Uchaguzi 2020 Yaliyojiri kampeni ya Dkt. Magufuli kuwania Urais 2020-2025 mikoani Iringa na Njombe (Sept 29, 2020)

mapokezi au fiesta, kumbuka hata Hashimu Rungwe angeambatana na watoa burudani plus kusomba watu kama mifugo kwenye mikutano yake pasingetosha...kiukwel watu wengi huenda kuona show ya bure kwenye mikutano ya Jiwe na ndio maana hata akimaliza kuhutubia watu huwa hawaondoki kwasabb show huwa inaendelea.
 
ndabila wa ileje vip ndugu...
 
Waelezee ukweli JPM anazidi kupasua anga balaa
 
Magufuli asitufanye Watanzania kuwa wajinga kama hao wanachama wa CCM kwani waliokuwa wanakwenda kutibiwa nchi za Nje walikuwa wananchi wanyonge au vigogo huko Chamani na Serikalini kama akina Ndugai aliyekwenda India na familia na wasaidizi wawili na kukaa Hotel ya Nyota 5 miezi 5. Magufuli Rais na Waziri wake wa Afya walikubali kulipa gharama hizo na zile kubwa za matibabu kwa kukaa nje ya Hospital na madaktari kwenda kumhudumia kumbe angeweza kupanga nyumba karibu na Hospital kama alivyofanya Nyerere London na Lissu Ubelgiji. Kama mtu yeyote angefuatilia matibabu ya Ndugai India angekuta Wahindi bado wanashangaa mgonjwa toka nchi masikini akakaa Hotelini miezi 5 kumbe angeweza kupata hata chumba cha VIP Hospitalini ikawa nafuu kwa Tanzania mlipaji. Mabilioni Serikali iliyolipa ndo umeleta urafiki wa kishetani (unholy alliance) kati ya Magufuli na Ndugai na kufanya Bunge kuwa kama Idara ya Serikali ya Magufuli ili kufunika kombe mwanaharamu apite.
Kuhusu matibabu anayodai sasa kwa juhudi za Awamu ya Tano yanapatikana nchini lakini nani wananufaika na matibabu hayo kama si walewale waliokuwa wanatibiwa nje ya nchi na kugharimiwa na Serikali kwa sababu gharama ni kubwa mno kwa mkulima au mfanyakazi wa chini kumudu. Bima ya Afya kwa wote amerukia tu ni mpango wa Lissu na wanachama wa CCM wamemponda sana wakihoji fedha atapata wapi utadhani Magufuli anatoa pesa mfukoni kwake kununua madege au kujenga Uwanja wa Kimataifa kijijini kwake. Hospitaliii ya Muhimbili ilijengwa na wakoloni na kuboreshwa mara kwa mara na Awamu ya Kwanza na Awamu zilizofuata, Mloganzila imejengwa na Kikwete, ya Dodoma na Mkapa RIP, KCMC na Bugando zimejengwa na Wakristo. Zahanati na Vituo vya Afya vinavyoimbwa kila wakati na kila mahali vingi vimejengwa kwa nguvu za wananchi na vingi vimekataliwa kufunguliwa kwa kujengwa chini ya viwango kwa sababu ya 10% ndo maana ni takwimu tu zinatajwa lakini havionekani. Wakazi wa Mkoa wa Njombe hawahitaji kiwanja cha Ndege kubeba ulanzi wanahitaji utekelezaji Mradi wa barabara toka Njombe mjini kupitia Lupembe mpaka Morogoro kuunganisha na TANZAM kufupisha safari kwenda Dar es Salaam. Mradi huu muhimu ulibuniwa Awamu ya Nne lakini Awamu ya Tano ya maneno bila vitendo ilipoingia madarakani ikawa mwisho wa safari na sasa anazungumzia Uwanja wa Madege.
 
Safi sana kamanda, umesomeka!
 
Aliyebaki kutibiwa nje na mabeberu ni Lisu tu

Ni kweli kabisa, kama Kingunge aliumwa na mbwa akafa akipatiwa matibabu kwenye hospitali yetu kubwa, Lisu kwa risasi 16 saa hii kampeni hizi Magufuli angeongea kisukuma? Ukiona mtu anatibiwa magonjwa makubwa hapa nchni, ujue kakosa hela ya kwenda nje na sio uzalendo.
 
CCM ndio magwiji wa siasa za Tanzania, mtaelewa tuu.

JPM ANATOSHA
CCM USHINDI NI JADI
 
Nani achague chama chakavu wewe.

Watu tunataka Haki ,Uhuru na Maendeleo ya Watu.
 
KWA UPUMBAVU HUU WEWE NI POLEPOLO AU BUSHIRI HUNA HATA AIBU! LAKINI SISHANGAI MAANA HATA MARINDA HUNA
 
Ukishajenga uwanja unamsaidiaje mkulima asiyepanda ndege au mmachinga azungushaye bidhaa mtaani au Mama ntilie huku mtaani. Wezesha wananchi wapate hela kisha kusanya kodi ujenge miundombinu yako. Unajenga hospital kwani watanzania wote ni wagonjwa?
 
Hovyooo kabisa, kwa taarifa yako muda huu anatokea Rombo anakuja Moshi baada ya kufanya mikutano Hai, Sanya Juu, Kamwanga, Tarakea, Mkuu, Himo.

MATAGA mjipange kudanganya wasiojua.
 
Hongera Sana jpm,nimekusikiliza hata huko mbeya mwanzo mwisho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…