Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 3,585
- 8,106
Shadraki, Meshaki na abednego waliokolewa kwenye tanuri la moto, kwenye hili nalo MUNGU atalisimamia
Hao hawakuwa magaidi ndiyo maana Mungu aliwasimamia
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Shadraki, Meshaki na abednego waliokolewa kwenye tanuri la moto, kwenye hili nalo MUNGU atalisimamia
Akiitwa lazima atasema yote..maana Kingai kasema walitaka kumdhuru Sabaya.Kwa sasa ameshaachana na mambo yenu ya kidunia!
Umejitahidi kweli kweli kuripotiRPC Kingai ameeleza hatua kwa hatua bila kuacha shaka jinsi Freeman Mbowe alivyopanga kumuuwa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai Ole Lengai Sabaya kwa kutumia perfume ya sumu kwa madai kuwa Sabaya alikuwa anatishia nafasi ya Mbowe kuendelea kuwa mbunge wa jimbo la Hai.
![]()
RPC Kingai aeleza Mbowe alivyopanga kumdhuru Sabaya
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Ramadhani Kingai akisoma maelezo ya mshtakiwa wa pili katika kesi ya uhujumu uchumi, Adam Kasekwa amesema mtuhumiwa huyo alisema Freeman Mbowe alipanga...www.mwananchi.co.tz
sawa TU. ILA TUJUA TU UKWELIRPC Kingai ameeleza hatua kwa hatua bila kuacha shaka jinsi Freeman Mbowe alivyopanga kumuuwa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai Ole Lengai Sabaya kwa kutumia perfume ya sumu kwa madai kuwa Sabaya alikuwa anatishia nafasi ya Mbowe kuendelea kuwa mbunge wa jimbo la Hai.
![]()
RPC Kingai aeleza Mbowe alivyopanga kumdhuru Sabaya
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Ramadhani Kingai akisoma maelezo ya mshtakiwa wa pili katika kesi ya uhujumu uchumi, Adam Kasekwa amesema mtuhumiwa huyo alisema Freeman Mbowe alipanga...www.mwananchi.co.tz
Kesi ya kipumbavu kabisaAaaa,Kama sio kudharirishana hii ndio Nini sasa?
* Nikaue mtu Hai
+ Nikakate miti iringa
*Nikachome vituo vya mafuta morogoro
Malipo 150,000/= watu wawili!
Mbona haingii akilini kwa muandika maelezo hata kwa mtoa maelezo pia, au nyinyi mnaonaje ndugu zangu.
Maana Mimi ninavyo jua hata kwa wale wazee wa Robbin hood za macho mekundu kule Shinyanga huwa nasikia wanapewa mpaka maksai 5 x 700,000/=
Makomandoo 75.000/= kazi 3 za kigaidi?
Akili yangu inakataa hata mzee wa Robbin hood hawaezi kubari hiyo biashara.
Lissu naye angekuwepo apige maswali ya kutosha mpaka ajinyee huyu mzee mpuuziTayari baadhi ya Wadau wa Maendeleo, akiwemo Mwakilishi wa Ubalozi wa Canada wamewasili Mahakamani.
Hadi saa 3:30 asubuhi hii Watuhumiwa walikuwa bado hawajaletwa Mahakamani.
====
Hatimaye Mbowe na wenzake wameletwa Mahakamani
Jaji Joachim Tiganga ameingia Mahakamani
Wakili wa serikali Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
1. Robert Kidando
2. Nassoro Katuga
3. Ignas Mwanuka
4. Esther Martin
5. Tulumanywa Majigo
6. Jenitreza Kitali
Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo Lake
1. Peter kibatala
2. Jeremiah Mtobesya
3. Michael Mwangasa
4. Nashon Nkungu
5. Dickson Matata
6. Alex Massaba
7. Jonathan Mndeme
8. Hadija Aron 9.
Idd Msawanga
Jaji anaomba Kuwaona Washitakiwa wote 1,2,3 na 4
Wanainuka Kwa kutajwa kwa Namba
Wakili wa Serikali anaomba kesi Kuendelea na Shahidi yupo tayari Lakini Kabla ya Kuendelea anaomba kufuatilia kuhusiana mabadiriko yaliyopalekea mpaka Mheshimiwa Jaji Kuja mwingine kwa mujibu ya kifungu cha 299 CPA (Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai).
JAJI: Upande wa utetezi
Peter Kibatala: hatotatumia Haki ya kumuita tena Shahidi kwa kesi Inayoendelea hapa.
Jaji anaandika.
