Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
Leo tena kama kawaida tunakuletea moja kwa moja yanayojiri kwenye Mahakama kuu , divisheni ya Uhujumu Uchumi , ambako kesi ya ugaidi unaogharimu kitita cha tsh laki 6 inaendelea.
---
Jaji ameshaingia
Kesi inatajwa
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021, Jamuhuri dhidi ya Halfan Bwire, Adam Hassana Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe
Jaji: Wakili wa Serikali
Wakili Kidando anatambulisha Jopo lake....
Wakili Kibatala anatambulisha Jopo lake
Mshitakiwa wa Pili - John Mallya
Mshitakiwa wa tatu - Fredrick Kiwhelo
Mawakili Wengine wote ni Kwa mshitakiwa wa Nne Freeman Mbowe
Jaji: Siku ya Ijumaa shahidi( Mshtakiwa wa pili) alikuwa hajakamilisha Utetezi wake. Arejee kwenye Kizimba tuweze Kuendelea
Shahidi anaenda
Jaji: Wakili wa Serikali mpo tayari..?
Jaji: Upande wa Utetezi mpo tayari?
Wote wapo tayari
Jaji: Shahidi bado upo chini ya Kiapo kama tulivyokuapisha Siku ya Ijumaa. Mawakili wa Serikali watakuhoji Maswali na Baadae Upande wa Utetezi hususani Wakili wako anaweza kuja kukuongoza tena Kwa Kukuuliza Maswali. Unaweza kuchagua Kukaa au Kusimama
Shahidi: Nitakaa Mheshimiwa Jaji
Jaji: Bila shaka. Wakili wa Serikali Chavula unaendelea. Tafadhali endelea
Wakili wa Serikali: Naam Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Awali siku ya Ijumaa kabla hatujaahirisha, nilikuuuliza kuhusiana na wale waliokuvamia maeneo ya Rau hawakupata kujitambulisha, Kweli au Si Kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Wale watu Mlivyotoka pale kwenda Kituo cha Polisi hawakulueleza Majina yao akina nani.? Kweli au Si Kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Walivyokutoa Moshi kukuleta Dar es salaam hawakukueleza wao Majina yao ni Akina nani. Walipokupeleka Mbweni hawakukueleza Majina yao akina nani?
Shahidi: Kweli hawakunieleza
Wakili wa Serikali: Haukupata Kuwafahamu amajina yao wakati wote?
Shahidi: Niliwafahamu kwa wao alipokuwa wanaitana Majina yao na Nikaja kuthibitisha Majina yao hapa Mahakamani walipojitambulisha
Wakili wa Serikali: Wakati wa Kukusafirisha Moshi Kuja Dar es salaam Watu wale walikufunga Kitambaa Usoni?
Shahidi: ni Sahihi
Wakili wa Serikali: ni Jacket, Si Ndiyo?
Shahidi: ni Jacket ndiyo
Wakili wa Serikali: Hukujua ni akina nani unasafiri nao
Shahidi: Kweli kama nilivyoeleza
Wakili wa Serikali: Na hata Ulipofika Dar es salaam ukafikishwa Kituo cha Kwanza cha Polisi hukujua upo wapi
Wakili wa Serikali: We Jibu swali langu Kweli au si Kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Umedai ulipokuwa unasafirishwa Ulikalishwa Chini kwenye gari,Kweli au si kweli
Shahidi: Ni kweli
Wakili wa Serikali: Uliweza Kujua ni sehemu gani ya gari ..?
Shahidi: Nilipita Upande wa Kulia Kwa Uelewa wangu siyo Kwa Kuona, Nikafahamu nimekaa nyuma ya gari
Wakili wa Serikali: Ulikaa nyuma ya gari
Shahidi: Ndani ya gari,Sehemu ya Nyuma
Shahidi: Siwezi Kujua ni gari gani
Wakili wa Serikali: Unakubaliana na Mimi ukiwa Umefungwa Machoni uwezi Kuona .?
Shahidi: Ndiyo uwezi Kuona, ila ukiwa unatendewa unahisi
Wakili wa Serikali: Ukiwa umefungwa macho uwezi kuona hata kile kifaa wanachokusababishia Maumivu
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali: Nakurudisha Moshi,umesema walipokuwa wanakutesa Moshi walikuwa wabakuuliza Umekuja Moshi Kufanya nini
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Wewe Ukajibu umekuja Moshi Kufanya VIP protection ni Sahihi
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Ulisema ulipofika Dar es salaam kituo cha kwanza cha Polisi walikupa Chakula .?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Ni Chakula gani
Shahidi: Ugali na Mboga za Majani
Wakili wa Serikali: na wakati wote ulipokuwa pale hukufanyiwa Mateso
Shahidi: Sahihi
Wakili wa Serikali: na hata ulipokuwa Mbweni hakuna aliyekuja Kukupiga..?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Alipokuja Ramadhani Kingai alipolutaka Uthibitishe Marlezo yako na Kutia Sahihi alikupa Vitisho wala hakukupiga.?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Ni Lipi Mahakama ichukue kati ya haya Mawili,Ulielezq Mahakama kwamba Wakati unatoa Maelezo hapa Mahakamani,kwamba ulitoa Maelezo kwa sababu ulikuwa unateswa,Sasa unasema kwamba Kingai na wenzake hawakukupatia Mateso isipokuwa Walipa Vitisho tuh
Shahidi: Rudia swali lako
Wakili wa Serikali: Wakati wa Kesi Kubwa Umesema Kuwa Kingai wenzake walichukua Maelezo yangu baada ya Mateso,Leo unasema Alikuja Bwana Kingai kunitishia
Shahidi: Umeuliza wakati wa Kuchukuliwa Maelezo, Mimi wakati wote nilikuwa Chini ya Mateso
Wakili wa Serikali: Aahaaaaaa
Wakili Mallya: OBJECTION. Naomba Shahidi akiwa anatoa Maelezo yake apewe nafasi ya Kumaliza Kujibu Maswali
Wakili wa Serikali: Ulipokuwa Dar es Salaam hukuteswa isipokuwa Bwana Kingai alikutishia.?
Shahidi: Aliniuliza kuhusu Kupigwa siyo Kuhusu mateso,kwa sababu, Mimi nilikuwa Chini yao na Nimefungwa pingu, bado hayo kwangu ni Mateso
Jaji: Shahidi nafikiri ungejibu sasa hilo unalotaka wala hakuna tatizo kwamba uliteswa au lah
Jaji: Naweza kukusomea
Shahidi: Ningependa unisomee Mheshimiwa Jaji
Jaji: Kingai "Hakunipiga tulipokuwa Mbweni, alinipiga na Kunitishia" Sasa tuambie nini kilichokuwa kimetokea
Shahidi: Vyote vichukue
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Mahakama ichukue Vyote
Jaji: Sasa niandike vipi Hukutoa Maelezo na Ulitoa Maelezo ..?
Shahidi: Ananiuliza Mambo Mawili tofauti ambayo ajayatenganisha, Mimi nilitoa Maelezo Moshi Chini ya Mateso,nalisaini bila Mateso
Jaji: Nilisaini Maelezo bila Mateso lakini nisaini baada ya Vitisho
Shahidi: ni sahihi Mheshimiwa Jaji
Mahakama Kichekooooooo
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kuletwa Dar es salaam tarehe 07,Kabla ya siku hiyo uliwahi Kufika Dar es salaam.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Makazi yako yapo Dar es salaam.?
Shahidi: Hapana
Wakili wa Serikali: unafahamu wapi?
Shahidi: Kambi ya Jeshi Twalipo na Maeneo ya Uwanja wa Taifa
Wakili wa Serikali: Ujawahi Kufika Tazara.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Ulishawahi Kufika Mbweni
Shahidi: Hapana
Jaji: Kwa hiyo Kabla ya kesi ujawahi kufika Tazara wala Mbweni
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Hakuna Wakati ,unafikishwa Kituo cha Polisi wakakuacha wazi.?
Shahidi: sijwahi Kutolewa nje ya kituo cha Polisi
Jaji: Mnaeleeana kweli..?
Jaji: Kutoka Tazara kwenda Mbweni ulifungwa Jacket.?
Shahidi: Nilifungwa Jacket Usoni Mheshimiwa
Jaji: Wakili ulimaanisha hivyo.?
Wakili wa Serikali: Ndiyo Mheshimiwa
Jaji: Sasa nitaomba Mnapomtajia Vituo vya Polisi Mtaje na Majina
Wakili wa Serikali: Naanza Upya Ulitolewa akitambaa ama Jacket lako ulipofilishwa ndani ya Kituo cha Tazara
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Mpaka Unaingia Kituo cha Polisi Tazara ulikuwa umefungwa Usoni
Wakili wa Serikali: Moshi Mlikamatwa wangapi
Shahidi: tulikamatwa wawili
Wakili wa Serikali: Na nani.?
Shahidi: Na Mohammed Abdilah Ling'wenya
Wakili wa Serikali: Wakati wote unasafirishwa hukujua yupo wapi
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Kingai na Mwenzake Mahita,walieleza Mahakama kwamba waliwasafirisha wewe na Ling'wenya Kwenye gari moja
Shahidi: Kweli walitoa Ushahidi huo
Wakili wa Serikali: Hakuna Mtu aliyewaambia Mashahidi wale kuwa Si kweli Nyie hamkusafirishwa pamoja.?
Shahidi: sasa
Wakili wa Serikali: Jibu swali langu
Jaji: Je ulisikia au Hukusikia.?
Shahidi: Sikusikia
Wakili wa Serikali: Kama wakati wote unasafirishwa Mpaka unafikishwa Kituo cha Polisi Tazara ulikuwa hufahamu Mohammed Abdilah Ling'wenya yupo wapi, Kweli au si Kweli
Shahidi: Sahihi
Wakili wa Serikali: Ulikuwa peke yako Kwenye mahabusu
Shahidi: Nilikuwa peke yangu kwenye Chumba Changu, ila Mahabusu wengine walikuwa Kwenye Vyumba vyao
Jaji: Kwa hiyo ulikuwa Mwenyewe Kwenye Chumba cha Mahabusu..?
Shahidi: Ndiyo
Jaji: Hapakuwa na Mahabusu wengine..?
Shahidi: Walikwepo kwenye Vyumba vyao
Jaji: Hapa naona tusingeelewana
Wakili Mallya: Shahidi alitupa Picha Kuwa kuna mahabusu Yenye Vyumba Vidogo Vidogo na yeye alikuwa kwenye kichumba Chake ndani ya mahabusu
Jaji: Naomba Kusoma "Nilifunguliwa Jacket nikawa naona Sasa,nikajivuta hadi Mlangoni nikaanza kuona Mahabusu wengime wakiwa kwenye Vyumba Vyao" nafikiri ndicho nilichoandika
Jaji: Sasa tujielekeze Hapo
Wakili wa Serikali: Umesema ulikuwa Peke yako Kwenye Chumba
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Kushoto na Kulia palikuwa na Ukuta
Shahidi: Ni sahihi Kabisa
Wakili wa Serikali: Ulikuwa kwenye tafakari kwanini haya yananiyokea, nimekosa nini.?
washitakiwa 1,2,na 3 walikubali wanafahamianina wa wakiwa wanafanya kazi Ngerengere KJ92
Wahitakiwa 1,2, na 3 Walikuwa wanafahamiana kabla ya Kesi Kuanza
Wakili wa Serikali: Hukubisha kwamba kwamba hukuondolewa Jeshini kwa Maswala ya Kinidhamu, na asasa unasema Uliondolewa Jeshini kwa Maswala ya Afya
Shahidi: Siwezi kulijibia
Wakili wa Serikali: Kwanini uwezi Kulijibia
Shahidi: Documents zote sijawahi kuzitolea Maelezo, zilikuja na kuletwa na watu walioandaa
Wakili wa Serikali: Documents zipi hizi?
Shahidi: Zilioletwa kufungulia Kesi ya Ugaidi
Wakili wa Serikali: Ulisaini hukusoma.?
Shahidi: Nilisaini
Wakili wa Serikali: Na Mahakama ilikusomea.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Unasema Ulikuwa kwenye Misheni Congo
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Ulikuwa Battalion ya 3, wewe ulikuwa kikosi cha Mizinga
Shahidi: Hapana
Wakili wa Serikali: Wewe ulikuwa unafanya nini
Shahidi: Nilikuwa Special Force
Wakili wa Serikali: Huko Special Force ulikuwa unafanya kazi gani
Shahidi: Kazi zote
Wakili wa Serikali: Zitaje
Shahidi: Zote kuanzia kupika Mpaka Kwenda Vitani
Wakili wa Serikali: Huko Vitani huwa mnajihusisha na Kuteka Watu
Shahidi: Siyo kazi yangu kuzungumzia Maswala ya Vita
Wakili wa Serikali: Lakini Vitani huwa watu wanatekwa
Shahidi: Ukingalia kwenye Muvi wanatekwa ila Mimi ya Vitani siwezi kuyaeleza, Kuna watu wake Maalum wa Kuyaeleza
Wakili wa Serikali: Moja ya kazi ni Kulinda Lindo, mnalinda dhidi ya nani?
Shahidi: Dhidi ya Adui
Wakili wa Serikali: Unapokuwa umemkamata Mtu lindo Moja ya jambo ni Kumfunga pingu ili asitoroke
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Kweli kwa sababu mmeyafanya huko Vitani
Wakili wa Serikali anaongea na Jopo lao
Wakili wa Serikali: Wewe huwa unatesa watu.?
Shahidi: Sijawahi
Wakili wa Serikali: Ukiwa umekamata Adui ukamfunga Pingu utakuwa umemtesa
Shahidi: Utakuwa hujamtesa, Ndiyo maana umemuita Adui
Wakili wa Serikali: Naomba kuwaachia wenzangu
Jaji: Nawakumbusha tuna dakika 20 kabla hatuja-break
Wakili wa Serikali 2: Mheshimiwa mimi ninayo Machache kati ya mengi yaliyoulizwa na Mwenzangu
Jaj: Labda nimuulize Shahidi Mwenyewe, Una nguvu au tunaweza kuendelea na Maswali?
Shahidi: Tuendelee Mheshimiwa Jaji
Wakili wa Serikali 02: Wakati umeanza kuulizwa na Wakili wa Serikali umeongea Ukweli, Tunaomba uendelee kusema Ukweli
Wakili wa Serikali 02: Wakati unakamatwa, Ling'wenya je yeye alikuwa umbali gani?
Shahidi: Alikuwa karibu yangu, Sababu nilikuwa Pembeni naongea na Simu
Wakili wa Serikali 02: Umesema Ling'wenya alishuhudia wakati Unawekewa Madawa ya Kulevya?
