Bado kuna baadhi ya wananchi na hasa wapinzani wanaamini kama mabadiliko Tanzania yataletwa na waliokuwa viongozi wakuu waandamizi ndani ya CCM na serikali ya CCM ambao ni Edward Lowassa na Maalim Seif.
Ikumbukwe kuwa Lowassa na Maalim Seif wanalishwa, kuvalishwa na kulindwa na serikali ya CCM. Hii ina maana na mantiki kubwa sana kwenye siasa za nchi za Afrika. Yaani wanakaa kupanga mikakati ya kuiangusha serikali ya CCM huku wakilindwa na maofisa waliotumwa kufanya kazi na Rais.
Aliyewahi kusema ‘’wajinga ndio waliwao’’ hakukosea kwa sababu hata Tanzania katika uwanja wa siasa kuna wajinga wengi sana ambao ''wanaliwa'' na baadhi ya wanasiasa ambao ni political entrepreneur.
Nilikuwa ninashangaa na kucheka kila nikisoma mabandiko ya baadhi ya watu wakisema ‘’Uchaguzi mdogo wa ubunge na madiwani katika kata 20 ni kipimo cha uongozi wa Rais Magufuli’’.
Nikawa ninajiuliza, kama chaguzi ndogo ndio mizani ya kipimio cha utendaji wa Rais Magufuli kwa kutumia mawe ya mizani yanayoitwa Lowassa na Maalim Seif, basi itakuwa ni kupoteza muda kwa sababu haya mawe hayafai kutumika katika mizani. Haya ni mawe ya kugushi (fake).
Matokeo ya Uchaguzi mdogo wa Mbunge na Udiwani katika kata 20 tumeyasikia na kuyaona. Ni kipigo na kilio kwenye kambi za upinzani.
Ninafahamu kuna baadhi ya watu watakuja na nyimbo zenye chorus zinazosema uchaguzi haukuwa huru na haki kama vile wanalazimishwa kuingia kwenye chaguzi.
Mwaka 2015 wakati vyama vya upinzani vinapanga mkakati wa kukabiliana na CCM, Lowassa alijitokeza na kuwaambia kazi hiyo wamwachie yeye, wao kazi yao iwe ni kupiga kura na kurudi nyumbani. Matokeo yake tunayafahamu.
Huko Zanzibar, wakati CUF inaendelea kufanya vizuri wakati wa zoezi la kuhesabu kura, Maalim Seif alijitokeza na kuvuluga uchaguzi baada ya kujitangaza mshindi kinyume cha sheria ya uchaguzi. Yaliyojiri baadaye ni historia.
Kwa sasa Maalim Seif amewashawishi tena CUF waingie kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Dimani, Zanzibar wakati huku Bara, Lowassa akiwashawishi CHADEMA waingie tena kwenye uchaguzi wa madiwani wakati hawajajipanga ipasavyo. Matokeo yake tumeyaona. Wamepata kipigo kama cha mwizi!
Waingereza hupenda kusema, “It is difficult to see the picture when you are inside of the frame.”
Wajinga wataendelea kuimba Mabadiliko Lowassa, Lowassa Mabadiliko huku CCM ikiendelea kuwapa kipigo cha kisiasa katika chaguzi mbali mbali.