JAJI: wote mnafahamu na mlikwepo siku ya tarehe 20 mwezi huu na Jaji aliyekuwepo alielekeza Jaji Mwingine atakuja kuendelea na Kesi hii, Na Jaji Mwingine Ndiyo Mimi, kwa mujibu wa sheria ya mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 Kifungu cha 299.
JAJI: Kwamba Upande wa Utetezi Mnahaki ya a Kumuita tena shahidi kwa kuwa Mmesema hamna nia nitawaruhusu Upande wa Jamhuri Kumuita sasa Shahidi wao tuweze Kuendelea. Mawakili wote Wanainuka ishara ya Kukubaliana na Uamuzi wa Jaji na Kupokea Maelekezo ya Mahakama.
Wakili wa Serikali anatoka Kwenda Kumuita Shahidi wa leo.
Mahakama ipo Kimya
ACP KINGAI anaingia na Kupanda Kizimbani.
Robert Kidando Wakili wa Serikali anamtaarifu Jaji Kuwa Shahidi amefika.
JAJI: Majina yako Tafadhali
SHAHIDI: ACP Ramadhan Kingai
JAJI: Unakumbuka Uliwahi Kufika Mahakamani, ukaapishwa kutoa Ushahidi, Mahakama inakukumbusha Upo chini ya Kiapo hicho. SHAHIDI: sawa Mheshimiwa
JAJI: Mtakumbuka Mawakili kuwa Siku ya Tarehe 20 Jaji alipokea Kielelezo, baada ya Kupokelewa Kinatakiwa Kusomwa Mahakamani. Naomba Kuanzia hapo Shahidi akabidhiwe Kielelezo aweze Kusoma Kielelezo.
WAKILI WA SERIKALI: Soma Sasa Kielelezo Kuanzia kurasa ya kwanza.
SHAHIDI: Adama Kasekwa anaishi Chalinze Maelezo ya Onyo Chini kifungu cha Sheria ya Makosa ya Jinai Sura ya 20. MIMI kingai nakuonya wewe Adam Kasekwa
SHAHIDI: Ulazimishwi kusema lolote Pia unaweza Kualika Ndugu, Jamaa au Mwanasheria Kushuhudia utoajo wako Maelezo. Mtuhumiwa akasaini na Mimi nikasaini.
MAJIBU YA ONYO
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo..
MIMI Adam Kasekwa anaonya na Kingai Chini ya Kifungu cha 24 cha Sheria Mwenendo wa Makosa ya Jinai Silazimishwi na yoyote Kutoa Maelezo yangu. Je, Upo tayari Kutoa Maelezo Yako.
Jibu, Ndiyo Nipo tayari.
Shahidi anasoma kielelezo: Maelezo yamechukuliwa Katika Ofisi ya RCO ilala MIMI Adam Kasekwa Nimezaliwa Mkoa wa Mbeya Wilaya ya Ileje... Mwaka 2011 nilijiunga na Recruting Maktopora. Nikachaguliwa Kujiung na Mafunzo Ukomando 92KJ.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Mwaka 2014 niliteukiwa kwenda kituo cha Msangani Kujifunza ulinzi, amani na nikachaguliwa Kwenda DR Congo. Mwaka 2017 nilimaliza Mkataba na kurejea Nilipata malipo na Kumuoa Mke wangu Lilian ambaye naishi naye Mpaka Leo.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Nimepata naye Mtoto Mmoja. Nilirudi nikaa Miezi 6 kazini Nikaugua Ugonjwa wa aKili Nikaachishwa kazi na kulipwa mafao ya Millioni 4 na Laki 6.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Je unamfahamu Luteni Denis? Ndiyo, nilikuwa Mkinga Mawasiliano hayapatikani. Niliporudi nikaambiwa mwenzangu ananitafuta.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Niliporudi nyumbani nilimpigia Simu Mwenzangu Mohammed Ling'wenya Kwamba Kuna kazi ya VIP protection. Akaniambia inabidi twende Morogoro Kumuona Luteni Urio. Tulipoenda akatuambia Kuna kazi ya VIP protection ya kumlinda Freeman Mbowe
