Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

attachment.php
attachment.php
 
Inavyoonekana JK anamrusha roho EL awe na kisebusebu na kutudanganya sie kuwa hakumpa swahiba yake lakini ndio chaguo lake atakae mtanganza.
 
Cc haitendi haki.umeiona ile speaker ya el.(kingngngmblemlu).anamsemea in public el.eakati wagombea wengine hawana pa kusemea wakati huu.kisha anaingia kikaoni huku anajina la mtu kibindoni.ningekuwa ni mmoja wa wagombea ningemgomea asiingie.hafai kuwa hakimu mzuri humo.
 
Nchi imekwisha,hatamaadili ya kiuongozi,hayafuatwi.el akipita basi wajue chama ni chake.sio cha watu tena.amekununua.kama mabilionea wanavyo nunua vilabu england.wapime upepo wa kesho ni hatari sana kumpitisha el,kuliko kumkata.
 
7.Makongoro mropokaji kama yule daaaa!!! Na imagine majibu yake yatakavyokuwa mpk hata sitamani labda kama kuna cheo cha msemaji wa NCHI kama cha Jery Muro

humfaham makongoro wewe!!
 
Kwani tatizo ni nini, si watamke tu kama ifuatavyo kama wanaona kigugumizi\
1. EL
2. Dr. Bilal
3. Makamba
4. Acha Rose
5. Jaji mstaafu halafu baadae

Wabaki EL
ASharose
Jaji mstaafu

Halafu baadae

EL ili tupambane nae sisi M4C
 
Nalala nikiamka najua nitakuta wametupatia fisadi wetu mkuu
 
Habari zilizonifikia hivi punde kutoka mkutanoni Dodoma ni kwamba, tayari yale majina 5 yameshapatikana na sasa mazingira yanatengenezwa ili kuyataja rasmi na kwa mlio Dodoma hapo chungulieni nje mnaona ugeni gani mkubwa wa ghafla wana ulinzi na usalama hapo?

Mnajua ni kwanini ulinzi huo umeimarishwa ghafla mchana huu? Muda wowote kuanzia sasa, hayo majina yatatajwa na mchana huu baada ya mapumziko kidogo wajumbe wanarudi upesi ukumbini kufanya mchujo na kuwabakisha watia nia 3 tu ambao kesho ndiyo watashindanishwa ukumbini na hatimaye kupatikana mmoja.

Ninaloweza kusema na ambalo ni fumbo kwenu sisi wazalendo tunamshukuru sana na mzee Philip Mangula, wazee wa CCM na wenye heshima kubwa na mdahalo ule wa juzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, kwani kilichopitishwa kimetokana na matamshi, matakwa na wosia wao na nasema kuwa chama sasa kimerudi katika misingi ya Baba wa Taifa na Watanzania wenzangu haswa wazalendo na wenye uchungu na nchi hii popote mlipo tafadhalini anzeni kufurahi kwani Mwenyezi Mungu amesikia kilio chetu. Nimefurahi na akhsante Mungu. Sasa nitalala usingizi.

Kazi imekwisha, hakuna cha kaskazini wala kusini na maslahi na ustawi wa chama ndiyo umezingatiwa ili kuua makundi ambayo yangekidhoofisha chama.

Mchana mwema nyote ila msikae mbali na radio zenu kwani muda wowote patakuwa na breaking news ya utangazwaji wa majina hayo yaliyoingia 5 bora. Mimi sasa kwa furaha iliyoje nakwenda zangu kufurahi. Nchi imerudi rasmi kwa wazalendo.

Usiniambie maneno hayo. Nitafurahii leo ukizingatia week end ndio inaanza. Nafurahi kabla hawajatangaza.
 
Ukongwe wa ccm umefanya viongozi wake waamini kuwa ccm itaishi milelele na viongozi wake wataishi daima, hicho ndicho kinachowapa jeuri kuamini kuwa vyama vingine ni wasindikizaji tu na kamwe hawawezi kufika Ikulu.

Fikira hizo ni mgando na ni kujidanganya kulikopindukia. Mwaka 2010 rais aliyeko madarakani alipata asilimia 61, matokeo yale nilidhani yangewastua na kujitahidi kujenga chama na kurudisha imani kwa wananchi ambao nadhani wameshawachoka.

Uadui na chuki kati ya wanachama ni dalili nyingine mbaya, nahisi ndani ya ccm kuna wanachama ambao sidhani kama wanaupendo na upenzi wa dhati na chama cha mapinduzi, ndio maana kila siku hutoa matamko ya kuudhi na ambayo hukibomoa chama, sijajua jeuri hii viongozi hawa wanapata wapi, hii ni kuthibitisha kuwa ndani ya vyama vingi kuna watu ambao ni mapandikizi ambayo wanahakikisha kuwa vyama hivyo vinakufa mchana kweupe.

CCM inakoelekea si kuzuri na mwisho kama haitajikosoa na kujirekebisha ni anguko ambalo wengi litawaumiza, wengi tunasubiri tuone minyukano hii inayoendelea ndani ya chama itakifikisha wapi chama hiki, ila nafikiri watanzania ifike sehemu tujiamini kuwa daima mwenye nguvu sio Kamati zinazoundwa na vyama bali ni kura yako.

Vuguvugu hili na kutoaminiana kwingi ndani ya CCM sidhani kama mwaka huu zile ghani zilizotukuka na kuhanikisha jogoo kuwika Dodoma sijui kama zitaimbwa kwa moyo mweupe, nahisi safari hii atakayewika ni Bata kuashiria kuwa uchuro umeshaingia kambini na baadae tuwasiliane na mzee Arap Moi wa Kenya atuonyeshe mahali alipoipeleka na kuizika KANU ili eneo hilo tuilaze CCM kwa amani
 
Lete taarifa makini huu siyo mtandao wa udaku. Unasema kumekucha wakati huna jipya!
 
Hebu waigilizie vile bata atakavyowika ndio nape asikie.
 
Membeeeeeeeh gooooooooooooooohh(watu weweeeeeeeeh) kumbe naota
 
Back
Top Bottom