Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

Bilali ni Muslim afu Ana wake wives yaani sio mistress sasa kama amna wasafi alternative hazijaisha bado tuna ukawa tuwape ao atuwezi kujigeuza lab rats et tufanyiwe majaribio ii ni nchi sio maabara

We naye sijui unaongea nini? Unapata wapi courage ya kuingilia maisha binafsi ya watu na kuwasonga kisa tu wako ccm!!!?

Huyo mke wa slaa ni mke halali? Amekuwa mchumba tangu lini na ndoa ni lini?! Mbowe kazaa na nani yule viti maalumu wake!! Lipumba unamjua mke wake?!
 
Sijui ulitaka kufikisha ujumbe gani, maana zote sifa hasi... kutojua kujieleza... mwizi... Ulitaka kusemaje?
 
magufuri is wisely,
he needs support from lowassa!
to win the election easly,,.
Its not the matter of Lowasa only, but the grieved followers of him! As a politician Lowasa can be reconciled to Magufuli but for us, nothing can quench our vengeance!
 
Amka TANZANIA Uliyelala mda mrefu hiz n enzi nyingine fumbua macho songa mbele MUNGU IBARIKI Tanzania MUNGU IBARIKI Africa
 

Hii midomo mirefu itawacost nawaambieni.

Naona mnajipongeza baada ya kumkata kipenzi cha watu na kumweka Mkandarasi ili alinde ufisadi wa mfalme na wafuasi wenu.

Amini nawaambieni hamuwezi kuzuiya mafuriko kwa mikono.

Mark my word

Urais ni taasis mkuu usikate tamaa wewe kubali matokeo kilichopo mbele yetu ni kukubaliana na yule ataeingia magogoni na kupiga makelele anapofanya blunder hata huyo unaemfikiria nae ana mapungufu. KUMBUKA MWANADAMU NI MTU ANAEBADIRIKA NDO SIFA KUU NA NDIO MAANA KUNA RAIA WEMA WAKAWA MAJAMBAZI NA MAJAMBAZI YAKAWA RAIA WEMA. Wanzanzibar waliwahi kupiga kura za maruhani wapendwa wao walipoondolewa hivyo na kwanini team Lowasa ambao wanawakilisha hao wananchi wanaomtaka jamaa wasingeshiriki kupiga kura kwa mtu ambae anawekwa kwa ajili ya kulinda mafisadi
 
 
ocampo four jana nilikutana nae NAM hotel hapa dom akihaha jinsi gani atarudi kwao maana akaunti na 4u yote anayo Bashe ambaye amechanganyikiwa kiasi cha kushindwa kupatikananika.
Amekuwa kama wale makomandoo wa Yanga ambao kuna wakati walienda Mwanza bila nauli wakidhani watakaa milangoni na kuvuna pesa za nauli, matokeo yake Manji akanunua mechi na kulipa 100m na hivyo watu kuingia bure. Makamandoo wakakwama ikabidi wajisalimishe kwa Manji kuomba nauli ya kurudi Dar.

Mpeni nauli arudi Dar aje tena haa JF na porojo zake.

Yupo pia Yericko Nyerere ambaye alikuwa na u Yahaya wake hapa kila kukicha naona naye kimya. Mkuu njoo tupate nadaha zako
 
Last edited by a moderator:
mkuu hii si hoja ,hakuna hoja hapa hizi ni delusions za mtu hapa!nadhani itakuwaa ni kujishusha tukijadili uwewesekaji huu!

Tuseme ukwel tu yule padri anaweza kusimama na makufuli kwel?tuache kujifariji ovyo
 

Hiyo post niliileta Mimi , na alieongezewa ulinzi alikuwa Makongoro Nyerere , kwa busara za baraza la ushauri, na ushauri wao ulikubaliwa na JK , na jk alikubali lakini top 5 ya wazee wa ushauri ilipoenda kanati kuu kikwete akaikataa na kuchukua yake na kuipitisha kimabavu na maghufuli hakuwemo ndipo wazee wakashaur tena awekwe maghufuli baada ya mapendekezo ya awali kukataliwa ambao walikuwa
1 Pinda
2 Bilal
3 Asha rose
4 Makongoro
5 Jaji ramadhani
Kikwete akawatosa wazee na kuja na list yake na walipomuuliza chaguo lake akasema Membe , ndipo mkapa akachukia wakachenjiana kwenye kikao ila kikwete akalazimisha ila akakubali maghufuli kwani alijua ni msindikizaji , baada ya kukubali marais wastaafu wa Tanzania na Zanzibar wakaomba maghufuli apigwe tafu na mchezo ndipo ulipoanzia , nazani wote mashahidi kilichotokea NEC kwa chaguo la kikwete na familia yake , ambapo ndani ya NEC ridhiwan alipiga kampeni za wazi kwa Membe na Asha rose