Shahidi: Siyo yeye tuh watu wote waliona kwa Sababu Jambo hilo lilifanyika hadharani mbele za watu
Wakili wa Serikali 02: Kati yako wewe na Ling'wenya nani Mtaalamu wa Madawa ya Kulevya
Shahidi: Hakuna, Suala la Madawa walisema wao Wenyewe kuwa "Tumemkuta na Madawa ya kulevya"
Wakili wa Serikali 2: Kwenye ushahidi wako wako ulisema kuwa kuhusiana na Suala la kusaini hati yakukabidhi vitu vyako
Shahidi: Sikusema
Wakili wa Serikali 02: Ulimuonyesha Jaji Kuhusu makovu, Je unamakovu Mangapi?
Shahidi: Mengine yapo kichwani
Wakili wa Serikali 02: Uliiambia Mahakama kuwa makovu haya mengine yatofautishwe na Miguuni
Shahidi: Mahakama haikuuliza,Kuwa hayo Mengine yametokana na nini
Wakili wa Serikali 02: Mahakama itatofautishaje sasa?
Shahidi: Hiyo ni kazi ya Mahakama siwezi kuifundisha
Wakili wa Serikali 02: Ulipokuwa Mbweni Kuna Askari alikwambia Upo Mbweni Baada ya Kuwaonea Huruma
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 02: Huyo wa Pili aliyekuwa anasema huyo Askari ni nani.?
Shahidi: Mohammed Abdilah Ling'wenya
Wakili wa Serikali 02: Kumbe mlikuwa naye na Mkaonana Mbweni
Shahidi: Kujua tupo naye nilijua nimesema, Sikuwahi kumuona kwa macho
Wakili wa Serikali 02: Umeiambia Mahakama aliyekupiga Rungu Moshi ni nani
Shahidi: Sikuwa namfahamu
Wakili wa Serikali 02: Maelezo aliyokuletea Bwana Kingai ukayasaini na Kuyathibitisha,Ukiyqona utayakumbuka.?
Shahidi: Siwezi Kuyakumbuka, Kwa sababu sikuyasoma, Labda sehemu za sahihi yangu na nilipoandika
Wakili wa Serikali 02: Wakati unateswa Moshi uliwajibu Kuwa umeenda kwa VIP PROTECTION ,ukawajibu upo kwenye mazungumzo
Shahidi: Ni Kweli
Wakili wa Serikali 02: Wakati Wakili Kibatala anakuuliza wakati wa Maelezo ulisema Ungeweza Kumuita Mwajiri wako
Shahidi: Muajiri Mtarajiwa
Wakili wa Serikali 02: Kwa hiyo Mahakama iandike hujawahi kuajiriwa na Mshitakiwa wa nne
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali 02: Kwa hiyo ni sahihi nikisema katika hayo Mazungumzo yenu mliwahi Kufanyia Aishi Hotel
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 02: Wakati mnafanya hayo Mazungumzo mlikuwa na Mshitakiwa wa 3.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 02: Wakati Upo Tazara unasema uligudua kwa Vitu Viwili Kwa Honi ya Treni na Kuambiwa hiki ni kituo cha Kuhifadhia Watuhumiwa wa Ugaidi
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 02: Ulishaiambia Mahakama Kwamba Unatuhumiwa kwa Ugaidi.?
Shahidi: Hapana
Jaji: Subiri Kidogo
Wakili wa Serikali 02: Nina swali moja la Mwisho
Jaji: Sawa endelea
Wakili wa Serikali 02: Wakati unachomwa na Bisibisi ushawahi kuiambia Mahakama walikuwa wanataka nini, kama vile Moshi walikuwa wanakuuliza Umefuata nini..?
Shahidi: Hapana
Jaji: Sawa tunapumzika kwa Muda tutarejea Baada ya Dakika 20
Jaji ananyanyuka
Mahakama imerejea
Jaji ameingia Leo Mapema sana kuliko watu wengi na Watuhumiwa. Imebidi Jaji asubiri watuhumiwa waletwe
Kesi imetajwaa
Jaji: Nataka kuanza Utamaduni wa Kuanza Kuzingatia muda. Nikisema naanza Saa 3 Mtanikuta humu. Nikisema tunaanza saa 3 itakuwa Saa 3 Kamili. Na Nikisema Saa 4 itakuwa Saa 4 Kamili. Itapendeza kama Tutazingatia Muda. Na huo ndiyo Ustaarabu,Ikitokea Mtu anadharula nijulishwe. Haipendezi kesi Ikianza milango inafunguliwa kila Saa
Jaji: Upande wa Jamuhuri wapo tayari Kuendelea?
Utetezi.?
Shahidi.?
Wote wapo Tayari
Wakili wa Serikali 03: Wakati tukiendelea na hii Kesi tangu Mwanzoni na kingai,Mawakili wako na Ushahidi wako ulihojiwa Mantle Status ya akili yako,Ni kweli Jambo hili limejitokeza.?
Shahidi: Ni kweli limejitokeza.?
Wakili wa Serikali 03: Kwa usahihi ukaita Battle Confusion.?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali 03: Kama Kweli hali hiyo imejitokeza Moja ya Jambo ambalo litakukumba ni Kupoteza kuona mambo kwa usahihi.?
Shahidi: Sijui
Wakili wa Serikali 03: Hujui kwa sababu hukumbuki wakati ukiwa na tatizo hilo nini kilikuwa kinakutokea.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 03: Umewahi Kupoteza Uwezo wa watu unaowatambua au maeneo unayoyafahamu.?
Shahidi: Sijawahi
Wakili wa Serikali: Vipi Kuhusiana kutambua Muda na Tarehe.? umewahi Kuwa na tatizo la kuchanganya hivi vitu.?
Shahidi: Hapana sijawahi
Wakili wa Serikali 03: Vipi kwenye Kuchukua Maamuzi Sahihi, Kwamba Umempiga Mtu bila Sababu halafu baadae ukaja Kukumbuka
Shahidi: Hapana sijawahi Kufanya Maamuzi ya namna hiyo
Wakili wa Serikali 03: Kwa sababu ya Jambo la Battle Confusion ujaeleza Kwanini lilikukuta
Shahidi: Nilieleza Mahakama kuwa tatizo hilo nililipata baada ya Kutoka Vitani
Wakili wa Serikali 03: Sababu ya Battle Confusion zipo Nyingi,utakubaliana na mimi
Shahidi: Mimi siyo Mtaalamu
Wakili wa Serikali 03: Moja ya Sababu ya Kupata Battle Confusion ni Matumizi ya madawa ya kulevya yaliyokithiri, Ni sawa.?
Shahidi: Sababu zenu hizo siwezi Kuwabishia
Wakili wa Serikali 03: Katika Kipindi cha hili tatizo ulipangiwa kazi..?
Shahidi: Nilipangiwa kwenda Hospitali
Wakili wa Serikali: Ilikuchukua Takribani Miezi 02 baada ya Kurudi Jeshini, kabla ya Kufukuzwa kazi kwa Sababu wewe uliendelea kutumia madawa ya kulevya
Shahidi: Sijawahi Kutumia Madawa ya Kulevya
Wakili wa Serikali 03: Post Dramatic Disorder ni Kitu gani.?
Shahidi: Sifahamu
Wakili wa Serikali 03: Kama ufahamu kuhusiana na Ugonjwa wa Post Dramatic Disorder limefikaje hapa Mahakamani, Umewahi Kumwambia nani
Shahidi: Sijawahi Kumwambia Mtu
Wakili wa Serikali 03: Utaribu baada ya Kurudi kazini ulikuwaje?
Shahidi: Nilitakiwa kuendelea kuriport Hospitali
Wakili wa Serikali 03: Kwa hiyo Ugonjwa huu ,umeathiri utimamu wa akili.?
Shahidi: Hapana
Wakili wa Serikali: Unasema ulienda Moshi Kufanya kazi ya VIP PROTECTION, Kile Kitabu chenye Orodha ya Mashahidi na Ushahidi wote we ulikipata.?
Shahidi: Ndiyo ninacho
Wakili wa Serikali 03: Kuna Chochote Mshitakiwa wa nne amesema alikuita wewe na wenzako kwa ajili ya VIP PROTECTION.?
Shahidi: Sijakiona
Wakili wa Serikali 03: Kwa hiyo hili suala lako la VIP PROTECTION hajalisema, hata alipopewa nafasi ya kusema hakuwahi Kulisema popote
Shahidi: Sijui yeye sasa, Miye niliulizwa ndiyo Maana nikajibu
Wakili wa Serikali 03: Ulipokuwa unahojiwa na Mawakili wa Serikali ulikuwa unachukua Muda Sana Kujibu, hata Wakati Mwingine Mheshimiwa Jaji alikuwa akitoa Mwongozo, Nikisema una uwezo Mdogo au Umeathirika kiakili
Shahidi: Kama wewe ni Daktari siwezi Kukubishia Uchunguzi wako, ila Miye nikiwa nashindwa kujibu kwa haraka kwa sababu Maswali yanazunguuuuuka hayajanyooka
Wakili wa Serikali 03: Nipo sahihi nikisema hali ya Akili yako ipo sawa sawa.?
Shahidi: Upo sahihi
Wakili wa Serikali 03: Ujatueleza Umuhimu wa Kutueleza Utimamu wa kwanini Umeieleza Mahakama Ya tatizo la Akili kwa wakati Fulani
Shahidi: Nimeeleza Umuhimu, kwa Kufuatia Swali nililoulizwa Mahakamani
Wakili wa Serikali 03: Ina uhusiano gani suala la Ugonjwa wako na Makosa ya Njama za Kutenda Ugaidi
Shahidi: Kwangu naona Vina uhusiano kwa Sababu nimeulizwa na Mahakama, Isingekuwa na Umuhimu nisingeulizwa
Wakili wa Serikali 03: Je, unajua umuhimu wa kwamba umewahi kupata Battle Confusion ..?
Shahidi: Umuhimu unajua Mahakama yenyewe iliyouliza hilo swali
Wakili wa Serikali 03: Mheshimiwa Jaji naomba tukomee Hapa hakuna Swali Lingine
Jaji: Wakili Mallya kama Una maswali ya marejeo
Mallya: Mheshimiwa Jaji ninayo Machache
Mallya: Swali langu la Kwanza kwamba wewe Ni Komandoo umefundishwa kukaa na Njaa na Kuhimili Mateso, JE uelewa Wako ni nini katika Swali hili
Wakili wa Serikali 03: OBJECTION hilo swali haliruhusiwi katika Re-Examination, Yeye ange recall tu katika yale aliyojibu katika Examination
Jaji: Mallya Unakubaliana na alichosema Wakili wa Serikali
Mallya: Sababu ya Muda naomba ni Rudie Swali tu
Jaji: Hapana, Je umekubaliana naye?
Mallya: Sikubaliani naye lakini sababu ya Muda Nirudie swali tu.
Jaji: Sasa hapo tulimalize kwanza kabla Ujaenda Mbali, Kuliko kwenda na Mambo ambayo Mtu hajaridhika nayo
Mallya: Sijaja na Swali Jipya napitia Maswali yale yale na majibu yaleyale
Jaji: Sawa unaweza ukaanza na Swali Mwanzoni
Mallya: Swali langu la Kwanza kwamba wewe Ni Komandoo umefundishwa kukaa na Njaa na Kuhimili Mateso, JE uelewa Wako ni nini katika Swali hili
Shahidi: Katika Upande wa Mafunzo una kanuni zake na taratibu zake na kwa Upande wa ukamataji wa watuhumiwa kuna Kanuni zake na Taratibu zake
Wakili wa Serikali: OBJECTION
Jaji: Subiri kwanza Shahidi ajibu kwanza tuone kama linahusika na mnachotaka kufanya Objection
Wakili wa Serikali: Hakuna sehemu tuliyomuuliza kuhusiana na kuvumilia njaa
Jaji: Mliuliza nini siku hiyo.?
Wakili wa Serikali Chavula: Katika Mafunzo yenu Mnafundishwa Kuvumilia Njaa.?
Jaji: Kwanini uliuliza hilo swali,Ulilenga Ku-Establish kitu gani?
Wakili wa Serikali: Nililenga Kuwa ni Mtu ambaye ni Trained na yale ya Kukaa na Njaa si Kitu kigeni kwake
Jaji: Sawa kaeni Chini nafikiri hakuna Kitu Kigeni kati ya mlichouliza, kilichoulizwa na Kinachojibiwa
Jaji: Namruhusu wakili Mallya Kuendelea
Mallya: Kwa uelewa wako kwanini uliulizwa swali hilo
Shahidi: Nimeelewa Kuwa kukaa na Njaa ni Haki kwangu, Kupitia Mateso ni Haki yangu na Kwamba Kukamatwa Bila kuzingatia Sheria ni Haki yangu kwa sababu tu ni Vitu nilivyowahi Kupitia
Mallya: Kuna sehemu umesema Ulipigwa na kuna sehemu Uliteswa mgawanyiko wa hili Jambo likoje?
Shahidi: Kupigwa ni sehemu ya mateso, Kutishiwa ni Sehemu ya mateso, Ndiyo maana nilisema anilipofika Dar es salaam nilikuwa bado nipo Ndani ya Mateso. Kitendo Cha Kutolewa Kwenye Chumba na kuambiwa Kitakurudia kilichokutokea Moshi ni sehemu ya mateso wakati huo Comfortability yangu imeshapotewa kwa sababu nilikuwa nasimamiwa na Bastola. Na Vilevile Kitendo Cha Kushinda na Njaa ni Mateso pia
Kitendo Cha Kutolewa kituo Kimoja kimoja cha Polisi na Kupelekwa Kingime na Kubadirishiwa jina unalotambulika na Ulimwengu,Kwangu iliniathiri na Nikaona bado Nipo Chini ya mateso
Mallya: Umeulizwa kumjua au Kumuona Mahabusu ya Tazara na Mbweni, ulipokuwa unasema Ulijua yupo ila sikumuona?
Shahidi: Nilikuwa nikimaanisha alipokuwa Mahabusu Nyingine tuliweza kusalimiana hata kwa sauti ya Juu, Lakini siyo Kuonana Kwa face to face
Mallya: Nia ya kuonesha Makovu ilikuwa ni nini.?
Shahidi: Kwa sababu kuonesha Kuwa baada Matendo yale yaliacha Alama za kuumia, ndiyo maana nikaonesha Makovu
Mallya: Umeulizwa Pia Kuhusiana na Kupigwa ukiwa moshi na Kuwaona waliokutesa moshi kama uliwatambua au hukuwatambua
Shahidi: Kwenye kile chumba nilichokuwa nateswa palikuwa na watu wengi, Wengine nilikuja kuwatambua mbele ya Mahakama na Mtu Mwingine sikuweza Kumfahamu
Mallya: Uliulizwa kuhusiana Kutobolewa na Bisibisi Kwenye Makalio...