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Akatupatia TSh 21,000 nauli ya Kwenda Moshi. Siku hiyo hiyo tulirudi Chalinze na kuanza Safari ya kwenda Moshi Tulipokelewa na Dereva wake anayeitwa Willy Alitupokea na Pick Up Nyeupe yenye maandishi ya M4C.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Tukaenda Mpaka Kwenye Hotel Ya Mheshimiwa Mbowe Huko tulimkuta Khalfani Bwire aliyetutambulisha kwa Mbowe, "Mkuu wale Vijana tuliowaagiza ndiyo hawa hapa." MBOWE akatueleza Kuwa Sabaya anamvuruga sana na anamvuruga wapiga Kura.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Kwamba anawatisha Wapiga kura wake kiasi cha Kuhatarisha Kurudi kwake. Na kwamba, akatuelekeza tumdhuru Kwa Njia yoyote. Akatuelekeza Maeneo yake ya Moshi na Arusha.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Tulipanga kumdhuru kwa Spray Spray ya sumu alitafuta Mohammed Ling'wenya
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Siku inayofuata tulikuwa Mimi na Mohammed na wanachana wawili siwakumbuki Majina Baada ya Kufika Dar es Salaam Tulimfikisha Mheshimiwa Mbowe Nyumbani
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Akatukabidhi TSh Laki 2 kwaaajili ya Kununua Nguo. Kwa sababu Kesho yake tulikuwa tunampokea Mheshimiwa Lissu. Na Siku ya tarehe 27 Julai Mbowe alitutumia Kila moja TSh 78 Elfu ya Nauli Ya Kwenda Moshi.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: SIKU ya Tarehe 01 August Tulienda Moshi Tukamkuta Mbowe akiwa na Khalfani Bwire Akatuelekeza Kuwa tufanye ile kazi yake Haraka Akatuelekeza Maeneo anayokaa Sabaya kama vile Milestone PIA Akatuelekeza Tuje DSM, Kuchoma Vituo Vya Mafuta.
Shahidi anaendelea kusoma kielelezo: Kwamba yeye anatachochea maandamano ILi Serikali ionekane Imeshindwa Kuandaa Uchaguzi. Tulienda Maeneo ya Boma Ng'ombe Njia ya kuelekea Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kumfuatilia.
Siku ya terehe 03 tulienda Maeneo ya RAU madukani kwa ajili ya kubana Matumizi. Kwa sababu Mheshimiwa alituachia Pesa Laki Moja na Nusu kwa ajili ya kukaa, isingetosha. Tulienda Kukaa kwa Dada yake kukaa kwaajili ya Kubana Matumizi.
Swala la Kupanga Ugaidi ni la kweli Na swala la a kukutwa na Silaha ni la kweli Wakati Polisi wananikamata pia walinikuta na Heroine Baada ya kuchukua Vitu hivyo Askari walisaini na Mimi nikasaini na Polisi walichukua Vitu hivyo kwenda Central
Baada ya Maelezo hayo Adam Kasekwa akasaini Na Mimi Kingai nikasaini Baada ya Kuchukua Maelezo hayo Muda ulikuwa ni saaa tatu.
Wakili wa Serikali: ACP Kingai Kutokana na Maelezo uliyoyasoma hapa mahakamani Yeye alikuelza nini Kutokana na Maelezo Uliyoyasoma Mahakamani Shahidi: alikiri kuwa anamfahamu Luteni Urio. Alikiri Kupewa Maelekezo ya kazi kutoka kwa Mheshimiwa Mbowe
Shahidi: Alikiri Pia alipewa Maelekezo ya kazi Kutoka akwa Mbowe Kupitia Kwa Luteni Deni Urio. Alikiri Pia kuwapo Moshi tarehe 24 Mwezi wa 07, 2020
Shahidi: Alikiri Pia kuwapo Moshi na wenzake Mohammed Ling'wenya na Mwenzake aliyemtaja Kwa Jina la Kakobe. Baada ya Ufutailiaji tukamfahamu ni Moses Lijenje. Alikiri Pia kufanya Mkutano yeye na wenzake wanne.
Yeye Mwenyewe, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya, Moses Lijenje (Aliyemtaja Kwa Jina la Kakobe) Khalfani Bwire na Freeman Mbowe
Wakili wa Serikali: kwa Mujibu wa Mkutano huo nini kiliendelea. Shahidi: Mbowe alitoa Maelezo kuwa Sabaya anamfanyia Vurugu, (Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai)
Wakili wa Serikali: kitu gani Kingine alikueleza Shahidi: Mtuhumiwa alikiri Kupewa Pesa 150,000/= kukidhi Mahitaji kipindi watakapokuwa hapo Moshi.
Wakili wa Serikali: tueleze Shahidi kuhusiana na kilichofuata Shahidi: Alikiri Kuwa Siku ya Tarehe 01 Mwezi wa Nane saa 11 Alfajiri kabla ya Safari ya Kuja DAR ES SALAAM Aliwaelekeza wamdhuru Ole Sabaya.
