Yaliyojiri katika Ziara ya Rais Samia Mkoani Morogoro

Yaliyojiri katika Ziara ya Rais Samia Mkoani Morogoro

Wakuu salaam,

Leo Julai, 7 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwasili mkoani Morogoro kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku mbili katika maeneo ya Msamvu manispaa ya Morogoro, Dumila wilayani Kilosa na wilaya ya Gairo.

Aidha Mkuu wa mkoa wa Morogoro Bw. Martin Shighela alisema ziara hiyo ya Samia Suluhu Hassan atakutana na Wananchi na hivyo akatoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kumlaki Rais wao.

Pia Rais Samia anatarajiwa kushiriki mkutano mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania utakao fanyika Julai 8 katika manispaa ya Morogoro.

Tutakuwa hapa sote kuwaeleza yanayojiri.
Mbona mambo hayajiri sasa! Bila updates uzi unakuwa mkavu,
 
Kila la kheri ziara hiyo vipi mpango kuumega Mkoa Morogoro? Vipi kuzungukia Kilombero Mahenge Malinyi Ulanga etc ? Karibu Morogoro Mama.....msisahau kujikinga Corona hali sio nzuri
Ashachanjwa huyo si mwenzako labda hizo nyomi zingine
 
Tanzania Ina Mikoa Tele Inataka Kugawanywa:-
  1. Tanga
  2. Ruvuma
  3. Geita
  4. Mwanza
 
Kama mapadre wanampa spichi ya kusoma,asiseme kwamba amesoma "Jeremiah"
Kuna tofauti kati ya yeye kusoma Biblia na kuitafakari,: au yeye kushushiwa aya ya kuwaeleza wananchi: au màaskofu kumshauri jsmvo la kusema.
 
Mnapopata bahati ya kuongea na Rais, muwe mnafikisha kero zinazoikabili jamii husika.

Mfano hapo Morogoro JPM alifanya ubabe kwa mwekezaji wa kile Kiwanda cha Tumbaku (TTPL) hadi wakasusa wakafunga kiwanda. Hivyo zaidi ya wakazi 10,000 wakajikuta wanakosa ajira sasahivi wapo mtaani.

Hivyo tumieni fursa hiyo mwambieni Mama amrudishe huyo mwekezaji.
Mkuu GEMBESON kilio chako cha mwaka jana Samia kasikia. Baada ya Shetani wa Chato kufa kuna habari njema hapa
 

Attachments

  • IMG-20220528-WA0048.jpg
    IMG-20220528-WA0048.jpg
    52.9 KB · Views: 6
  • IMG-20220528-WA0049.jpg
    IMG-20220528-WA0049.jpg
    48.4 KB · Views: 6
Back
Top Bottom