Wakili wa Serikali: OBJECTION. Aulize Yaliyojitokeza kwenye Examination, Hii kwamba elezea hiyo, Ni Maswali ambayo hayaruhusiwi
Jaji: Wakili Mallya?
Mallya: Re examination wajibu wake ni Kufanya Explanation
Jaji: Nafikiri Wakili wa Serikali yupo sahihi, unachouliza Unaacha uwanja Mpana wa Shahidi Kueleza Jambo Jipya badala Kuziba Mwanya wa Kilichoulizwa
Mallya: Wale waliokuwa wanakuchoma Bisibisi, Walikuwa wanataka nini?
Shahidi: Ilikuwa ni sehemu ya Mateso. Walikuwa wanasema Nyinyi si mmejifanya kutusaliti, sasa mtaona
Jaji: Nafikiri sasa tunafungu Box kwa kile nilichokuwa naeleza
Mallya: Mawakili wa Serikali alikuuliza Swali kwamba waliokuwa wanakuchoma bisibisi walitaka Kujua nini.?
Jaji: Naona Mawakili wa serikali wanataka mshauriane hapo, Inaruhusiwa
Mallya: Nitarudi baadae kwenye swali hilo. Je hapa Kwa ufahamu wako kinachoendelea Mahakamani ni Jambo gani?
Shahidi: Ni Shauri dogo katika Shauri Kubwa
Jaji: Lile swali lako umeuliza kweli?
Mallya: Nimeliweka akiba nitalirejea
Mallya anaenda Kushauriana na Jopo lake
Mallya: Wakati wanakuchoma walikuwa wanataka nini?
Shahidi: Muendelezo wa Mateso
Mallya: Nafikiri nimemaliza
Shahidi (Mshitakiwa wa pili) Anatoka Kizimbani
Jaji: Wakili Mallya endelea Uwanja ni Wako...
Mallya: Tunae shahidi mwingine Mohammed Abdilah Ling'wenya
Jaji: Jitambulishe
Shahidi: Mohammed Abdilah Ling'wenya.
Shahidi: Dini Muislamu
Jaji: Thibitisha Wallah Billah taalah Natihibitisha mbele ya Mahakama hii Ushahidi nitakaotoa utakuwa ni Kweli tupu,Eeh Mwenyezi Mungu Nisaidie
Jaji: Tutapisha Hadhana halafu tutaendelea
Hadhana Inaendeleeeee
Jaji: Wakili Kibatala Ulitaka Kuzungumza
Kibatala: Naomba nimtambulishe Wakili Dickson Matata kwa ajili ya Mshitakiwa watatu
Jaji: Sawa nakushukuru. Hapa Kuna Maelezo
Jaji: Kuna Shida Kumuita Mshitakiwa watatu kuwa Shahidi, Serikali.?
Jaji: Kiwhelo Kuna tatizo kwa Mshitakiwa wako kuwa Shahidi?
Wakili Kiwhelo: Hapana
Mallya: Makazi yako kwa sasa hivi Kimara King'ong'o?
Jaji: Makazi yako kwa sasa hivi?
Shahidi: Natokea Gereza la Ukonga
Mallya: Kabla ya Kukamatwa ulikuwa wapi
Shahidi: Mtwara kampuni DOT kampuni ya kusaga Kokoto
Mallya: Kabla ya hapo..?
Shahidi: Nilikuwa Ngorongoro
Mallya: Unamfahamu Mshitakiwa wa 2
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Umemfahamu wapi.?
Shahidi: Jeshini KJ 92 JWTZ Ngerengere
Mallya: Umeanza Lini?
Shahidi: Mwaka 2008 Mpaka 2017
Mallya: Kazi gani ulikuwa unafanya .?
Shahidi: Komandoo,Special Force
Mallya: Unamfahamu Vipi Mshtakiwa wa Pili
Shahidi: Nilikuwa nipo Mtwara nikapigiwa Simu na Askari Mwenzangu ambaye nilikuwa nipo naye Jeshini anaitwa Dennis Urio kwamba Kuna kazi ya kwenda kumlinda Mtu bila kunitajia huyo Mtu ni nani. Nikamwambia asubiri nikifika Nyumbani aongee na Baba akikubali sawa. Nilipofika Nyumbani akapiga simu nikampa akaongea na Baba. Baba akauliza si unamfahamu, nikasema Ndiyo akaniambia nakuombea Dua nenda
Mallya: Siku ya tarehe 05 Mwezi 08 2021 Maeneo ya Rau Madukani kulitokea kitu gani?
Shahidi: Nilikuwa kwa Dada yangu Mmoja anaitwa Asma, akiwa Dukani kwake mimi na Adamoo tukawa tunasubiria Chakula
Mallya: Kilichokupeleka Rau Moshi ni kitu gani?
Shahidi: Tulikuwa tunaenda kukutana na Mwajiri wetu ili tuje kukubaliana naye
Mallya: Mshitakiwa wa pili alikuwa anafanya kitu gani?
Shahidi: Wakati nipo Dukani, Kwenye Upenyo Coridor nikasikia Kelele sana, Nikataka niende kuona. Nikakuta Adamoo ameshanyanyuliwa na Kukabwa. Nikauliza Tatizo ni nini.? Nikashikwa Mkono wakaniuliza wewe Unamfahamu huyu?
Mallya: Ulipata Kujua ni akina nani.?
Shahidi: Niliwaona kwa mara ya kwanza. Wakaniuliza unamfahamu huyu.? Akatoka mwingine akasema ana pistol ana pistol ana pistol
Alinyofoa Kutoka amwilini Kwa Adamoo Upande wa Kulia akasema ana pistol ana pistol akasema na madawa ya kulevya anayo
Mallya: Eleza sasa Pistol anatoa wapi.?
Wakili wa Serikali: OBJECTION anamfeed Majibu
Mallya: Baada ya kumkuta Adamoo amenyanyuliwa Juu kitu gani kiliendelea? Ukisema alimtolea bastola unataka Mahakama ipate apicha gani
Shahidi: Baada ya Kuona Wanamfanyia Adamoo yale na Adamoo namfahamu na nilikuwa naye muda mrefu, Nikauvuta Mkono wangu kwa aliyekuwa amenishika. Nikawaambia Kuwa adamoo hakuwa na hivyo Vitu, nikatoa Simu na wallet nikaweza Kibarazani
Jaji: Ulitoa simu na nini
Shahidi: Simu na wallet
Mallya: Kusema walimuwekea unamanisha nini.?
Shahidi: Kwa Sababu nilianza Safari ya kwenda Moshi na Adamoo kuanzia Chalinze, Nafahamu hakuwa na Vitu hivyo. Nikasema huyu Mtu kwakuwa mmemuwekea na Mimi ngoja nitoe Vitu vyangu.
Mallya: Wakati huo Adamoo Yupo wapi?
Shahidi: Wamemshusha Chini ila wanampiga pale pale chini
Mallya: Uliweka vitu vyako wapi?
Shahidi: Waliochukua walikuwa ni Polisi?
Mallya: Kwenye wallet kulikuwa na nini.?
Shahidi: Palikuwa na Pesa.?
Mallya: Kiasi gani.?
Shahidi; Laki tatu
Mallya: Zipo wapi?
Shahidi: Hapana sielewi
Mallya: Watu waliomvamia Adamoo Unaweza Kujua walikuwa ni watu wangapi.?
Shahidi: Walikuwa Zaidi ya watano
Mallya: Baada ya Kupanda gari Mmlielekea Wapi.?
Shahidi: Central Moshi
Mallya: Kichofuata nini.?
Shahidi: Waliotuleta wakatoka, baada ya kutuacha. Walitutenganisha. Nakumbuka Mmoja alikuwa Askari Bonge nilimueleza kuwa mimi nilikuwa mwanajeshi. Wakauliza Kama nawajua Komba na Mselem
Jaji: Komba ni Mtu Mwingine na Msellemu Mtu Mwingine
Mallya: Nini ulishuhudia Kinachomuhusu Adamoo?
Shahidi: Nilishihudia akiwa yeye ni wa Kwanza kuinginzwa selo yake na Mimi nikawekwa selo Nyingine
Mally: Walipomtoa selo Ulionaje.?
Shahidi: Selo ya Kwanza Ya Kwangu na Yapili,Wakati wanamuingiza Cello yake sikumuona ila wakati wanamtoa alikuja Mtu kwenye Cello yangu akaita Ling'wenya Nyuma yake wakampitisha amtu wamemuinamisha
Mallya: Ulimtambuaje..?
Shahidi: Alikuwa na Jinzi Nyeusi na Shati la maua Maua
Mallya: nini Kilifuata?
Shahidi: Nilisikia kilio huko alipopelekwa Kwa Sababu haikuwa mbali na selo yangu, Nilisikia kilio akilia na nilimtambua kwa Sauti sababu namuitaga sauti ya zege
Mallya: Ulitambua sauti ni ya nani.?
Shahidi: Nilitambua ni Sauti ya Adamoo
Mallya: Ilikuwa ni Sauti ya namna gani.?
Shahidi: Ya amtu anayepigwa, alikuwa analia Eeeehiii Ehiiiiiii Ehiiiiiiiiiiiiiiii ya mtu anayeteswa
Mallya: Ilidumu kwa Muda gani
Shahidi: Sina uhakika ila ni Kama Nusu saa
Mallya: Umesikia Sauti ya zege analia kwa Nusu saa,Nini Kilifuata
Shahidi: Baada ya muda amfupi Kupita akapitishwa Mtu yule yuke aliyevaa Jinzi Nyeusi na shati la maua akiwa hawezi kutembea alishikwa huku kushoto na kulia na kwamba wakamburuza hadi Cello inayofuata baada ya kwangu
Mallya: Nini Kilifuata
Shahidi: Nikajua anayefuata ni mimi
Mallya: Baada ya kujia Unayefuata ni wewe, kilifuata nini
Shahidi: Walinichukua Mimi wakanipeleka huko, Nikaenda nikakuta watu wamekaa na wana simu zao wananirekodi
Wakasema taja majina Matatu
Nikawatajia
Wakaniuliza Unafanya kazi gani
Nikawatajia nimetoka Mtwara
Wakanipiga Buti wakasema wanajua mimi nimefuata nini Moshi
Mallya: Mahita yupi unayemzungumzia.?
Shahidi: Mara ya Mwisho nilimuona hapa mahakamani akitoa Ushahidi
Mallya: Hapo Mlikuwa sehemu gani?
Shahidi: Ni ndani ya Central Police palepale, nilitolewa Cello nikapalekwa kwenye Kijumba Kidogo. Palikuwa na Bomba refu, nikiwa nimefungwa Mikono na miguu, Mimi kwa ufahamu wangu inaitwa killing zone
Mallya: Killing zone ni Kitu gani?
Shahidi: Unakuwa Unaning'inizwa Miguu Juu Kichwa chini
Mallya: Kilifuata kitu gani..?
Shahidi: Nilipigwa sana kwenye Unyayo kwa sababu zilikuwa zimekaa Juu
Mallya: Wakati wanakupiga wanasemaje?
Shahidi: Aliyenipiga ni Mahita tu
Mallya: Walikuwa wanahitaji kitu gani?
Shahidi: Niliwaambia nimekuja kwa kazi ya VIP PROTECTION Kwa Kumlinda Mwenyekiti wa Chadema. Wakasema Utasema tu?
Mallya: Ilichukua Muda gani
Shahidi: Kama Nusu saa
Mallya: Ikawaje
Shahidi: Alikuja Mtu Mtu aliyevaa kiraia akatoa Amri "Mwacheni sasa msimpige
Wakawa wameniweka nimekaa Chini nikiwa na Pingu na Mguuni nimefungwa kamba
Jaji: Miguuni Ulifungwa nini?
Shahidi: Miguuni nilifungwa kamba
Mallya: Baada ya hapo Ulipelekwa wapi?
Akaniambia huku Hoi na yeye akaniambia Mimi Mwenyewe Huku Hoi
Jaji: Ukisema Mimi Huku hoi unamaanisha nini.?
Shahidi: Yaani nimeumia sana na kuchoka sana
Mallya: Mahita alikuwa anakupiga na Kitu gani?
Shahidi: Sijakishika vizuri lakini kama Shaba Nzito
Mallya: nini Kilifuata?
Shahidi: Ni kwamba kwa wao walivyonipiga walifikiri sitoweza Kutembea, Lakini Mimi walipomaliza Kunipiga niliweza Kutembea na palepale Walipomaliza Kunipiga nikiwa nimekaa chini niliwaomba waniruhusu nirukeruke kutuliza Maumivu. Wakati wanajitoa Nje Afande Jumanne akaropoka " Mwenzako amepigwa Sana, Bahati yako Ulipata Mtetezi"
Wakati mimi nikiwa tayari ndani ya gari tayari nilimuona Adamoo anatolewa kwa kukokotwa, Wakaniwahi Mahita akampa Goodluck shuka wakanifunga Kichwani
Nikawa nimetulia, Nikaona Mlango wa gari umefunguliwa, na Mtu akaingia na kuanza Safari.
Mallya: Baada ya kumuona Adamoo wakakuzuia na kukufunika usoni, Je ulimuona akiwa na Hali gani?
Shahidi: Nilimuona akiwa anakokotwa hawezi hata kutembea
Mallya: Baada ya kuinamishwa kichwa na kufungwa Shuka usoni kitu gani Kilifuata?
Shahidi: Nilikuwa kimya wakati huo gari ikawa wakati wote inatembea
Mallya: Wakati huo nini Kilifuata
Shahidi: Mimi nilikuwa katikatika nimekalishwa Kushoto yupo Goodluck na Kulia yupo Jumanne. Na Hali hiyo niliishuhudia kabla sijapigwa Shuka usoni
Mallya: Wakati huo nini Kiliendelea?
Shahidi: Ilikuwa wakati wote kimya hata nikiiinua shingo Kujinyoosha wananirudisha tena chini
Mallya: Unakadiria ilikuwa ni safari ya namna gani?
Shahidi: Ilikuwa ni safari ndefu kama ya mkoa kwa mkoa. Baada ya kufika na gari Kusimama nilishushwa kwa kushikwa nyuma kwa kuinamisha na kitambaa changu Vilevile Mpaka wakafungua Geti, nilipoingia wakanitoa Kitambaa
Mallya: Wakati huo wote mlisimama Kula Chakula.?
Shahidi: Hatukusimama Popote kula chakula. Waliponitoa tu Kitambaa alijitokeza Jamaa Mmoja wa kirangi, Mweupe akaniuliza nini shida.?