Shahidi: Akawaonyesha Picha ya Ole Sabaya Kupitia Simu yake ya mkononi Aliwapa Maelekezo Kufanya kazi hiyo na Kwamba baada ya hapo atawataka warudi Dar es Salaam. Alipanga kuwapa kazi ya kwenda Kulipua Vituo Vya Mafuta. Alipanga kufanya Vurugu kwenye masoko.
Mtobesya: OBJECTION Naomba Shahidi ajielekeze Kwenye kikichoandikwa kwenye Statement Mambo ya Kituo cha Mafuta na Masoko havijatajwa.
Jaji: Kwahiyo a some?
Mtobesya: ajielekeze kikichoandikwa hata kama ana Rudia Kuelezea, Sheria inasema Statement itajielezea Yenyewe.
JAJI: Upande wa Mashitaka
Wakili wa Serikali: Sahihi Mheshimiwa tutarekebisha.
Wakili wa Serikali: Alikueleza Lengo ilikuwa ni nini
Shahidi: Lengo ni Serikal ionekane imefeli Alikiri Pia kukamatwa na Polisi Siku ya tarehe 05 Mwezi wa 08, 2020 akiwa Rau Madukani.
Alikiri Pia kukamatwa na Pistol aina ya Ruvern ikiwa na Risasi 03.
Shahidi ACP KINGAI: Alikiri kukamatwa na Kete 58 za Madawa aina ya Heroine.
Wakili wa Serikali: baada ya kuwa umeandika Maelezo hayo, yeye ulimpeleka wapi kwa Siku hiyo.
Shahidi ACP KINGAI: ilikuwa Siku ya tarehe 07 Mwezi wa 08, 2020 nilimrudisha Mahabusu.
Wakili wa Serikali: Shughuli gani Nyingine ili endelea baada ya Shughuli hii
Shahidi ACP KINGAI: tuliendelea na Upelelezi ya Kuwatafuta watuhumiwa wengine. Maeneo ya Chang'ombe tulimkamata Khalfani Bwire.
Wakili wa Serikali: Kwa tuhuma Gani
Shahidi ACP KINGAI: Kwa tuhuma hizi hizi za Kula Njama kutenda Matendo ya Ugaidi.
Wakili wa Serikali: nini kiliendelea
Shahidi ACP KINGAI: nikimtaka Khalfani Bwire aandike Maelezo yake
Wakili wa Serikali: elezea Kuhusu Kumkamata kwake
Shahidi ACP KINGAI: baada ya a kuwasiliana na Askari aliyekuwa kwenye Pointi akiwa kwenye gari, tukielekeza Gari iingie Kituo cha polisi Chang'ombe. Tukawa tumeingia pale na Inspector Mahita na ASP Jumamne.
Jaji: ASP nani? Shahidi: Jumanne
Wakili wa Serikali: baada ya Kumkamata Mlimpeleka wapi
Shahidi: tuliekeza Superitendent Lukangira wa hapo hapo Chang'ombe. Hii ni baada ya Mtuhumiwa kutuelekeza hana Makazi hapa Dar es Salaam ni Mkazi wa Ngerengere.
Wakili wa Serikali: Nia ya Kuuliza kwake ni wapi ilikuwa ni ya nini
Shahidi: nia ilikuwa kufanikisha Shughuli za kiupepelezi
Wakili wa Serikali: baada ya Lukagingira kuandika Maelezo yake nini Kilifuata
Shahidi: Tukawa tunaendelea Kufuatilia Makazi yake, Tofauti na Taarifa alivyokuwa ametoa yeye kwakuwa tulijua haiwezekani awe kila Siku anaenda Ngerengere.
Wakili wa Serikali: Wakati Unapata Taarifa ana makazi Wilaya ya Temeke, elezea Sasa Maelezo yalikuwa yanaandikiwa wapi
Shahidi: Maelezo yalikuwa yanachukuliwa Kituo cha Polisi Chang'ombe na Mimi niliweka Bass Central polisi (Ilala).
Wakili wa Serikali: baada ya Kutoa Maelekezo Hatua Kuchukua Maelezo Isimame, nini kilifuata
Shahidi: tulipata Taarifa Mtuhumiwa anakaa Temeke Makangarawe, Tuliungana na Detective John wa Temeke na RCO kwa ajili ya kwenda Kumpekua Makazi yake.
