Yaliyojiri katika Chaguzi Ndogo: Uchaguzi wa ubunge jimbo la Dimani na madiwani Tanzania Bara

kweki chadema media yani mtu mmoja apige wananchi wote
 
Acha Mapovu yawatoke Chadomo wamekung'utwa mpaka kata ya Matevez Arusha.

Ndo faida ya chama kununuliwa
kwa arusha hayo yalitegemewa. gambo amesimama imara kuhakikisha anabomoa chadema arusha kwa kumfunga LEMA na hata kupambana na madiwani wa arusha. kwa tume hii chini ya wakurugenzi hawa makada wapinzani wasahau.
 
Mwenye empty talks nani? Upinzani? Na nyie empty ballots?
 
Unajua watanzania ni watu wa ajabu sana. Ninyi wapinzani kamwe hamtashinda kwa mfumo huu wa uendeshaji uchaguzi ulivyo. Tume ya uchaguzi sio taasisi huru hawawezi wakasimamia haki hawa. Yaani wasimamizi wa uchaguzi ni makada wa chama tawala halafu nyie wapinzani mnategemea mtashinda?

Mkurugenzi wa halmashauri ambae ni kada wa chama tawala ndie msimamizi wa uchaguzi!!!

Mkuu wa wilaya ambae anatajwa kwamba ndie mwnyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ni kada wa chama tawala.

Amkeni kutoka kwenye usingizi, agenda yenu namba moja iwe ni mabadiliko ya katiba hasa eneo hili la uchaguzi.

Uwanja wa kwao
Refa wa kwao
Washika vibndera wa kwao
Kamisaa wa kwao

Halafu mnategemea kushinda????

Usikimbie kama huna breki
 
Matokeo yaliyotufikia toka kijichi ni km iguatavyo
Ccm 61%
CUF 22%
CDM 14%
Wapiga kura walikuwa 5000 na kidogo kati ya wapiga kura zaidi ya elfu 20 waliotarajiwa
Source wakala mkuu chadema
Kassim Bingwe
 

Jakaya aliwalatea Katiba Mpya yenye Tume huru ya Uchaguzi wakataa kuendelea na Mchakato wa Katiba Mpya akawaita Ikulu akawabembeleza na Chai isiyo na Pipi Bali bites wakapewa wakakubali kuendelea na Katiba Mpya.

Waliporudi Bungeni akili Wakaacha Guest house wakamkabidhi Lipumba awaongoze nae akawaambia wasuse waondoke na kweli Wakaondoka!

Pamoja na Kususa na Jk akijua anakabidhi Nchi kwa Mtata akawaomba wamuunge Mkono walau tupige kura ya Maoni kabisa na Kazi ya Rais ajae iwe kutekeleza tu ya Katiba Mpya wakakataa nae kwa Uungwana wake akaridhia japo kwa Shingo Upande!

Wapinzani wangekuwa na Think tanks za Kutosha wakati wa Jk wangeweka Misingi mingi na mizuri sana ya Demokrasia Tatizo ni kuwa Wote waliwekeza akili zao kwa Lipumba na Tundu Lissu kuwaamulia cha kufanya!
 
mkuu huo ni uwongo. fuatilia taarifa zako vizuri
 
Mkuu hiki ulichokiandika ni kikubwa sana kwa akili yake ndogo kuelewa.
 
Lowassa fisadi..CDM
Lowassa siyo fisadi .. CCM
Lowassa fisadi...CCM
Lowassa siyo fisadi...CDM

Tushike lipi?
Mwenye majibu sahihi tafadhali yasiyo ya kisiasa.
Mimi sijawahi kusikia CCM wakisema Lowasa siyo fisadi.
 
Bado kuna binadamu mwenye akili timamu anapanga foleni kuipigia kura ccm,!!! maajabu haya
Dharau zenu ndio zinazofanya ccm iendelee kushinda. Siajabu mkaja na threads kutukana waliopiga kura.
 

Chama cha upinzani ni kupinga kila kitu maana kwa akili zao za mchangani wenye uwezo wa kushinda ni wao, chama tawala kikishinda ni fujo na kudai wameibia. Puuuuu!!!!!
 

Nadhani ifike mahali watanzania tujue kuwa Haya ni matumizi mabaya ya kodi zetu. Uchaguzi gani huu, si wateuliwe kutoka chama tawala hatuna sababu ya kuharibu fedha za umma wakati chama tawala kimeshateua viongozi wake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…