Fukara
JF-Expert Member
- Dec 28, 2013
- 1,625
- 928
Mgeni rasmi ni Rais Jakaya kikwete, namuona Ali shein, Kinana na Makamu wa rais Billal.
Rais kikwete anatoa hotuba fupi na kuwashukuru watanzania na wana CCM
Hitilafu inatokea mic zinagoma wanabaki kushangaa.
Bado anazungumzia jengo jipya na kuhusu pia niya ya kukodisha jengo hilo kwa shughuli mbalimbali.. anasema CCM inaviwanja vingi na vingine wakubwa wanagawana.
Anawasifia UVCCM, UWT,na Jumuiya ya Wazazi kwa kuonyesha mfano mzuri kutumia viwanja vyao vizuri, kuwekeza kwa tija
Namuona pia balozi wa China.
Anawashukuru wajenzi na kumshukuru Kinana na kumuita 'jembe' shukurani maalum anasema ukiona vya elea ujue vimeundwa.
Rais anazindua jengo rasmi wajumbe wa kamati kuu wanaitwa na ndugu Nape kupiga picha na rais.
Rais na balozi wa china wanafungua jengo kwa kufungua pazia, kwenye jiwe la msingi
====
Ukumbi huu una uwezo wa kubeba zaidi ya watu 3,000 na ulianza kujengwa na kampuni ya CRJE mwaka 2014. Jina rasmi la ukumbi ni CCM Convection Centre. Shughuli imeanza muda na anaeongea kwa sasa ni mwenyekiti wa chama.
Kikwete: Sera ya kujitegemea ndani ya chama sijui kama inasomwa, sera yetu sisi ni wafadhili. Kuna vitu tunavyoweza tukavifanya na tukapa pesa yetu clean kabisa, ni wakati sasa katibu mkuu tukaunda ofisi ya inspector kwenye chama chetu, tena sio auditor bali inspector kabisa.
Mikoa yenye viwanja waombeni Jitegemee waje, hiki chama hakina sababu ya kuwa kinaomba omba kwa rasilimali tulizanazo, tufungue jengo letu na tulitumie kwa tukio la kihistoria.
Nawashukuru wajenzi, namshukuru katibu mkuu 'jembe', usione vianaelea ujue vimeundwa. Ukitimiza wajibu wako umefanya jambo jema na sasa tufungue jengo letu. (King'ora kinabonyezwa na mwenyekiti kuashiria ufunguzi)
====
RAIS KIKWETE AFUNGUA UKUMBI MPYA WA MIKUTANO WA CCM, MJINI DODOMA JULAI 09, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM),, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akizungumza wakati wa wakati wa hafla ya ufunguzi wa Ukumbi mpya wa mikutano wa CCM wa Dodoma Convention Centre, uliopo njia ya kuelekea Chuo Kikuu cha UDOM, mjini Dodoma leo Julai 9, 2015.Kulia kwake ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal na kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Mzee Phillip Mangula.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akibonyeza kitufe cha kengere kuashiria ufunguzi rasmi wa Ukumbi mpya na wakisasa wa mikutano wa CCM unaofahamika kwa jina la Dodoma Convention Centre, uliopo njia ya kuelekea Chuo Kikuu cha UDOM, mjini Dodoma leo Julai 9, 2015.Kulia kwake ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Balozi wa China nchini Tanzania, Dkt. Lu Youqing. Wengine ni Makamu Mwenyekiti wa CCM – Bara, Mzee Phillip Mangula (wa pili kulia), Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Abdulrahman Kinana pamoja na Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa China nchini Tanzania, Dkt. Lu Youqing wakifunua kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Ukumbi mpya na wakisasa wa mikutano wa CCM wa Dodoma Convention Centre, uliopo njia ya kuelekea Chuo Kikuu cha UDOM, mjini Dodoma leo Julai 9, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jakaya Kikwete, akimkabidhi mfano wa ufunguo wa Ukumbi mpya wa mikutano wa CCM wa Dodoma Convention Centre, Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Abdulrahman Kinana, baada ya kuufungua rasmi ukumbi huo leo Julai 9, 2015 mjini Dodoma.
Picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Chama na Serikali baada ya uzinduzi huo.
July 9, 2015 | Chanzo: Ikulu
Rais kikwete anatoa hotuba fupi na kuwashukuru watanzania na wana CCM
Hitilafu inatokea mic zinagoma wanabaki kushangaa.
Bado anazungumzia jengo jipya na kuhusu pia niya ya kukodisha jengo hilo kwa shughuli mbalimbali.. anasema CCM inaviwanja vingi na vingine wakubwa wanagawana.
Anawasifia UVCCM, UWT,na Jumuiya ya Wazazi kwa kuonyesha mfano mzuri kutumia viwanja vyao vizuri, kuwekeza kwa tija
Namuona pia balozi wa China.
Anawashukuru wajenzi na kumshukuru Kinana na kumuita 'jembe' shukurani maalum anasema ukiona vya elea ujue vimeundwa.
Rais anazindua jengo rasmi wajumbe wa kamati kuu wanaitwa na ndugu Nape kupiga picha na rais.
Rais na balozi wa china wanafungua jengo kwa kufungua pazia, kwenye jiwe la msingi
====
Ukumbi huu una uwezo wa kubeba zaidi ya watu 3,000 na ulianza kujengwa na kampuni ya CRJE mwaka 2014. Jina rasmi la ukumbi ni CCM Convection Centre. Shughuli imeanza muda na anaeongea kwa sasa ni mwenyekiti wa chama.
Kikwete: Sera ya kujitegemea ndani ya chama sijui kama inasomwa, sera yetu sisi ni wafadhili. Kuna vitu tunavyoweza tukavifanya na tukapa pesa yetu clean kabisa, ni wakati sasa katibu mkuu tukaunda ofisi ya inspector kwenye chama chetu, tena sio auditor bali inspector kabisa.
Mikoa yenye viwanja waombeni Jitegemee waje, hiki chama hakina sababu ya kuwa kinaomba omba kwa rasilimali tulizanazo, tufungue jengo letu na tulitumie kwa tukio la kihistoria.
Nawashukuru wajenzi, namshukuru katibu mkuu 'jembe', usione vianaelea ujue vimeundwa. Ukitimiza wajibu wako umefanya jambo jema na sasa tufungue jengo letu. (King'ora kinabonyezwa na mwenyekiti kuashiria ufunguzi)
====
RAIS KIKWETE AFUNGUA UKUMBI MPYA WA MIKUTANO WA CCM, MJINI DODOMA JULAI 09, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM),, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akizungumza wakati wa wakati wa hafla ya ufunguzi wa Ukumbi mpya wa mikutano wa CCM wa Dodoma Convention Centre, uliopo njia ya kuelekea Chuo Kikuu cha UDOM, mjini Dodoma leo Julai 9, 2015.Kulia kwake ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal na kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Mzee Phillip Mangula.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akibonyeza kitufe cha kengere kuashiria ufunguzi rasmi wa Ukumbi mpya na wakisasa wa mikutano wa CCM unaofahamika kwa jina la Dodoma Convention Centre, uliopo njia ya kuelekea Chuo Kikuu cha UDOM, mjini Dodoma leo Julai 9, 2015.Kulia kwake ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Balozi wa China nchini Tanzania, Dkt. Lu Youqing. Wengine ni Makamu Mwenyekiti wa CCM – Bara, Mzee Phillip Mangula (wa pili kulia), Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Abdulrahman Kinana pamoja na Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa China nchini Tanzania, Dkt. Lu Youqing wakifunua kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Ukumbi mpya na wakisasa wa mikutano wa CCM wa Dodoma Convention Centre, uliopo njia ya kuelekea Chuo Kikuu cha UDOM, mjini Dodoma leo Julai 9, 2015.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jakaya Kikwete, akimkabidhi mfano wa ufunguo wa Ukumbi mpya wa mikutano wa CCM wa Dodoma Convention Centre, Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Abdulrahman Kinana, baada ya kuufungua rasmi ukumbi huo leo Julai 9, 2015 mjini Dodoma.
Picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Chama na Serikali baada ya uzinduzi huo.
July 9, 2015 | Chanzo: Ikulu
