1.Members:.Huyu ni ndugu na kipenzi wa mwenyekiti na familia kwa ujumla, alishaandaliwa toka siku nyingi,ndo maana hata jana Rais alipoteua wasaidizi wake Ikulu ilikua lazima mtu ufikirie Mara mbili mbili na huyu ndiye mgombea atakayepeperusha bendera ya chama.
2.Magufuli:Huyu nae utendaji wake pekee ndiye uliempatia nafasi hakuna kiingine japo nae ni swahiba wa karibu wawenyekiti.Kwake kupenya kwenye vikao vya mbele ni ngumu sana Labda busara ya kawaida tu itumike.Anaweza kua PM japo kiuhalisia yeye ni bora kuliko wote walioteuliwa.
3.Asha Rose Migiro: Huyu kwanza jinsia ndiyo kigezo pekee japo nae alikwishaandaliwa toka siku nyingi lakini baadae upepo ukahamia kwa mebe. Kwake kupenya mbele inategemeana na kelele za wanawake wenzake mkutano mkuu.
4.Mama Amina: Huyu jinsia na Uzanzibar wake kama mwanamke ndivyo vilivyombeba, Kuna uwezekano mkubwa akawa makamu wa Rais maana naye kupenyeza kwake mbele ni kelele za wanawake wenzie huko mkutano mkuu.
5.January Makamba: Ikumbukwe kwamba huyu bwana baba yake aliwahi kua katibu mkuu wa chama, hiyo pia ni sababu kwahiyo kuna uwezekano kwamba hii ni fadhila na anaandaliwa kwa baadae kumrithi atakaekua Rais,Sidhani kama Janauary Makamba Anaweza kumkaribia Mwigulu nchema kiutendaji wa kazi.Anayo nafasi kubwa sana kupenyeza huko mbele maana wanaomuunga mkono ni wengi lakini atawekwa kando kama JK 1995 nasubiri baadae.
Ukweli na uhalisia ndo huo!