Wakili wa Serikali: Mlienda sehemu ipi haswa huko Mkangarawe
Shahidi: Ule Mtaa Jina Limenitoka
Wakili wa Serikali: Uliwezaje Kuutambua sasa
Shahidi: tukielekezwa na Watu hadi Nyumba alipokuwa amepanga Mtuhumiwa.
Wakili wa Serikali: Elezea sasa hiyo Shughuli ilifanyikaje na Khalfani Bwire alikuwa wapi.
Shahidi: Tuliongozana na Mtuhumiwa, Tukamtafuta Mwenyekiti wa Ule mtaa, Tukamkuta na Mwenye nyumba aliyempangisha Khalfani Bwire na hata Mke wake alikwepo.
Wakili wa Serikali: huyu Mwenyekiti ni wanini?
Shahidi: Ni Mwenyekiti wa Mtaa
Wakili wa Serikali: Nini Kilifuata
Shahidi: Nilimuelekeza ASP Jumanne Kwa Kushirikiana na Detective John Kutoka Ofisi ya RCO Temeke na kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Mtaa na hata Mke wake.
Wakili wa Serikali: Elezea sasa Katika Upekuzi huo Mlikuta nini?
Shahidi: Vitu mbalimbali vilipatikana kama Uniforms za JWTZ, Masharti ya JWTZ, Tshirt za JWZT, name tags za kwake za JWTZ.
Wakili wa Serikali: baada ya Kupata Uniforms na Vifaa Mbalimbali nini Kilifanyika baada ya Kupata Vitu hivyo.
Shahidi: Viliorodheshwa katika Hati ya Uchukuaji Mali. Wakati wa Upekuzi tulikuta Kidaftari kilichokuwa na Ramani na Majina ya Vituo Vya Mafuta.
Wakili wa Serikali: baada ya kuorodhesha kitu gani kilifanyika
Shahidi: baada ya Kuwa Viliorodheshwa yaliandikwa Majina ya walioshuhudia Upekuzi huo. Pia wakasaini Hati ya Uchukuaji Mali. Mtuhumiwa pia alisaini Hati ya Uchukuaji Mali na aliyepekua alisaini Hati hiyo.
Wakili wa Serikali: Baada ya Kukamilisha Hati ya Uchukuaji Mali, Kitu gani Kiliendelea
Shahidi: Nilikuwa nimeelekeza Mashahidi walioshuhudia waandikwe Maelezo pale pale
Wakili wa Serikali: baada ya Kukamilisha
Shahidi: Tulichukua Vitu tulivyo orodhesha na Mtuhumiwa akarudishwa a kituo Cha Polisi.
Wakili wa Serikali: Kituo gani cha Polisi Shahidi: Chang'ombe
Wakili wa Serikali: Baada ya kumrudisha Kituo cha Polisi Chang'ombe Kitu gani pia Kiliendelea.
Shahidi: Mtuhumiwa tulimkamata na Kidaftari chenye Ramani ya Vituo Vya Mafuta Dar es salaam, Soko la Kilombero Arusha.
Tukachukua Sampuli za Miandiko ya Watuhumiwa wote. Lakini pia tuliendelea na hatua ya kuwatafuta watuhumiwa wengine
Wakili wa Serikali: watuhumiwa gani wengine Mlikuwa mnawatafuta
Shahidi: Watuhumiwa wengine tuliokuwa tunawafutilia ni Mtu alikuwa anaitwa Gabriel, Lijenje, Malima, Khalid na Jamaa Mmoja anaitwa Kaaya.
Wakili wa Serikali: nini hatima ya hao mliokuwa mnawafuatilia
Shahidi: Ukimuondoa Mtu Mmoja anaitwa Malima, Watuhumiwa wote walifikishwa mahakamani.
Wakili wa Serikali: vipi kuhusu moses Lijenje Shahidi: bado hatujafanikiwa Kumpata
Wakili wa Serikali: Hapa Mahakamani kuna Washitakiwa Wanne inakuwa je hao wengine hawapo Mahakamani kama Walifumgukiwa Mashitaka
Shahidi: walifutiwa Mashitaka baada ya Kuonekana Ushahidi hakuwa wakutosha ukilinganisha na wenzao.
Wakili wa Serikali: ACP kingai katika Ushahidi wako tangu Mwanzoni umezungumzia kukamatwa Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Khalfani Bwire Vipi ukamatwaji wake Mshitakiwa wa Nne.
