Uchaguzi 2020 Yaliyojiri kampeni ya Dkt. Magufuli kuwania Urais 2020-2025 mikoani Iringa na Njombe (Sept 29, 2020)

Uchaguzi 2020 Yaliyojiri kampeni ya Dkt. Magufuli kuwania Urais 2020-2025 mikoani Iringa na Njombe (Sept 29, 2020)

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Leo mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi yuko mkoani Njombe na kwa sasa anaongelea afya na Bima ya Afya.

Ameeleza kuwa walianza na vituo vya afya na kinachofata ni bima ya afya, pia ameelezea walishaanza na wamejitahidi kutoa huduma za bure kwa wazee, watoto wenye umri chini ya miaka mitano na wagonjwa wenye magonjwa makubwa wanahudumiwa na serikali.

8D533B5B-88E2-4002-818D-52B764BFA55A.jpeg


Magufuli amesema katika kipindi cha miaka mitano, wagonjwa kusafirishwa nje wamepungua kwani hata operesheni za moyo zinafanyika Dar es Salaam, operesheni za kubadilisha figo zinafanyika Dodoma na hospitali ya Njombe ikikamilika pia hayo yatafanyika.

Endelea kuwa nami kukujuza yanayojiri Njombe

===========
1CB93151-FAC4-47A4-A71D-2F7B8BF76311.jpeg

AAF38BE4-32B4-410C-8D9E-F98958E39A1C.jpeg

172E163B-3A7C-4A72-A68C-61B016A75D20.jpeg


MAGUFULI: Ndio maana tumekuja tena kuomba kura kwa sababu tunafahamu mikakati, tunafahamu mbinu lakini pesa pia zipo. Hatuitaji fedha za kukopa nje, fedha ziko hapahapa, zilikuwa zimekaliwa na mafisadi, mafisadi tumewabana zinaenda kwa wananchi.

===
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. John Magufuli amesema sababu ya kugombea Urais kwa Muhula wa Pili ni mipango mizuri waliyonayo kwenye Ilani yao ya Uchaguzi

Kati ya mipango hiyo, ametaja pia kujenga Uwanja wa Ndege Mkoani Njombe, kwa kuwa watu wa Njombe ni wakulima wazuri. Amewatania kwa kusema, ndege pia zitatumika kusafirisha Ulanzi kuwafikia watu wa Dar

Pia, amesema atakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Rufaa Njombe na kuwezesha watanzania wote kuwa na Bima ya Afya na kabla ya kuwa na Bima ya Afya, kwanza wamepanga kujenga Vituo vya Afya, Hospitali na kuongeza bajeti ya kununua madawa

Ameyasema hayo alipokuwa Viwanja vya Polisi, Makambako Mkoani Njombe katika mkutano wa kampeni.

 
Gonjwa la CORONA nalo limepunguza safari za waendao kupata tiba nje ya nchi, ndio maana siku hizi wakubwa na wenye fedha wanatibiwa hapa hapa nchini.
 
Hahahhh eti pesa zipo
ccm mmewaona WaTz mazuzu kweli
Njombe watafanya yao 10.28.20
Mateso wanayopitia wakulima ni Mungu tu mtetezi wao
Wakulima wa Mahindi Maparachichi mnawaletea wahuni toka Kenya kununua kwa bei wanayoitaka wao. Kilimo cha mbao mmewanyang'anya umiliki
Kulima alime mwingine bei muwapangie kwa kukuuza muwaelekeze na vikundi vyenu sijui nini
ccm ni wauaji

Kumkomboa Mkulima ni kura yako
Ccm iwe basi
 
Naomba kuuliza Swali: kwa hivyo tumewaafikiana kwamba miaka 5 ya kwanza ya bwana magufuki , maisha ya wananchi hayajaboreshwa? Kwani alivyoomba Kura 2015, si alisema maisha ya wananchi yataboreshwa na tutakuwa Ulaya? Kama kashindwa awamu ya kwanza, kwanini apewe awamu ya pili?
Huna sera kaa kimya, uliona wapi ulaya inajengwa kwa 5 yrs!? Labda ulaya ya tabora.
 
Aliyebaki kutibiwa nje na mabeberu ni Lisu tu
Uwe unatumia akili basi mara moja moja! Vipi kuhusu mgonjwa ghali zaidi duniani ambaye ni Job Ndugai?

Hujaona akisema wagonjwa wanaotibiwa nje wamepungua na siyo kuisha? Sasa hao wengine ambao wanatibiwa nje anaowamaanisha inamaana anamaanisha Lissu? Kwa kesi ya Lissu kutibiwa nje ya nchi mtu mwenye akili timamu anaweza kuhoji kweli?
Acheni upumbavu, shwain!

Hizi chuki zenu dhidi ya Lissu ndio zinamfanya azidi kupendwa na watanzania!
 
Leo mgombea wa CHADEMA Mh Tundu Antipasi Munghwai Lissu alipaswa kufanya mikutano yake ya kampeni mkoani Kilimanjaro. Ratiba iliyotolewa awali ilisema TUNDU atafanya mkutano mkubwa Wilayani Hai.

Taarifa zilizotufikia zinasema kuwa Mh TUNDU ameshindwa kuendelea na kampeni baada ya kuona mapokezi makubwa ya Dkt. Magufuli aliyoyapata Mkoani IRINGA Jana. TUNDU amelazimika kupumzika ili aweze kujitathimini na kutafuta njia mpya ya kumkabili Dkt. Magufuli. TUNDU aliaminishwa IRINGA ni ngome yake, lakini baada ya mtiti wa jana TUNDU amechanganyikiwa.

Wakati Tundu akitafuta njia ya kurudi tena Iringa, mgombea Ubunge wa Jimbo la IRINGA kupitia CHADEMA Mchungaji Peter Msigwa amefungua program ya kutafuta wafuasi wa kumsaidia mitandaoni.

Mikutano iliyoendelea Leo Ifunda, Mafinga, Nyololo, Makambako na Silali inazidi kumchanganya Tundu.

#JPM2020
 
Hakuna mapokezi ya maana iringa zaidi ya kuwasafirisha watu kwa malori toka sehemu mbali mbali za mkoa huo na kuwalazimisha wafantakazi kutokwenfa makazin ili kuhudhuria mkutano huo.

Kumlazimsha mtu kuja kt mkutano wako kunamlazimisha tena kukupigiankura?? La hasha
Leo mgombea wa CHADEMA Mh Tundu Antipasi Munghwai Lisu alipaswa kufanya mikutano yake ya kampeni mkoani Kilimanjaro. Ratiba iliyotolewa awali ilisema TUNDU atafanya mkutano mkubwa Wilayani Hai.

Taarifa zilizotufikia zinasema kuwa Mh TUNDU ameshindwa kuendelea na kampeni baada ya kuona mapokezi makubwa ya JPM aliyoyapata Mkoani IRINGA Jana. TUNDU amelazimika kupumzika ili aweze kujitathimini na kutafuta njia mpya ya kumkabili JPM. TUNDU aliaminishwa IRINGA ni ngome yake, lakini baada ya MTITI wa jana TUNDU amechanganyikiwa.

Wakati TUNDU akitafuta njia ya kurudi tena IRINGA, mgombea Ubunge wa Jimbo la IRINGA kupitia CHADEMA Mchungaji Peter Msigwa amefungua program ya kutafuta wafuasi wa kumsaidia mitandaoni.

Mikutano iliyoendelea Leo Ifunda, Mafinga, Nyololo, Makambako na Silali inadhidi kumchanganya Tundu.

#JPM2020
 
Back
Top Bottom