Kwa mwonekano wake walikuwa na Ndevu ndefu na Juu alikuwa amevaa Combat lakini siyo ya kitanzania
Nikamwambia Mimi nimekamatwa na tumeletwa hapa sijui ni Wapi
Akaniambia "Hapa ni Tazara Kituo cha Polisi"
Wakati naongea na Yule mrangi kuna mwingine akajitokeza kijana Mweusi, nikawambia nimeletwa hapa lakini Mimi nilikuwa ni Askari
Yule akijana Mweusi akasema Vipi MIC? MIC ni neno la Kijeshi
Nikamwambia Mbona wewe upo hapa.?
Akaniambia Mimi ni Askari nilikuwa naswali kwa Azizi Ally kambi yangu ni Twalipo
Alipokuwa amepaki Pikipiki nje akiwa anaswali ndani, wakamsubiri atoke wakampini wakamleta Tazara na akasema yupo Tazara kwa Miezi nane.
Nikamuuliza shida nini.?
Akasema wanaoletwa hapa ni Kesi za Kigaidi.
Mallya: Alikuwa anasema hapa, anamaanisha hapa Wapi?
Shahidi: Hapa Tazara
Nikamuomba aangalie Cello inayofuata kama kuna Mwenzangu kwa sababu wao Cello yao ilikuwa haijafungwa na walikuwa wakifanya Mpaka Usafi mle ndani
Wao Cello yao walikuwa wanaona Kila kitu, wakaniambia Kuna Wenzako Mmoja yupo Cello ya Mbele
Nikaanza Kuita Adamoo Adamoo Adamooo
Kuna Askari Mmoja akasema tuache Kelele yeye hajatuleta
Shahidi: Nikawa naendelea kupiga Story na Yule Mwanajeshi niliyemkuta pale
Wenzake wakamsii asiongee na Mimi na Mimi wakanipa ishara kwamba watu wenu wanakuja
Mallya: Kitu gani kilifuata?
Shahidi: Nikawa nachungulia Kwenye Cello yangu, hawakufika kwenye Cello yangu
Mallya: Wakati gani tena ulimuona mshitakiwa wa Pili?
Shahidi: Siku inayofuata nikiwa kwenye Cello siku inayofuata nikasikia Kilio, nikachungulia Kule Nyuma nikaona watu niliiokuwa nao Depo JKT , TPDF na 92KJ Komandoo (Wadepo wangu)
Mapumziko
Jaji anaingia.
Shauri Limetajwa Tayari.
Jaji: Lin'gwenya aendelee
Jaji: Leo saa Kumi tunafunga hadi kesho.
Jaji Kamkumbusha Lin'gwenya Tulipoishia
Shahidi: Nilishuhudia Chuma Chugulu na Alex akiwa na Kijitabu na wenzie wakiwa Wanadepo Wenzangu Kupitia Matundu ya Dirisha walikuwa wanamtesa Mtu. Ambapo baade nilimfahamu yule Mtu Kwa Majina anatolewa Kwenye Magari Mabovu alipokuwa anateswa kwa kushikwa na Mtu Mmoja na Mmoja yupo nyuma yake nilimfahamu aliyekuwa anateswa Kuwa ni Dennis Urio ambaye ni Luteni wa Jeshi ambaye alinitafutia hii Kazi ya VIP PROTECTION kwa Mwenyekiti wa Chadema
Mallya: Awali ulisikia Kilio baadae ukaona Mtu Mwenye kitabu na Rungu na baadae Urio anatolewa Kule kwenye Magari Mabovu, kwa aufahamu wako nani alikuwa anateswa Kule?
Shahidi: Kwa nilivyoona Mimi Leteni Dennis Urio ndiye alikuwa anateswa. Siwezi Kuwa na Ukahika nao ila Kama Dakika 15 Mpaka 20
Mallya: Kipi ulitangulia Kuona Kwanza Kati ya Wanadepo Wenzio na baade Askari Polisi na Urio?
Shahidi: Nilishuhudia Alex ndiye wa kwanza Kutoka baadae katoka Chuma Chungulu na Mapolisi wakiwa na Urio
Mallya: Kilifuata nini..?
Shahidi: Ilipofika Usiku nilitolewa nikafungwa Kitambaa
Mallya: Ulifungwa Kitambaa Ukiwa wapi.?
Shahidi: Ndani ya Gari
Mallya: Kabla ya Kufungwa Kitambaa Uliwatambua waliokuwa ndani ya Gari.?
Shahidi: Nilimtambua Goodluck na Mahita
Mallya: Ni Kabla ya Gari Kuondoka ndiyo Ulifungwa Kitambaa.?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Unaweza kutambua Gari ilitumia Muda gani.?
Shahidi: Ni Muda Mrefu sana,Ila siyo Kama Ule wa Kwenda Mkoani
Mallya: Kitu gani Kiliendelea..?
Shahidi: Maaskari wakasema Mwenzenu Moses Lijenje tumeshamtupa, Ameshatangulia huku wakinigusa Kichwani na Kitu nilichokuwa nahisi kuwa ni Bastola, Ukileta Ujanja Ujanja na wewe tunakutupa
Mallya: Maneno haya ulikuwa unaambiwa wakati gani wakati wa Safari au baada ya Kufika
Shahidi: Wakati wa Safari. Tulipofika nilikuwa nimebakia kwenye gari, Nilihisi watu wakifungua milango na Kushuka
Ikatoka Amri nishushwe, nikashushwa wakaniinamisha chini nikiwa bado na Kitambaa Usoni Pale Mapokezi nilipahisi hivyo kwa sababu tulisimama na Kuulizwa naitwa nani.? Mmoja akajibu Johnson John Wakaniinamisha Kichwa Wakanipeleka Mpaka Cello kule nilipoingia ndiyo wakanitoa Kitambaa
Mallya: Ulijuaje pale ni Cello
Shahidi: Nilipofikishwa tuh ile sehemu nikatolewa Kitambaa nikaanza Kuona Mazingira kama ya Tazara, Kama Milango ya Chuma na Vingine
Mallya: Huyu Johnson John waliyemtambulisha ulipata Kumjua??
Shahidi: Sikupata Kumjua, Walinipa Jina la Bandia
Kesho yake wakati wanakagua Mahabusu Johnson John halikuitwa hilo Jina, Wakapita Mpaka Kwenye Cello yangu wakaniuliza we unaitwa nani. Nikawajibu naitwa Johnson John
Mallya: Unasema Uliambiwa Usema Jina lako Unaitwa Johnson John, Nani alikwambia utaitwa Johnson John
Shahidi: Na Jumanne. Alinipa na Kikaratasi Kuwa Kuanzia Leo Mtu yoyote akija Utasema wewe ni Johnson John
Mallya: Alipopita Mtu akakuuliza baada ya Kutoitwa Jina lako.?
Shahidi: Nikamwambia naitwa Johnson John, Akawaita Askari wengine,Nahisi yule Mwanamama alikuwa ni Mkuubwa Kituo na alipotoka
Akaja Askari Mwingine akaniambia sasa tuambie Jina lako la Ukweli
Mallya: Ukajibu Vipi
Shahidi: Nikawapa Jina langu la Ukweli, wakaniuliza na Hili la Johnson John.?
Nikawajibu Kuwa hili nimepewa hapahapa
Wakaniuliza Una kesi gani?
Nikawajibu nimekamatwa Moshi baada ya kwenda kumlinda Mwenyekiti wa CHADEMA, Sijajua nimeshikiliwa kwa Kesi zaidi
Mallya: Ulifanya jitihada gani Kujua pale ulipo ni wapi?
Shahidi: Baada ya Ile zamu alikuja Koplo Mweupe nikaanza Kuongea naye
Nikamwambia mimi ni Mzaliwa wa Mwanza, akaniambia na yeye alishawahi kuishi Mwanza
Nikamwambia nilishawahi Kuwa Mwanajeshi wa KJ 92
Akaniambia kuwa kama Ulikuwa Mwanajeshi wa 92 KJ basi mmeshafika hapa watatu sasa
Mallya: Unaweza Kutueleza Mahakamani Ulijuaje ni Koplo.?
Shahidi: Kwa Uniform zake na Jinsi Renki zilivyokaa
Mallya: Kuna wakati gani ulimwambia hapa ni wapi?
Shahidi: Baada ya Kuniambia tumeshafika watatu na hapa ni Mbweni
Mallya: Ulipata kujua au Kumuona Mshitakiwa wa Pili Adamoo?
Shahidi: Alinimbia Mmoja yupo ila hakai sana Mlangoni anajificha ficha sana Kwenye Kona ktk Cello yake
Jaji: Umesema Mmoja..?
Shahidi: Kwenye Cello yake hakai Mlangoni anajibu akiwa apembeni Ila Mmoja nimeongea naye kajitambulisha ni Luteni wa Jeshi anatoka KJ 92. Anaitwa Dennis Urio
Mallya: Unaposema anatoka 92 KJ Unamaanisha nini..?
Shahidi: Anatokea Kikosi cha Komandoo
Jaji: Subiri Kidogo
Ulimtumia?.?
Shahidi: Nikimtumia Yuleyule Askari kuwa yule aliyejificha anaitwa Adamoo Mwambie Ling'wenya anakuuliza Vipi hali?
Mallya: Ulijuaje aliyejificha ni Adamoo
Shahidi: Ni kwa Ufahamu wangu baada ya Kuambiwa tupo watatu na na Adamoo na Urio nimewaona Tazara nikajua ndiyo hao hao
Mallya: Kitu gani kilifuata baada ya hapo?
Shahidi: Aliniambia anaendeela Vizuri, Tukawa tumezoeana hata alipokuwa anaingia kazini alikuwa lazima aaanze Kuita " Sauti ya zegeeeeee" hata akija kiraia
Mallya: Unaweza kukumbuka pale Mbweni ulikaa kwa Muda gani.?
Shahidi: Nilikaa kuanzia Tarehe 09 Mpaka tarehe 19 Nilipofikishwa Mahakamani
Jaji: Tarehe 19 ya Mwezi gani .?
Shahidi: 09 ya Mwezi wa 08 Mpaka Tarehe 19 ya Mezi 08 Mwaka 2020
Mallya: Nakurudisha Moshi, Ulipopigwa Kwa marungu ukaomba Kurukaruka nini Maana yake.?
Shahidi: Niliomba Kurukaruka ili nichezeshe Visigino,Maumivu yasikae sana
Wakili wa Serikali: OBJECTION wakati Shahidi anatoa Ushahidi wake Asubuhi hakusema kuwa Mahita ndiye aliyempiga
Jaji: What is your Concern katika hilo
Wakili wa Serikali: Mwanzo halikutajwa Jina la Mahita ndiye aliyempiga
Jaji: Lilisemwa au halikusema
Jaji: Sasa itabidi nirejee nilichokiandika Asubuhi
Jaji anasoma
" Wakati anatoa ushahidi wake Mshtakiwa alisema alipigwa na Mahita peke yake" Wengine walikuwa wanauliza Kwanini nilikuwa Moshi
Jaji: Bila shaka Mahita ndiye aliyetajwa Kufanya kazi hiyo, Tunaweza Kuendelea
Mallya: Kile Kitendo cha Kuomba Kurukaruka maana yake ni nini?
Shahidi: Yale Maumivu ya Kupigwa kwenye Nyayo kama ningekaa yangezidi,Kwangu niliona Bora Kurukaruka kuyapunguza, Sikutaka Kukaa kabisa
Mallya: Wakati Unasafirishwa Kutoka Kilimanjaro Kuja Dar es salaam Mikono yako ilikuwaje
Shahidi: Ilikuwa imefungwa Pingu
Mallya: Na Uliposhuka pale Tazara Mikono yako ilikuwa katika hali gani
Shahidi: Ilikuwa na Pingu
Mallya: Na Ulipokuwa Mbweni Mikono yako ilikuwaje
Shahidi: Nilikuwa na Pingu
Jaji: Kwa hiyo ukiwa Cello Tazara na Mbweni Mikono yako wakati wote ilikuwa na Pingu
Shahidi: Ndiyo Mheshimiwa Jaji
Mallya: Wakati wote huo unafungwa pingu unaweza Kuielezea Mahakama Ulikuwa unajisikiaje
Shahidi: Sikuwa najisikia Vizuri,Ukizungatia Goodluck lazima azibane Sana zile Pingu hata Nikimwambia Mahita,Yeye anasema muache hivyo hivyo
Mallya: Wakati wote huo Ukiwa Mbweni Adamoo ulimsikia tena
Shahidi: nilimsikia kwa sababu kila Siku Asubuhi lazima Nimuita Vipi hukooooooo,Yeye anajibu Mdogo Mdogo
Mallya: Katika Kesi hii Ndogo elezea uhusika na Ushiriki wake
Shahidi: Pale Rau yeye Ndoye alikuwa anatoa Amri zote Kama Kutupiga pingu, Kutuchukua Kutuweka kwenye gari
Mahita wakati ananishughulikia katika Kijumba nilipopatia Mateso yeye ndiye alikuwa akinihoji
Mallya: kwa hiyo ASP Kingai akikwepo wakati Unafanyiwa mateso
Shahidi: Alikwepo
Mallya: Na uwepo wake alikuwa anafanya kitu gani
Shahidi: Yeye ndiye aliyekuwa anatoa Amri, pale Tazara Kingai alikwepo na Goodluck akaniambia kiukweli Mwenzako anatumia madawa ya kulevya, Nikajibu si kweli akasema Ngoja tuone mbeleni
Mallya: Unasema Ulimuona Kingai pale Mbweni
Shahidi: Alikwepo
Mallya: Ulimuona kiwa anafanya nini.?
Jaji: Subirni Hadhana inalia
Mahakama Kimyaaaaaaaaaa
Jaji: Tunaweza Kuendelea
Jaji: Unasema ulimuona Kingai Mbweni ulipotolewa Nje ,ulitolewa nje na nani.?
Mallya: Ulimuona Wakati gani
Shahidi: Wakati Goodluck na Mahita Wananitoa nilipishana naye nikapelekwa kwenye Kile Chumba
Mallya: Mheshimiwa Jaji Sina swali la ziada
Jaji: Sijui kama Muda Uliobakia Unatosha kwa Maswali au Tu break Mpaka Kesho
Kibatala ananyanyuka na kwenda kwa Mawakili wa Serikali kwa Mashauriano
Jaji: Wakili Kibatala...
Kibatala: Busara inatuongoza tupumzike Mpaka Kesho
Jaji: nashukuru sana Tunaahirisha Mpaka kesho Saa 3 Kamili Asubuhi ambapo Shahidi wa Pili wa Utetezi ataendelea Kutoa Ushahidi wake
---
Jaji ameshaingia
Kesi inatajwa
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021, Jamuhuri dhidi ya Halfan Bwire, Adam Hassana Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe
Jaji: Wakili wa Serikali
Wakili Kidando anatambulisha Jopo lake....