Leo ndo leo uchaguzi wa ubunge jimbo la Dimani Zanzibar na uchaguzi wa madiwani kata 20 Tanzania bara.<br /><br />Ni chaguzi zitazotoa mwelekeo na mabadiliko na ukubalikaji wa vyama tangu uchaguzi mkuu wa 2015.<br /><br />Karibuni tupeane updates na matukio yanayojiri huko.<br /><br /><b>.......Updates...........</b><br /><br />* Uchaguzi wa Ubunge unafanyika kwenye jimbo la Dimani, Wilaya ya Magharibi “B”, Mkoa wa Mjini Magharibi – Zanzibar<br /><br />Uchaguzi wa madiwani unafanyika kwenye kata Ishirini (20) katika Halmashauri Kumi na Tisa (19) za Tanzania Bara, kata hizo ni...<br /><br />1. Ngarenanyuki (Meru DC, Arusha),<br />2. Igombavanu (Mufindi DC, Iringa),<br />3. Ikweha (Mufindi DC, Iringa),<br />4. Kiwanja cha Ndege (Morogoro MC, Morogoro),<br />5. Ihumwa(Dodoma MC, Dodoma),<br />6. Kijichi (Temeke MC, Dar es Salaam),<br />7. Kahumulwa (Sengerema DC, Mwanza)<br />8. Maguu (Mbinga DC, Ruvuma),<br />9. Ng’hambi (Mpwapwa DC, Dodoma),<br />10. Kimwani (Muleba DC, Kagera),<br />11. Kinampundu (Mkalama DC, Singida),<br />12. Isagehe (Kahama TC, Shinyanga),<br />13. Kasansa (Mpimbwe DC, Katavi),<br />14. Duru (Babati DC, Manyara),<br />15. Malya (Kwimba D.C, Mwanza),<br />16. Misugusugu (Kibaha TC, Pwani),<br />17. Mateves (Arusha D.C, Arusha),<br />18. Nkome (Geita DC, Geita),<br />19. Lembeni (Mwanga DC, Kilimanjaro) na<br />20.Uchaguzi udiwani Kata ya Ngarenanyuki DED na ccm wapora daftari la wapiga kura
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru Bwana Christopher Kazeri anatembelea vituo akiwa ameambatana na viongozi wa ccm.Sheria za uchaguzi haziruhusu viongozi wa vyama vya siasa kupiga kambi kwenye vituo vya uchaguzi.Hii imeweza kutokea Ngarenanyuki tu mkurugenzi wa halmashauri ambaye ni msimamizi wa uchaguzu kutembea na viongozi wa ccm.<br /><br />mkurugenzi akiwa ameambatana na makada wa ccm wamewanyang'anya mawakala wa vyama daftari lenye majina ya wapiga kura.<br /><br />Safari ya demokrasia kwa nchi yetu bado sana.<br />Hii haikubaliki popote.<br /><br />Tume ya taifa ya uchaguzi kwa mtindo huu huu uchaguzi hauwezi kuwa huru na haki.<br /><br />--<br /><b>
Francis12</b>, <font color="[HASHTAG]#b30000[/HASHTAG]">UPDATES MCHAGUZI MDOGO JIMBO LA Kumetokea mgogoro kati ya mawakala wa CUF na Askari Polisi. Hali hii imepelekea mawakala wa CUF kuondolewa kwa nguvu kwenye vyumba vya kupigia kura na hivyo mawakala wa CCM kubaki peke yao.Sababu za mgogoro huu ni kama ifuatavyo:Mawakala wa CUF amegundua baadhi ya masanduku yamejazwa kura ambazo zimeshapigwa tiki kwa mgombea wa CCM.-Mawakala wa CUF wamegundua kuwa kuna watu hawamo ndani ya daftari la kupiga kura ila wamekuja kupiga kura na wameruhusiwa kupiga licha ya majina yao kukosekana kwenye daftar
i.Chumba number 6 kituo cha Kibondeni, imegundilikana kwamba masunduku yote yaliyopo yamejazwa kura ambazo zimeshapigwa tayari.Wapiga kura wengi jimbo la Dimani ni hewa.
Police wameanza kupiga watu maeneo ya Fuoni kituo cha Kibondeni baada ya watu hao kudai kuna kura feki kwenye kituo hicha.Katika kituo hicho cha Fuoni mabasi yamekua yakisomba watu na kuwaleta kupiga kura. Watu hao si wakazi wa jimbo la Dimani. Picha hapo chini inaonesha moja ya mabasi yanayotumika kusomba watu na kuwapeleka vituoni kupiga kura
USHABIK MBAYA SANA UPO JF WENZIO WAPO VITUON