Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

habari wanajanvi, mda huu dodoma hali si ya kawaida kama ilivyozoeleka , wapambe watia nia mbali mbali wameonekana kusononeka sana na wengine kutoweka kabisa karibia na eneo la tukio la mchakato mzima wa kumpata mtia nia, wameanza kuwapunguza wengi hasa ambao hawana vigezo kamili na mlolongo wa ukataji ulikuwa hivi
1. ametolewa ambaye elimu yake si sawa na anayetakiwa, yule mtia nia wa kigoma mr mahale,
2.wakatolewa wenye kashfa nzito sana na ni vigumu kuwasafisha hapa tuna, edward lowassa..richmond, . sospeter muhongo ,, tegeta escrow, sumaye.. uuzwaji wa nyumba zza serikali na uuzaji wa mashirika ya umma ovyo, membe kaponea chupuchupu kukatwa ana makundi ya kukigawa chama, wasira ana kashfa ya rushwa mwaka 1995,
3.uzoefu na umri, japo wote wametimiza umri lakini bado hawajawa na uzoefu wa kutosha, hapa ni kigwangala, na mwigulu nchemba.

waliotangulia kuingizwa kwenye list ni
1.asha rose migiro gender factor , uwajibikaji wake na usafi wake
2.augustino ramadhan zanzibar factor na kutokuwa na makundi na uwajibikaji wake,
3.makongoro nyerere, uwajibikaji na kuchukia rushwa kukemea hadharani wala rushwa na hali ya juu ya uthubutu kwenye maslahi ya wengi hana woga, pia nyerere factor usafi na kumuenzi mwalimu nyerere,
4.pombe magufuri, uwajibikaji wake na hasa kutekeleza sheria bila kupindishwa, na muwajibikaji wa hali ya juu
5. mizengo pinda , ni kiongozi mkuu wa serikali imekuwa vigumu serikali yenyewe kushindwa kutompitisha mtekelezaji mkuu wa ilan ya chama hicho bungeni na pia akikatwa itaonekana serikali nzima ilikuwa haifai, pia ni mtu msafi mwenye busara
6. samwel sitta, kwakuwa anasimamia sana matakwa ya chama na ameweza kutoyumbishwa wakati wa katiba mpya, amepitisha mapendekezo asilimia kubwa yaliyokuwa yanapendelewa na chama chake,mbali ya hapo ana uthubutu na ni mwajibikaji,
7.mark mwandosya
8.bernad membe


hapo ndo itatoka tano bora ,tatu mpaka moja bora,

Hivi mnajisikiaje mkitumia muda mwingi kuandika habari za uongo mtupu wakati hamna kitu kama hicho. Tulia Nape ataleta habari rasmi. watu tunaingia jf ili tuone Nape kaongea nini baada ya vikao make hizo ndizo habari sahii na rasmi kama huna habari tulia kama sisi usubiri jibu utalipata leo hii.
 
Yeye anatumwa tu itabidi ataje tu ndiyo siasa.

Kwa uzoefu wako wa siasa za CCM mfano akapita Lowassa je kutakwa na uadui kati yake na Nape au ni mchezo wa fitna wa kawaida katika Siasa?
 
jamani taarifa ni ya uhakika asilimia mia moja lowassa amekatwa rasmi na viongozi wameamua kwa pamoja liwale na liwe tu pinda kapeta pamoja na jaji ramadhani wengine sijapata waliobakia ila ni za uhakika

Kwa muonekano wako kwenye profile picture yako wala huwezi kuwa na habari za ukweli hizo ni porojo nyingine zinazoendelea na tumeshazizoea wala hatushutuki hadi Nape aongee habari rasmi baadae
 
Naona wazee wa kubet wanaendelea kuweka mizigo hii deal ningempa mdosi angepiga pesa sana.

Mimi hapa napiga Kilimanjaro yangu kimyaaa,nasubiri SAA kumi na mbili top five maana cc ndo imekaa muda si mrefu.nikisikia tu mamvi kakatwa nageukia wine fasta maana chama ni maarufu kuliko kingunge na rostam
 
kuna kitu nashindwa kuelewa kama ma ccm mnajua kua lowasa ndo anatakiwa kushinda sasa mbona mmejaa upepo sana na leo ndo mtajua kua mwanga iko singida au kilimanjaro
 
Migiro mgombea mwenza. Tumsubiri prezdaa.. Kati ya magufuli na judge. Habari hii ni ya uhakika.
 
tatzo nyotaaah lowasa asipopita alvyohonga na kugaramia mabiliOn kwenye kutangaza nia si atafariki kwa wasiwas
leo kitanuka bwayy
 
Team el tujipe pole tu, mi nalia tu hapa. Naelekea kula viroba walau npunguze machungu.
 
Taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na mmoja wa viongozi wakuu wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM) zinasema, jina la Lowassa limeondolewa kutokana na
shinikizo kutoka kwa baadhi ya viongozi.

Ni kweli kuwa jina la Lowassa
limeondolewa katika kinyanganyiro hiki. Wakubwa wamekuja na msimamo na wameapa kuwa hawataki kumsikia mtu anayeitwa Lowassa akikatiza kuingia NEC , ameeleza mtoa taarifa wa gazeti hili.

Vikao vya uteuzi vya CCM Kamati
ya Maadili, Kamati Kuu (CC) na
Halamashauri Kuu tayari vimeanza mjini Dodoma mchana huu. Kikao cha NEC kinatarajiwa kuanza saa mbili usiku.

Wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema, ikiwa jina la Lowassa litaondolewa katika hatua hiyo ya awali, basi ndoto za mwanasiasa huyo kushika madaraka ya urais tangu mwaka 1995, zitakuwa zimezimwa.

Habari zinasema, kuzimwa kwa ndoto za Lowassa, kunafuatia taarifa kuwa mchakato wa uchujaji majina ya wasaka urais, kuendeshwa na idara ya usalama ya chama ambayo imesheheni wabaya wake.

Katika hatua nyingine, taarifa
zinamnukuu mmoja wa viongozi wa kamati kuu akisema, chombo hicho muhimu katika uteuzi wa wagombea urais, imegawanyika.

Mganyiko unatokana na baadhi ya watu kutaka Lowassa asikatwe, huku wengine wakisema, sharti aondolewe,
anasema mmoja wa watoa taarifa wa gazeti hili.
 
Acha utani ndugu..kuna watu wananitegemea nitoe majibu yakueleweka kabla habari hazijasambaa..wanajanvi mtanifanya nisiaminike tena hapa kazini

Pole mkuu nimemakizia hapo lakini kwamba ni ndoto teh teh teh
 
Back
Top Bottom