- Robert Kidando
- Nassoro Katuga
- Ignas Mwanuka
- Esther Martin
- Tulumanywa Majigo
Wakili Kibatala anatambulisha Jopo lake
- Adv Peter Kibatala
- Adv Sisty Aloyce
- Adv Gaston Garubindi
- Adv Idd Msawanga
- Adv Alex Massaba
- Adv Evaresta Kisanga
- Adv Hadija Aron
- Adv Michael Mwangasa
- Adv Faraji Mangula
- Adv Fredrick Kiwhelo
- Adv Nashon Nkungu
- Adv Jonathan Mndeme
- Adv John Mallya
Mshitakiwa wa Pili - John Mallya
Mshitakiwa wa tatu - Fredrick Kiwhelo
Mawakili Wengine wote ni Kwa mshitakiwa wa Nne Freeman Mbowe
Jaji: Siku ya Ijumaa shahidi( Mshtakiwa wa pili) alikuwa hajakamilisha Utetezi wake. Arejee kwenye Kizimba tuweze Kuendelea
Shahidi anaenda
Jaji: Wakili wa Serikali mpo tayari..?
Jaji: Upande wa Utetezi mpo tayari?
Wote wapo tayari
Jaji: Shahidi bado upo chini ya Kiapo kama tulivyokuapisha Siku ya Ijumaa. Mawakili wa Serikali watakuhoji Maswali na Baadae Upande wa Utetezi hususani Wakili wako anaweza kuja kukuongoza tena Kwa Kukuuliza Maswali. Unaweza kuchagua Kukaa au Kusimama
Shahidi: Nitakaa Mheshimiwa Jaji
Jaji: Bila shaka. Wakili wa Serikali Chavula unaendelea. Tafadhali endelea
Wakili wa Serikali: Naam Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Awali siku ya Ijumaa kabla hatujaahirisha, nilikuuuliza kuhusiana na wale waliokuvamia maeneo ya Rau hawakupata kujitambulisha, Kweli au Si Kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Wale watu Mlivyotoka pale kwenda Kituo cha Polisi hawakulueleza Majina yao akina nani.? Kweli au Si Kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Walivyokutoa Moshi kukuleta Dar es salaam hawakukueleza wao Majina yao ni Akina nani. Walipokupeleka Mbweni hawakukueleza Majina yao akina nani?
Shahidi: Kweli hawakunieleza
Wakili wa Serikali: Haukupata Kuwafahamu amajina yao wakati wote?
Shahidi: Niliwafahamu kwa wao alipokuwa wanaitana Majina yao na Nikaja kuthibitisha Majina yao hapa Mahakamani walipojitambulisha
Wakili wa Serikali: Wakati wa Kukusafirisha Moshi Kuja Dar es salaam Watu wale walikufunga Kitambaa Usoni?
Shahidi: ni Sahihi
Wakili wa Serikali: ni Jacket, Si Ndiyo?
Shahidi: ni Jacket ndiyo
Wakili wa Serikali: Hukujua ni akina nani unasafiri nao
Shahidi: Kweli kama nilivyoeleza
Wakili wa Serikali: Na hata Ulipofika Dar es salaam ukafikishwa Kituo cha Kwanza cha Polisi hukujua upo wapi
Wakili wa Serikali: We Jibu swali langu Kweli au si Kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Umedai ulipokuwa unasafirishwa Ulikalishwa Chini kwenye gari,Kweli au si kweli
Shahidi: Ni kweli
Wakili wa Serikali: Uliweza Kujua ni sehemu gani ya gari ..?
Shahidi: Nilipita Upande wa Kulia Kwa Uelewa wangu siyo Kwa Kuona, Nikafahamu nimekaa nyuma ya gari
Wakili wa Serikali: Ulikaa nyuma ya gari
Shahidi: Ndani ya gari,Sehemu ya Nyuma
Shahidi: Siwezi Kujua ni gari gani
Wakili wa Serikali: Unakubaliana na Mimi ukiwa Umefungwa Machoni uwezi Kuona .?
Shahidi: Ndiyo uwezi Kuona, ila ukiwa unatendewa unahisi
Wakili wa Serikali: Ukiwa umefungwa macho uwezi kuona hata kile kifaa wanachokusababishia Maumivu
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali: Nakurudisha Moshi,umesema walipokuwa wanakutesa Moshi walikuwa wabakuuliza Umekuja Moshi Kufanya nini
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Wewe Ukajibu umekuja Moshi Kufanya VIP protection ni Sahihi
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Ulisema ulipofika Dar es salaam kituo cha kwanza cha Polisi walikupa Chakula .?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Ni Chakula gani
Shahidi: Ugali na Mboga za Majani
Wakili wa Serikali: na wakati wote ulipokuwa pale hukufanyiwa Mateso
Shahidi: Sahihi
Wakili wa Serikali: na hata ulipokuwa Mbweni hakuna aliyekuja Kukupiga..?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Alipokuja Ramadhani Kingai alipolutaka Uthibitishe Marlezo yako na Kutia Sahihi alikupa Vitisho wala hakukupiga.?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Ni Lipi Mahakama ichukue kati ya haya Mawili,Ulielezq Mahakama kwamba Wakati unatoa Maelezo hapa Mahakamani,kwamba ulitoa Maelezo kwa sababu ulikuwa unateswa,Sasa unasema kwamba Kingai na wenzake hawakukupatia Mateso isipokuwa Walipa Vitisho tuh
Shahidi: Rudia swali lako
Wakili wa Serikali: Wakati wa Kesi Kubwa Umesema Kuwa Kingai wenzake walichukua Maelezo yangu baada ya Mateso,Leo unasema Alikuja Bwana Kingai kunitishia
Shahidi: Umeuliza wakati wa Kuchukuliwa Maelezo, Mimi wakati wote nilikuwa Chini ya Mateso
Wakili wa Serikali: Aahaaaaaa
Wakili Mallya: OBJECTION. Naomba Shahidi akiwa anatoa Maelezo yake apewe nafasi ya Kumaliza Kujibu Maswali
Wakili wa Serikali: Ulipokuwa Dar es Salaam hukuteswa isipokuwa Bwana Kingai alikutishia.?
Shahidi: Aliniuliza kuhusu Kupigwa siyo Kuhusu mateso,kwa sababu, Mimi nilikuwa Chini yao na Nimefungwa pingu, bado hayo kwangu ni Mateso
Jaji: Shahidi nafikiri ungejibu sasa hilo unalotaka wala hakuna tatizo kwamba uliteswa au lah
Jaji: Naweza kukusomea
Shahidi: Ningependa unisomee Mheshimiwa Jaji
Jaji: Kingai "Hakunipiga tulipokuwa Mbweni, alinipiga na Kunitishia" Sasa tuambie nini kilichokuwa kimetokea
Shahidi: Vyote vichukue
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Mahakama ichukue Vyote
Jaji: Sasa niandike vipi Hukutoa Maelezo na Ulitoa Maelezo ..?
Shahidi: Ananiuliza Mambo Mawili tofauti ambayo ajayatenganisha, Mimi nilitoa Maelezo Moshi Chini ya Mateso,nalisaini bila Mateso
Jaji: Nilisaini Maelezo bila Mateso lakini nisaini baada ya Vitisho
Shahidi: ni sahihi Mheshimiwa Jaji
Mahakama Kichekooooooo
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kuletwa Dar es salaam tarehe 07,Kabla ya siku hiyo uliwahi Kufika Dar es salaam.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Makazi yako yapo Dar es salaam.?
Shahidi: Hapana
Wakili wa Serikali: unafahamu wapi?
Shahidi: Kambi ya Jeshi Twalipo na Maeneo ya Uwanja wa Taifa
Wakili wa Serikali: Ujawahi Kufika Tazara.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Ulishawahi Kufika Mbweni
Shahidi: Hapana
Jaji: Kwa hiyo Kabla ya kesi ujawahi kufika Tazara wala Mbweni
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Hakuna Wakati ,unafikishwa Kituo cha Polisi wakakuacha wazi.?
Shahidi: sijwahi Kutolewa nje ya kituo cha Polisi
Jaji: Mnaeleeana kweli..?
Jaji: Kutoka Tazara kwenda Mbweni ulifungwa Jacket.?
Shahidi: Nilifungwa Jacket Usoni Mheshimiwa
Jaji: Wakili ulimaanisha hivyo.?
Wakili wa Serikali: Ndiyo Mheshimiwa
Jaji: Sasa nitaomba Mnapomtajia Vituo vya Polisi Mtaje na Majina
Wakili wa Serikali: Naanza Upya Ulitolewa akitambaa ama Jacket lako ulipofilishwa ndani ya Kituo cha Tazara
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Mpaka Unaingia Kituo cha Polisi Tazara ulikuwa umefungwa Usoni
Wakili wa Serikali: Moshi Mlikamatwa wangapi
Shahidi: tulikamatwa wawili
Wakili wa Serikali: Na nani.?
Shahidi: Na Mohammed Abdilah Ling'wenya
Wakili wa Serikali: Wakati wote unasafirishwa hukujua yupo wapi
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Kingai na Mwenzake Mahita,walieleza Mahakama kwamba waliwasafirisha wewe na Ling'wenya Kwenye gari moja
Shahidi: Kweli walitoa Ushahidi huo
Wakili wa Serikali: Hakuna Mtu aliyewaambia Mashahidi wale kuwa Si kweli Nyie hamkusafirishwa pamoja.?
Shahidi: sasa
Wakili wa Serikali: Jibu swali langu
Jaji: Je ulisikia au Hukusikia.?
Shahidi: Sikusikia
Wakili wa Serikali: Kama wakati wote unasafirishwa Mpaka unafikishwa Kituo cha Polisi Tazara ulikuwa hufahamu Mohammed Abdilah Ling'wenya yupo wapi, Kweli au si Kweli
Shahidi: Sahihi
Wakili wa Serikali: Ulikuwa peke yako Kwenye mahabusu
Shahidi: Nilikuwa peke yangu kwenye Chumba Changu, ila Mahabusu wengine walikuwa Kwenye Vyumba vyao
Jaji: Kwa hiyo ulikuwa Mwenyewe Kwenye Chumba cha Mahabusu..?
Shahidi: Ndiyo
Jaji: Hapakuwa na Mahabusu wengine..?
Shahidi: Walikwepo kwenye Vyumba vyao
Jaji: Hapa naona tusingeelewana
Wakili Mallya: Shahidi alitupa Picha Kuwa kuna mahabusu Yenye Vyumba Vidogo Vidogo na yeye alikuwa kwenye kichumba Chake ndani ya mahabusu
Jaji: Naomba Kusoma "Nilifunguliwa Jacket nikawa naona Sasa,nikajivuta hadi Mlangoni nikaanza kuona Mahabusu wengime wakiwa kwenye Vyumba Vyao" nafikiri ndicho nilichoandika
Jaji: Sasa tujielekeze Hapo
Wakili wa Serikali: Umesema ulikuwa Peke yako Kwenye Chumba
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Kushoto na Kulia palikuwa na Ukuta
Shahidi: Ni sahihi Kabisa
Wakili wa Serikali: Ulikuwa kwenye tafakari kwanini haya yananiyokea, nimekosa nini.?
washitakiwa 1,2,na 3 walikubali wanafahamianina wa wakiwa wanafanya kazi Ngerengere KJ92
Wahitakiwa 1,2, na 3 Walikuwa wanafahamiana kabla ya Kesi Kuanza
Wakili wa Serikali: Hukubisha kwamba kwamba hukuondolewa Jeshini kwa Maswala ya Kinidhamu, na asasa unasema Uliondolewa Jeshini kwa Maswala ya Afya
Shahidi: Siwezi kulijibia
Wakili wa Serikali: Kwanini uwezi Kulijibia
Shahidi: Documents zote sijawahi kuzitolea Maelezo, zilikuja na kuletwa na watu walioandaa
Wakili wa Serikali: Documents zipi hizi?
Shahidi: Zilioletwa kufungulia Kesi ya Ugaidi
Wakili wa Serikali: Ulisaini hukusoma.?
Shahidi: Nilisaini
Wakili wa Serikali: Na Mahakama ilikusomea.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Unasema Ulikuwa kwenye Misheni Congo
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Ulikuwa Battalion ya 3, wewe ulikuwa kikosi cha Mizinga
Shahidi: Hapana
Wakili wa Serikali: Wewe ulikuwa unafanya nini
Shahidi: Nilikuwa Special Force
Wakili wa Serikali: Huko Special Force ulikuwa unafanya kazi gani
Shahidi: Kazi zote
Wakili wa Serikali: Zitaje
Shahidi: Zote kuanzia kupika Mpaka Kwenda Vitani
Wakili wa Serikali: Huko Vitani huwa mnajihusisha na Kuteka Watu
Shahidi: Siyo kazi yangu kuzungumzia Maswala ya Vita
Wakili wa Serikali: Lakini Vitani huwa watu wanatekwa
Shahidi: Ukingalia kwenye Muvi wanatekwa ila Mimi ya Vitani siwezi kuyaeleza, Kuna watu wake Maalum wa Kuyaeleza
Wakili wa Serikali: Moja ya kazi ni Kulinda Lindo, mnalinda dhidi ya nani?
Shahidi: Dhidi ya Adui
Wakili wa Serikali: Unapokuwa umemkamata Mtu lindo Moja ya jambo ni Kumfunga pingu ili asitoroke
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Kweli kwa sababu mmeyafanya huko Vitani
Wakili wa Serikali anaongea na Jopo lao
Wakili wa Serikali: Wewe huwa unatesa watu.?
Shahidi: Sijawahi
Wakili wa Serikali: Ukiwa umekamata Adui ukamfunga Pingu utakuwa umemtesa
Shahidi: Utakuwa hujamtesa, Ndiyo maana umemuita Adui
Wakili wa Serikali: Naomba kuwaachia wenzangu
Jaji: Nawakumbusha tuna dakika 20 kabla hatuja-break
Wakili wa Serikali 2: Mheshimiwa mimi ninayo Machache kati ya mengi yaliyoulizwa na Mwenzangu
Jaj: Labda nimuulize Shahidi Mwenyewe, Una nguvu au tunaweza kuendelea na Maswali?
Shahidi: Tuendelee Mheshimiwa Jaji
Wakili wa Serikali 02: Wakati umeanza kuulizwa na Wakili wa Serikali umeongea Ukweli, Tunaomba uendelee kusema Ukweli
Wakili wa Serikali 02: Wakati unakamatwa, Ling'wenya je yeye alikuwa umbali gani?
Shahidi: Alikuwa karibu yangu, Sababu nilikuwa Pembeni naongea na Simu
Wakili wa Serikali 02: Umesema Ling'wenya alishuhudia wakati Unawekewa Madawa ya Kulevya?