Shahidi: Freeman Mbowe alikamatwa 21 July 2020 akiwa Mwanza
Wakili wa Serikali: Kwa tuhuma gani
Shahidi: Kwa tuhuma hizi hizi
Wakili wa Serikali: Wakati Unatoa Ushahidi wako Ulizungumzia kukamatwa hawa wengine Mwaka 2020 na huyu 2021 elezea Ilikuwa je hapa Mahakamani.
Shahidi: Tulikuwa tunajirishisha haswa uhusika wake. Tulikuwa bado tunaendelea Kufuatilia mawasiliano Na Uchunguzi wa Forensic ambao ulikuwa unahusiana na Shauri hili
Wakili wa Serikali: Sababu ukamataji ulifanyika 21 July Mwaka 2020, ni lini taarifa zilifahamika rasmi.
Shahidi: Zilifahamika Mwanzoni July 2020
Wakili wa Serikali: wakati anakamatwa Upelelezi ulikuwa umefikia Hatua gani
Shahidi: Upelelezi wetu kwa muda huo tunamkamata ulikuwa umekamilika.
Wakili wa Serikali: Upelelezi wa aina gani ulikuwa unaendelea kwa Mshitakiwa nne
Shahidi: Tulifanya Forensic na Divices za Kieletronic tuliokuwa tunafuatilia Kujiridhisha dhidi yake na Tuhuma zilizokuwa zinamkabili.
Wakili wa Serikali: wakati Unatoa Ushahidi wako Mwanzoni ulisema Ulielezea Kuwa Umelekeza kufungua Jalada la Tuhuma za Kigaidi.
Shahidi: Kulingana na Taarifa ambazo tulikuwa tumezipata kwa Luteni Urio na aina Ya Vitendo vilivyokuwa Vimepangwa na Watuhumiwa Ilikuwa ni Kudhuru Viongozi wa Serikali, kufanya Vurugu sehemu zenye watu wengi, Kulipua Vituo Vya Mafuta, Hata Miti kwenye highway kukatwa Kuzuiwa Magari yasipite, Hasa katika Barabara ya Morogoro kwenda Iringa.
Wakili wa Serikali: Ukatafsiri ni Vitendo gani
Shahidi: Vitendo vyenye kuleta hofu kwa Wanachi Kujiona hawapo salama, Ni Vitendo vinavyoleta Tafsiri la Shitaka la Ugaidi
Wakili wa Serikali: ulisema katika Taarifa ya Luteni Urio ulisema walipanga Kuonyesha kuwa Nchi haitawaliki.
Mtobesya: OBJECTION kaka yangu Wakili Msomi ajielekeze Kwenye fact siyo Opinion Maana huyo ni Shahidi wa Fact, He is doing too Much Sasa Maana Mwanzo tulijua ameteleza.
Wakili wa Serikali: Sawa Mheshimiwa Jaji nitaomba nijielekeze sawa Sasa.
Wakili wa serikali: Vitendo hivi vilipangwa Vifanyike wapi
Shahidi: Mwanza, Moshi, Dar es Salaam na Arusha
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vifanyike Lini
Shahidi: Kabla ya Uchaguzi wa Mwaka Jana
Wakili wa Serikali: ni hayo tu Kwa sasa Mheshimiwa Jaji
Jaji: Upande wa utetezi
Mtobesya: Asante Mheshimiwa Jaji nitaomba niendelee kwa Niaba ya Mshitakiwa wa kwanza.
Mtobesya: ni sahihi Shahidi wewe ulikuwa ni sehemu ya waliokuwa wanahusika na upelelezi wa Kesi hii
Shahidi: ni sahihi
Mtobesya: ni sahihi kuwa Baada ya kupokea Maelezo kwa DCI BOAZI mkafungua Jalada
Shahidi: Ni sahihi
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji ni lini Mlifungua Jalada
Shahidi: Yalikuwa Majalada Mawili la upelelezi na Kesi
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Lilifunguliwa Jalada la Uchunguzi
Mtobesya: Uchunguzi au Upelelezi
Shahidi: yote ni yale yele labda useme unataka Jalada gani
Mtobesya: wewe Ndiye unayetoa Ushahidi
Shahidi: Sawa Mwanzo Lilifumguliwa Jalada la Uchunguzi wa Kula njama. Ilikuwa July Mwaka Jana.
