Kuna mtu alisema toka mwanzo kuwa huyo jaji atasema kuwa mazingira ya kesi nyingine zote ziluzorehewa yalikuwa mazingira tofauti, na ndicho alichofanya.
Niliwaambia toka mwanzo, kwenye kesi hii, hakuwezi kupatikana haki yoyote kwa sababu Serikali ndiyo inashtaki, maafisa wa TISS waliopo mahakamani ndio wanaopangwa kuisikiliza.
Kwa wasiofahamu ni kuwa marehemu Magufuli alimteua afisa wa Wasiojulikana kuwa msajili wa mahakama kwa lengo maalum. Lengo kubwa ni kuhakikisha zile kesi ambazo serikali inataka kuwakomoa watu, jaji atakayesikiliza ni lazima awe afisa wa Wasiojulikana.
Fikiria sasa hivi, jaji mkuu TISS, msajili wa mahakama TISS, Jaji kiongozo TISS. Sasa hivi management yote ya judiciary ipo chini ya Wasiojulikana. Hata ikitokea Mbowe akashinda kwenye kesi, msije mkadanganyika na kujipongeza, Wasuojulikana watakuwa wameamua iwe hivyo kwa lengo fulani.
Hata hukumu ya Sabaya siyo ya kufurahia, aliyehukumu ni afisa wa Wasiojulikana, lakini siyo kwa mfumo huru wa mahakama.