Baada ya kupigwa NEC JK aliishiwa pozi ikabidi nguvu iende kwa asha rose migiro akimtumia riz one na membe wampigie kampeni akiwemo nape na makonda, dili likashtukiwa maana iliundwa propaganda ya ni zamu ya mwanamke , wajumbe MM walipozipata wakasema OK tutapiga kura za kukuonesha sisi ndio CCM na sio wewe

Upepo ukaanza someka baada ya maghufuli kuingia ukumbini yaani ni kelele na vifijo hali ambayo nape hakuipenda pia kikwete mwenyewe hadi kuwaambia kwa sauti watu wa geita tulieni hii ilikuwa ni kutengrneza UFA wa kikabila lakini ilishindikana , na MM imemuonesha adabu kikwete na familia yake , pia MZEE Warioba,Dr salim , kinana, MZEE mkapa, MZEE mwinyi na Karume wamefurahi sana kwani jamaa aliwadharau sana wakati yeye ndiye aliwaomba ushauri na akasema watakachokubaliana yeye atanaliki ,


Pia amesahau akistaafu na yeye ataenda baraza la ushauri , hivyo watamcheka sana kwani hatakuwa na nguvu tena ,

Magufuli haziivi na kikwete mtu asiwadanganye, kumbukeni kikwete alikuwa anamchukia sana magufuli 2005 hadi akataka ampoteze kisiasa kwa kumpa wizara ya samaki,

Magufuli ni zao la rais mkapa, na MZEE mkapa sasa atakuwa huru sana na kufurahi chaguo lake kushinda


Ngoja nifatilie mkutano, now pinda anaongea

Itaendeleea kujua , zaidi wakati wa uteuz na vikao vya maridhiano
 

Kijiji cha Magufuli pale Chato kinawapa ushawishi baadhi ya watu kumuona Magufuli kama fisadi!

Hebu tujaribu kuiuliza historia na hisabati ili tuweze kumjadili vizuri. John Magufuli (JM) amekuwepo Bungeni na Serikalini tangu awamu ya 3 ya Mhe. Ben Mkapa hadi awamu hii ya 4 ya JK. Ni wazi kuwa JM amekuwepo kwenye taasisi hizo takribani tangu miaka 20 iliyopita. Nyumba 60 kila moja inaweza kuwa na construction value isiyozidi Tsh. 35,000,000/= ambapo jumla yake ni takribani 2.1 billion/-. Ukichukua 2.1billion ukawagawanya kwa miaka 20 utapata Tsh. 105,000,000/= kwa mwaka. Ukienda mbali kidogo ukagawa 105,000,000/= kwa miezi 12 utapata Tsh. 8,750,000/= kwa mwezi, kipato ambacho ni cha kawaida tu hata kwa mtu ambaye siyo mbunge wala waziri. Ikumbukwe pia kuwa Enzi za Mkapa kachukua Gratuity ya Bunge mara 2, kipindi cha Kikwete kachukua Gratuity ya Bunge mara 1 na sasa anachukua nyingine ya 2. Kiwango cha Gratuity ya Bunge unakijua vizuri. Aidha zipo fursa nyingi za mikopo kwa wale wanaoukwaa ubunge hivyo kwa mtu mwenye vision ya maisha haitamsumbua kujenga nyumba 60 kama za JM pale Chato.
 
Kweli chama cha mapinduzi mnatisha sana, yaani mlichofanya ni sawa na kukaba mwili wa messi wakati ana mpira obviously utaaibika tu, ndugu zangu UKAWA wameshindwa hata pa kuanzia na wasiwasi wangu mechi itaisha 6-0 labda mechi iahirishwe.

Mkuu usilinganishe Kishkwambii na Iphone...!
CCM tumeyaona toka juzi.. Katiba kuvunjwa kisa kukamiana.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…