Steph Curry
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 5,936
- 4,707
Sasa nayakumbuka yale maneno ya JK aliposema kuwa kuna mgombea aliwachukua watu kwa gari lake wakampigie kura. Alipokosa aliwatelekeza watu hao
Hakuna kitu kisicho na mwisho lakini mwisho utakuja zaidi pale tu jina la membe likipitishwa kama mgombea urais wa ccm team lowasa wataiua kabisa ccm yangu macho tu
Wakuu mwenye kujua Asha Rose dini gani?
Edo forever....!!!
Dr. Slaa chaguo langu la Pili...!!!
Wakimwacha Lowassa, CCM inakufa leo leo... Ukawa mapema wanachukua usukani....!!!
Lowassa nenda kokote UTASHINDAAA...
Tena ukitoka mapema hii kuwa Upinzani wananchi watazidi mara kumi ya sasa kukufuata, najua ww ni SHUJAA WA TAIFA LETU...!!
Atakayeungwa mkono na Lowasa ndiye atapita.Ifahamike kuwa makucha ya JK hayafui dafu ktk kura za NEC na mkutano mkuu.Kama Lowasa ana nguvu huko,tegemea kura za kumkomoa JK,Magufuli anapita kilaini kabisa
Mkuu heshima kwako. Ninaomba tusubiri mzee wetu wa LUMUMBA labada atakuwa na mengi toka DODOMA. Na huyu si mwingine bali VUTA NI KUVUTE wa Lumumba.Wana bodi,Ule msemo kwamba CCM inamilikiwa na mafisadi unatimia, kundi hilo kubwa sasa linapambana na vifisadi katika kile kinachoitwa kugombea Urais. CCM haina pa kutokea zaidi ya kufa kwa kupoteza katika chaguzi zake zote. Binafsi nilikuwa nina hofu na EL ,Makongoro na Agustino Ramadhani.Ndio wagombea pekee wa CCM ambao wangeweza kupambana na Ukawa. Hawa waliopo ukiongeza na mgawanyiko huu mnyukano ni wazi kabisa kuwa Ukawa watumie nafasi hii nyeti. CCM kwisha habari
Watu now wanawacheka team Lowassa ..
tumesahau kuna team Makongoro nao wanastahili pole za kutosha tu
Kwa kweli hiki kilio ni kikuubwa sana
Halafu kuna team Mwigulu ya kina Shonza na Mtella mwampamba
dah.....huu msiba ni mkubwa mno kumbee
poleni saana.....sasa tutazame yajayo
Huku ni kukifukia chama kaburi asubuh na mapema. Ngoja mimi niweke hakiba ya maneno lakini udini unakiangamiza chama cha Mapinduzi. Ingesound kama wangemtoa na MEMBE lakini kumuweka Membe ni kutaka tuamini sasa kwamba hii vita ya makundi ya kidini imefikia pabaya.