Mtobesya: yote Mawili Mlifungua kwa Pamoja au Tofauti
Shahidi: Kuna Utaratibu wa Kiupelelezi labda kwa sababu ujawa mpelelezi Ndiyo Maana Unahangaika Kuna Jalada la Awali la Uchunguzi lakini unapopata Taarifa unafungua Jalada la Kesi ya kula njama Lilifunguliwa na Mkaguzi wa Polisi Msaidizi anaitwa Swila
MTOBESYA: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kabla hamjawakamata Watuhumiwa Mlikuwa mmekusanya Taarifa zipi kwa wakati huo
Shahidi: Taarifa za kutaka kuwadhuru Viongozi wa Serikali, Kufanya Maandamano ya siyo na Kikomo, Taarifa za Kukata Miti na Kufanya Uporaji Magari yasipite na Kutaka Nchi isitawarike
MTOBESYA: kwa hiyo hizo Taarifa ndiyo zilitengeneza Kosa la Kula Njama
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Mwambie Mheshimiwa Jaji hizo Taarifa Mlizipata kabla au Baada ya Kumchukua Maelezo Mshitakiwa wa Pili
Shahidi: Kabla
MTOBESYA: kabla ya Kesi Ndogo unakumbuka ulisema Urio aliwapatia Taarifa kuwa Vijana wamepatikana, Unakumbuka ulisema tarehe Ngapi.
Shahidi: Ilikuwa tarehe 04 Mwezi wa Saba Mwaka Jana
MTOBESYA: wakati unaelezea (Kusoma) unakumbuka Kielelezo ulipata wasaa wakujua Urio alishiriki Vipi katika swala hili?
Shahidi: sijaelewa Vizuri
MTOBESYA: Statement hii ambayo unasema uliandika unakumbuka Urio alishiriki namna gani?
Shahidi: naomba Jaji anisomee anapoparejea
Jaji: labda tuweke, Ushiriki wa urio ulikuwa Vipi
Shahidi: Urio ameshiriki kwa kuwatafuta Vijana, ameshiriki kuwapatia nauli na ameshiriki Kutafuta Vijana waliofukuzwa Jeshi
Mtobesya: Umesema kwenye Maelezo alifanya hayo Tarehe ngapi
Shahidi: Sikumbuki tarehe
MTOBESYA: sasa nije kwenye Maelezo uliyoyachukua, kwa ajili ya Kumbukumbu Unakubaliana na Mimi Kuwa kuna namna tatu za Kuchukuliwa Maelezo. moja, Kwa Anateyetaka Kuchukuliwa Maelezo kuomba Karatasi na kalamu na kuandika Mwenyewe. Pili, kwa anayehojiwa kuongozwa Tatu, kwa njia ya Maswali na Majibu Wewe ukichagua Njia gani?
Shahidi: Mimi nilitumia Maswali na Majibu
Mtobesya: naomba niishie hapa
Wakili Malya: naomba Kielelezo (Statement) Mahakama inampatia John Malya
Wakili Malya: Unasimu ya mkononi
Shahidi: Ndiyo
Wakili Malya: unaweza kututajia EMEI namba ya Simu yako
Shahidi: Hapana Siwezi
Wakili Malya: kwanini..?
Shahidi: Sijaamua kuishika
Wakili Malya: Una ya mtu yoyote wa Karibu yako unayoikumbuka
Shahidi: Hapana
Wakili Malya: sasa Katika maelezo Adam alikutajia EMEI namba Kutoka wapi
Shahidi: Alikuwa na kikaratasi
Wakili Malya: Ulizungumza kwamba Mshtakiwa alikuwa na kikaratasi?
Shahidi: Sikuzungumza
Wakili Malya: ni sahihi unapoandika Maelezo unaandika kwa usahihi kabisa
Shahidi: Sahihi Kabisa
Wakili Malya: kwa uelewa wako Unapotaja Sheria, kwa Mbele Mwaka Unatajwa, Maana ya Kuwa na Miaka katika Sheria.
Shahidi: Mimi siyo Mwanasheria
Wakili Malya: Nafahamu wewe siyo Mwanasheria ila Umeandika Mwenyewe Vifungu Vya Sheria ili Mtu ajue Haki yake
Shahidi: Ndiyo nafahamu. Sasa Unatoa somo
Wakili Malya: Kwa hiyo wewe Unaweza kuandika Mwaka wowote tu.
Shahidi: am not aware of It
Wakili Malya: kwa hiyo wewe Unaweza Kuandika Sheria na Mwaka ukaweka Wowote tu
Shahidi: Hapana naweka na Sheria
Wakili Malya: na Mwaka kama imefanyika amendment Zake? Sasa Kwa Maelezo hayo uliyoyashika Tusomee hapa.
