo muda bado haujafika !! 🙏🙏

1. Nadhani hakiwezi kuzaliwa bila hili:

Mbowe, Lissu wafundeni wafuasi Falsafa ya Chama

2. Watu hawajui rafiki au adui ni nani.

3. Taifa limepoteza dira na hakuna mwelekeo.

4. Nani anaongea lugha hizi leo?

Your browser is not able to display this video.


5. Kwanini Nyerere akiongea hivyo? Alikuwa kwenye kujifurahisha?

6. Mola atuswamehe.
 
Exactly kabla ya oct 7 mtu angeyasema haya angeonekana kichaa ila leo wote tumeshuhudia hadi meli zikigoma kwenda israel

Ni mbuzi watu wenye kujitoa ufahamu wanaoweza kujilazimisha kutotaka kuukiri hadharani.
 
Hao HAMAS huwa wanatumia silaha kwa ajili ya kulipa kisasi, wakati mwingine husababisha vifo, sasa bado nashangaa unavyohusisha mashambulizi yao kwa adui zao sawa na harakati zetu za kudai Katiba Mpya, nakuona unatumia nguvu nyingi sana kulazimisha mambo mawili ambayo hayafanani kabisa.

- Sisi tunaitafuta Katiba Mpya kwa njia ya mazungumzo, na nyingine zitakazohusisha ruhusa ya kisheria, lakini sio kwa kujitoa mhanga kama wanavyofanya hao jamaa unaowapigia debe hapa, ajabu umeonekana kuzikebehi njia hizo kwa kuwataka CCM washikilie hapo hapo!.

Pale juu naona umenitag na neno bovu umetumia, hebu tuliza akili ndugu, tazama vizuri kama vita ya Hamas na Israel inafanana na mapambano yetu ya kudai Katiba Mpya, hasa mbinu zinazotumika kujikomboa, i doubt kuna hidden factor inayoufanya upeo wako kuwa chongo kwenye hili.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 

1. Mkuu vita vya HAMAS ni vya ukombozi:



2. Msingi wa vita vyao ni falsafa yao thabiti ya kudai haki hata ikibidi kufa.

3. Huu ni ushahidi kwao zaidi:



4. Utayajua matakwa ya wapalestina zaidi kuliko wao?

5. HAMAS ni chama cha ukombozi kama SWAPO, ANC, NRM, RPF, FRELIMO, MPLA, FRELIMO nk.

6. Ni kawaida kutumia nguvu popote njia zote za amani zikishindikana.

7. Tuliza akili kujiridhisha vinginevyo weka ushahidi kuthibitisha vinginevyo.
 
Wewe una mental case wahi hospital,yaani unakiri Mazayuni kupigwa lkn unawatahadharisha Hamas! Pathetic
 
Wewe upo bara Mkuu! Halafu mbona sisiemu wenyewe washasema hawataachia Dola by any means Pathetic!
 
HAMAS wanatumia mbinu zipi kwenye hiyo vita yao? mbinu zao na zetu zinafanana?

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
HAMAS wanatumia mbinu zipi kwenye hiyo vita yao? mbinu zao na zetu zinafanana?

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

1. Kumbuka madai ya ukombozi wa wapalestina yapo tokea 1948.

2. Zipo resolutions nyingi za UN in favor ya wapalestina ambazo Israel anazikaidi.

3. Kwenye jitihada za ukombozi HAMAS ni chama kilichoundwa 1987 kama vingine vingi kwenye kupigania ukombozi huu wa wapalestina.

4. Kama mkoloni angeridhia madai kabla ya 1987 HAMAS isingeundwa.

5. Mkoloni wao kama alivyo wetu mweusi hakuwahi kukubali hata kufanya nao mazungumzo tu.

6. Tunajua kupitia Oct 7 mkoloni huyu na mjomba wake alikaa chini nao kwa mara ya kwanza katika historia kuongea na kukubaliana.

6. Alipo sasa mkoloni huyu ataongea na hata kukubaliana na Hezbollah pia, si kwa kuwa kapenda.

7. Wakoloni wote wanafanana kwenye kukataa mazungumzo na maridhiano yenye tija.

8. Wakoloni wote hutaka wanazoziiita wao siasa za kistaarabu zisizokuwa na madhara kwao, wakati wao si wastaarabu.

9. HAMAS hatimaye kabeba silaha baada ya jitihada zote za huko nyuma kushindwa, kwa sababu ndiyo njia pekee mkoloni huyu anayoielewa.

10. Bado huoni wapi vita vyetu au vyovyote vya kudai haki, usawa na uhuru yaani demokrasia na vya HAMAS vinapofanana?
 
Suala la Palestina ni tofauti sana na suala la makaburu wa SA. Unalingamisha embe na kitumbua.

Palestine ni ardhi ambayo imekaliwa na jamii kubwa tatu kwa miongo mingi, huku wayahudi wakiwa ndiyo jamii kubwa, mpaka wakati wa Ottoman. Wakati wa Otyoman empire ndipo Wayahudi wengi walielekea Ulaya, na hivyo kuifanya jamii ua Waarabu kuwa majority kqenye eneo la Palesrine.

Mwaka 1947, UN iliamua Palestine land ugawanywe maeneo mawili, eneo moja ambalo lilikuwa 60% ya eneo la Palestine, liunde Taofa la Israel; na 40% ikabakizwa kwa waarabu. Mgawanyo ulizingatia proportionality ya historical population. Kwa ujinga tu, waarabu wakagoma kwa madai kuwa Israel imepewa maeneo mazuri ya kilimo na uvuvi. Kwa kudanganywa na Iran, Misri na Syria, Waarabu wa Palestine wakaaminishwa kuwa nchi za kiarabu zitawasaidia hao waarabu wa Palestine kuwaua na kuwapoteza kabisa Wayahudi. Mambo yakawaendea kinyume. Mwaka 1948, wakapigwa na kupoteza 60% ya ile 40% waliyopewa. Mwaka 1956 wakajaribu tena, wakapigwa na kupoteza tena maeneo mengine. Mwaka 1967, wakaandaa vita kubwa zaidi, wakapigwa na kupoteza maeneo mengine mengi zaidi ikiwemo milima ya Golan, Gaza na Westbank. Kama siyo ujinga na ubinafsi wa nchi za kiarabu, sahizi waarabu wa Palestina, wangekuwa na nchi yao.

Hakuna aliyewapora haki, zaidi ya ujinga na ubinafsi yao. Waliikataa 40%, leo wanalilia mipaka irudi ya mwaka 1967, ambayo kiuhalisia ni kama 15% ya eneo walilokuwa wamepewa mwaka 1948.

Mwaka 1993, makubaliano yakafikiwa kuwa kuanzishwe Taifa la Palestine lakini kwa hatua. Kwanza wapewe mamlaka ya ndani, huku wakiangaliwa uadilifu na uaminifu wao maana waarabu hawaaminiki. Na hilo hata Gadafi aliwahi kulinena. Wakapewa mamlaka ya ndani, mara wakaanza kupigana wenyewe kwa wenyewe, mara kwenda kujilipua ndani ya Israel, mara mashambukizi ya kushtukiza. Wakawa wameshindwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…