Shahidi: Siyo yeye tuh watu wote waliona kwa Sababu Jambo hilo lilifanyika hadharani mbele za watu
Wakili wa Serikali 02: Kati yako wewe na Ling'wenya nani Mtaalamu wa Madawa ya Kulevya
Shahidi: Hakuna, Suala la Madawa walisema wao Wenyewe kuwa "Tumemkuta na Madawa ya kulevya"
Wakili wa Serikali 2: Kwenye ushahidi wako wako ulisema kuwa kuhusiana na Suala la kusaini hati yakukabidhi vitu vyako
Shahidi: Sikusema
Wakili wa Serikali 02: Ulimuonyesha Jaji Kuhusu makovu, Je unamakovu Mangapi?
Shahidi: Mengine yapo kichwani
Wakili wa Serikali 02: Uliiambia Mahakama kuwa makovu haya mengine yatofautishwe na Miguuni
Shahidi: Mahakama haikuuliza,Kuwa hayo Mengine yametokana na nini
Wakili wa Serikali 02: Mahakama itatofautishaje sasa?
Shahidi: Hiyo ni kazi ya Mahakama siwezi kuifundisha
Wakili wa Serikali 02: Ulipokuwa Mbweni Kuna Askari alikwambia Upo Mbweni Baada ya Kuwaonea Huruma
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 02: Huyo wa Pili aliyekuwa anasema huyo Askari ni nani.?
Shahidi: Mohammed Abdilah Ling'wenya
Wakili wa Serikali 02: Kumbe mlikuwa naye na Mkaonana Mbweni
Shahidi: Kujua tupo naye nilijua nimesema, Sikuwahi kumuona kwa macho
Wakili wa Serikali 02: Umeiambia Mahakama aliyekupiga Rungu Moshi ni nani
Shahidi: Sikuwa namfahamu
Wakili wa Serikali 02: Maelezo aliyokuletea Bwana Kingai ukayasaini na Kuyathibitisha,Ukiyqona utayakumbuka.?
Shahidi: Siwezi Kuyakumbuka, Kwa sababu sikuyasoma, Labda sehemu za sahihi yangu na nilipoandika
Wakili wa Serikali 02: Wakati unateswa Moshi uliwajibu Kuwa umeenda kwa VIP PROTECTION ,ukawajibu upo kwenye mazungumzo
Shahidi: Ni Kweli
Wakili wa Serikali 02: Wakati Wakili Kibatala anakuuliza wakati wa Maelezo ulisema Ungeweza Kumuita Mwajiri wako
Shahidi: Muajiri Mtarajiwa
Wakili wa Serikali 02: Kwa hiyo Mahakama iandike hujawahi kuajiriwa na Mshitakiwa wa nne
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali 02: Kwa hiyo ni sahihi nikisema katika hayo Mazungumzo yenu mliwahi Kufanyia Aishi Hotel
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 02: Wakati mnafanya hayo Mazungumzo mlikuwa na Mshitakiwa wa 3.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 02: Wakati Upo Tazara unasema uligudua kwa Vitu Viwili Kwa Honi ya Treni na Kuambiwa hiki ni kituo cha Kuhifadhia Watuhumiwa wa Ugaidi
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 02: Ulishaiambia Mahakama Kwamba Unatuhumiwa kwa Ugaidi.?
Shahidi: Hapana
Jaji: Subiri Kidogo
Wakili wa Serikali 02: Nina swali moja la Mwisho
Jaji: Sawa endelea
Wakili wa Serikali 02: Wakati unachomwa na Bisibisi ushawahi kuiambia Mahakama walikuwa wanataka nini, kama vile Moshi walikuwa wanakuuliza Umefuata nini..?
Shahidi: Hapana
Jaji: Sawa tunapumzika kwa Muda tutarejea Baada ya Dakika 20
Jaji ananyanyuka
Mahakama imerejea
Jaji ameingia Leo Mapema sana kuliko watu wengi na Watuhumiwa. Imebidi Jaji asubiri watuhumiwa waletwe
Kesi imetajwaa
Jaji: Nataka kuanza Utamaduni wa Kuanza Kuzingatia muda. Nikisema naanza Saa 3 Mtanikuta humu. Nikisema tunaanza saa 3 itakuwa Saa 3 Kamili. Na Nikisema Saa 4 itakuwa Saa 4 Kamili. Itapendeza kama Tutazingatia Muda. Na huo ndiyo Ustaarabu,Ikitokea Mtu anadharula nijulishwe. Haipendezi kesi Ikianza milango inafunguliwa kila Saa
Jaji: Upande wa Jamuhuri wapo tayari Kuendelea?
Utetezi.?
Shahidi.?
Wote wapo Tayari
Wakili wa Serikali 03: Wakati tukiendelea na hii Kesi tangu Mwanzoni na kingai,Mawakili wako na Ushahidi wako ulihojiwa Mantle Status ya akili yako,Ni kweli Jambo hili limejitokeza.?
Shahidi: Ni kweli limejitokeza.?
Wakili wa Serikali 03: Kwa usahihi ukaita Battle Confusion.?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali 03: Kama Kweli hali hiyo imejitokeza Moja ya Jambo ambalo litakukumba ni Kupoteza kuona mambo kwa usahihi.?
Shahidi: Sijui
Wakili wa Serikali 03: Hujui kwa sababu hukumbuki wakati ukiwa na tatizo hilo nini kilikuwa kinakutokea.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali 03: Umewahi Kupoteza Uwezo wa watu unaowatambua au maeneo unayoyafahamu.?
Shahidi: Sijawahi
Wakili wa Serikali: Vipi Kuhusiana kutambua Muda na Tarehe.? umewahi Kuwa na tatizo la kuchanganya hivi vitu.?
Shahidi: Hapana sijawahi
Wakili wa Serikali 03: Vipi kwenye Kuchukua Maamuzi Sahihi, Kwamba Umempiga Mtu bila Sababu halafu baadae ukaja Kukumbuka
Shahidi: Hapana sijawahi Kufanya Maamuzi ya namna hiyo
Wakili wa Serikali 03: Kwa sababu ya Jambo la Battle Confusion ujaeleza Kwanini lilikukuta
Shahidi: Nilieleza Mahakama kuwa tatizo hilo nililipata baada ya Kutoka Vitani
Wakili wa Serikali 03: Sababu ya Battle Confusion zipo Nyingi,utakubaliana na mimi
Shahidi: Mimi siyo Mtaalamu
Wakili wa Serikali 03: Moja ya Sababu ya Kupata Battle Confusion ni Matumizi ya madawa ya kulevya yaliyokithiri, Ni sawa.?
Shahidi: Sababu zenu hizo siwezi Kuwabishia
Wakili wa Serikali 03: Katika Kipindi cha hili tatizo ulipangiwa kazi..?
Shahidi: Nilipangiwa kwenda Hospitali
Wakili wa Serikali: Ilikuchukua Takribani Miezi 02 baada ya Kurudi Jeshini, kabla ya Kufukuzwa kazi kwa Sababu wewe uliendelea kutumia madawa ya kulevya
Shahidi: Sijawahi Kutumia Madawa ya Kulevya
Wakili wa Serikali 03: Post Dramatic Disorder ni Kitu gani.?
Shahidi: Sifahamu
Wakili wa Serikali 03: Kama ufahamu kuhusiana na Ugonjwa wa Post Dramatic Disorder limefikaje hapa Mahakamani, Umewahi Kumwambia nani
Shahidi: Sijawahi Kumwambia Mtu
Wakili wa Serikali 03: Utaribu baada ya Kurudi kazini ulikuwaje?
Shahidi: Nilitakiwa kuendelea kuriport Hospitali
Wakili wa Serikali 03: Kwa hiyo Ugonjwa huu ,umeathiri utimamu wa akili.?
Shahidi: Hapana
Wakili wa Serikali: Unasema ulienda Moshi Kufanya kazi ya VIP PROTECTION, Kile Kitabu chenye Orodha ya Mashahidi na Ushahidi wote we ulikipata.?
Shahidi: Ndiyo ninacho
Wakili wa Serikali 03: Kuna Chochote Mshitakiwa wa nne amesema alikuita wewe na wenzako kwa ajili ya VIP PROTECTION.?
Shahidi: Sijakiona
Wakili wa Serikali 03: Kwa hiyo hili suala lako la VIP PROTECTION hajalisema, hata alipopewa nafasi ya kusema hakuwahi Kulisema popote
Shahidi: Sijui yeye sasa, Miye niliulizwa ndiyo Maana nikajibu
Wakili wa Serikali 03: Ulipokuwa unahojiwa na Mawakili wa Serikali ulikuwa unachukua Muda Sana Kujibu, hata Wakati Mwingine Mheshimiwa Jaji alikuwa akitoa Mwongozo, Nikisema una uwezo Mdogo au Umeathirika kiakili
Shahidi: Kama wewe ni Daktari siwezi Kukubishia Uchunguzi wako, ila Miye nikiwa nashindwa kujibu kwa haraka kwa sababu Maswali yanazunguuuuuka hayajanyooka
Wakili wa Serikali 03: Nipo sahihi nikisema hali ya Akili yako ipo sawa sawa.?
Shahidi: Upo sahihi
Wakili wa Serikali 03: Ujatueleza Umuhimu wa Kutueleza Utimamu wa kwanini Umeieleza Mahakama Ya tatizo la Akili kwa wakati Fulani
Shahidi: Nimeeleza Umuhimu, kwa Kufuatia Swali nililoulizwa Mahakamani
Wakili wa Serikali 03: Ina uhusiano gani suala la Ugonjwa wako na Makosa ya Njama za Kutenda Ugaidi
Shahidi: Kwangu naona Vina uhusiano kwa Sababu nimeulizwa na Mahakama, Isingekuwa na Umuhimu nisingeulizwa
Wakili wa Serikali 03: Je, unajua umuhimu wa kwamba umewahi kupata Battle Confusion ..?
Shahidi: Umuhimu unajua Mahakama yenyewe iliyouliza hilo swali
Wakili wa Serikali 03: Mheshimiwa Jaji naomba tukomee Hapa hakuna Swali Lingine
Jaji: Wakili Mallya kama Una maswali ya marejeo
Mallya: Mheshimiwa Jaji ninayo Machache
Mallya: Swali langu la Kwanza kwamba wewe Ni Komandoo umefundishwa kukaa na Njaa na Kuhimili Mateso, JE uelewa Wako ni nini katika Swali hili
Wakili wa Serikali 03: OBJECTION hilo swali haliruhusiwi katika Re-Examination, Yeye ange recall tu katika yale aliyojibu katika Examination
Jaji: Mallya Unakubaliana na alichosema Wakili wa Serikali
Mallya: Sababu ya Muda naomba ni Rudie Swali tu
Jaji: Hapana, Je umekubaliana naye?
Mallya: Sikubaliani naye lakini sababu ya Muda Nirudie swali tu.
Jaji: Sasa hapo tulimalize kwanza kabla Ujaenda Mbali, Kuliko kwenda na Mambo ambayo Mtu hajaridhika nayo
Mallya: Sijaja na Swali Jipya napitia Maswali yale yale na majibu yaleyale
Jaji: Sawa unaweza ukaanza na Swali Mwanzoni
Mallya: Swali langu la Kwanza kwamba wewe Ni Komandoo umefundishwa kukaa na Njaa na Kuhimili Mateso, JE uelewa Wako ni nini katika Swali hili
Shahidi: Katika Upande wa Mafunzo una kanuni zake na taratibu zake na kwa Upande wa ukamataji wa watuhumiwa kuna Kanuni zake na Taratibu zake
Wakili wa Serikali: OBJECTION
Jaji: Subiri kwanza Shahidi ajibu kwanza tuone kama linahusika na mnachotaka kufanya Objection
Wakili wa Serikali: Hakuna sehemu tuliyomuuliza kuhusiana na kuvumilia njaa
Jaji: Mliuliza nini siku hiyo.?
Wakili wa Serikali Chavula: Katika Mafunzo yenu Mnafundishwa Kuvumilia Njaa.?
Jaji: Kwanini uliuliza hilo swali,Ulilenga Ku-Establish kitu gani?
Wakili wa Serikali: Nililenga Kuwa ni Mtu ambaye ni Trained na yale ya Kukaa na Njaa si Kitu kigeni kwake
Jaji: Sawa kaeni Chini nafikiri hakuna Kitu Kigeni kati ya mlichouliza, kilichoulizwa na Kinachojibiwa
Jaji: Namruhusu wakili Mallya Kuendelea
Mallya: Kwa uelewa wako kwanini uliulizwa swali hilo
Shahidi: Nimeelewa Kuwa kukaa na Njaa ni Haki kwangu, Kupitia Mateso ni Haki yangu na Kwamba Kukamatwa Bila kuzingatia Sheria ni Haki yangu kwa sababu tu ni Vitu nilivyowahi Kupitia
Mallya: Kuna sehemu umesema Ulipigwa na kuna sehemu Uliteswa mgawanyiko wa hili Jambo likoje?
Shahidi: Kupigwa ni sehemu ya mateso, Kutishiwa ni Sehemu ya mateso, Ndiyo maana nilisema anilipofika Dar es salaam nilikuwa bado nipo Ndani ya Mateso. Kitendo Cha Kutolewa Kwenye Chumba na kuambiwa Kitakurudia kilichokutokea Moshi ni sehemu ya mateso wakati huo Comfortability yangu imeshapotewa kwa sababu nilikuwa nasimamiwa na Bastola. Na Vilevile Kitendo Cha Kushinda na Njaa ni Mateso pia
Kitendo Cha Kutolewa kituo Kimoja kimoja cha Polisi na Kupelekwa Kingime na Kubadirishiwa jina unalotambulika na Ulimwengu,Kwangu iliniathiri na Nikaona bado Nipo Chini ya mateso
Mallya: Umeulizwa kumjua au Kumuona Mahabusu ya Tazara na Mbweni, ulipokuwa unasema Ulijua yupo ila sikumuona?
Shahidi: Nilikuwa nikimaanisha alipokuwa Mahabusu Nyingine tuliweza kusalimiana hata kwa sauti ya Juu, Lakini siyo Kuonana Kwa face to face
Mallya: Nia ya kuonesha Makovu ilikuwa ni nini.?
Shahidi: Kwa sababu kuonesha Kuwa baada Matendo yale yaliacha Alama za kuumia, ndiyo maana nikaonesha Makovu
Mallya: Umeulizwa Pia Kuhusiana na Kupigwa ukiwa moshi na Kuwaona waliokutesa moshi kama uliwatambua au hukuwatambua
Shahidi: Kwenye kile chumba nilichokuwa nateswa palikuwa na watu wengi, Wengine nilikuja kuwatambua mbele ya Mahakama na Mtu Mwingine sikuweza Kumfahamu
Mallya: Uliulizwa kuhusiana Kutobolewa na Bisibisi Kwenye Makalio...