Shahidi: Cap 20 REV 2018
Wakili Malya: sasa hiyo Sheria Hakuna. Wewe umechukua Maelezo ya Onyo kwa Sheria ambayo haipo, Unasemaje kwa hilo
Shahidi: Hiyo ni Typing Error kwa sababu imechapwa. Ile niliyoandika kwa Mkono wangu huenda sikuandika hivi.
WAKILI mallya: wakati unaisoma hapa Mahakamani Ulisema hapa kwamba hii siyo au ulikariri ukawa unaisoma tu Hapa
Shahidi: kwenye eneo hili Onyo Chini ya Kifungu Cap Rev 2002 badala Ya kusomeka 2018.
Wakili Malya: kwa hiyo ulipaswa Kusomeka Vinginevyo siyo hiyo
Shahidi: Ndiyo
MALYA: ushawahi Kusikia Kiongozi wa Polisi Liberatus Barrow aliuwawa
Shahidi: Ndiyo Wakili Malya: aliuwawa?
Shahidi: Ndiyo WAKILI
Mallya: waliomuua Walikamatwa Ndiyo
Shahidi: Ndiyo
WAKILI mallya: walishitakiwa na Makosa gani?
SHAHIDI: mauaji
WAKILI mallya: Lakini Kumdhuru Sabaya ni Ugaidi?
Shahidi: kuleta Vurugu kwenye Masoko, Kukata Miti Barabara, Kuzia Magari yasipite ni Vitendo vingeleta hofu na Wasiwasi Vitendo hivi Vinaashiria ni Vitendo Vya Ugaidi.
Wakili Mallya: umerudi Viongozi sana Ukimtoa lengai Ole Sabaya Kiongozi Mwingine nani..?
Shahidi: ni Maelezo ya Adam Kasekwa, Siyo ya kwangu
Wakili Mallya: ulipomkamatia Adamoo Moshi na Kilichokufanya usichukue Maelezo Moshi ni sababu zipi
Shahidi: Sababu za Kiupelelezi
Mallya: wakati Unatoka Moshi ulipitia Njia ipi ya Chalinze au Bagamoyo
Shahidi: Msata
Mallya: ulitoka Msata kwenda Central Njia kuna Mbweni na Oysterbay kwanini uliamua kwenda Central
Shahidi: Sababu za Maelezo na Pili Ndipo kesi ilipofunguliwa
Wakili Mallya: Wewe kwa sasa ni RPC KINONDONI Je unafahamu kuwa Kinondoni inajitegemea
Shahidi: Ndiyo, zikiwa Chini ya Kanda Maalum Dar es Salaam
Wakili Mallya: ulieza Mahakama Kwanini Huyu achukuliwe Maelezo Temeke Mkoa Mwingine wa Kipolisi na kwanini hakusafirishwa kama wenzie kuja Mkoa wa Ilala
Shahidi: Hapana sikueleza
Wakili Mallya: umesema Yalifunguliwa Majalada mawili
Shahidi: Ndiyo
Wakili Mallya: nani alifungua hayo Majalada Shahidi: Inspector swila
Wakili Mallya: Umemtaja Sabaya, Alikuwa Mkuu wa Wilaya wa wapi Vile?
Shahidi: Hai
Wakili Mallya: je pale Hai Pana Ofisi ya Mkuu wa upelelezi?
Shahidi: Ndiyo
WAKILI: mallya Je Kilimanjaro Kuna Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi?
Shahidi: Ndiyo
Wakili Mallya: Ni hayo tu
JAJI: naomba Tubreak Kwa Lisa limoja Tutarudi hapa Saa 7 na Dakika 20
Jaji anatoka
Mpaka sasa saa saba na nusu, Jaji hajaingia.
Mahakama imerejea
Wakili Robert Kidando anaomba Kumtambulisha Wakili Nasorro Katuga
Jaji: nilipo Break tulikuwa tumemaliza Maswali ya Dodoso ya Wakili wa Mshitakiwa wa Pili, Nipo sahihi..? Wawakili wa Pande zote Mbili wanaitikia, NDIYO
Jaji: namruhusu Wakili wa Mshtakiwa wa tatu aendelee, WAKILI MATATA
Kwa sasa Sabaya ameshakuwa kiumbe kipya na mabaraza ya namna hiyo siyo sehemu yake tena.Akiitwa lazima atasema yote..maana Kingai kasema walitaka kumdhuru Sabaya.
spana alizopigwa na Kibatala hatosahau hadi kiamaLissu naye angekuwepo apige maswali ya kutosha mpaka ajinyee huyu mzee mpuuzi