Yaliyojiri Bungeni Dodoma: Jumatatu, Tarehe 10 Machi 2014

Yaliyojiri Bungeni Dodoma: Jumatatu, Tarehe 10 Machi 2014

Wadau, nipo ndani ya ukumbi wa Bunge na kwa jinsi inavyoonekana kikao hakiwezi kuanza muda huu. Mahudhurio bado ni machache. Pia kile kikao cha Mashauriano kinaendelea
 
Wadau, amani iwe nanyi.

Kama kawaida yetu tutaendelea kuwaletea mtiririko wa mijadala Bungeni Dodoma. Kwa sasa Bunge lipo kwenye mchakato wa kukamilisha kupitisha vifungu vya Kanuni za Bunge. Mtakumbuka kuwa vifungu vyote 87 vimepitishwa isipokuwa kifungu cha 37 na 38 ambavyo kwa ujumla wake vinahusu ufanywaji wa maamuzi ndani ya Bunge Maalum. Mjadala hapa ni ama matumizi ya Kura ya Wazi au ya Siri. Mtakumbuka kuwa siku ya Ijumaa ya tarehe 7 Machi, Mwenyekiti Kificho aliunda Kamati ya Mashauriano kuhusu vipengele hivyo. Kamati bado haijamaliza kazi yake na leo wanaendelea na mashauriano. Semina kwa siku ya leo itaendelea kuanzia saa 5 Asubuhi mara baada ya Kamati ya Mashauriano kumaliza kazi yake.

kama kawaida, nitakuwa sambamba na wadau wengine kuwaletea updates zote. Natarajia kupata ushirikiano kutoka kwa mdau wetu ambaye ni Mbunge wa Bunge hili Maalum, Simiyu Yetu. Pia kwenye Mjadala, natarajia kuwaona akina Skype na MaishaPesa. ​Stay Connected

kaka nimekukubali sana katika update za bunge, jumamosi nimepitia update zote safi sana
 
mida yenyewe hiyo tusiokuwa bungeni na kwenye tv tunawategemea sana.

Twende kazini
 
Taswira ya Ukumbi wa Bunge dakika tatu kabla ya saa 5 kamili asubuhi
image.jpg
 
Tanganyika nchi ninaekupenda tunakuhitaji
Hasa ktk kipindi hiki muhimu tutakupigania
Kwa njia zote
 
Wadau, nipo ndani ya ukumbi wa Bunge na kwa jinsi inavyoonekana kikao hakiwezi kuanza muda huu. Mahudhurio bado ni machache. Pia kile kikao cha Mashauriano kinaendelea

Hapa ndipo penye matatizo yote.
 
Tanganyika nchi ninaekupenda tunakuhitaji
Hasa ktk kipindi hiki muhimu tutakupigania
Kwa njia zote
Mkuu, wakati ukifika sote kwa pamoja tutaimba wimbo huo. Ila kwa sasa tujadili Kanuni za Bunge Maalum
 
kaka nimekukubali sana katika update za bunge, jumamosi nimepitia update zote safi sana
Nashukuru sana kaka. Tupo pamoja na tutaendelea kuwa pamoja kwa uwezo wa Rabana mpaka mwisho wa Bunge hili
 
@Chabruma na wewe ni mjumbe??? kweli JK aliona viazi
Simiyu Yetu ni yule jamaa aliyeiba simu bungeni P.M
Mkuu, swali hili nimelijibu kwenye mijadala iliyopita hasa ule wa Jumamosi. Mie si mjumbe ila Simiyu Yetu ndo mjumbe. Hatujuani ila tunafahamiana kikazi
 
Mkuu, si matatizo bali ndo chombo muhimu katika kulipatia ufumbuzi suala hili

Ndiyo ni chombo muhimu lakini kwa kadiri wanavozidi kuchelewa kufikia maamuzi ndivyo kodi zetu zinavyozidi kuteketea, mkuu mimi nina uchungu na kodi zetu tu na si vinginevyo japo napenda maridhiano yaliyo bora.
 
Haya mkuu, majina ya wajumbe wote haya hapa.
Mkuu Skype heko sana, nafikiri mdau alihitaji list ya wajumbe wanaounda kamati ya mashauriano, namu napenda kuwajua ni akina nani ili tujue uamuzi wa siri/wazi utakuwa muelekeo upi?
 
mwigulu si yuko kalenga au kasharudi?
Mkuu, Mwigulu alikuwepo sikunya Ijumaa na Jumamosi. Leo sijamuona ila nina hakika kuwa yupo kwq vile kuna vikao vya CCM vinaendelea na Mwenyekiti taifa yupo hapa kwa siku tatu
 
Simiyu yetu kanuni zenyewe anazielewa kweli? Nategemea atakuwa mtu wa ndiyoooooooo! na kugonga meza kama magamba wenzake hasa mwigulu anapochangia kwa kila jambu bila hata kuelewa vizuri.
 
Back
Top Bottom