Wakili wa Serikali: OBJECTION. Aulize Yaliyojitokeza kwenye Examination, Hii kwamba elezea hiyo, Ni Maswali ambayo hayaruhusiwi
Jaji: Wakili Mallya?
Mallya: Re examination wajibu wake ni Kufanya Explanation
Jaji: Nafikiri Wakili wa Serikali yupo sahihi, unachouliza Unaacha uwanja Mpana wa Shahidi Kueleza Jambo Jipya badala Kuziba Mwanya wa Kilichoulizwa
Mallya: Wale waliokuwa wanakuchoma Bisibisi, Walikuwa wanataka nini?
Shahidi: Ilikuwa ni sehemu ya Mateso. Walikuwa wanasema Nyinyi si mmejifanya kutusaliti, sasa mtaona
Jaji: Nafikiri sasa tunafungu Box kwa kile nilichokuwa naeleza
Mallya: Mawakili wa Serikali alikuuliza Swali kwamba waliokuwa wanakuchoma bisibisi walitaka Kujua nini.?
Jaji: Naona Mawakili wa serikali wanataka mshauriane hapo, Inaruhusiwa
Mallya: Nitarudi baadae kwenye swali hilo. Je hapa Kwa ufahamu wako kinachoendelea Mahakamani ni Jambo gani?
Shahidi: Ni Shauri dogo katika Shauri Kubwa
Jaji: Lile swali lako umeuliza kweli?
Mallya: Nimeliweka akiba nitalirejea
Mallya anaenda Kushauriana na Jopo lake
Mallya: Wakati wanakuchoma walikuwa wanataka nini?
Shahidi: Muendelezo wa Mateso
Mallya: Nafikiri nimemaliza
Shahidi (Mshitakiwa wa pili) Anatoka Kizimbani
Jaji: Wakili Mallya endelea Uwanja ni Wako...
Mallya: Tunae shahidi mwingine Mohammed Abdilah Ling'wenya
Jaji: Jitambulishe
Shahidi: Mohammed Abdilah Ling'wenya.
Shahidi: Dini Muislamu
Jaji: Thibitisha Wallah Billah taalah Natihibitisha mbele ya Mahakama hii Ushahidi nitakaotoa utakuwa ni Kweli tupu,Eeh Mwenyezi Mungu Nisaidie
Jaji: Tutapisha Hadhana halafu tutaendelea
Hadhana Inaendeleeeee
Jaji: Wakili Kibatala Ulitaka Kuzungumza
Kibatala: Naomba nimtambulishe Wakili Dickson Matata kwa ajili ya Mshitakiwa watatu
Jaji: Sawa nakushukuru. Hapa Kuna Maelezo
Jaji: Kuna Shida Kumuita Mshitakiwa watatu kuwa Shahidi, Serikali.?
Jaji: Kiwhelo Kuna tatizo kwa Mshitakiwa wako kuwa Shahidi?
Wakili Kiwhelo: Hapana
Mallya: Makazi yako kwa sasa hivi Kimara King'ong'o?
Jaji: Makazi yako kwa sasa hivi?
Shahidi: Natokea Gereza la Ukonga
Mallya: Kabla ya Kukamatwa ulikuwa wapi
Shahidi: Mtwara kampuni DOT kampuni ya kusaga Kokoto
Mallya: Kabla ya hapo..?
Shahidi: Nilikuwa Ngorongoro
Mallya: Unamfahamu Mshitakiwa wa 2
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Umemfahamu wapi.?
Shahidi: Jeshini KJ 92 JWTZ Ngerengere
Mallya: Umeanza Lini?
Shahidi: Mwaka 2008 Mpaka 2017
Mallya: Kazi gani ulikuwa unafanya .?
Shahidi: Komandoo,Special Force
Mallya: Unamfahamu Vipi Mshtakiwa wa Pili
Shahidi: Nilikuwa nipo Mtwara nikapigiwa Simu na Askari Mwenzangu ambaye nilikuwa nipo naye Jeshini anaitwa Dennis Urio kwamba Kuna kazi ya kwenda kumlinda Mtu bila kunitajia huyo Mtu ni nani. Nikamwambia asubiri nikifika Nyumbani aongee na Baba akikubali sawa. Nilipofika Nyumbani akapiga simu nikampa akaongea na Baba. Baba akauliza si unamfahamu, nikasema Ndiyo akaniambia nakuombea Dua nenda
Mallya: Siku ya tarehe 05 Mwezi 08 2021 Maeneo ya Rau Madukani kulitokea kitu gani?
Shahidi: Nilikuwa kwa Dada yangu Mmoja anaitwa Asma, akiwa Dukani kwake mimi na Adamoo tukawa tunasubiria Chakula
Mallya: Kilichokupeleka Rau Moshi ni kitu gani?
Shahidi: Tulikuwa tunaenda kukutana na Mwajiri wetu ili tuje kukubaliana naye
Mallya: Mshitakiwa wa pili alikuwa anafanya kitu gani?
Shahidi: Wakati nipo Dukani, Kwenye Upenyo Coridor nikasikia Kelele sana, Nikataka niende kuona. Nikakuta Adamoo ameshanyanyuliwa na Kukabwa. Nikauliza Tatizo ni nini.? Nikashikwa Mkono wakaniuliza wewe Unamfahamu huyu?
Mallya: Ulipata Kujua ni akina nani.?
Shahidi: Niliwaona kwa mara ya kwanza. Wakaniuliza unamfahamu huyu.? Akatoka mwingine akasema ana pistol ana pistol ana pistol
Alinyofoa Kutoka amwilini Kwa Adamoo Upande wa Kulia akasema ana pistol ana pistol akasema na madawa ya kulevya anayo
Mallya: Eleza sasa Pistol anatoa wapi.?
Wakili wa Serikali: OBJECTION anamfeed Majibu
Mallya: Baada ya kumkuta Adamoo amenyanyuliwa Juu kitu gani kiliendelea? Ukisema alimtolea bastola unataka Mahakama ipate apicha gani
Shahidi: Baada ya Kuona Wanamfanyia Adamoo yale na Adamoo namfahamu na nilikuwa naye muda mrefu, Nikauvuta Mkono wangu kwa aliyekuwa amenishika. Nikawaambia Kuwa adamoo hakuwa na hivyo Vitu, nikatoa Simu na wallet nikaweza Kibarazani
Jaji: Ulitoa simu na nini
Shahidi: Simu na wallet
Mallya: Kusema walimuwekea unamanisha nini.?
Shahidi: Kwa Sababu nilianza Safari ya kwenda Moshi na Adamoo kuanzia Chalinze, Nafahamu hakuwa na Vitu hivyo. Nikasema huyu Mtu kwakuwa mmemuwekea na Mimi ngoja nitoe Vitu vyangu.
Mallya: Wakati huo Adamoo Yupo wapi?
Shahidi: Wamemshusha Chini ila wanampiga pale pale chini
Mallya: Uliweka vitu vyako wapi?
Shahidi: Waliochukua walikuwa ni Polisi?
Mallya: Kwenye wallet kulikuwa na nini.?
Shahidi: Palikuwa na Pesa.?
Mallya: Kiasi gani.?
Shahidi; Laki tatu
Mallya: Zipo wapi?
Shahidi: Hapana sielewi
Mallya: Watu waliomvamia Adamoo Unaweza Kujua walikuwa ni watu wangapi.?
Shahidi: Walikuwa Zaidi ya watano
Mallya: Baada ya Kupanda gari Mmlielekea Wapi.?
Shahidi: Central Moshi
Mallya: Kichofuata nini.?
Shahidi: Waliotuleta wakatoka, baada ya kutuacha. Walitutenganisha. Nakumbuka Mmoja alikuwa Askari Bonge nilimueleza kuwa mimi nilikuwa mwanajeshi. Wakauliza Kama nawajua Komba na Mselem
Jaji: Komba ni Mtu Mwingine na Msellemu Mtu Mwingine
Mallya: Nini ulishuhudia Kinachomuhusu Adamoo?
Shahidi: Nilishihudia akiwa yeye ni wa Kwanza kuinginzwa selo yake na Mimi nikawekwa selo Nyingine
Mally: Walipomtoa selo Ulionaje.?
Shahidi: Selo ya Kwanza Ya Kwangu na Yapili,Wakati wanamuingiza Cello yake sikumuona ila wakati wanamtoa alikuja Mtu kwenye Cello yangu akaita Ling'wenya Nyuma yake wakampitisha amtu wamemuinamisha
Mallya: Ulimtambuaje..?
Shahidi: Alikuwa na Jinzi Nyeusi na Shati la maua Maua
Mallya: nini Kilifuata?
Shahidi: Nilisikia kilio huko alipopelekwa Kwa Sababu haikuwa mbali na selo yangu, Nilisikia kilio akilia na nilimtambua kwa Sauti sababu namuitaga sauti ya zege
Mallya: Ulitambua sauti ni ya nani.?
Shahidi: Nilitambua ni Sauti ya Adamoo
Mallya: Ilikuwa ni Sauti ya namna gani.?
Shahidi: Ya amtu anayepigwa, alikuwa analia Eeeehiii Ehiiiiiii Ehiiiiiiiiiiiiiiii ya mtu anayeteswa
Mallya: Ilidumu kwa Muda gani
Shahidi: Sina uhakika ila ni Kama Nusu saa
Mallya: Umesikia Sauti ya zege analia kwa Nusu saa,Nini Kilifuata
Shahidi: Baada ya muda amfupi Kupita akapitishwa Mtu yule yuke aliyevaa Jinzi Nyeusi na shati la maua akiwa hawezi kutembea alishikwa huku kushoto na kulia na kwamba wakamburuza hadi Cello inayofuata baada ya kwangu
Mallya: Nini Kilifuata
Shahidi: Nikajua anayefuata ni mimi
Mallya: Baada ya kujia Unayefuata ni wewe, kilifuata nini
Shahidi: Walinichukua Mimi wakanipeleka huko, Nikaenda nikakuta watu wamekaa na wana simu zao wananirekodi
Wakasema taja majina Matatu
Nikawatajia
Wakaniuliza Unafanya kazi gani
Nikawatajia nimetoka Mtwara
Wakanipiga Buti wakasema wanajua mimi nimefuata nini Moshi
Mallya: Mahita yupi unayemzungumzia.?
Shahidi: Mara ya Mwisho nilimuona hapa mahakamani akitoa Ushahidi
Mallya: Hapo Mlikuwa sehemu gani?
Shahidi: Ni ndani ya Central Police palepale, nilitolewa Cello nikapalekwa kwenye Kijumba Kidogo. Palikuwa na Bomba refu, nikiwa nimefungwa Mikono na miguu, Mimi kwa ufahamu wangu inaitwa killing zone
Mallya: Killing zone ni Kitu gani?
Shahidi: Unakuwa Unaning'inizwa Miguu Juu Kichwa chini
Mallya: Kilifuata kitu gani..?
Shahidi: Nilipigwa sana kwenye Unyayo kwa sababu zilikuwa zimekaa Juu
Mallya: Wakati wanakupiga wanasemaje?
Shahidi: Aliyenipiga ni Mahita tu
Mallya: Walikuwa wanahitaji kitu gani?
Shahidi: Niliwaambia nimekuja kwa kazi ya VIP PROTECTION Kwa Kumlinda Mwenyekiti wa Chadema. Wakasema Utasema tu?
Mallya: Ilichukua Muda gani
Shahidi: Kama Nusu saa
Mallya: Ikawaje
Shahidi: Alikuja Mtu Mtu aliyevaa kiraia akatoa Amri "Mwacheni sasa msimpige
Wakawa wameniweka nimekaa Chini nikiwa na Pingu na Mguuni nimefungwa kamba
Jaji: Miguuni Ulifungwa nini?
Shahidi: Miguuni nilifungwa kamba
Mallya: Baada ya hapo Ulipelekwa wapi?
Akaniambia huku Hoi na yeye akaniambia Mimi Mwenyewe Huku Hoi
Jaji: Ukisema Mimi Huku hoi unamaanisha nini.?
Shahidi: Yaani nimeumia sana na kuchoka sana
Mallya: Mahita alikuwa anakupiga na Kitu gani?
Shahidi: Sijakishika vizuri lakini kama Shaba Nzito
Mallya: nini Kilifuata?
Shahidi: Ni kwamba kwa wao walivyonipiga walifikiri sitoweza Kutembea, Lakini Mimi walipomaliza Kunipiga niliweza Kutembea na palepale Walipomaliza Kunipiga nikiwa nimekaa chini niliwaomba waniruhusu nirukeruke kutuliza Maumivu. Wakati wanajitoa Nje Afande Jumanne akaropoka " Mwenzako amepigwa Sana, Bahati yako Ulipata Mtetezi"
Wakati mimi nikiwa tayari ndani ya gari tayari nilimuona Adamoo anatolewa kwa kukokotwa, Wakaniwahi Mahita akampa Goodluck shuka wakanifunga Kichwani
Nikawa nimetulia, Nikaona Mlango wa gari umefunguliwa, na Mtu akaingia na kuanza Safari.
Mallya: Baada ya kumuona Adamoo wakakuzuia na kukufunika usoni, Je ulimuona akiwa na Hali gani?
Shahidi: Nilimuona akiwa anakokotwa hawezi hata kutembea
Mallya: Baada ya kuinamishwa kichwa na kufungwa Shuka usoni kitu gani Kilifuata?
Shahidi: Nilikuwa kimya wakati huo gari ikawa wakati wote inatembea
Mallya: Wakati huo nini Kilifuata
Shahidi: Mimi nilikuwa katikatika nimekalishwa Kushoto yupo Goodluck na Kulia yupo Jumanne. Na Hali hiyo niliishuhudia kabla sijapigwa Shuka usoni
Mallya: Wakati huo nini Kiliendelea?
Shahidi: Ilikuwa wakati wote kimya hata nikiiinua shingo Kujinyoosha wananirudisha tena chini
Mallya: Unakadiria ilikuwa ni safari ya namna gani?
Shahidi: Ilikuwa ni safari ndefu kama ya mkoa kwa mkoa. Baada ya kufika na gari Kusimama nilishushwa kwa kushikwa nyuma kwa kuinamisha na kitambaa changu Vilevile Mpaka wakafungua Geti, nilipoingia wakanitoa Kitambaa
Mallya: Wakati huo wote mlisimama Kula Chakula.?
Shahidi: Hatukusimama Popote kula chakula. Waliponitoa tu Kitambaa alijitokeza Jamaa Mmoja wa kirangi, Mweupe akaniuliza nini shida.?
Kwa mwonekano wake walikuwa na Ndevu ndefu na Juu alikuwa amevaa Combat lakini siyo ya kitanzania
Nikamwambia Mimi nimekamatwa na tumeletwa hapa sijui ni Wapi
Akaniambia "Hapa ni Tazara Kituo cha Polisi"
Wakati naongea na Yule mrangi kuna mwingine akajitokeza kijana Mweusi, nikawambia nimeletwa hapa lakini Mimi nilikuwa ni Askari
Yule akijana Mweusi akasema Vipi MIC? MIC ni neno la Kijeshi
Nikamwambia Mbona wewe upo hapa.?
Akaniambia Mimi ni Askari nilikuwa naswali kwa Azizi Ally kambi yangu ni Twalipo
Alipokuwa amepaki Pikipiki nje akiwa anaswali ndani, wakamsubiri atoke wakampini wakamleta Tazara na akasema yupo Tazara kwa Miezi nane.
Nikamuuliza shida nini.?
Akasema wanaoletwa hapa ni Kesi za Kigaidi.
Mallya: Alikuwa anasema hapa, anamaanisha hapa Wapi?
Shahidi: Hapa Tazara
Nikamuomba aangalie Cello inayofuata kama kuna Mwenzangu kwa sababu wao Cello yao ilikuwa haijafungwa na walikuwa wakifanya Mpaka Usafi mle ndani
Wao Cello yao walikuwa wanaona Kila kitu, wakaniambia Kuna Wenzako Mmoja yupo Cello ya Mbele
Nikaanza Kuita Adamoo Adamoo Adamooo
Kuna Askari Mmoja akasema tuache Kelele yeye hajatuleta
Shahidi: Nikawa naendelea kupiga Story na Yule Mwanajeshi niliyemkuta pale
Wenzake wakamsii asiongee na Mimi na Mimi wakanipa ishara kwamba watu wenu wanakuja
Mallya: Kitu gani kilifuata?
Shahidi: Nikawa nachungulia Kwenye Cello yangu, hawakufika kwenye Cello yangu
Mallya: Wakati gani tena ulimuona mshitakiwa wa Pili?
Shahidi: Siku inayofuata nikiwa kwenye Cello siku inayofuata nikasikia Kilio, nikachungulia Kule Nyuma nikaona watu niliiokuwa nao Depo JKT , TPDF na 92KJ Komandoo (Wadepo wangu)
Mapumziko
Jaji anaingia.
Shauri Limetajwa Tayari.
Jaji: Lin'gwenya aendelee
Jaji: Leo saa Kumi tunafunga hadi kesho.
Jaji Kamkumbusha Lin'gwenya Tulipoishia
Shahidi: Nilishuhudia Chuma Chugulu na Alex akiwa na Kijitabu na wenzie wakiwa Wanadepo Wenzangu Kupitia Matundu ya Dirisha walikuwa wanamtesa Mtu. Ambapo baade nilimfahamu yule Mtu Kwa Majina anatolewa Kwenye Magari Mabovu alipokuwa anateswa kwa kushikwa na Mtu Mmoja na Mmoja yupo nyuma yake nilimfahamu aliyekuwa anateswa Kuwa ni Dennis Urio ambaye ni Luteni wa Jeshi ambaye alinitafutia hii Kazi ya VIP PROTECTION kwa Mwenyekiti wa Chadema
Mallya: Awali ulisikia Kilio baadae ukaona Mtu Mwenye kitabu na Rungu na baadae Urio anatolewa Kule kwenye Magari Mabovu, kwa aufahamu wako nani alikuwa anateswa Kule?
Shahidi: Kwa nilivyoona Mimi Leteni Dennis Urio ndiye alikuwa anateswa. Siwezi Kuwa na Ukahika nao ila Kama Dakika 15 Mpaka 20
Mallya: Kipi ulitangulia Kuona Kwanza Kati ya Wanadepo Wenzio na baade Askari Polisi na Urio?
Shahidi: Nilishuhudia Alex ndiye wa kwanza Kutoka baadae katoka Chuma Chungulu na Mapolisi wakiwa na Urio
Mallya: Kilifuata nini..?
Shahidi: Ilipofika Usiku nilitolewa nikafungwa Kitambaa
Mallya: Ulifungwa Kitambaa Ukiwa wapi.?
Shahidi: Ndani ya Gari
Mallya: Kabla ya Kufungwa Kitambaa Uliwatambua waliokuwa ndani ya Gari.?
Shahidi: Nilimtambua Goodluck na Mahita
Mallya: Ni Kabla ya Gari Kuondoka ndiyo Ulifungwa Kitambaa.?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Unaweza kutambua Gari ilitumia Muda gani.?
Shahidi: Ni Muda Mrefu sana,Ila siyo Kama Ule wa Kwenda Mkoani
Mallya: Kitu gani Kiliendelea..?
Shahidi: Maaskari wakasema Mwenzenu Moses Lijenje tumeshamtupa, Ameshatangulia huku wakinigusa Kichwani na Kitu nilichokuwa nahisi kuwa ni Bastola, Ukileta Ujanja Ujanja na wewe tunakutupa
Mallya: Maneno haya ulikuwa unaambiwa wakati gani wakati wa Safari au baada ya Kufika
Shahidi: Wakati wa Safari. Tulipofika nilikuwa nimebakia kwenye gari, Nilihisi watu wakifungua milango na Kushuka
Ikatoka Amri nishushwe, nikashushwa wakaniinamisha chini nikiwa bado na Kitambaa Usoni Pale Mapokezi nilipahisi hivyo kwa sababu tulisimama na Kuulizwa naitwa nani.? Mmoja akajibu Johnson John Wakaniinamisha Kichwa Wakanipeleka Mpaka Cello kule nilipoingia ndiyo wakanitoa Kitambaa
Mallya: Ulijuaje pale ni Cello
Shahidi: Nilipofikishwa tuh ile sehemu nikatolewa Kitambaa nikaanza Kuona Mazingira kama ya Tazara, Kama Milango ya Chuma na Vingine
Mallya: Huyu Johnson John waliyemtambulisha ulipata Kumjua??
Shahidi: Sikupata Kumjua, Walinipa Jina la Bandia
Kesho yake wakati wanakagua Mahabusu Johnson John halikuitwa hilo Jina, Wakapita Mpaka Kwenye Cello yangu wakaniuliza we unaitwa nani. Nikawajibu naitwa Johnson John
Mallya: Unasema Uliambiwa Usema Jina lako Unaitwa Johnson John, Nani alikwambia utaitwa Johnson John
Shahidi: Na Jumanne. Alinipa na Kikaratasi Kuwa Kuanzia Leo Mtu yoyote akija Utasema wewe ni Johnson John
Mallya: Alipopita Mtu akakuuliza baada ya Kutoitwa Jina lako.?
Shahidi: Nikamwambia naitwa Johnson John, Akawaita Askari wengine,Nahisi yule Mwanamama alikuwa ni Mkuubwa Kituo na alipotoka
Akaja Askari Mwingine akaniambia sasa tuambie Jina lako la Ukweli
Mallya: Ukajibu Vipi
Shahidi: Nikawapa Jina langu la Ukweli, wakaniuliza na Hili la Johnson John.?
Nikawajibu Kuwa hili nimepewa hapahapa
Wakaniuliza Una kesi gani?
Nikawajibu nimekamatwa Moshi baada ya kwenda kumlinda Mwenyekiti wa CHADEMA, Sijajua nimeshikiliwa kwa Kesi zaidi
Mallya: Ulifanya jitihada gani Kujua pale ulipo ni wapi?
Shahidi: Baada ya Ile zamu alikuja Koplo Mweupe nikaanza Kuongea naye
Nikamwambia mimi ni Mzaliwa wa Mwanza, akaniambia na yeye alishawahi kuishi Mwanza
Nikamwambia nilishawahi Kuwa Mwanajeshi wa KJ 92
Akaniambia kuwa kama Ulikuwa Mwanajeshi wa 92 KJ basi mmeshafika hapa watatu sasa
Mallya: Unaweza Kutueleza Mahakamani Ulijuaje ni Koplo.?
Shahidi: Kwa Uniform zake na Jinsi Renki zilivyokaa
Mallya: Kuna wakati gani ulimwambia hapa ni wapi?
Shahidi: Baada ya Kuniambia tumeshafika watatu na hapa ni Mbweni
Mallya: Ulipata kujua au Kumuona Mshitakiwa wa Pili Adamoo?
Shahidi: Alinimbia Mmoja yupo ila hakai sana Mlangoni anajificha ficha sana Kwenye Kona ktk Cello yake
Jaji: Umesema Mmoja..?
Shahidi: Kwenye Cello yake hakai Mlangoni anajibu akiwa apembeni Ila Mmoja nimeongea naye kajitambulisha ni Luteni wa Jeshi anatoka KJ 92. Anaitwa Dennis Urio
Mallya: Unaposema anatoka 92 KJ Unamaanisha nini..?
Shahidi: Anatokea Kikosi cha Komandoo
Jaji: Subiri Kidogo
Ulimtumia?.?
Shahidi: Nikimtumia Yuleyule Askari kuwa yule aliyejificha anaitwa Adamoo Mwambie Ling'wenya anakuuliza Vipi hali?
Mallya: Ulijuaje aliyejificha ni Adamoo
Shahidi: Ni kwa Ufahamu wangu baada ya Kuambiwa tupo watatu na na Adamoo na Urio nimewaona Tazara nikajua ndiyo hao hao
Mallya: Kitu gani kilifuata baada ya hapo?
Shahidi: Aliniambia anaendeela Vizuri, Tukawa tumezoeana hata alipokuwa anaingia kazini alikuwa lazima aaanze Kuita " Sauti ya zegeeeeee" hata akija kiraia
Mallya: Unaweza kukumbuka pale Mbweni ulikaa kwa Muda gani.?
Shahidi: Nilikaa kuanzia Tarehe 09 Mpaka tarehe 19 Nilipofikishwa Mahakamani
Jaji: Tarehe 19 ya Mwezi gani .?
Shahidi: 09 ya Mwezi wa 08 Mpaka Tarehe 19 ya Mezi 08 Mwaka 2020
Mallya: Nakurudisha Moshi, Ulipopigwa Kwa marungu ukaomba Kurukaruka nini Maana yake.?
Shahidi: Niliomba Kurukaruka ili nichezeshe Visigino,Maumivu yasikae sana
Wakili wa Serikali: OBJECTION wakati Shahidi anatoa Ushahidi wake Asubuhi hakusema kuwa Mahita ndiye aliyempiga
Jaji: What is your Concern katika hilo
Wakili wa Serikali: Mwanzo halikutajwa Jina la Mahita ndiye aliyempiga
Jaji: Lilisemwa au halikusema
Jaji: Sasa itabidi nirejee nilichokiandika Asubuhi
Jaji anasoma
" Wakati anatoa ushahidi wake Mshtakiwa alisema alipigwa na Mahita peke yake" Wengine walikuwa wanauliza Kwanini nilikuwa Moshi
Jaji: Bila shaka Mahita ndiye aliyetajwa Kufanya kazi hiyo, Tunaweza Kuendelea
Mallya: Kile Kitendo cha Kuomba Kurukaruka maana yake ni nini?
Shahidi: Yale Maumivu ya Kupigwa kwenye Nyayo kama ningekaa yangezidi,Kwangu niliona Bora Kurukaruka kuyapunguza, Sikutaka Kukaa kabisa
Mallya: Wakati Unasafirishwa Kutoka Kilimanjaro Kuja Dar es salaam Mikono yako ilikuwaje
Shahidi: Ilikuwa imefungwa Pingu
Mallya: Na Uliposhuka pale Tazara Mikono yako ilikuwa katika hali gani
Shahidi: Ilikuwa na Pingu
Mallya: Na Ulipokuwa Mbweni Mikono yako ilikuwaje
Shahidi: Nilikuwa na Pingu
Jaji: Kwa hiyo ukiwa Cello Tazara na Mbweni Mikono yako wakati wote ilikuwa na Pingu
Shahidi: Ndiyo Mheshimiwa Jaji
Mallya: Wakati wote huo unafungwa pingu unaweza Kuielezea Mahakama Ulikuwa unajisikiaje
Shahidi: Sikuwa najisikia Vizuri,Ukizungatia Goodluck lazima azibane Sana zile Pingu hata Nikimwambia Mahita,Yeye anasema muache hivyo hivyo
Mallya: Wakati wote huo Ukiwa Mbweni Adamoo ulimsikia tena
Shahidi: nilimsikia kwa sababu kila Siku Asubuhi lazima Nimuita Vipi hukooooooo,Yeye anajibu Mdogo Mdogo
Mallya: Katika Kesi hii Ndogo elezea uhusika na Ushiriki wake
Shahidi: Pale Rau yeye Ndoye alikuwa anatoa Amri zote Kama Kutupiga pingu, Kutuchukua Kutuweka kwenye gari
Mahita wakati ananishughulikia katika Kijumba nilipopatia Mateso yeye ndiye alikuwa akinihoji
Mallya: kwa hiyo ASP Kingai akikwepo wakati Unafanyiwa mateso
Shahidi: Alikwepo
Mallya: Na uwepo wake alikuwa anafanya kitu gani
Shahidi: Yeye ndiye aliyekuwa anatoa Amri, pale Tazara Kingai alikwepo na Goodluck akaniambia kiukweli Mwenzako anatumia madawa ya kulevya, Nikajibu si kweli akasema Ngoja tuone mbeleni
Mallya: Unasema Ulimuona Kingai pale Mbweni
Shahidi: Alikwepo
Mallya: Ulimuona kiwa anafanya nini.?
Jaji: Subirni Hadhana inalia
Mahakama Kimyaaaaaaaaaa
Jaji: Tunaweza Kuendelea
Jaji: Unasema ulimuona Kingai Mbweni ulipotolewa Nje ,ulitolewa nje na nani.?
Mallya: Ulimuona Wakati gani
Shahidi: Wakati Goodluck na Mahita Wananitoa nilipishana naye nikapelekwa kwenye Kile Chumba
Mallya: Mheshimiwa Jaji Sina swali la ziada
Jaji: Sijui kama Muda Uliobakia Unatosha kwa Maswali au Tu break Mpaka Kesho
Kibatala ananyanyuka na kwenda kwa Mawakili wa Serikali kwa Mashauriano
Jaji: Wakili Kibatala...
Kibatala: Busara inatuongoza tupumzike Mpaka Kesho
Jaji: nashukuru sana Tunaahirisha Mpaka kesho Saa 3 Kamili Asubuhi ambapo Shahidi wa Pili wa Utetezi ataendelea Kutoa Ushahidi wake